Mzee Mohamed Said acha kupindisha historia, ni Nyerere aliyetuletea uhuru, sio wengine

Mzee Mohamed Said acha kupindisha historia, ni Nyerere aliyetuletea uhuru, sio wengine

Sio ali mwinyi pekee sio abdul syke au mwapachu waliokua na mchango katika ukombozi wa tanzania tunakubai walikuepo na wengine wengii tuuh lakini historia haiez kuandika kila mtu au mchango wa kila mtu sababu watu wazalendo walikua ni wengii, mfano inasemekana kulikua na matawi zaidi ya 30 ya TAA sasa historia haiez kuchambua na kueleza kila member katika kila tawi kama unavyotaraji wewe... .. ila tunatizama key players katika kufanikisha ile adhima iliyokuwa ikikusudiwa ndio tunamsikia JKN aliekua kifua mbele....

Lakini kuwaacha watu waliokua na mchango mkubwa na muhimu ni wizi wa fadhila.
 
Nyerere ni kama ilivyotokea kwa Maradona..Napoli, walikuwa hawajapata lolote, mpaka Maradona alipojiunga na timu.. Nafasi ya kiongozi mwenye ushawishi, ufahamu na uthubutu mara zote zipo na hao mara nyingi historia huwa inawatambua kwa haraka, ingawa wengine wapo lakini hawavumi.

Acha ujinga, Usitake kujaribu kuaminisha kuwa Tanzania isingepata Uhuru kama Nyerere asingekuepo
 
Tanganyika as a Mandate Territory
Britain was administering Tanganyika under articles 76 and 77 of the Charter of the United Nations.

As the administering authority, Britain was expected to establish and promote political, economic and social advancement of Tanganyika until such time as its people were ready for self-rule.

In spite of this international commitment, the British were more interested in safeguarding their own colonial interests and those of other minorities but-not those of the indigenous African majority. [1]

In order to pre-empt African reaction to this injustice, in 1949 Governor Twining invited proposals from prominent individuals, welfare societies and from Native Authorities,
[2] as to how Tanganyika should be governed.

The TAA political committee submitted a memorandum to the Constitutional Development Committee which was signed by the entire executive: Sheikh Hassan bin Ameir, Abdulwahid Sykes, Vedasto Kyaruzi, Hamza Mwapachu, John Rupia, Stephen Mhando and Said Chaurembo.
[3]

In his annual report for 1950, Abdulwahid was to write:


''For the welfare of the Africans and to safeguard the interests of this Association and those of the African community as a whole, this Association has arranged for an advocate to stand by and to advise the Association on the technical side of the law. This advocate is Mr. E.E. Seaton of Moshi. He has from time to time written to the Association on various political subjects, and helped a great deal with his advices when this Association was compiling its memorandum on constitutional development.'' [1]

[1] Annual Report of the secretary of TAA, ibid.
 
Inaelekea wewe ni kizazi baada ya uhuru ila kwa wale ambao walikuwa na akili zao ingawa watoto walishuhudia mengi na anachoandika Mohamed Said kwa yeyote yule alizaliwa miaka ya 40 na 50 na kukulia dar anaelewa.

Mimi ninakumbuka zile enzi ambapo bibi Titi na wenzake walikuwa wanapita nyumba hadi nyumba kuhamasisha akina mama kuingia Tanu.

Na ninamkumbuka mwalimu kipindi kile ambacho alikuwa anakuja mtaa wa sukuma na mafia yalipokuwa makazi ya Yanga kwenye vikao pamoja na wazee wetu. Wacha kupotosha wenzako.
Daah, kumbe wewe ni babu kabisa aisee! Hongera kwa kula chumvi nyingi.
 
Lakini mzee wangu Mohamed Said huyo sheikh Ilunga tabia yake ilikuwa mbaya na alikuwa mfano mbaya kabisa tofauti kabisa na ninavyowafahamu waislamu ninaoishi nao mitaani kwetu na hata makazini . Kuna video zake kadhaa kwenye youtube ameonekana na kusikika akiwahimiza waislamu waue mapadri, kardinali na maaskofu, eti kulipiza kisasi cha sheikh aliyeuawa na polisi kule Kenya. Nilimshangaa sana na kumdharau kabisa. Eti polisi wakiua mtu Kenya basi inahalalisha watanzania kuua wenzao kwamba wanalipiza kisasi? Kisasi kipi? Kardinali au askofu au hata paroko wa Tanzania anahusikaje na polisi wa Kenya, kuna ushahidi gani kuwa ndiye aliyewatuma hao polisi wamuue huyo sheikh?
Najisikia vibaya sana kwa mtu ninayemheshimu kama Maalim Mohamed Said kumshabikia au kuunga mkono vitendo na kauli za Sheikh Ilunga zilizokuwa na nia ovu ya kusababisha shari.
mkuu ukiona mtu anakubali harakati za bwanailunga Allah amrehemu basi jua huyo mtu eidha ni mjinga na mwenye jazba na uislamu.

Ilunga hakuwa mtu ambaye anatakiwa asikilizwe na waislamu kwa sababu alikuwa anaeneza chuki zisizo na msingi na kuwatia waislamu katika matatizo.

mtu anakataa sensaa eti na kuwaambia waslamu wagome kwa sababu ipi ya msingi...?

waispamu wanajazwa ujinga kirahisi na watu kama akina ilunga wanaotumia Mlango wa historia kutujaza chuki na Ndugu zetu wasiokuwa waislamu.

mtu kauliwa kenya yeye anaona inafaa kuua padre tanzania.

ILUNGA ALIKUWA NI MTU MJINGA AMBAYE KATIKA BAADHI YA MAMBO YA DINI HAKUWA NA TAFAKKURI NZURI YA KUCHAMBUA MAMBO.
 
Niwie radhi kama sijakuelewa vizuri lakini katika post yako kumhusu naona umemjaza masifa kedekede! Nami tangu siku nilipoona video zake katika youtube za kuhimiza watu kuua wengine roho yangu ilikataa kabisa kupatana na chochote kinachomhusu!
Lakini nitafurahi na kufarijika sana ukitamka mwenyewe kuwa hukubaliani na mahubiri ya marehemu Sheikh Ilunga yanayowataka waislamu waue kardinali, maaskofu na maparoko kulipiza kisasi.
Ralph...
Nimemwandika Sheikh Ilunga kama nilivyomfahamu na katika blog yangu hiyo ndiyo makala iliyosomwa na watu wengi sana zaidi ya 10,000.

Ama kuhusu tamko lake baada ya kuuliwa Sheikh Rogo mjadala ule ulishafungwa na Sheikh Ilunga ni marehemu.
 
Kitu kimoja , Mzee Mohamed Said amesaidia kuonyesha historia ambayo ilikuwa haikupewa nafasi sana. Udhaifu wake ni kuonyesha ulifanywa , kama waislam. Nafasi ya Nyerere ilikuwa muhimu kutokana na elimu aliyopata kule Edinburg na pamoja ujuzi wa kujua na kufuatilia hali ya kisiasa Tanganyika.

Wakati Nyerere yupo Edinburg - Abdul Sykes, Steven Mhando, Dr. Kyaruzi, DR . Seree , Mwapachu walitengeneza " Memorandum for Political Independence " hili dodoso waliloliwakilisha kwenye ofisi ya Umoja Wa Mataifa, inayohusu Makoloni, iliwaletea shida watu mbalimbali akiwemo, Mwapachu hadi akahamishiwa Ukerewe.

Hivyo Mwapachu, akamwandikia barua Nyerere akiwa Edinburg kuhusiana na hali nyumbani. Utagundua , Nyerere akiwa Edinburg vuguvugu la mabadiliko lilikuwa linaendelea nchini na kukaibuka viongozi mbalimbali kusongesha mapambano.
Saadani Abdu Kandoro, Said Maswanya na Bhoke Munanka kutoka maeneo ya Majimbo ya Ziwa ( Lake Province)

Kwa hiyo ukiangalia historia ya uhuru na mapambano ya Tanganyika , ilipita kwa michango wa watu tofautitofauti wa kada mbalimbali.. Tukitafuta kwenye historia zaidi, tutakuta makundi ya michango ya wafanyakazi, wakulima, wavuvi , wafanyakazi toka vyama mbalimbali na maeneo tofauti tofauti. Na makundi zaidi bado yapo .

Hii inanipa hamasa kuendelea kutafuta historia ya Tanganyika , ili kuweka mjumuiko mzuri. Kazi hii si ya kitoto au ndogo.. Na wakati tunaendelea na hayo na bado yataendelea sana, isifanye ionekane kuwa ni watu fulani wa madhehebu fulani, kutoka eneo fulani ndio waliochangia uhuru wa Tanganyika.
Newazz,
Hapakuwa na kitu kinaitwa, ''Memorandu for Political Independence,'' ila kulikuwa na ''Memorandum to Constitutional Development Committee,'' na hii iliandikwa na TAA Political Subcommittee Commitee ambao wajumbe wake walikuwa hawa wafuatao: Mufti Sheikh Hassan bin Ameir, Abdulwahid Sykes, Hamza Kibwana Mwapachu, Sheikh Said Chaurembo, Dr. Vedasto Kyaruzi, John Rupia na Steven Mhando.

Hii memorandum haikupelekwa UNO bali iliwasilishwa kwa Gavana Edward Francis Twining kwani yeye ndiye aliyeomba maoni kutoka kwa wananchi wa Tanganyika katika jumuia zao na TAA wakachukua nafasi hii pamoja na taasisi nyingine zilizokuwapo.

Hii memorandum ilijadiliwa mwaka wa 1954 katika mkutano ulioasisi TANU na mapendekezo ya hii memorandum ndiyo yaliyowasilishwa UNO na Nyerere mwaka wa 1955.

Kamati hii ilidai kwanza pawepo na uchaguzi wa kura moja mtu mmoja na Tanganyika ipewe uhuru baada ya miaka 13.

Serikali ilishtushwa sana na mapendekezo haya na ikaamua kuwaadhibu wale waliokuwa wafanyakazi wa serikali.

Dr. Kyaruzi akahamishiwa Kingolwira Prison, Hamza Mwapachu akapelekwa Nansio Ukerewe na Abdul Sykes manusra apoteze kazi yake kama Market Master, Kariakoo Market.

Hapa ndipo wazalendo hawa na wao wakaamua sasa ili kupambana na Waingereza mipango ianze ya kuunda chama cha siasa.

Hii ndiyo kamati ndani ya TAA iliyokiongoza chama hiki kuelekea kuunda TANU 1954 na uhuru ukapatika 1961.

Hii document ina sahihi ya hawa wanakamati wote.

Bahati mbaya hii document imepotea na inaaminika imetolewa kwa kunyofolewa katika nyaraka za TANU na katika nyaraka za Tanganyika National Archives (TNA).

Lakini hii document ipo Rhodes House, Oxford, Uingereza.

Katika watafiti wa historia ya uhuru wa Tanganyika ni waandishi watatu tu Judith Listowel (The Making of Tanganyika, 1965), ndiyo walioigusia katika vitabu vyao, Cranford Pratt (The Critical Phase in Tanzania, 1976) na mwandishi (The Life and Times of Abdulwahid Sykes...1998).

Hii document ni muhimu sana katika historia ya TAA.

Namaliza kwa kusema kuwa mtu aliyetoa mchango mkubwa katika kuitayarisha hii document alikuwa Earle Seaton mwanasheria kutoka Bermuda aliyekuwa rafiki wa Abdul Sykes.

Hotuba ya Mwalimu Nyerere UNO mwaka wa 1955 inatoka katika document hii.
 
mkuu ukiona mtu anakubali harakati za bwanailunga Allah amrehemu basi jua huyo mtu eidha ni mjinga na mwenye jazba na uislamu.

Ilunga hakuwa mtu ambaye anatakiwa asikilizwe na waislamu kwa sababu alikuwa anaeneza chuki zisizo na msingi na kuwatia waislamu katika matatizo.

mtu anakataa sensaa eti na kuwaambia waslamu wagome kwa sababu ipi ya msingi...?

waispamu wanajazwa ujinga kirahisi na watu kama akina ilunga wanaotumia Mlango wa historia kutujaza chuki na Ndugu zetu wasiokuwa waislamu.

mtu kauliwa kenya yeye anaona inafaa kuua padre tanzania.

ILUNGA ALIKUWA NI MTU MJINGA AMBAYE KATIKA BAADHI YA MAMBO YA DINI HAKUWA NA TAFAKKURI NZURI YA KUCHAMBUA MAMBO.

Mbona unaonekanwa kama wewe ndio mjinga?
 
@Da'Vinci,

Tanganyika haikuwa koloni la nchi yoyote ile.
Ilikua chini ya Umoja wa Mataifa. - UN Mandate
Hata kama TANU isingeundwa Nchi ingepewa Uhuru wake
Tu na UN.

Nchi zilopigania Uhuru EA ni Kenya peke yake. Hivyo huyu kafanya nini yule kasaidia kile ni Propaganda tu.
Sana Nyerere alikua mstari wa mbeli kujitwalia madaraka hakuna chingine
 
Sawa umetoa mfano mzuri ila usisahau kila team ina key player na uwezo wa huyo key player ndo unasababisha wengine waonekane mchango wao mdogo na ni kitu ambacho ni ukweli, mfano lione messi akikosekana kwenye team ya barca ni ngumu ile timu kupata ushindi kadhalika ndo ilivokua kwa TAA tunazungumza nyerere kwa sababu ndo alikua kichwa na mwenye mawazo chanya yaliyoweza kumtikisa mzungu na kuamua kutupa uhuru wetu peaceful... JKN anazungumziwa pekee sababu ukisoma historia mtu aliekua akisafiri nchi zote zaa ughaibuni kudai uhuru ni yeye pekee hatujasikia hao ndugu zenu wakina sykes sijui abdul wala nani.....kwa hiyo u anatakiwa umuheshimu sana huyu mzre kwa kutufikisha kwenye azima ya uhuru,,, bila yeye nakuakikishia blaza ungekua oman unaosha vyombo saiv..
Barcelona ile ya kampa kampa tena!! Wakuzungumziwa ni messi pekee!!? Vipi iniesta, vipi xavi, busquet, carles puyol, eric abidal, dani alves hawa historia imewafunika, vipi Leicester city iliyobeba ubingwa, ni vardy pekee kisa alikuwa mgungaji bora, kina mahrez, drinkwater, kante, okazaki, kasper schemeichel, wes Morgan, robert huth hawa ndio historia yao izikwe!?
 
Kuna wapuuzi washaanza kurecord as if wamefanya Tafiti wao na hawajulikani kabisa...

I hope ni Watoto wa Mohamed Said
 
Tanganyika haikuwa koloni la nchi yoyote ile.
Ilikua chini ya Umoja wa Mataifa. - UN Mandate
Hata kama TANU isingeundwa Nchi ingepewa Uhuru wake
Tu na UN.
Nchi zilopigania Uhuru EA ni Kenya peke yake. Hivyo huyu kafanya nini yule kasaidia kile ni Propaganda tu.
Sana Nyerere alikua mstari wa mbeli kujitwalia madaraka hakuna chingine
Bopwe,
Hayo usemayo kuwa ungepatikana uhuru bila ya kuupigania si kweli ushahidi wa historia ya uhuru wa Tanganyika unapingana na hivyo usemavyo.

Inakubidi usome historia ya Tanganyika.

Ingia hapo chini usome vikwazo ambavyo Waingereza waliviweka kuzuia uhuru wa Tanganyika:


1567618417011.png
 
Kuna wapuuzi washaanza kurecord as if wamefanya Tafiti wao na hawajulikani kabisa...

I hope ni Watoto wa Mohamed Said
Dudu...
Iko toka juzi lakini kuna makosa.

Aziz Ali hakuwa mwanasiasa kabisa yeye alijikita zaidi katika biashara.

1567618942486.png

Aziz Ali

Aliyekuwa mwanasiasa ni mwanae Dossa.

 
Dudu...
Iko toka juzi lakini kuna makosa.
Aziz Ali hakuwa mwanasiasa kabisa yeye alijikita zaidi katika biashara.


Aliyekuwa mwanasiasa ni mwanae Dossa.

Ndio tatizo nalo lipinga kila siku upotoshaji unasambaa sana. . Kama dini
 
Ndio tatizo nalo lipinga kila siku upotoshaji unasambaa sana. . Kama dini
Dudu...
Akina Dossa wana bahati mbaya Mwalimu Nyerere tarehe 27 April, 1985, alitunuku jumla ya medali 3,979 kwa Watanzania waliotoa mchango mkubwa katika taifa.

Jina la Dossa halikuwapo.

Namtaja Dossa kwa kuwa wengi ambao ilitegemewa wangetunukiwa medali hawakupata lakini Dossa yeye ilikuwa kasauliwa kwani siku ya pili aliitwa Ikulu peke yake akapewa.

Si ajabu kuwa hata historia yao haifahamiki waandishi wanaieleza kama watakavyo.


1567626043060.png

Mwalimu Nyerere akimtunuku Dossa Aziz medali Ikulu
 
Ahsante kwa pongezi.. Kwakweli mzee wetu ajikague upya aangalie Wapi walipokosea wao wenyewe na falsafa za dini yao.
Kaka chukulia jambo moja,je kama kweli waislamu wanaonewa yeye hatakiwi kusema ? Kwa maana ukweli uafiche ?

Je kama yeye ameamua kuuwasemea Waislamu kuna ubaya ?

Hasa mimi sijakuelewa hapo.
 
Back
Top Bottom