kelphin
JF-Expert Member
- Dec 24, 2019
- 9,872
- 16,319
Kufa angekufa tu hata kwa kuchomwa na miiba kwa hiyo kama mpango wa Mungu ni kumuua baba yako na atakufa.
Watu wenye akiri kama zako
Ningekua rais msingeliishi nchini mwangu!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kufa angekufa tu hata kwa kuchomwa na miiba kwa hiyo kama mpango wa Mungu ni kumuua baba yako na atakufa.
Huo ni uuwaji wa kudhamiria. Sawa na unyang'anyi wa kutumia nguvu tu.Pole sana ndugu yangu.
Watanzania waliowengi hasa wasio na access ya vyombo vya habari vya kisasa kama hizi smartphone hawana taarifa juu ya hali halisi ya Korona nchini.
Serikali imewaacha wananchi kwenye mataa
Mpige stop kwenye msiba wowote ule mikusanyiko ndio inasababisha maambukizi kwa kasi kwenye lile kundi liliotajwa (wazee na watu wenye kinga zilizoshuka chini) so asiende tu kwenye mikusanyiko period✋🏽Mimi nawashauri wazee kijijini kwetu msiba wowote unatokea mjini, kama ajali haijahusika, wasihudhurie hata kama waliofariki ni watoto wao.Full Stop!
Hivi wewe umeshawahi kukaa kujijini,unawajua watu wa kijijini walivyo?Kipindi kile cha mlipuko wa kipindupindu ,serikali ilitumia nguvu kubwa sana kupiga marufuku nyingi ili kipindupindu kisisambae.Sasa leo umewapa uhuru wa kufanya mambo yao kwa uhuru kwa kuwapa tahadhari ya mdomo,unategemea watafuata unachokisema?Ni kujiongeza tu rafiki, mtu akifa kwa tatizo la upumuaji basi nyie ndugu chukueni tahadhari. Pole sana mtoa mada
pole sana mkuu,Naandika huku naumia sana.
Maisha ya mzee wangu yako hatarini sana anapumua kwa shida sana.
Chanzo cha kuumwa.
Kuna rafiki yao mzee mwenzao alifariki, wakaambiwa kuwa chanzo cha kifo cha huyo rafiki yao ni mapafu.
Kutoka hospital ya Bugando ndugu wa marehemu walipewa mwili kwenda kuzika kijijini geita bila tahadhari wakiamini kafa kwa ugonjwa wa kawaida.
Alipofikishwa huko kijijini, ndipo wazee wenzake wakawa wamejiandaa kumzika mwenzao kama ilivyo ada yao.
Jukumu la kubeba mwili kuzika, lilifanywa na wazee kama ishara ya heshima kwa mwenzao.
Miongoni mwa wazee hao! Na mzee wangu alishiriki.
Msiba ulikuwa na msongamano mkubwa kama ada na mila za vijijini.
Wazee hawa maskini ya Mungu pasipo kujua walibeba mwili bila tahadhari! Hadi atua ya mwisho ya kumzika mwenzao.
Baada ya hapo jioni mzee akanisimulia ilivyokuwa, akadai pia walibeba na jeneza liliwavujia majimaji.
Baada ya siku kadhaa wazee hawa wameanza kuumwa.
Watatu wana hali mbaya sana, na mzee wangu usiku wa kuamkia Leo kabanwa mbavu haswa! Ametumia dawa ya malimao, vitunguu, pilipili na tangawizi lakini hali si hali, kwanza kaanza kuchanganyiwa na haongei tena.
Yuko hospital kalazwa lakini hali ni mbaya sana.
Huenda serikali wangetangaza tahadhari hasa misibani haya yasingetokea.
Huenda serikali ingetangaza wazi misiba ya korona ingezikwa na vijana walivalia kinga.
Hapa najaribu kuwaza kama hali iko hivi, maambukizi yameathiri wangapi kwa uzembe wa serikali?
Hatuhitaji lockdown, lakini chamhimu tamko litoke lifike hata kijijini watu wapewe mbinu.
Imeniuma sana kwa uzembe huu mkubwa! Kama nitapoteza busara za mzee wangu, yamkini na mama yangu atakuwa kaambukizwa maana wanalala pamoja mda wote wa kuuguza.
Yamkini tungeweza kuwalinda wazee lakini watoto wa shule hawa wadogo bado ni Carrier wa kuleta homa hiyo nyumbani.
Serikali ingefunga shule hata kwa miezi miwili ingesaidia kupunguza kasi kama mwaka 2020 sambamba na kuchukua tahadhari.
Utafaa nini utajiri katikati ya misiba?
Serikali ingeweza hata kuja na mikakati, kama hawana pesa za chanjo, wangeipokea hata watu wakachomwa kwa hiari hata kwa malipo tungelipa.
Katiba imuondolee mamlaka mtu mmoja kutegemewa kutoa tamko ili kuliokoa taifa.
Inauma sana.
Yaani nafsi yangu naipenda sana siwezi kusubiri mtu aniambie nichukue tahadhari. Nyumbani kwangu nina sauti inayosikilizwa na watu wanatii . Tunachukua tahadhari kwa kadri ya uwezo wetu . Inabidi kila mtu ailinde nafsi yake. Usiikabidhi nafsi iendeshwe na serikali shauri lako 🤓🤓🤓
Haya maneno ni makari sanaUtafaa nini utajiri katikati ya misiba?
Kwahyo hata ile combine iliyokuleta duniani nayo ni mapimbi sio? Je wajomba zako walioko kiparanga ambapo hakuna hata network zaid ya kusikiliza Radio watajuje kuwa korona ipo ili wachukue tahadhari? Sawa Rais kasema tuchukue tahadhari vipi kuhusu kusambaza vipeperushi huko vijijin kuhusiana na tahadhari za mdudu endelea kula ugali kwa shemeji yako ambae ni kada wa mtukuf
Utavaa barakoa ila wengine hawJikingi wanakuletea, mwaka jana kila mtu alikuwa makini corona tukaishinda saa mbili ila sasa watu wengi wagonjwaMpendwa usingoje mpaka Serikali jikingeni kwenye Familia uko mkumbushane hata kwa njia ya simu kuvaa barakoa ni lazima kunawa mikono ni lazima Mimi nimekuwa nikimkumbusha mama yangu mara kwa mara maumivu yako ya kuondokewa na mpendwa(japosiombei itokee )wako huwezi kugawana na serikali.
Hiiiiii bagosha!Huko kwenu wazee ndio wanabeba jeneza kupeleka mazikoni, sio vijana! Hao wazee walikuwa wanapokezana jeneza linalowavujia maji vijana wa huko huwa wapi?
Vijijini hawana elimu yoyote kuhusiana na Corona!Ni kujiongeza tu rafiki, mtu akifa kwa tatizo la upumuaji basi nyie ndugu chukueni tahadhari. Pole sana mtoa mada
Kama wanasubiri tamko watasubiri sanaMimi naww hatungoji tamko Sababu tunaelewa vipi wa huko kijjn wanaoamini Rais ndio kila kitu
Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
kuna part unaweza kucheza wewe binafsi kuna part ni ya serikali, kwa mfano huna uwezo wa kufunga mashule ili watoto wasiambukizane na kuuleta home lakini serikali inawezaKama wanasubiri tamko watasubiri sana