Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Viroba nomaaa
Mkapa aliwahi kumtukana prof libumbu kuwa ni prof uchwara.
tatizo lenu ukawa hampendi kuambiwa ukweli na ukweli ndo huo
Heshima yenu wanabodi!
Nimesikitishwa sana na kitendo cha Rais wa tatu wa Tanzania Mh.Benjamin Mkapa kuporomosha matusi jukwaani badala ya kujenga hoja!
Mkapa amekuwa mtu wa kupanic sana tangu alipokuwa Rais,aliwatukana waandishi wa habari wa Tanzania hadharani na kuwaita wasiofaa huku akiwakumbatia waandishi wa nje.
Wakati wa kampeni za ubunge jimbo la arumeru mashariki Mkapa pia aliporomosha matusi kwa wapinzani badala ya kujenga hoja matokeo yake Chadema ilishinda asubuhi na yeye kukimbilia uwanja wa ndege na kuondoka mapema sana asubuhi!
Mkapa amerudia kuporomosha matusi jana kwenye uzinduzi wa kampeni za CCM na kuwaita watu malofa na wapumbavu! Hivi mh.Mkapa pamoja na kukaa ikulu miaka kumi anashindwa kujenga hoja kweli na anaamua kutumia matusi kama sehemu ya kampeni kweli?
Wapinzani fanyeni kampeni ya kistaarabu acheni kujibu matusi ya Mkapa,waelezeni watanzania mtawafanyia nini mkipewa ridhaa,wananchi wanataka maendeleo sio matusi!
Kila la heri UKAWA kila la heri Lowassa na maalimu Seif.
Heeeee, Heeee ni tuna masikitiko makubwa kwa kauli ya MATUSI aliyotoa Mh. Rais mstaafu Ben Mkapa jana katika uzinduzi wa kampeni kwa chama tawala (CCM). Alisema wapinzani ni WAPUMBAVU na akarudia ni WAPUMBAVU SANA.
Sasa kwa masharti yaliyotolewa na tume ya uchaguzi ya kutotoa kauli za kuudhi wala kashfa huyu naye mbona alikiuka?
Mzee Mkapa iga mfano kwa Rais mstaafu mwenzio Mzee Mwinyi alivyotoa hotuba ya busara.
Kwa wadhifa wako hukupaswa kutukana kabisa, kwa hapo Mh umekididimiza chama.
Sasa sisi wananchi ni jukumu letu tarehe 25 Octoba,2015 kuondokana na watu wa chama kile kile miaka yoooote toka uhuru ambao hawana lugha nzuri kwa kizazi kijacho.
Jamaaaaaaniii eeeee akili kumkichwa, Oct, 25