ngoma ya ukae
JF-Expert Member
- Feb 8, 2017
- 611
- 618
Kumbe wazee humu tumebaki wachache sana...mkiambiwa sisi ni watu wazima huwa mnatukejeli, "mzee uwe wewe. ..wazee walishakufa " nyie mabinti kwa msemo wenu wa sasa... Mungu anawaona.Huyu ni nani ?Ndo namsikia Leo aisee.RIP mzee.
Vipindi vya ukulima wa kisasa na ufugaji nyuki.ALikuwa mkurugenzi wa RAdio Tanzania kabla hujazaliwa baadaye alikuwa Katibu wa Raisi Nyerere
Aiseee.. MUNGU akuhurumie mzee binti ameuliza swali matokeo yako unatoa povu badala ya kumpa jibu sahihiKumbe wazee humu tumebaki wachache sana...mkiambiwa sisi ni watu wazima huwa mnatukejeli, "mzee uwe wewe. ..wazee walishakufa " nyie mabinti kwa msemo wenu wa sasa... Mungu anawaona.
Sasa napata picha kwanini mafao yake yalileta mushkeli2005 alikuwa mwenyekiti wa kamati ya maadili ya CCM iliyopitia sifa za waliotaka kuogombea kwa kupitia CCM.
Kwa maoni ya kamati yake Kikwete alikuwa hafai kuwa rais.
Poleni wafiwa. Hawa wazee,tutawakumbuka kwa uzalendo wao. Sina uhakika kama ipo taasisi endelevu,inayoweka kumbukumbu sahihi za kiutendaji za hawa wazee wetu. Tuna mengi ya sisi wa sasa na wajao ya kujifunza kutoka kwao! Lengo,tuwe na muendelezo wa yale mema waliyotuachia!Yule Mzee Mkongwe na Gwiji la siasa l za Tanzania Mzee Sozigwa amefariki Dunia.Rest in peace Mzee wetu
Mbona mimi simjui??Yule Mzee Mkongwe na Gwiji la siasa l za Tanzania Mzee Sozigwa amefariki Dunia.
Sozigwa alikuwa mwandishi wa habari wa Hayati Baba wa Taifa.
Rest in peace Mzee wetu
Alipewa nenda kagawiwe na wew wabongo mnapenda kujua ya wenzenuAlipew mafao yake?
Tufafanulie alimpigiaje ,simu wakati miaka kulikuwa hakuna simu za mkononi?Yule Mzee Mkongwe na Gwiji la siasa l za Tanzania Mzee Sozigwa amefariki Dunia.
Sozigwa alikuwa mwandishi wa habari wa Hayati Baba wa Taifa.
Rest in peace Mzee wetu
=======
Byendangwero Said
Kwa maoni yangu, sifa kuu inayompambanua mzee Sozigwa katika maisha yake yote ya siasa hapa alihubiri kile alichokiamini.
Katika miaka ya sabini, akiwa mkugenzi wa Redio Tanzania, alianzisha kipindi redioni kilichojulikana kwa jina la; "Mikingamo" katika mojawapo ya vipindi vyake, alisema kuwa ubepali ulikuwa unyama. Na kweli, mzee Sozigwa hata baada ya kusambaratika kwa siasa ya ujamaa aliendelea kuishi kama mjamaa.
Nakumbuka mwishoni mwa miaka ya 1990, akiwa mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM alikuja Bukoba kwa shughuli za kikazi; mh. Kimiti wakati huo akiwa mkuu wa mkoa (k) alimtumia gari ya kwenda kumpokea melini; dereva alipomtafuta katika vyumba vyote vya daraja la kwanza hasimpate akarudi na kuripoti kwa bosi wake kuwa mzee hakuja; kumbe yeye alikuwa amekuja kwenye daraja ya tatu. Baadaye alimpigia mh. Kimiti kumjulisha kuwa alikuwa tayari amewasili na amefikia coffee Tree Inn.
Baadaye wakati tukinywa chai pamoja yule dereva alikuja kuomba msamaha huku akijitetea kuwa alikuwa amepita kwenye vyumba vyote vya daraja la kwanza lakini hakumuona.
Kitu alichomjibu mzee yule ni;"wewe nani alikwambia kuwa chama kina fedha za kupoteza kwa kusafirisha watu daraja la kwanza." Na aliyasema hayo miaka mingi baada ya azimio la Zanzibar kuiweka CCM katika njia ya ubepari.
Wakati wa mchakato wa kumpata mgombea wa urais kupitia CCM wakati wa uchaguzi mkuu wa 2005, sekretariati ya CCM chini ya Philip Mangula iliazimia kuondoa mgombea yeyote atakakayebainika kutoa rushwa kwenye kinyanganyiro.
Mzee Sozingwa akiwa anasimamia idara ya nidhamu katika sekretariati hiyo akalivalia njuga azimio hilo, Nakumbuka wakati Kikwete alipokuja Bukoba kusaka wadhamini, mzee Sozigwa alikuwepo akifuatilia nyendo zote zilizoashiria kuwepo kwa mazingira ya rushwa.
Inasemekana wakati wa kujadili wagombea urais katika kamati kuu taarifa aliyokuwa ameiandaa ilitupwa kapuni, na hatimaye sekretarati yote ilifungiwa virago baada ya JK kuukwea wenyekiti wa CCM.
Wacha kuweka habari za kizushi wewe! Mwandishi wa Rais na Katibu wa Rais ni vitu viwili tofauti. Katibu wa Rais alikuwa Mzee Kasori na pengine Mzee Butiku!
Hazina ya kumbukumbu na utendaji uliotukuka imeondoka...RIP, comrade, Mzee Paul Sozigwa....Yule Mzee Mkongwe na Gwiji la siasa l za Tanzania Mzee Sozigwa amefariki Dunia.
View attachment 508065
Paul Sozigwa ndiye Katibu wa kwanza wa Rais (IKULU-HABARI).
Mbali na kuwa katibu wa Ikulu, nyadhifa nyingine alizoshika ni Mkurugenzi wa kwanza wa Redio Tanzania(RTD), DO Wilaya ya Kisarawe katika serikali ya kikoloni na katibu Mkuu, Wizara ya Habari na Utangazaji.
Vilevile alishawahi kushika nafasi mbalimbali ndani ya CCM zikiwemo za Mjumbe wa NEC, CC na M/kiti Tume ya Taifa ya Udhibiti na Nidhamu na M/kiti wa CCM mkoa wa Pwani.
Rest in peace Mzee wetu
=======
Byendangwero Said
Kwa maoni yangu, sifa kuu inayompambanua mzee Sozigwa katika maisha yake yote ya siasa hapa alihubiri kile alichokiamini.
Katika miaka ya sabini, akiwa mkugenzi wa Redio Tanzania, alianzisha kipindi redioni kilichojulikana kwa jina la; "Mikingamo" katika mojawapo ya vipindi vyake, alisema kuwa ubepali ulikuwa unyama. Na kweli, mzee Sozigwa hata baada ya kusambaratika kwa siasa ya ujamaa aliendelea kuishi kama mjamaa.
Nakumbuka mwishoni mwa miaka ya 1990, akiwa mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM alikuja Bukoba kwa shughuli za kikazi; mh. Kimiti wakati huo akiwa mkuu wa mkoa (k) alimtumia gari ya kwenda kumpokea melini; dereva alipomtafuta katika vyumba vyote vya daraja la kwanza hasimpate akarudi na kuripoti kwa bosi wake kuwa mzee hakuja; kumbe yeye alikuwa amekuja kwenye daraja ya tatu. Baadaye alimpigia mh. Kimiti kumjulisha kuwa alikuwa tayari amewasili na amefikia coffee Tree Inn.
Baadaye wakati tukinywa chai pamoja yule dereva alikuja kuomba msamaha huku akijitetea kuwa alikuwa amepita kwenye vyumba vyote vya daraja la kwanza lakini hakumuona.
Kitu alichomjibu mzee yule ni;"wewe nani alikwambia kuwa chama kina fedha za kupoteza kwa kusafirisha watu daraja la kwanza." Na aliyasema hayo miaka mingi baada ya azimio la Zanzibar kuiweka CCM katika njia ya ubepari.
Wakati wa mchakato wa kumpata mgombea wa urais kupitia CCM wakati wa uchaguzi mkuu wa 2005, sekretariati ya CCM chini ya Philip Mangula iliazimia kuondoa mgombea yeyote atakakayebainika kutoa rushwa kwenye kinyanganyiro.
Mzee Sozingwa akiwa anasimamia idara ya nidhamu katika sekretariati hiyo akalivalia njuga azimio hilo, Nakumbuka wakati Kikwete alipokuja Bukoba kusaka wadhamini, mzee Sozigwa alikuwepo akifuatilia nyendo zote zilizoashiria kuwepo kwa mazingira ya rushwa.
Inasemekana wakati wa kujadili wagombea urais katika kamati kuu taarifa aliyokuwa ameiandaa ilitupwa kapuni, na hatimaye sekretarati yote ilifungiwa virago baada ya JK kuukwea wenyekiti wa CCM.
Simu zilikuwepo tangu wakoloni wapo.Tufafanulie alimpigiaje ,simu wakati miaka kulikuwa hakuna simu za mkononi?