Mzee Warioba: Siyo lazima Mbunge aitwe Mheshimiwa

Mzee Warioba: Siyo lazima Mbunge aitwe Mheshimiwa

Kweli kabisa. Moja ya maamuzi ya kipuuzi kutokea katika Bunge la Tanzania, ni lile la kuondoa Wabunge kuitwa 'ndugu' na kubadilishwa na 'mheshimiwa'. Katika nchi inayojaribu kuleta usawa na kupambana na ulevi wa madaraka, kitendo hiki kimechangia kwa Wabunge wengi, Spika wa sasa, kujiona Mungu-mtu. Uheshimiwa ni sifa ya mtu anayejistahi, mwenye hekima na sera njema.

Anayefanya kazi kwa kujitolea zaidi akiangalia maslahi ya watu na si binafsi, mpinga rushwa, ubadhirifu.... ni wangapi katika bunge hivi sasa?

Kama nikiwa kiongozi, nitaamuru wote serikalini na mihimili mingine waitwe 'mtumishi'. Bwana mtumishi kadhaa, bibi mtumishi kadhaa. Hii itatia dhana katika vichwa vyao kuwa wananchi ndiyo maboss wao, na siyo kama sasa ambapo wengi wanadhani wanatutendea 'fadhila' na kwamba mmoja wao akifa au akiondoka maisha yetu yataingia dosari!
 
Unapomuita mtu"MHESHIMIWA" unakuwa umejiridhisha kuwa anastahili heshima kwa jinsi anavyoendesha maisha yake katika jamii anayoishi!! Heshima haiombwi bali hutengenezwa na muhusika.

Leo hii kumuita Ndugai "MUHESHIMIWA ni kumkejeri kwani hastahili heshima kwa jinsi jamii inavyo muona!!
Khaaaa! Hii nayo tafsiri yako sema hauko kisheria sasa kwahivo haiezi kutumika
 
Yaani mtu/mbunge umwajiri wewe mwananchi kupitia kura yako halafu umwite mheshimiwa? Khaa
Wivu upo wapi hapo
Huyo uliyemuajiri ndiye anayekuamulia maisha yako..ndiye aliyejitungia sheria pale kazini kwake wewe muajiri wake umuite mheshimiwa na ukiwa na jambo lako ukamuombe akiridhia sawa akikukatalia pia sawa!
 
Nyerere hakuwahi kuitwa 'mtukufu rais', hiyo ya kuitana 'mtukufu' ilianzishwa wakati wa awamu ya pili.
Mawatu ya pwani haya kwa kupenda ubwanyenye hawajambo!

Rais ana utukufu gani?? Ati mtukufu Rais Mwinyi? Doolhh!!

Ifike mahali tujitambue sasa! Haya mambo ya kuabudu watu yasitishwe.
 
Kutokana na yanayoendelea Bunge letu chini ya kiongozi wao Mbunge Ndugai kuanzia sasa TUONDOE NENO HILI MHESHIMIWA NA TUWAITE NDUGU MBUNGE AU MBUNGE TUU sioni kinachofanywa na hao WABUNGE hasa kwa Serikali ya awamu ya SITA ndio tulijua hili ni genge la kugawana pesa tuu shetia mbovu sana na miswaada mibovu hata uwezo wa kuhoji watu waliopotea au mbunge mwenzao kupigwa risasi hawana sasa HUO UHESHIMIWA UNATOKA WAPI ??hasa awamu hizi 5 na sita HILI SIO BUNGE NI GENGE LA WANYONYAJI MAANA WOTE WALIOPO MLE KWANZA WALIPISHWA BILA DEMOKRASIA NDIO MAANA WANAPIGANIA UHESHIMIWA WAKATI WAO HAWANA HESHIMA
 
Mawatu ya pwani haya kwa kupenda ubwanyenye hawajambo!

Rais ana utukufu gani?? Ati mtukufu Rais Mwinyi? Doolhh!!

Ifike mahali tujitambue sasa! Haya mambo ya kuabudu watu yasitishwe.
Yaani tunarudi kwenye enzi za ujima za kumtukuza mkoloni kisa kavaa kaptula nyeupe.
 
Mwinyi aliitwa Mtukufu Rais, Mkapa ndio akakataa hiyo title.
Kama Mwinyi aliitwa Mtukufu basi haikuwa rasmi kama ilivyokuwa "Ndugu" na ilivyo hivi sasa "Mheshimiwa". Waliomwita Mwinyi Mheshimiwa watakuwa wale chawa walikua wanajikomba kutafuta uteuzi au kudumisha teuzi zao.
 
Mtu aliyepewa cheo na wananchi ni mheshimiwa na ni vyema kupewa heshima yake hiyo! Mbunge amechaguliwa na wananchi kwahiyo ni mheshimiwa, mwenyekiti wa kijiji amechaguliwa na wananchi ni mheshimiwa pia! Gar la mbunge likipita linapeperusha bendera askari anarakiwa kuipigia salut bendera! Tuache wivu!
Sasa hao waliompa Ubunge wakiamua kutomuita hivyo, walazimishwe?! Tuache kutojiamini na kupenda kukwezwa.
 
Khaaaa! Hii nayo tafsiri yako sema hauko kisheria sasa kwahivo haiezi kutumika
Wewe mwenyewe ndio sheria, utaamua kama mkikutana na Ndugai utamuita "MHESHIMIWA" au la!!! Kwani sio kila mmoja wetu anaingia mjengoni!! Mambo ya ndani ya Bunge waachie wabunge waitane wanavyotaka!
 
Mzee Warioba anasikitika kusikia makundi ya vyeo MTU kujiita
Mheshimiwa,
Serikali yangu,
Wizara yangu,
Idara yangu nk
Amedai watu wananuna wasipoabudiwa.

Hakatai kuitwa Mh,Bali anashauri waitane wawapo kwenye vikao vya Bunge.

Hata mawakili wasomi huitana wawapo kwenye vyumba vyao vya kazi.
 
Ndugu Rais
Juzi Morogoro, kiongozi wa wafanyakazi alimwita Jaji mstaafu na waziri mkuu wa zamani J. S. Warioba, "Ndugu Jaji mstaafu Warioba". Pale pale ukumbini baadhi walishika midomo, inasemekana na kimemo alipigwa kiongozi huyo na mkuu wake wa kazi!

Chakufurahisha, Jaji Warioba ameliweka sawa hili.
 
Back
Top Bottom