Mzee mwanakijiji na Humphrey Polepole mbona mpo kimya kuhusu ufisadi wa Lugumi!!?

Inawezekana unatumia neno mantiki bila kujua. Sio kila jambo unahitaji kuwa na facts ndiyo useme hasa linapokuwa katika hatu za mwanzo. Ni busara kulisemea kimanti huwezi laumiwa au kosolewa labda kwa mtu siyemwelewa!
Ukosefu wa facts unamlazimisha mtu kutumia maneno kama huenda, nahisi, labda nk. Wengine hawataki maneno hayo. Mantiki bila facts? I beg to differ
 
Jpm huwa anapita pita hapa.. Na atawateua kwa hasira
 
Ukosefu wa facts unamlazimisha mtu kutumia maneno kama huenda, nahisi, labda nk. Wengine hawataki maneno hayo. Mantiki bila facts? I beg to differ
Facts bila utashi pia bado ni tatizo. Sio mbaya katika hatua za mwanzo kwa kuwa hatuna facts za kutosha, madhalani mwenye utashi anapoulizwa badala ya kunyamaza akasema kama kweli itagundulika Lugumi ililipwa pesa yote 99% wakati wameleta vifaa vituo 14 tu out of 108 hapo kuna mazingira ya ufisadi hivyo hatua kali zichukuliwe zidi ya wahusika. Hapo utakuwa umekosea nini? Au kujua kuwa jambo fulani ni baya unahitaji pia facts!
 
Tunaongea lugha moja. Hapo umetumia neno kama itagundulika. Wengine hukwepa maneno hayo kwenye hoja zao.
 
Ngoma wapige wao; na lele mama walie wao halafu sisi turukie tu na kuanza kucheza. Itakuwaje kama ni ya unyago? Hekima inatuita tutulie na kupata taarifa zote za kutosha juu ya hii ngoma. Hatuzungumzi ili tuonekane na sisi tunajua wimbo! Kwa wanaonifahamu wanajua kabisa sijawahi kurukia jambo kwa haraka na kama ni nimewahi kufanya hivyo sikuchelewa kujirudi.
 
Mzee hekima ipi hiyo ?? Mbona swala la Mwapachu Kurudi CCM ulileta uzi humu tena maneno yaliyotungwa kwenye mitandao ,ukaishia kumuhukumu Mzee Mwapachu ??

Toa msimamo wako kuhusu Lugumi acha kutapatapa
 
Hao ni speaker za mafisadi, hawajaambiwa cha kusema. Subiri wapewe cha kujibu uone watakavyolipuka
kama ni spiker bado waya hazijaungwa, tusubiri ziungwe na kuwashwa.....
 
Hivi ni ufisadi gani uliopigiwa kelele na serikali ikaukiri na ww ndo ukatoa maoni yako?? Hivi jambo la Lugumi unaweza kusema ni uzushi? Issue ya mwaka 2011 leo ni miaka 5 mzabuni hajafanya hata 20% na amelipwa kwa 99% mtu unayejiita una hekima unakosa kitu cha kusema?? Uwe mkweli mwanakijiji,yote unayofanya unawinda uteuzi km yule mwenzio ambae nae yupo kimya. Mnajifanya wazalendo kumbe mnapigia chapuo ulaji wenu..!!
 
Hivi maada zinaanzishwa ili mtu yeyote mwenye mawazo yake achangie au lazima watu fulani wachangie?
Uhuru wa mawazo ni pamoja na kutochangia kama mtu haoni sababu.
Sasa umezuka mtindo wa kupinga au kuunga mkono hoja almradi imetolewa na mtu fulani. Hoja iliyopo mezani haina maana tena. Huo ni uzuzu.
Hoja ipingwe au kuungwa mkono kwa merits zake na si kwa sababu fulani kasema!
 
Njaa mbaya sana wengi humu huja kutetea upuuzi kwa ajili ya UJIRA tena wa kutupwa hadi shs 10,000/=
 


Sikubaliani na wewe kabisa.
Haki inabaki kuwa haki tu. Na haki ina pande mbili ya kutiwa hatiani au kuachiwa huru.
Kesi yoyote inaanza kama tuhuma.

Kila ufisadi ulianza kama tuhuma na tetesi kwenye vyombo vya habari.

Wewe kama mtu uliyejipambanua kama mpigania haki hutakiwi kukaa kimya mpaka wengine wapige kelele. Ukweli utakapo bainika ndipo uje upige kalele za kupongeza.

Piga kelele za kutaka ukweli ujulikane na haki itendeke.
Hili ni suala nyeti kwa taifa
Haiwezekani liwe linachunguzwa na mamlaka ile ile inayojaribu kwa kila namna kulificha jambo hili.

Nilitegemea uwe umetoa kauli ya kumtaka Rais kuunda tume ya majaji wanaheshimika sana walichunguze jambo hili kwa kina na kuliweka wazi ili kuondoa upotoshaji unaozagaa.

Kwa nini nasema Mh. Rais aunde tume ya k
Majaji kwa sababu jambo hili limeenda mbali zaidi kwa kuwataja watu wengi akiwemo mwanafamilia wa rais mtaafu na Waziri mwenye dhamana ya wizara. Huyo waziri sio kutajwa tu bali ametajwa kama rafiki wa karibu sana wa Rais Magufuli. Hapo haki itaeleweka vipi kwa wananchi bila kuliundia tume maalumu. Tume hiyo ni lazima ifanye kazi yake bila kujali maslahi ya posho zilizoea kutengwa kwa mamilioni kwenye tume zilizokua zinaundwa .Itumie gharama ndogo kutupa ukweli.

Tayari tumeshaambiwa ama kwa kudanganywa au huenda kuna ukweli kuwa Kitwanga na Magufuli ni Rafiki wa ukweli. Sasa hatutaki amuonee au avunje urafiki wake kwa tetesi. Lakini pia hatutaki apuuzie tetesi kwa kulinda urafiki wao. Na hatutaki jambo hili kubwa lifanyike au lichunguzwe kwa siri.

Kila mtu abebe mzigo wake mwenyewe.

Urafiki, udini,ukanda ,ukabila,ushabiki ,undugu na uchama tuuweke pembeni kwanza.
Wote tumelikuta taifa hili na wote tutaliacha.
Hakuna chama wala dini wala kabila wala mtu mmoja aliyemwomba Mungu na kumshawishi ili aweke rasilimali zote zilizopo kwenye nchi hii. Zote ameziweka kwa mapenzi yake kwenyewe. Hivyo ni vema tukawakataa wote wanaotaka kuzifanya zimewekwa kwa hisani yao.
Cha msingi taifa letu tuliache katika maendeleo ya wote na historia bora yenye ukweli na uadilifu.
 
du nimepata kitu hapa kumbe ni marafiki hawakukutana barabarani mwee!!! ukisikia kesi ya nyani kula mahindi kapewa ngedere ndo hivi....inauma sanaa!!!
 
pole pole anasaga lami mara leo itv, mara chanel 10 mara star tv mara tbc kuongea ujinga akisubir nafasi ya uteuz wa rais
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…