Mzee Mohamed Said acha kupindisha historia, ni Nyerere aliyetuletea uhuru, sio wengine

Mzee Mohamed Said acha kupindisha historia, ni Nyerere aliyetuletea uhuru, sio wengine

Katika mada zako nyingi za historia ya taifa hili hua nikiangaliama Context naona mada zako zote zinalia kwa uchungu huku zikitoa ujumbe kua Waislamu tunaonewa, nikimaanisha kwamba mada zako karibu zote hua zina chembe chembe za Udini.
Nimesoma mara tatu huu uzi wako nikawa najishauri nikujibu au nisikujibu au nijibu kwa namna gani,lakini nafsi ikasita,nikajisemea nina kitu cha kusema hapa kisha nitatoa msimamo wangu mwishoni.

Kwamba je haya anayoyasema ni ya uongo au sababu yeye ameeleza yale ambayo hatukuyasikia au hatukupenda kuyasikia ? Nafsi ina maajabu yake sana.

Hivi mathalani mimi nikitetea haki yangu na kueleza sababu ya kukosa haki yangu ni dini yangu,nitakuwa mdini ?

Je haya anayoyasimulia mzee wetu ushawahi kujiuliza kwanini hayakusomeshwa vitabuni mwetu ? Je walifanya makusudi au kwa bahati mbaya ? Kama walifanya kwa bahati mbaya kwanini waliandika Historia bila kuchunga misingi ya kuandika Historia ?

Kila elimu ina takiwa ifate misingi 10,narudia tena kila elimu inatakiwa ifate misingi 10,ukiikosa misingi hiyo kaa ukijua hutaipata elimu hiyo. Misingi hiyo sitaitaja kwa sasa,kama ikibidi huko mbeleni nitaitaja. Maneno haya aliyasema mwanachuoni mkubwa Ali Swabaani.
Baadhi ya member hasa mkuu @Pascal Mayalla USER=262438]GUSSIE[/USER] wamejaribu kuchambua mada zako na kuonyesha ni jinsi gani zilivyojaa mahaba ya dini,na upotoshaji wa historia pia hata wasomaji wako ambao mko imani moja wanadiriki kuupinga hata ukweli ili tu kumtetea mwarabu na dini yake. ...mfano kwenye mada aliyoanzisha mkuu pasco akionyesha jinsi warabu walivyowatesa wazawa wa zanzibar watu wengi (isalms) waliukataa ukweli huona na kukubali kumtetea mwarabuu kisa tu ndio alieleta dini hiyo.
Kila fani ya kielimu ina namna yake ya ukosoaji ila kwenye asili ndiko majambo hurudishwa.

Leo hii wewe ukitaka kuikosoa historia ambayo aliiandika mtu fulani basi na wewe rudi kule kule kwa wenye Historia yao kisha uikosoe ili ambayo iko dhidi.

Pia,kuna maneno ya uongo unayasema na haya bila shaka umeandika kwa chuki pia hali ya kuwa unataka kujaribu kuamisha ya kuwa huna chuki,ya kwamba muarabu ana dini,Muarabu hana dini,sababu kwa waarabu kuna wapagani,washirikina na wasio kuwa hao. Hili umelisema lakini ukiombwa ushahidi naamini hata ukipewa miaka mia hutaweza kuthibitisha ya kuwa Uislamu wa waarabu. Kwahiyo unatakiwa ukiandika uandike kwa haki.

Mathalani mnaposema Historia aliyoiandika mzee wetu ina Udini,basi mlitakiwa kuonyesha au kuandika Historia ya kweli ambayo inaonyesha haina Udini huku mkirejea kwa wenye Historia.
mzee wangu wewe ni mwandishi na unazifahamu vyema Ethics za mwandishi, moja ya sifa kuu za Mwandishi ni kutokuandika habari fulani kwa kuweka mbele emotions na mahaba yake juu ya kitu anachotaka kutoa taarifa, mwandishi unatakiwa uandike/utoe habari ya kitu hicho ukiwa kwenye Free state, yaani uandike kitu kama kilivyo bila kuweka mahaba yako juu kitu hiko. Kwa hilo mzee wangu naona umefeli kulitekeleza labda lengo lako kuu hua ni kuonyesha jinsi gani ndugu zetu mnavyo kandamizwa.
Hili na wewe linakuhusu bali hata mimi,na wale pia. Huu uzi wewe ndio umeziruhusu hisia zikuongoze ndio maana umeandika ya uongo mengi na moja wapo ni hilo la kusema Uislamu ni wa waarabu.

Hivi mfano wewe ukitaka ukiandika Ukweli labda kuhusu watu wako lakini katika ukweli huo kuna madhila na dhiki kubwa sana zilizo wakuta watu wako,ukweli huu ukitaka kuuwasilisha unauwasilishaje ? Je kwenye huzuni utaweka bashasha ?
Nikupe mfano kidogo, humu JF kuna mwandishi wa makala mbalimbali anaitwa The Bold (@habibu B Anga) ni mwislamu pure! Lakini kamwe akiandika kitu ambacho hua kinagusa imani yake hua anaandika kama kilivyo bila kuweka upendeleo. Ref uzi wa:Adhabu ya kuchinjwa mbele ya kadamanasi Saudia.

Kwangu mimi mtu kama huyu hakupaswa kuruhusiwa kuandika makala kama zile au kwanza apewe masharti kabla ya kutuma makala zake wahakikishe ameweka na marejeo,kwani Elimu ni amana na amana huwa inarudishwa kwa watu wake,kama kweli watu wanapenda kusoma na kujifunza mambo. Tatizo kubwa la muandishi huyu ni kuwa maandiko yake hayarudishi kwenye asili yaani hana marejeo,pili mambo ya uhalisia anayasimulia kama kama habari za kubuni,mwisho wake anakuwa anapunguza au kuzidisha. Uzi huu naukumbuka na kuna nukta kadhaa nilimkosoa na kuna swali nilimuuliza lakini hakujibu,sijui kama labda huo ndio utaratibu wake au la ! Mimi namdhania kheri.

Kwanza alichokosea yeye ni jambo la kidini kulizungumza kihuni kwa kutaka kutenganisha dini na jambo lile,inaonekana huko anakochukua ambako huwa hatuonyeshi ni kuwa wtu hao hawaijui dini.

Nakumbuka nilimkosoa katika kichwa habari,katika Kiswahili hakuna sentensi "....mbele ya kadamnasi..." kuandika hivi ni kufanya makosa. Tamko "kadamnasi" limejitosheleza kwa lenyewe kwani ni muunganiko wa atamshi mawili nayo ni "kadamu" kwa maana ya mbele ya kitangulia na tamko la pili ni "nasi" kwa maana ya watu,makosa hayo ni sawa na kuandika "......mbele mbele ya watu ....." hakuna Kiswahili cha namna hii.

Angalizo anatakiwa akiwa anazungumzia mambo ya dini basi ahakikishe ana ujuzi na maarifa mapana juu mambo hayo.
Lakini mzee hata mimi mwenyewe ni mkatoliki lakini kama nikichangia mada au kundika mada juu ya mauaji yaliyofanywa na kanisa hili siwezi kubisha au kuandika tofauti na ilivyokua kisa ni kanisa langu, siwezikubisha wala kuandika kwa upendeleo kua kanisa katoliki kipindi cha Holocust liliagiza (Papa) wananchi wote wa nchi ya Uholanzi
(Netherlands) wauawe.
Kuna mambo mengine kutokana na umaarufu wake hata kama una hila ya kwapa,huwezi kuuficha ukweli zaidi ya kujibaraguza kwenda na hatua na mirindimo husika. Hapa kuna tegemeana.

Hilo jambo mpaka umelijua wewe ujue watu wengi wamelijua,lakini kuhusu Historia hiyo ya uhuru wengi hawakuwa wakiujia Ukweli,sasa hapa ndipo utakapo jiuliza kama nilivyo gusia huko,je walifanya makusudi kuificha au walikuwa naaarifa machache juu ya uandish wa Historia na kama walikuwa na maarifa machache juu ya kuandika Historia kwanini waliiandika na kuitawanya ?
NB: Yote hayo najaaribu kukuonyesha ni jinsi gani kuna udini kwenye mada zako, lakini lengo langu sijaandika uzi huu ili tujadili udini wala dini yako ila lengo langu hasa kuandika huu uzi ni

Hu ni mtazamo wangu tu,kwangu mimi sijaona udini katika maandiko yangu,na mwisho nitatoa msimamo wangu juu ya maandiko ya mzee wetu.
Mkuu kama nilivyokwisha kukuonyesha jinsi mada zako zilivyo na udini, sasangoja niende kwenye lengo la uzi huu..Mada zako nyingi nilizowahi kusoma kuhusu historia ya uhuru wa Tanganyika, ukiangalia nyuma ya pazia ujumbe ulio jificha unaonyesha kua Mwl. Nyerere hakutakiwa kuwa recognise kama mtu aliye tuletea Uhuru nchini toka kwa wakoloni, Bali kuna wazee wa kiisalmu wa hapo Dar kama Sykes familly n.k ndio wamehangaika zaidi kuleta uhuru.

Mimi nilicho kiona ni kuwa mzee wetu ametuoyesha ya kuwa kumbe kuna watu wengine hawatajwi japokuwa walicheza nafasi kubwa sana katika jambo hilo la uhuru.

Hivi kwani wewe hapo kabla hao wazee alio wazungumzia mzee wetu ulikuwa unawajua ? Kama ulikuwa huwajui kwanini ulikuwa huwajui ? Je tatizo ni lako au tatizo ni la wale walio andika Historia ?

Au jalia tukwamba hao wazee hawakutoa mchango mkubwa kihivyo je ni kwa lipi hawakutajwa ?

Je hawakustahili kutajwa na kwanini ?
Mkuu ni kweli wamechangia kiasi kikubwa kupatika uhuru hapa lakini, ukweliutabaki pale palekua ni J.K.Nyerere the Almighty ndio kaleta uhuru Tanganyika na sio hao wengine bila kuzingatia kigezo cha udini. kwanini nasema hivi?

Kawaida katika wengi lazima wawepo wawakilishi kwanini umtaje yeye Nyerere pekee kwani kule alipewa uhuru baada ya kupigana au aliupora au alipewa tu baada ya muda kufika ? Hii hata lugha inakataa kukata na kumuweka yeye pekee.
Kila mtu akizaliwa hapa duniani huja na kusudi (Purpose) aliloletwa kulitimiza, kwa mantiki hiyo Mwalimu aliletwa kwa kusudi la kuikomboa Tanganyika kutoka kwenye mikono ya
Hili sio lengo bali ni matokeo,kwani lengo la sisi kuumbwa ni kumuabudu Mola pekee,haya mengine yanayotokea ni sehemu ya maisha wala hutokuja kuulizwa kwanini hukupigania uhuru wala kwanini wewe ulipigania uhuru.

Huu ni uongo,mkubwa sana,je kusudi huwa unalijua kabla au baada ?
Mwalimu nyerere kazaliwa 1922 lakini mwaka 1945 akiwa ana miaka 23 tu aliweza kuhudhuria mkutano wa 5 wa Pan African Congress jijini Manchester hivyo basi waweza kuona ni jinsi gani alivyikua ashajua kusudinla yeye kuja dunianina kuanza kulifanyia kazi. mkuu hatima ya uhuruwa Tanzania ilikua mikononi mwa mwalimu, na kama inavyojulikana "You can escape your Destiny, Nobody can take away your Destiny"
Hii sio hoja bali ni malalamiko,huu ni uwakilishi ambao ulikuwa na sababu.
Mfano kidogo ili kuenea kwa imani ya kiislamu duniani allah ilibidi amletee Mtume maswahaba ambao walimsaidia pakubwa kusambaza uislam kwenye maeneo ya makafiri, vilievile ili YESU kueneza wokovu duniani ilibidi awe na wanafunzi na mitume wa kusambaza Habari za wokuvu ulimwengu mzima, kupitia wanafunzi wake Yesu aliweza kutimiza kusudi lake la kueneza wokuvu, Mwisho wa siku tunasema Yesu katuleta wokuvu mpaka kwetu huku ndani ndani ( ila hatusemi mitume wanatakiwa ndio wtambulike kama walioleta wokovu duniani bali Yesu) Mkuu hata wewe hadi kufika hapo ulipo kuna watu walisimama nawe hadi kua wewe uliyoko sasa hivi, ila hatusemi kwamba wale wiloku-push kipindi cha nyuma ndio wanaotakiwa kufahamika kama wanaoandika makala humu jF bali mzee Mohamed Said.

Hapa uko sahihi kabisa lakini wale wote walio kuwa bega kwa bega na mitume tunawajua na michango yao inajulikana tangu mwanzo mpaka kiyama kinasimama na tunawaombea dua kila kukicha,je hao waliomsaidia Nyerere mbona hawatajwi,mpaka mzee wetu alipokuja kuelezea upande wa pili au wewe uliwasoma hao hapo kabla ?

Kutetea hila na uongi wa watu wa ovu kuna ujasiri na kujitoa akili.
Kwa mantiki hiyo namaanisha kwamba ili kutimiza kusudi fulani ulilopewa na Mungu basi Mungu hukuandalia watu ambao watafanya kazi bega kwa bega ili kutimiza kusudi lako (mfano mzuri ni wazazi/walezi). hivi mkuu unatambua kua kuna watu hua wamezaliwa kusudi lao la kuzaliwa likiwa ni kuja kumsaidia mtu fulani aje kutimiza kusudi lake alopewa na Mungu,mfano mzuri ni Yohana mbatizaji. kusudi lake hata kwenye vitabu vinasema alikuja kuandaa njia/kusudi la Masihi Kristo....Hivyo hivyo kwa Mwalimu wetu Kuna watu wengi sana waliletwa hapa Tanganyika kuja kutimiza kusudi hilo. Ili kutimiza kusudi lake la kuiletea nchi yetu uhuru ilibidi watu wengi washirikiane nae. hatimaye aliweza kufanikiwa kuleta uhuru, hivyo basi hakuna suala la udini wala nini The Godman Nyerere atabakia kutambuliwa kama shujaa aliyeleta uhuru Tanganyika haijalishi ni wangapi walishirikiana nae.

Sasa haya ndio mahaba niue na aya yako ya mwisho imesisitiza hilo.

Sisi huwa tunasema hivi "Kitengeneze kiti chako kwanza kabla ya kukitia nakshi"
Niombe radhi kwa yoyote ambae andiko langu limemuudhi kwa namna moja au nyingine.

Ciao
- Da'Vinci

Mimi binafsi nimekupa udhuru sababu umetumia hisia sana kuliko ukweli na maarifa. Hisia zako nimekuachia mwenyewe.

MSIMAMO WANGU.

Waislamu tukiona tunakuwa wadhaifu sana na kuhisi tunaonewa basi tukae tukijua kwamba sisi ndio sababu basi lazima turudi nyuma na kujitathmini upya.

Kama kuna lolote ambalo nimekosea basi ni kwa udhaifu wangu.
 
Zurri,
Ahsante sana.

Nimesoma ndugu yangu anasema kuwa Julius Nyerere alihudhuria mkutano wa Manchester 1945 akiwa na umri wa miaka 23.

Hapana hakuhudhuria.

Kuna kitabu cha Thomas Morlon, "Nyerere The Early Years," asome kitamsaidia.

Mimi nikiandika Abdul Sykes alifanya mkutano na Jomo Kenyatta Nairobi 1950 akiwa na umri wa miaka 26 na nawawekea ushahidi wa confidential report za Special Branch kutoka Rhodes House Oxford wananitukana.
 
Waislamu wanaonewa wapi..? Mbona mwapenda kunungunika
 
Kaka chukulia jambo moja,je kama kweli waislamu wanaonewa yeye hatakiwi kusema ? Kwa maana ukweli uafiche ?

Je kama yeye ameamua kuuwasemea Waislamu kuna ubaya ?

Hasa mimi sijakuelewa hapo.
Wapi mwaonewa? Na nani? Kwanini muonewe ninyi tu?
 
Mkuu. Waweza niambia ni mambo gani mnaona ninyi mnakandamizwa..na sababu unaweza ziorodhesha?
Swali kama hili ukimuuliza mtu kama mzee Mohamed Said ni kutomtendea haki. Unaonaje kwanza ukaenda kusoma vile vitabu kikiwemo cha profess Hamza Njonzi ambacho kipo kwa kiswahili halafu ndio utakuwa na maswali haswa ya kumuuliza mzee wetu
 
Swali kama hili ukimuuliza mtu kama mzee Mohamed Said ni kutomtendea haki. Unaonaje kwanza ukaenda kusoma vile vitabu kikiwemo cha profess Hamza Njonzi ambacho kipo kwa kiswahili halafu ndio utakuwa na maswali haswa ya kumuuliza mzee wetu
Relief...
Wanaotuhumiwa wamekuwa kimya baada ya kuomba ushahidi ambao uliwekwa wazi ndani ya kitabu cha Prof. Njozi.

Akisoma kitabu hicho atajifunza mengi.

Na yeye kama ni mtu makini angejiuliza kwa nini serikali imezuia wananchi wake wasijue kilichoandikwa mle nini hofu yao?

Serikali inajua kuwa tunachosema Waislam ni kweli lakini haijapata ujasiri wa kukubali ukweli kwa kuhofia matokeo ya kukubali kuwa kumekuwa na njama ya kubagua jamii moja katika misingi ya dini.
 
Relief...
Wanaotuhumiwa wamekuwa kimya baada ya kuomba ushahidi ambao uliwekwa wazi ndani ya kitabu cha Prof. Njozi.

Akisoma kitabu hicho atajifunza mengi.

Na yeye kama ni mtu makini angejiuliza kwa nini serikali imezuia wananchi wake wasijue kilichoandikwa mle nini hofu yao?

Serikali inajua kuwa tunachosema Waislam ni kweli lakini haijapata ujasiri wa kukubali ukweli kwa kuhofia matokeo ya kukubali kuwa kumekuwa na njama ya kubagua jamii moja katika msingi ya dini.
na hiyo ni illa katika ilmu.

ni khiyaana katika elimu.

leo historia ya uislamu inatuambia kwaba kulitokea fitna kubwa baina ya waislmu wakauwana wenyeqe kwa wenyewe.

lakini licha ya tukio hilo baya uislamu haukuona busara kuificha historia hiyo kwa sabbu kupindisha historia ni katika mambo yanayovunja uaminifu
 
Mohamed Said,

Umeandika vizuri kabisa na nimekuelewa. Hongera sana Mohamed Said kwa kuthubutu kufanya kile unachoamini na kukisimamia. watu wa aina hiyo ni adimu sana hapa Tanzania. wengi tunapenda kuimba nyimbo za Chama na Serikali bila hata kuelewa maana yake.
 
Umeandika vizuri kabisa na nimekuelewa. Hongera sana Mohamed Said kwa kuthubutu kufanya kile unachoamini na kukisimamia. watu wa aina hiyo ni adimu sana hapa Tanzania. wengi tunapenda kuimba nyimbo za Chama na Serikali bila hata kuelewa maana yake.
Mindi,
Tunawajibu sisi kama raia kuileza serikali yetu na viongozi wake kuwa ndani ya serikali kumejengeka mfumo ambao unabagua wananchi katika misingi ya dini zao ili ifahamu na kuchukua hatua kurekebisha.
 
Hammaz,
Tatizo ninaloliona kukukabili wewe ni kule kutoijua historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika kwa ukamilifu wake.

Miaka michache iliyopita hapa JF niliweka bandiko lililoeleza kuwa hotuba ya Mwalimu Nyerere UNO mwaka wa 1955 ilikuwa katika mafaili ya TAA toka 1950 na waandishi wa hotuba ile wanatoka katika TAA Political Subcommitee ambao wajumbe wake ni: Sheikh Hassan bin Ameir, Abdul Sykes, Dr. Vedasto Kyaruzi, Hamza Mwapachu, Said Chaurembo, John Rupia na Steven Mhando.

Wako wasomaji walighadhibika sana na kuniita mimi muongo.
Tofauti yangu na wao ni kuwa mimi nimezisoma Nyaraka za Sykes zote na nimena mengi.

Sasa nataka nikusaidie wewe nikutoa huko kwenye ujinga wa kutojua historia ya kweli ya Tanganyika.

Ingia hapo chini:

Shukrani Mzee Mohammed Said.
 
Hammaz,
Tatizo ninaloliona kukukabili wewe ni kule kutoijua historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika kwa ukamilifu wake.

Miaka michache iliyopita hapa JF niliweka bandiko lililoeleza kuwa hotuba ya Mwalimu Nyerere UNO mwaka wa 1955 ilikuwa katika mafaili ya TAA toka 1950 na waandishi wa hotuba ile wanatoka katika TAA Political Subcommitee ambao wajumbe wake ni: Sheikh Hassan bin Ameir, Abdul Sykes, Dr. Vedasto Kyaruzi, Hamza Mwapachu, Said Chaurembo, John Rupia na Steven Mhando.

Wako wasomaji walighadhibika sana na kuniita mimi muongo.
Tofauti yangu na wao ni kuwa mimi nimezisoma Nyaraka za Sykes zote na nimena mengi.

Sasa nataka nikusaidie wewe nikutoa huko kwenye ujinga wa kutojua historia ya kweli ya Tanganyika.

Ingia hapo chini:

Mzee wangu,

Nimesoma maelezo yaliyomo kwenye link uliyonipatia lakini bado yameniacha na shauku kubwa! Vitabu ulivyoviambatisha kwenye simulizi iliyopo kwenye Blog yako nitavipatia wapi?

Ukinelekeza itatosha, nitafika Mungu akipenda.
 
Bopwe,
Hayo usemayo kuwa ungepatikana uhuru bila ya kuupigania si kweli ushahidi wa historia ya uhuru wa Tanganyika unapingana na hivyo usemavyo.

Inakubidi usome historia ya Tanganyika.

Ingia hapo chini usome vikwazo ambavyo Waingereza waliviweka kuzuia uhuru wa Tanganyika:


Mzee wangu, Vitabu vyako Mkuki na Nyota vinapatikana?
 
Mzee wangu,

Nimesoma maelezo yaliyomo kwenye link uliyonipatia lakini bado yameniacha na shauku kubwa! Vitabu ulivyoviambatisha kwenye simulizi iliyopo kwenye Blog yako nitavipatia wapi?

Ukinelekeza itatosha, nitafika Mungu akipenda.
Hammaz,
Kitabu kipo Msikiti wa Manyema na Mtoro Ibn Hazm Bookshop bei shs: 10,000.00.
 
na hiyo ni illa katika ilmu.

ni khiyaana katika elimu.

leo historia ya uislamu inatuambia kwaba kulitokea fitna kubwa baina ya waislmu wakauwana wenyeqe kwa wenyewe.

lakini licha ya tukio hilo baya uislamu haukuona busara kuificha historia hiyo kwa sabbu kupindisha historia ni katika mambo yanayovunja uaminifu
Safuher,
Mimi nimejiuliza sana kwa nini zilifanyika juhudi za kufuta historia ya kweli na kuweka historia ambayo haikuwa sawasawa.

Mtu wa kwanza kukutana na hali hii ya kutaka kubadili historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika ilimkuta Abdul Sykes mwenyewe miaka ya mwanzo ya uhuru pale TANU yenyewe ilipotaka kuandika historia yake na Abdul na Dr. Wilbard Kleruu wakakabidhiwa kazi hii.

Yale aliyokutananayo Abdul aliamua kujitoa lakini Dr. Klerruu alikamilisha kazi ingawa kazi hiyo haikuchapwa kitabu ikabaki mswada katika maktaba ya TANU Mtaa wa Lumumba hadi ilipochukuliwa na kuchapishwa kitabu na Abubakr Olotu baada ya mswada kufanyiwa mabadiliko ya hapa na pale.

Kitabu hiki kinaitwa. ''Historia ya TANU,'' (1971) na hakina tofauti na kitabu cha Chuo Cha CCM Kivukoni, ''Historia ya YANU 1954 -1977.(1981).
 
Back
Top Bottom