Mzee wake ndiye aliyempa zawadi ya muhimu kuliko zote, ndiyo silaha yake kwa sasa

Mzee wake ndiye aliyempa zawadi ya muhimu kuliko zote, ndiyo silaha yake kwa sasa

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Jana nilikutana na class mate wa utotoni. Tuliachana tukiwa shule ya msingi, mzee wao alistaafu walirudi kwao huko mikoa ya Bara.

Huyu rafiki alikuwa mmoja wa vipanga darasani na aliitendea haki akili yake. Ana nafasi nzuri sana huko aliko. Katika maisha yake binti aliyemuoa alitoka famila ya matawi ya juu.

Jana alikuwa ananieleza magumu wanayopitia kwenye ndoa yao. Ana kumbuka siku ya harusi yao, familia yake ilitoka Bara huko na wakati wa kutoa zawadiilikuwa tofauti na upande wa mke waliowazawadia vitu vya thamani kama gari , kiwanja, ticket za honeymoon. Mzee wake alifunga Bible kwa unadhifu na alimkabidhi meza kuu.

Ananiambia kipindi hiki anatambua kuwa zawadi ya muhimu kuliko zote. Mali zilileta mzozo wala ha itamani. Tegemeo la furaha yake liko kwenye Bibilia ambayo mzee wake Alimhusia asimalize siku bila kuisoma.
 
Za asubuhi dada huko kwa mtogole hawajambo
Ngoja wenye dini waje watakupa mwongozo
 
Ulivyoelewa

Mama vipi mbona una harakaharaka unawahi wapi?
 
Nazingua tu mtoa mada

Biblia ndiyo kila kitu ndipo uzima ulipo.

Najua Kiranga na mwenzie Nyani ngabu na waislamu watapinga.
 
Ni kweli hakuna zawadi bora zaidi ya ukumbusho wa neno la Mwenyezi MUNGU. Mali nzuri za kutafuta wenyewe baada ya ndoa, mali za zawadi si mali na isitoshe hata kama ni za kutafuta mwenyewe mali huja na kupotea lkn neno la Mwenyezi MUNGU litasimama. Na kama mali zimetolewa na familia ya mke na endapo mwanamke asipokuwa makini zinaweza kuwa chanzo cha migogoro. Huwa sifurahii sana kuziona zawadi za ndoa zimejazana nyumbani mwangu
 
Mali nzuri za kutafuta wenyewe baada ya ndoa, mali za zawadi si mali, na kama zimetolewa na familia ya mke na endapo mwanamke asipokuwa makini zinaweza kuwa chanzo cha migogoro. Huwa sifurahii sana kuziona zawadi za ndoa zimejazana nyumbani mwangu
Hapo point ni bible bwasheee.
 
Hamkupasha kiporo?mliwaze mwenziio na stress za ndoa [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Jana nilikutana na class mate wa utotoni. Tuliachana tukiwa shule ya msingi, mzee wao alistaafu walirudi kwao huko mikoa ya Bara.

Huyu rafiki alikuwa mmoja wa vipanga darasani na aliitendea haki akili yake. Ana nafasi nzuri sana huko aliko. Katika maisha yake binti aliyemuoa alitoka famila ya matawi ya juu.
Mzee wake alifunga Bible kwa unadhifu na alimkabidhi meza kuu.
Tegemeo la furaha yake liko kwenye Bibilia ambayo mzee wake Alimhusia asimalize siku bila kuisoma.
Hakuna kinachotoa amani ya moyo kama kukubaliana na ukweli.

Kuna siku niliwasikia wadada fulani wakisema "wanaume masikini huwa wanajifanya wana mapenzi ya dhatiii".

Kingine watajifanya wacha Mungu kwa kuwa hawakubarikiwa upande wa pili.

Vyovyote vile umasikini ni mbaya sana, wala hautakiwi kuutafutia faraja badala ya kupambana nao.
 
Jana nilikutana na class mate wa utotoni. Tuliachana tukiwa shule ya msingi, mzee wao alistaafu walirudi kwao huko mikoa ya Bara.

Huyu rafiki alikuwa mmoja wa vipanga darasani na aliitendea haki akili yake. Ana nafasi nzuri sana huko aliko. Katika maisha yake binti aliyemuoa alitoka famila ya matawi ya juu.

Jana alikuwa ananieleza magumu wanayopitia kwenye ndoa yao. Ana kumbuka siku ya harusi yao, familia yake ilitoka Bara huko na wakati wa kutoa zawadiilikuwa tofauti na upande wa mke waliowazawadia vitu vya thamani kama gari , kiwanja, ticket za honeymoon. Mzee wake alifunga Bible kwa unadhifu na alimkabidhi meza kuu.

Ananiambia kipindi hiki anatambua kuwa zawadi ya muhimu kuliko zote. Mali zilileta mzozo wala ha itamani. Tegemeo la furaha yake liko kwenye Bibilia ambayo mzee wake Alimhusia asimalize siku bila kuisoma.
Huu sasa ni umbea.
 
Back
Top Bottom