Mzee wangu yupo hoi, huenda Serikali ingeweka wazi, Mzee wangu asingeshiriki kuzika rafiki yao aliyefariki kwa changamoto

Mzee wangu yupo hoi, huenda Serikali ingeweka wazi, Mzee wangu asingeshiriki kuzika rafiki yao aliyefariki kwa changamoto

Pole sana ndugu yangu.

Watanzania waliowengi hasa wasio na access ya vyombo vya habari vya kisasa kama hizi smartphone hawana taarifa juu ya hali halisi ya Korona nchini.

Serikali imewaacha wananchi kwenye mataa
Huo ni uuwaji wa kudhamiria. Sawa na unyang'anyi wa kutumia nguvu tu.
 
Mimi nawashauri wazee kijijini kwetu msiba wowote unatokea mjini, kama ajali haijahusika, wasihudhurie hata kama waliofariki ni watoto wao.Full Stop!
Mpige stop kwenye msiba wowote ule mikusanyiko ndio inasababisha maambukizi kwa kasi kwenye lile kundi liliotajwa (wazee na watu wenye kinga zilizoshuka chini) so asiende tu kwenye mikusanyiko period✋🏽
 
Ni kujiongeza tu rafiki, mtu akifa kwa tatizo la upumuaji basi nyie ndugu chukueni tahadhari. Pole sana mtoa mada
Hivi wewe umeshawahi kukaa kujijini,unawajua watu wa kijijini walivyo?Kipindi kile cha mlipuko wa kipindupindu ,serikali ilitumia nguvu kubwa sana kupiga marufuku nyingi ili kipindupindu kisisambae.Sasa leo umewapa uhuru wa kufanya mambo yao kwa uhuru kwa kuwapa tahadhari ya mdomo,unategemea watafuata unachokisema?
 
Naandika huku naumia sana.

Maisha ya mzee wangu yako hatarini sana anapumua kwa shida sana.

Chanzo cha kuumwa.
Kuna rafiki yao mzee mwenzao alifariki, wakaambiwa kuwa chanzo cha kifo cha huyo rafiki yao ni mapafu.
Kutoka hospital ya Bugando ndugu wa marehemu walipewa mwili kwenda kuzika kijijini geita bila tahadhari wakiamini kafa kwa ugonjwa wa kawaida.

Alipofikishwa huko kijijini, ndipo wazee wenzake wakawa wamejiandaa kumzika mwenzao kama ilivyo ada yao.
Jukumu la kubeba mwili kuzika, lilifanywa na wazee kama ishara ya heshima kwa mwenzao.
Miongoni mwa wazee hao! Na mzee wangu alishiriki.

Msiba ulikuwa na msongamano mkubwa kama ada na mila za vijijini.

Wazee hawa maskini ya Mungu pasipo kujua walibeba mwili bila tahadhari! Hadi atua ya mwisho ya kumzika mwenzao.

Baada ya hapo jioni mzee akanisimulia ilivyokuwa, akadai pia walibeba na jeneza liliwavujia majimaji.
Baada ya siku kadhaa wazee hawa wameanza kuumwa.
Watatu wana hali mbaya sana, na mzee wangu usiku wa kuamkia Leo kabanwa mbavu haswa! Ametumia dawa ya malimao, vitunguu, pilipili na tangawizi lakini hali si hali, kwanza kaanza kuchanganyiwa na haongei tena.
Yuko hospital kalazwa lakini hali ni mbaya sana.
Huenda serikali wangetangaza tahadhari hasa misibani haya yasingetokea.
Huenda serikali ingetangaza wazi misiba ya korona ingezikwa na vijana walivalia kinga.
Hapa najaribu kuwaza kama hali iko hivi, maambukizi yameathiri wangapi kwa uzembe wa serikali?

Hatuhitaji lockdown, lakini chamhimu tamko litoke lifike hata kijijini watu wapewe mbinu.

Imeniuma sana kwa uzembe huu mkubwa! Kama nitapoteza busara za mzee wangu, yamkini na mama yangu atakuwa kaambukizwa maana wanalala pamoja mda wote wa kuuguza.

Yamkini tungeweza kuwalinda wazee lakini watoto wa shule hawa wadogo bado ni Carrier wa kuleta homa hiyo nyumbani.
Serikali ingefunga shule hata kwa miezi miwili ingesaidia kupunguza kasi kama mwaka 2020 sambamba na kuchukua tahadhari.

Utafaa nini utajiri katikati ya misiba?

Serikali ingeweza hata kuja na mikakati, kama hawana pesa za chanjo, wangeipokea hata watu wakachomwa kwa hiari hata kwa malipo tungelipa.

Katiba imuondolee mamlaka mtu mmoja kutegemewa kutoa tamko ili kuliokoa taifa.

Inauma sana.
pole sana mkuu,
 
Yaani nafsi yangu naipenda sana siwezi kusubiri mtu aniambie nichukue tahadhari. Nyumbani kwangu nina sauti inayosikilizwa na watu wanatii . Tunachukua tahadhari kwa kadri ya uwezo wetu . Inabidi kila mtu ailinde nafsi yake. Usiikabidhi nafsi iendeshwe na serikali shauri lako 🤓🤓🤓

Wale wasio na access na taarifa sahihi nao unasema je?

Kwa vile wewe una taarifa sahihi nini kinakufanya udhani ni hivyo kwa kila mtu?

Au watanzania wote ni wewe tu mkuu?
 
Huko kwenu wazee ndio wanabeba jeneza kupeleka mazikoni, sio vijana! Hao wazee walikuwa wanapokezana jeneza linalowavujia maji vijana wa huko huwa wapi?
 
Jana hapa kijijin nilipo palikua na ufunguz wa bar moja
Njemba zimeminyana ndani
Bia wanakunya haziishi kumbe mijasho yao inajaa kwenye chupa
 
Kwahyo hata ile combine iliyokuleta duniani nayo ni mapimbi sio? Je wajomba zako walioko kiparanga ambapo hakuna hata network zaid ya kusikiliza Radio watajuje kuwa korona ipo ili wachukue tahadhari? Sawa Rais kasema tuchukue tahadhari vipi kuhusu kusambaza vipeperushi huko vijijin kuhusiana na tahadhari za mdudu endelea kula ugali kwa shemeji yako ambae ni kada wa mtukuf

Hata wewe unaweza kuwa pimbi pia, Rais kasema tuchukue tahadhari we unatakaje tena?
Vipeperushi? Kwahiyo kama hakuna vipeperushi ndio huwezi kuchukua tahadhari? Pimbi wengi sana hata JF humu
 
Pole mkuu,ila serikali wafunge shule za msingi na sekondari,vyuo waache,watu tunakula kupitia vyuo wakifunga hali itakua mbaya kwa baadhi yetu
 
Mheshimiwa wetu Hana huruma Wala hataki ku sympathize na raia wake awe na huruma na aseme sasa kila corner ni mwendo wa barakoa, kila sehemu kunawa kuwe na marufuku na misongamano isiyo na lazima shule zifungwe hata mwezi hatari itapungua bila hvo Hali itakuwa mbaya. Raisi wetu asiwe na roho ngumu ka ya farao Hadi apate pigo ndo ashtuke
 
Mpendwa usingoje mpaka Serikali jikingeni kwenye Familia uko mkumbushane hata kwa njia ya simu kuvaa barakoa ni lazima kunawa mikono ni lazima Mimi nimekuwa nikimkumbusha mama yangu mara kwa mara maumivu yako ya kuondokewa na mpendwa(japosiombei itokee )wako huwezi kugawana na serikali.
Utavaa barakoa ila wengine hawJikingi wanakuletea, mwaka jana kila mtu alikuwa makini corona tukaishinda saa mbili ila sasa watu wengi wagonjwa
 
Pole sana ndugu Mungu ni mwema atamponya....ila pia nna maswali mawili.

1. km ugonjwa wa corona unaambukizwa kwa njia ya hewa na mtu hapumui tena na kafungiwa kwenye jeneza kubeba jeneza kuna shida gani?

2. Mtu akifariki anaanza kukauka, damu inaganda..hayo majimaji yanatoka wapi, tena mpaka yatoke nje ya jeneza?

Otherwise tuchukue tahadhari...kuzilinda Afya zetu ni jukumu letu sio la serikali wala mtu wa pembeni, we need to be smart on this.
 
Huko kwenu wazee ndio wanabeba jeneza kupeleka mazikoni, sio vijana! Hao wazee walikuwa wanapokezana jeneza linalowavujia maji vijana wa huko huwa wapi?
Hiiiiii bagosha!

IMG_20210218_174254_207.jpg


Watauliza hata rangi za vyupi za wabeba jeneza. Lengo likiwa lile lile kujaribu kuwapoteza wowote maboya.

Ama hakika iziraeli mtoa roho za watu yu mwema mno kuliko nyie!
 
Back
Top Bottom