Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mwana...Huu ndio unaitwa UDINI. Why Mapadri? Uhuru wa nchi hii haukutafutwa kwa makundi kiasi iandikwe Historia ya Mapadri, Mashehe, Mabudha, Wapemba, Wageni, Wazawa na wengineo.
Nimepotosha vipi hapo mkuu. Sawa walikua wanahamasisha, sasa niambie nini kilitokea adi akafahamika JK ndio kaletaa uhuru.. hawa wengine kiliwakuta nini?Inaelekea wewe ni kizazi baada ya uhuru ila kwa wale ambao walikuwa na akili zao ingawa watoto walishuhudia mengi na anachoandika Mohamed Said kwa yeyote yule alizaliwa miaka ya 40 na 50 na kukulia dar anaelewa.
Mimi ninakumbuka zile enzi ambapo bibi Titi na wenzake walikuwa wanapita nyumba hadi nyumba kuhamasisha akina mama kuingia Tanu.
Na ninamkumbuka mwalimu kipindi kile ambacho alikuwa anakuja mtaa wa sukuma na mafia yalipokuwa makazi ya Yanga kwenye vikao pamoja na wazee wetu. Wacha kupotosha wenzako.
Ninafahamu fika kuwa wewe unataka malumbano kwani nina uhakika unafahamu chachu za uhuru walikuja nazo baba zetu baada ya kutoka WWII.Nimepotosha vipi hapo mkuu.. Sawa walikua wanahamasisha.. sasa niambie nini kilitokea adi akafahamika JK ndio kaletaa uhuru.. hawa wengine kiliwakuta nini..?
Da 'Vinci, mwanangu una hoja dhaifu mno yani umeniangusha kwa ili bandiko lako man yaani unataka kuniambia kwamba since 1920 hakuna watu ambao walikuwa wanapambania uhuru its seem that watu walikuwa wamerelax alafu mzed baba Nyerere ndo akaje iyo 1947 akaanzisha harakati za mapambano kiukweli mzee hujawatemdea ukweli wapigania uhuru wa tanganyika mzee yaani daaah Da vinc nimeshusha baadhi ya nyota zako una hoja dhaifu mno mno mzee mohamed alicho andika ndo ukweli halisi kabisa.Namimi naomba nikuulize unadhani kwanini afahamike JKN kama aliyetuletea uhuru ilihali kulikua na watu walioanza kabla..?
Hivi mbonai George Washington ambaye ndiye baba wa Taifa USA alikuwa anavuma sana,? mbona yeye alikuwa anavuma na General Nathanael Greene hajulikani kabisa?Mm sijataka kuanzisha malumbano.. swali la msingi ni ilitokea nini hao wengine wakashindwa kua recognised kama waliotuletea uhuru.. bali ni wapigania uhuru..
Inaelekea hata hujui usemalo. Na hao waarabu ambao unasema walikuwa wanawauza ndugu zako kama watumwa. Je, hao watumwa walikuwa wanawapata wapi?Kabla ya hilo kundi kudai uhuru watu walikuwa wanafurahia kunyonywa..., Tangia muarabu aanze kuja kuuza ndugu zetu kama watumwa watu walikuwa wananungunika na kugombana kutoka katika hali ya Unyonyaji.., Mjerumani alivyokuja wapo kina Mkwakwa n.k.
Sasa kusema kwamba hilo kundi ndio lilikuwa na wazo la kudai uhuru na Nyerere alikuwa tu pugu anashika chaki.., basi hilo kundi lisingemfuata Nyerere bali lingemfuata jamaa yoyote pale mtaani...,
Mkuu wewe ni mwepesi sana kujibishana na mzee mohamed, huyo ni level nyingine we endelea kutuletea habari za kutunga za kina tesla. Narudia tena mzee said humuwezi sio level yako.Mkuu. Waweza niambia ni mambo gani mnaona ninyi mnakandamizwa..na sababu unaweza ziorodhesha?
Daaah mi mwenyewe mshikaji nimeshangaa sana leo yaani jamaa kaja na hoja dhaifu mno, mno, mno kupitiliza. Nina mashaka mawili, either jamaa acc yake imedukuliwa ama jamaa pasword zake kampa demu wake nando anayeandika hii nyuzi huu sio uqezo wa Da Vinc ata kidogo.Mkuu wewe ni mwepesi sana kujibishana na mzee Mohamed, huyo ni level nyingine we endelea kutuletea habari za kutunga za kina tesla. Narudia tena mzee said humuwezi sio level yako.
Swallow Abdul Sykes alipokuwa antique Mchango Wa kupigania uhuru Alicia kama musical aunt mdanganyika!vipi hao madaktar 5 wore no waislam!kwa tusingumzie utanganyika Wa nyerere bali tuungalie Mchango wake kwa mtazamo Wa ukatoriki?Da ' Vinci,
Ahsante sana kwa kuniandikia.
Hakika mimi nimeandika historia ya Waislam jinsi walivyokuwa mstari wa mbele katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika wala sikatai na wala sijuti kwa kufanya hivyo.
Wengi wameumizwa na historia hii kwa kuwa hawakuwa wanaijua, historia waliokuwa wanaijua ni ile historia rasmi ambayo ndiyo iliyokuwa imepasishwa na kusomeshwa kuanzia shule za msingi hadi Chuo Kikuu.
Hii ndiyo historia niliyoikuta mimi ikisomeshwa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam nilipokuwa mwanafunzi na nilikuwa nawashangaza hadi walimu wangu ninapowaambia kuwa historia hiyo ina upungufu mkubwa.
Laiti mimi nisingeliaandika kitabu cha ''Maisha na Nyakati za Abdul Sykes...'' historia hii ilikuwa imeshafutika na kupotea kabisa na hakuna jamii katika ulimwengu huu ambayo inaweza kukubali au kuvumilia kuona historia yake inafutwa.
Hakuna mahali popote ambapo mimi nimedogosha mchango wa Julius Nyerere katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika na laiti ningelikuwa mjinga nikafanya hivyo ningekiua kitabu changu kwani wasomaji wangenipuuza.
Nilichofanya mimi ni kueleza kuwa ikiwa ni historia ya TANU basi haiwezekani kuanza na Julius Nyerere 1954 itabidi turudi nyuma hadi 1924 na tusome mswada wa Kleist Sykes alioandika kabla ya kifo chake 1949 akieleza historia ya African Association yeye akiwa mmoja wa waasisi wa chama hicho (mswada huu mwaka wa 1973 ukawa moja ya sura ya kitabu kilichohaririwa na John Iliffe, ''Modern Tanzanians).
Katika mtiririko wa historia hii kuna wazalendo wengi kama Hassan Suleiman na Ali Juma Ponda, Hamza Kibwana Mwapachu na wale madaktari watano - Dr. Joseph Mutahangarwa, Dr. Vedasto Kyaruzi, Dr. Wilbard Mwanjisi, Dr. Michael Lugazia na Dr. Luciano Tsere.
Pamoja na hawa ndipo wanapoingia Abdul Sykes na mdogo wake Ally katika historia ya TAA, TANU na harakati za kudai uhuru na ndipo pia nilipotumia nyaraka waliazokuwanazo kuanzia miaka ya 1920 zinazoeleza na kuthibitisha historia yao katika kuunda TANU na mchango wao katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Kwa nini historia hii ilifutwa swali hili nitakuachia wewe ulijibu.
Naamini hujusikii vibaya kwa kuandikwa historia hii.
Ama kuhusu manung'uniko ya Waislam yapo na si mimi peke yangu ambae nimeandika kuhusu tatizo hili.
Somo hili limeandikwa na Bergen (1981), Sivalon (1992) na Njozi (2002) ingawa kitabu cha Njozi kimepigwa marufuku.
Kwa nini kitabu cha Njozi kimepigwa marufuku badala ya serikali kujibu yaliyosemwa hili swali pia nakuachia wewe ulijibu.
Tatizo la udini tunalo nchini na serikali inalijua na Waislam hawajajificha katika kulieleza tatizo hili na linafahamika.
Ikiwa wewe huamini kuwa lipo kwangu ni sawa pia.
Kughitilafiana kwa binadamu katika fikra hili haliepukiki.
Sina tatizo na kutambuliwa kwa Nyerere kama shujaa wa uhuru wa Tanganyika na narudia tena kusema kuwa laiti ningelikuwa mjinga na kudogosha mchango wa Mwalimu Nyerere katika historia ya TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika kitabu changu kingelikufa mapema sana.
Kitabu kimepokelewa vyema kote katika Vyuo Vikuu wanakosemesha African History na baadhi ya vyuo hivi wamenialika kuzungumza katika vyuo vyao kwa mnasaba wa kitabu hiki nilichoandika.
Kitabu kimepata ''review,'' tatu ndani ya Cambridge Journal of African History na kimechapwa kama ''series'' katika, The East African Magazine (Nairobi) na katika baadhi ya magazeti hapa nyumbani.
Kitabu hiki kinatambulika kama ''corrective history,'' yaani imesahihisha historia ambayo kwa bahati mbaya ilikuwa na makosa.
Wako waliopendezwa na kitabu changu na ndiyo maana sasa tunakwenda toleo la tatu Kiingereza na la nne Kiswahili.
Halikadhalika wako ambao hawakupendezwa na kitabu changu wangependa historia ibaki kama ilivyokuwa zamani kwa kufuta historia za wazalendo wengine katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika ibakie historia ya Mwalimu Nyerere peke yake.
Muhali wa hili ni kuwa wale waliokuwa na Mwalimu Nyerere katikaTANU mimi ni wazee wangu kutoihifadhi historia yao ni kujidhulumu mimi mwenyewe na kizazi changu.
Unaweza kuisoma historia ya babu yangu Salum Abdallah katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika hapo chini:
![]()
BABU YANGU SALUM ABDALLAH
Uncle Jei Jei: Tatizo Nyerere si muislam kwa dini wala mmanyema kwa kabila. Na kibaya zaidi, baba wa mwandishi huyu, a...mohamedsaidsalum.blogspot.com
![]()
SIKU BABU YANGU SALUM ABDALLAH ALIPOMKABILI FREDERICK MCHAURU KATIKA MGOMO WA WAFANYAKAZI WA TANGANYIKA RAILWAYS TABORA 1947
SIKU BABU YANGU SALUM ABDALLAH ALIPOMKABILI FREDRICK MCHAURU KATIKA MGOMO WA WAFANYAKAZI WA TANGANYIKA RAILWAYS TABORA 1947 Frederick ...mohamedsaidsalum.blogspot.com
Hata wewe ungelitoka katika mifupa ya wazee kama wangu usingestahamili kuona historia yao inafutwa.
Kabla ya hilo kundi kudai uhuru watu walikuwa wanafurahia kunyonywa..., Tangia muarabu aanze kuja kuuza ndugu zetu kama watumwa watu walikuwa wananungunika na kugombana kutoka katika hali ya Unyonyaji.., Mjerumani alivyokuja wapo kina Mkwakwa n.k.
Sasa kusema kwamba hilo kundi ndio lilikuwa na wazo la kudai uhuru na Nyerere alikuwa tu pugu anashika chaki.., basi hilo kundi lisingemfuata Nyerere bali lingemfuata jamaa yoyote pale mtaani...,
Inaelekea hata hujui usemalo. Na hao waarabu ambao unasema walikuwa wanawauza ndugu zako kama watumwa. Jee hao watumwa walikuwa wanawapata wapi??? Ni machifu wetu wenyewe ndiyo walikuwa wanakamata hao watumwa aidha mateka wa vita au vinginevyo ndiyo walikuwa wanabadilishana na bidhaa ambazo waarabu walikuwa wanaziuza na waarabu hao nao kuwauza kwa wanunuzi ambao nao walikuwa maajenti wa wazungu.
Nani alikuwa mfanyabiashara wa watumwa maarufu katika Arab Slave Trade AKA East African Slave Trade.Utumwa ilikuwa ni biashara ya kimataifa, biashara hii haikufanywa Tanganyika pekee, wala watumwa hawakuwa wafrika pekee, nchi nyingi Duniani zimezalisha watumwa ikiwemo nchi za Ulaya.
Vinginevyo waarabu walinunua watumwa Afrka na kwenda kuwauza barani Ulaya na Amerika ambako ndipo kulikokuwa na soko kubwa