Mzee Tashrif kafariki leo na kazikwa leo. Waislam wanajua heshima, umuhimu na maana ya mazishi

Hata hizo hukumu zinatekelezwa basi kaka, waislam wangapi leo hii wanaenda kwa Mwamposa wanaconvert lakini hawa waarabu pori wapo kimya, wajaribu waone serikali itakachowafanya.
Twende kwa fact, kwann usibadili utaratibu wa Swala kama unapenda kwenda na teknolojia? Yaan kwann usianzishe basi swala 8 au swala 3 ili kuendana na teknolojia?
 
Tatizo la nyie mliokaririshwa dini huwa hampendi chalenge, huo ujinga utawaisha lini?
Wewe sio Muislam, hakuna muislam mwehu, anayeweza kujipangia vitu kijinga na reasoning capacity ndogo kama yako.
 
Wachaga ndo wanakaa na maiti sana.

Hata Bwana Yesu alikufa leo na kuzikwa siku hiyo hiyo
 
Hizi nyuzi nyingine zinaonesha mwandishi ana msongo wa mawazo. Wewe ukifiwa ukaamua kuzika saa hiyo hiyo au dk hiyo hiyo si dhambi na hukatazwi kabisa. Mnapata shida bure waislamu kutaka mfanano na wakristo. Ni ukosefu tu wa afya ya akili. Maana vitu vingine unaonekana tu una msongo wa mawazo. Fanya utakavyo wewe. Wala hulazimishwi sheikh. Tena ukienda kwa wahindi wao ni bora zaidi wanachoma moto maiti. Unaweza amua hili ili upate mavumbi
 
We jamaa maiti ni kama shule ulisoma secondary sio ww .wahindi wanazichoma
 
Sheria na mafundisho ya uislamu ni timeless ndio kitu unatakiwa ukifahamu.
 
Post ya kiboya sana
 
Hauzuiliwi kubadili dini.
 
Wachaga ndo wanakaa na maiti sana.

Hata Bwana Yesu alikufa leo na kuzikwa siku hiyo hiyo
Lakini hawakuja kukuomba hata kumi kama mchango na ukihudhuria msibani unakula na kunywa chai

Wewe fanya utakavyo hujazuiwa
 
Mkuu kwa mujibu wa uislam mtu anapokata roho huwa anapata maumivu makali sana, na Yale maumivu hayakomi mpaka azikwe
Nadhani hii ni sababu kuu mtume wetu akatuasa swala hili liwe miongoni mwa Mambo ya haraka zaidi
Yaani Mtu ameshakata roho (Amekufa) halafu anaendelea kupata maumivu kisa hajazikwa???

Maumivu anapataje na hana hisia zozote na nerves zote zimekufa??

Sheikh tuache pls [emoji23]
 
Kukaa na mzoga ndani usio kuwa na faida yeyote siku tano ni moja wapo ya dalili ya upumbavu.
Upumbavu zaidi ni kuamini kuwa Mzoga unaendelea kupata maumivu kisa haujazikwa [emoji23][emoji23][emoji23]

Na akifika kaburini anaanza kuhojiwa na kuadhibiwa mdogomdogo [emoji23]
 
Kuzika Ni desturi! Haiwezi kufanana!
Burying is tradition! Can't be homogeneous all over!

Yesu alizikwa siku hiyo hiyo siku ya tatu wanawake walienda kaburini ili waupake mwili mafuta ya mane mane Kama ilivyo desturi ya wayahudi! Walipofika na kuchungulia kaburini walikuta alishafufuka!

Yesu alizikwa na Yusuph wa Armathaya kwenye bustani ambako kulikua na kaburi ilihochongwa katika mwamba mithili ya pango ambako kuliviringishwa Jiwe kubwa kuziba mlango wa kaburi;

Awali je;
1. Ingawa waislam wanazika siku hiyo hiyo, je siku ya tatu wanawake huenda kaburini kupaka mwili wa marehemu mafuta au hata ya alizeti?
-kuna neno katika biblia "kama ilivyokua desturi ya wayahudi"
Hii inaonesha mazishi Ni desturi ya watu Fulani na haiwezi kufanana na watu wengine,
Ukisoma Egyptiology wanafanya mummification je unajua pengine wanapofanya mummification?

Huko uchagani zamani zamani baadhi ya maeneo watu walipokufa walizikwa jikoni Tena wakiwa wamekaa na baada ya muda mabaki yakifukuliwa na kuwekwa sehemu Fulani migombani na ilifanyika sherehe maalum ya kufukua!

2. Yesu alizikwa katika kaburi likokua tayari limechongwa! Kwa nature au geography ya maeneo yake haukua rahisi kuchimba mashimo Kama huko kwenu au wao hawakua na utaratibu wa kuchimba Kama wafanyavyo waislam au watu wa maeneo mengine na kumlaza marehemu huku wakiweka ubao juu yake kwenye Ile mini-grave!
Nikuulize Nani alimwekea Yesu Udogo? Kumbe haikua desturi ya wayahudi kuwekea udongo katika kaburi!

Zamani wamasai mtu akifa wanakimbia boma (manyata) na Wala hawaziki, was hivi hawafanyi hivyo; kwa sababu desturi yaweza kubadilika kutokana na muingiliano wa watu wenye desturi tofautu!! Ingawa sijawahi kuona msiba wa wamasai!

Jifunze kitu katika historia! Kuzika Ni desturi na haiwezi kufanana popote ukiacha hizi dini zilizoleta ufanano kwa wafuasi wake!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…