Mzee Warioba: Siyo lazima Mbunge aitwe Mheshimiwa

Mzee Warioba: Siyo lazima Mbunge aitwe Mheshimiwa

sahihi kwa 100%, wanasiasa akishaitwa mheshimiwa tayari anajiona yeye ni mtu maalum sana wakati kiuhalisia ni tofauti.

kuna watu kibao huku kitaa wapo smart sana kichwani kuliko hako kakikundi kanakoongozwa na Ndugai pale Dodoma!
Tofautisha mbunge na huyo smart wako wa mtaan!
 
Mtu aliyepewa cheo na wananchi ni mheshimiwa na ni vyema kupewa heshima yake hiyo! Mbunge amechaguliwa na wananchi kwahiyo ni mheshimiwa, mwenyekiti wa kijiji amechaguliwa na wananchi ni mheshimiwa pia! Gar la mbunge likipita linapeperusha bendera askari anarakiwa kuipigia salut bendera! Tuache wivu!
Hakuna lolote hapo ni kujikweza tuu, kwanza hivyo vyeo kama ubunge majority waliiba kura, wengine walipita kwa figisu bila kupigiwa kura, sasa hoja kwamba wamepewa cheo na wananchi haina mashiko. Hivi ukiitwa ndugu mbunge au ndugu mwenyekiti akili kichwani itahama au busara zitahama??
 
Iko wazi mbona: Ili uitwe Mheshimiwa ni lazima ujiheshimu kwanza, vinginevyo ukiitwa Mheshimiwa kama hustahili, unapakwa tu mafuta kwa mgongo wa chupa.
 
Wewe na yeye mzee Warioba nani anajua zaidi mambo ya kiutawala?

Huyo mzee ni waziri mkuu mstaafu unaleta usukununu wako hapa?
Pia amewahi kuwa mbunge na amewahi kuwa jaji, achilia mbali tume mbalimbali zilizoundwa na rais ambapo yeye aliteuliwa kuwa mwenyekiti mfano tume ya rasimu ya katiba pendekezwa
 
Nakumbuka wakati wa Mwalimu hakukuwa na neno Mheshimiwa kwa mtu yeyote, viongozi wote walikuwa wakiitwa Ndugu kasoro Rais ambaye alikuwa pia akiitwa Mtukufu Rais! Baada ya Mwalimu Nyerere kutoka madarakani, ukaibuka mjadala Bungeni Wabunge wakitaka waitwe Waheshimiwa (Honorable). Mwalimu alipinga lakini wakamwambia mbona Uingereza wanaitwa Honorable. Wakapitisha sheria wakaanza kuitana Waheshimiwa. Siyo wakati wa akina Waryoba kweli?? Tafuta wazee watukumbushe. Ila wakati Waryoba ni PM Rais wake alikuwa akiitwa Mtukufu Rais, na Mzee sikumsikia akisema kitu kwa kuwa labda alikuwa na kitu.
Warioba ndiyo kundi la Nyerere ambao walipinga but walishindwa na hilo kundi la wengi..
 
Mzee wetu Waziri Mkuu Mstaafu Joseph Sinde Warioba amesema kulazimisha watu wakuite wewe kuwa ni mheshimiwa mbunge, mheshimiwa waziri ,mheshimiwa diwani huko ni kuweka matabaka kwenye jamii ya watanzania.

Hii inapingana na Naibu Spika alivyogombana na Mbunge wa Mbeya Mjini Mbilinyi. Tulia alilazimisha kuitwa Mheshimiwa Naibu Spika

Hakika mzee Warioba ni tegemeo la watanzania kwa busara.

Chanzo dakika 45 itv.
Ndiye mzee pekee mwenye busara aliyebaki kwa sasa
 
Acha uwongo. Nyerere hakuwa anaitwa mtukufu Rais. Alikuwa akiitwa Ndugu Rais. Kenya walikuwa wanamwita mtukufu Rais Arap Moi, wote watanzania tulikuwa tunashangaa. Wakati huo nikiwa chipukizi, nilimvisha Mwalimu skafu mara 2, mara zote nilimwita Ndugu Rais ..... Mwinyi ndiye kwa mara ya kwanza aliitwa Mtukufu Rais, na wabunge wakajiita waheshimiwa.
Ushahidi upo humu ni kweli Nyerere J. K. Aliitwa Ndugu, ipo video youtube chipukizi akimkaribisha kukagua gwaride alimwita ndugu.., alikuwa na utu toka damuni
 
Mtu aliyepewa cheo na wananchi ni mheshimiwa na ni vyema kupewa heshima yake hiyo! Mbunge amechaguliwa na wananchi kwahiyo ni mheshimiwa, mwenyekiti wa kijiji amechaguliwa na wananchi ni mheshimiwa pia! Gar la mbunge likipita linapeperusha bendera askari anarakiwa kuipigia salut bendera! Tuache wivu!
Wewe ni mdharauliwa?

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
 
Pia amewahi kuwa mbunge na amewahi kuwa jaji, achilia mbali tume mbalimbali zilizoundwa na rais ambapo yeye aliteuliwa kuwa mwenyekiti mfano tume ya rasimu ya katiba pendekezwa
Umeonaeee?
Tanzania tuna watu wa ajabu sana kama huyu anahoji weledi wa mzee Warioba kisiasa!
 
Mtu aliyepewa cheo na wananchi ni mheshimiwa na ni vyema kupewa heshima yake hiyo! Mbunge amechaguliwa na wananchi kwahiyo ni mheshimiwa, mwenyekiti wa kijiji amechaguliwa na wananchi ni mheshimiwa pia! Gar la mbunge likipita linapeperusha bendera askari anarakiwa kuipigia salut bendera! Tuache wivu!
Yaani mtu/mbunge umwajiri wewe mwananchi kupitia kura yako halafu umwite mheshimiwa? Khaa
Wivu upo wapi hapo
 
Mtu aliyepewa cheo na wananchi ni mheshimiwa na ni vyema kupewa heshima yake hiyo! Mbunge amechaguliwa na wananchi kwahiyo ni mheshimiwa, mwenyekiti wa kijiji amechaguliwa na wananchi ni mheshimiwa pia! Gar la mbunge likipita linapeperusha bendera askari anarakiwa kuipigia salut bendera! Tuache wivu!
Siyo lazima aitwe mheshimiwa, ni ndugu tu inatosha
 
Mzee wetu Waziri Mkuu Mstaafu Joseph Sinde Warioba amesema kulazimisha watu wakuite wewe kuwa ni mheshimiwa mbunge, mheshimiwa waziri, mheshimiwa diwani huko ni kuweka matabaka kwenye jamii ya watanzania.

Hii inapingana na Naibu Spika alivyogombana na Mbunge wa Mbeya Mjini Mbilinyi. Tulia alilazimisha kuitwa Mheshimiwa Naibu Spika

Hakika mzee Warioba ni tegemeo la watanzania kwa busara.

Chanzo dakika 45 itv.
huyu mzee angekuwa rais wa sasa wa jamhuri ya muungano wa tanzania nchi ingekaa sawa sana.,
 
Mtu aliyepewa cheo na wananchi ni mheshimiwa na ni vyema kupewa heshima yake hiyo! Mbunge amechaguliwa na wananchi kwahiyo ni mheshimiwa, mwenyekiti wa kijiji amechaguliwa na wananchi ni mheshimiwa pia! Gar la mbunge likipita linapeperusha bendera askari anarakiwa kuipigia salut bendera! Tuache wivu!
Hiyo tafsiri kapeleke kijijini kwenu! Nyerere mwenyewe alikuwa anaitwa ndugu. Tulia ndo nani!
 
Nakumbuka wakati wa Mwalimu hakukuwa na neno Mheshimiwa kwa mtu yeyote, viongozi wote walikuwa wakiitwa Ndugu kasoro Rais ambaye alikuwa pia akiitwa Mtukufu Rais! Baada ya Mwalimu Nyerere kutoka madarakani, ukaibuka mjadala Bungeni Wabunge wakitaka waitwe Waheshimiwa (Honorable).

Mwalimu alipinga lakini wakamwambia mbona Uingereza wanaitwa Honorable. Wakapitisha sheria wakaanza kuitana Waheshimiwa. Siyo wakati wa akina Waryoba kweli?? Tafuta wazee watukumbushe. Ila wakati Waryoba ni PM Rais wake alikuwa akiitwa Mtukufu Rais, na Mzee sikumsikia akisema kitu kwa kuwa labda alikuwa na kitu.
Ngoja tusahihishe kidogo.
Wakati wa Nyerere akiwa rais hakuitwa Mtukufu, aliitwa Ndugu rais, au Mwalimu.
Wabunge waliitwa Ndugu mbunge.
Nadhani ni Mzee Mwinyi aliyekuja kuitwa Mtukufu.
Wabunge nao wakapitisha hoja kuwa waitwe waheshimiwa.
 
Back
Top Bottom