Mzee Mohamed Said acha kupindisha historia, ni Nyerere aliyetuletea uhuru, sio wengine

Mzee Mohamed Said acha kupindisha historia, ni Nyerere aliyetuletea uhuru, sio wengine

Lililokuuma "dini yao" au wazee waliosahauliwa kwenye historia ya kivukoni na kuja kukumbukwa na Allama@Mohamed Said?
Dini yao kuacha elimu sana nyuma inafanya wanakosa nyazfa nyingi serikalini hasa kipindi hiko cha nyuma. Mwisho wanakuja kulalamika
 
Dini yao kuacha elimu sana nyuma inafanya wanakosa nyazfa nyingi serikalini hasa kipindi hiko cha nyuma. Mwisho wanakuja kulalamika
Kumbe tatizo lako ni "dini yao" na siyo wao! Ni heri umejisemea ukweli wako.

Sasa kuna ubaya upi Allama Mohamed Said akiwakumbuka kwa michango yao katika harakati za kutafuta Uhuru?
 
Labda huelewi kiwa elimu yote na ustaarabu ulio nao umetokana na dini yao.

Unafahamu kuwa hata hizo "alphabets" unazotumia leo hii kuandikia nazo pia ni "Alif Bee Tee"?
It doesn't matter bibie. Hata sie tuna madini kubao ila hatunufaiki nayo kwa ujimga wetu
 
It doesn't matter bibie. Hata sie tuna madini kubao ila hatunufaiki nayo kwa ujimga wetu
Kumbe tatizo lako ni "dini yao" na siyo wao! Ni heri umejisemea ukweli wako.

Sasa kuna ubaya upi Allama Mohamed Said akiwakumbuka kwa michango yao katika harakati za kutafuta Uhuru?
 
Kumbe tatizo lako ni "dini yao" na siyo wao! Ni heri umejisemea ukweli wako.

Sasa kuna ubaya upi Allama Mohamed Said akiwakumbuka kwa michango yao katika harakati za kutafuta Uhuru?
Mimi sina shida na dini yao. Ila ni vile ambavyo dini yao inawafanya wasifuatilie elimu ya upande wa pili kiuhakika afu wanabaki kuona wanaonewa
 
Mimi sina shida na dini yao. Ila ni vile ambavyo dini yao inawafanya wasifuatilie elimu ya upande wa pili kiuhakika afu wanabaki kuona wanaonewa
Ooh na wewe ndiyo umekuja kuwatatulia tatizo la "dini yao"?

Bado hujajibu swali, kuna ubaya upi Allama Mohamed Said akiwakumbuka kwa michango yao katika harakati za kutafuta Uhuru?
 
Mohamed Said,
Sidhani kama nimesema Mwalimu alikuwa na chama, bali nimesema Mwalimu alikuwa na mpango wa kuanzisha chama cha kupigania uhuru awali kabisa akiwa chuoni, nina uhakika na hili kwa 100% nikifanikiwa kupata vielelezo vyangu nitakuja navyo maana nimeshindwa kuvipata kwa siku za hivi karibuni.

Kuhusu kuandika Historia, mimi sio Mwanahistoria, bali ni mfuatiliaji tu wa historia, na napenda kusoma/kusikiliza vyanzo mbalimbali na hii husaidia kukwepa historia zenye muelekeo mmoja kama ninazoziona kwako.

Ninaposema "Wenzako" nimepandisha kipande cha video hapo chini. Na hakuna njia nitawatenganisha Watu hawa na hizi makala zako, maana muelekeo ni huo huo, plus kuna clip aliipandisha mshirika wako wa karibu Faiza, ya bw anayesema kwamba Wajerumani walitaka kuhamisha makaburi ya Waislam wakawa wanatokewa na watu wasioonekana na kuchapwa viboko...hekaya kama hizi siwezi kuzitenganisha na makala zako.

Kuhusu historia ya TANU, upo sahihi kabisa, mimi sio mbobezi wa historia, ni mfuatiliaji tu...na hii isiwe fimbo kwako kutushindilia taarifa zenye mlengo wa upande mmoja..yapo niliyoyasikia kuhusu TANU ila kwako unayahepa.

Hayo mengine niliyoeleza kwenye andiko langu umsikilize Mzee Bilal hapa chini.

 
May Day,
Nitakuomba tu heshima kwa huyu mzee.

Huyu Bilal Rehani Waikela ni baba yangu kwa hiyo unapomzungumza na huu ni mjadala tu nakusihi chunga ulimi wako umtaje kwa heshima.
 
May Day,
Nitakuomba tu heshima kwa huyu mzee.

Huyu Bilal Rehani Waikela ni baba yangu kwa hiyo unapomzungumza na huu ni mjadala tu nakusihi chunga ulimi wako umtaje kwa heshima.
Hakuna mahali nimemkosea heshima huyu Mzee, au ni hilo neno "Mwenzako" linaleta ukakasi niliondoe?

Ila pointi ya msingi umemsikia alichosema kuhusu UNO?.
 
Unasema maandiko ya Mzee Allama Mohamed Said lakini huweki nukuu hata moja ya hayo maandiko.

Naona umeleta yako unaswma ya @Allama Mohamed Said.

Tuwekee nukuu zake kama ushahidi zilizokufanya uandike hayo. Simpo.
Nimetoa kwenye maandiko tofautitofauti ya Mzee Said, na nilichofanya hapo ni mjumuisho tu kwa hiyo siwezi kuweka kama nukuu rasmi.
 
Nimetoa kwenye maandiko tofautitofauti ya Mzee Said, na nilichofanya hapo ni mjumuisho tu kwa hiyo siwezi kuweka kama nukuu rasmi.
Kwa hiyo hayo uliyoyaandika ni yako na hauna nukuuu hata moja ya kumshutumu Allama Mohamed Said. Au sivyo ulivyomaanisha?
 
Hakuna mahali nimemkosea heshima huyu Mzee, au ni hilo neno "Mwenzako" linaleta ukakasi niliondoe?

Ila pointi ya msingi umemsikia alichosema kuhusu UNO?.
May Day,
Hebu fikiri mimi nikuambie jambo inalomuhusu baba yako na nikamtaja baba yako kama mwenzako.
Wewe unaonaje?
 
Wewe una baba wangapi?
Lubuzo,
Nina baba zaidi ya mmoja.

Kwa malezi yetu ya Kiswahili mwanamke yeyote umri wa mama yako au kupita au anakaribia umri wa mama yako ni mama yako.

Ni hivyo hivyo kwa wanaume.

Lakini Mzee Waikela kwangu mimi ni zaidi ya hivyo anawajua wazee wangu wote.

Nimeandika makala siku chache zilizopita na nimemueleza kama hivi:

''Katika kujua kwangu naamini kuna watu wawili tu ambao kwa sasa ndiyo waliobakia katika waasisi wa TANU ambao waliona yote katika historia ya TANU kuanzia mwanzo wake 1954 hadi uhuru unapatikana mwaka wa 1961 na wakamjua Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa karibu sana katika miaka ile ya kupigania uhuru.

Watu hawa ni Bilali Rehani Waikela na Abbas Kleist Sykes na wote hawa waliwajua vizuri sana wazee wangu.

Abbas Sykes na kaka zake Abdulwahid na Ally na baba yangu Said Salum walikulia mtaa mmoja Kipata Street nyumba zao zikiangaliana.''

1568116390366.png

Kushoto ni Mzee Bilal Rehani Waikela na anaefuatia ni Mwandishi Mahakama ya Morogoro tukisikiliza kesi ya Sheikh Issa Ponda

 
Back
Top Bottom