Mzee Warioba: Siyo lazima Mbunge aitwe Mheshimiwa

Mzee Warioba: Siyo lazima Mbunge aitwe Mheshimiwa

Mzee wetu Waziri Mkuu Mstaafu Joseph Sinde Warioba amesema kulazimisha watu wakuite wewe kuwa ni mheshimiwa mbunge, mheshimiwa waziri ,mheshimiwa diwani huko ni kuweka matabaka kwenye jamii ya watanzania.

Hii inapingana na Naibu Spika alivyogombana na Mbunge wa Mbeya Mjini Mbilinyi. Tulia alilazimisha kuitwa Mheshimiwa Naibu Spika

Hakika mzee Warioba ni tegemeo la watanzania kwa busara.

Chanzo dakika 45 itv.
Hata huyu enzi zake aliitwa mheshimiwa. Asiwe na wivu kwa waheshimiwa wa sasa
 
Mzee wetu Waziri Mkuu Mstaafu Joseph Sinde Warioba amesema kulazimisha watu wakuite wewe kuwa ni mheshimiwa mbunge, mheshimiwa waziri ,mheshimiwa diwani huko ni kuweka matabaka kwenye jamii ya watanzania.

Hii inapingana na Naibu Spika alivyogombana na Mbunge wa Mbeya Mjini Mbilinyi. Tulia alilazimisha kuitwa Mheshimiwa Naibu Spika

Hakika mzee Warioba ni tegemeo la watanzania kwa busara.

Chanzo dakika 45 itv.
Huyu babu bado yupo vizuri sn kichwani na bado ana kumbukumbu nyingi sema CCM wanaweza kumtafuna any time
 
Acha uwongo. Nyerere hakuwa anaitwa mtukufu Rais. Alikuwa akiitwa Ndugu Rais. Kenya walikuwa wanamwita mtukufu Rais Arap Moi, wote watanzania tulikuwa tunashangaa. Wakati huo nikiwa chipukizi, nilimvisha Mwalimu skafu mara 2, mara zote nilimwita Ndugu Rais ..... Mwinyi ndiye kwa mara ya kwanza aliitwa Mtukufu Rais, na wabunge wakajiita waheshimiwa.
Du hongera mkuu
 
Mtu aliyepewa cheo na wananchi ni mheshimiwa na ni vyema kupewa heshima yake hiyo! Mbunge amechaguliwa na wananchi kwahiyo ni mheshimiwa, mwenyekiti wa kijiji amechaguliwa na wananchi ni mheshimiwa pia! Gar la mbunge likipita linapeperusha bendera askari anarakiwa kuipigia salut bendera! Tuache wivu!
Wapuuzi kama wewe bado mpo wengi sn Tz
 
Waheshimiwa walikuwa zamani sio hawa wa siku hizi kwani 'wengi wao' hata matendo yao ndani na nje ya mjengo hayana maadili.
Angalia hata miswada waliyotunga hasa kipindi cha 'huyu mtu' ni hovyo na isiyo na tija kwa wananchi zaidi ya ukandamizaji.
Wamebaki kutetea matumbo yao na sio ya jamii iliyowapeleka huko!
Nashauri waitwe NDUGU kama zamani kama hawataki waache huo ubunge waje mtaani tupambane na hali zetu,
 
Nyerere hakuwahi kuitwa 'mtukufu rais', hiyo ya kuitana 'mtukufu' ilianzishwa wakati wa awamu ya pili.
Okay, ila ikaishia hapo hapo. Wakati huo Mzee Waryoba alikuwa akihudumu; kwanza kama PM na baadaye Waziri wa TAMISEMI. Kwa hiyo kwenye utawala huo walianzisha kuitana Mtukufu, mbona anapiga kelele kuhusu Mheshimiwa?
 
Waheshimiwa walikuwa zamani sio hawa wa siku hizi kwani 'wengi wao' hata matendo yao ndani na nje ya mjengo hayana maadili.
Angalia hata miswada waliyotunga hasa kipindi cha 'huyu mtu' ni hovyo na isiyo na tija kwa wananchi zaidi ya ukandamizaji.
Wamebaki kutetea matumbo yao na sio ya jamii iliyowapeleka huko!
Nashauri waitwe NDUGU kama zamani kama hawataki waache huo ubunge waje mtaani tupambane na hali zetu,
Naunga hoja yako mkono kwa 100%
 
Hapa umeongea ki emotional zaidi.
Mbunge Hana thamani mbele ya mjeda labda hao Askari wanaowabambikizia kesi.
M jwtz ni mtu mkubwa Sana.
Mbunge hawezi pigiwa salute na mjeda hujui unachokiongea Ila DC rc anasalimiwa
Hivi una akili kweli mpaka leo hujui kwamba hata jwtz ni askari pia !!!?
Mwanajeshi ni neno linatokana na maneno mawili yaani Mwana+Jeshi=Mwanajeshi
Majeshi ni kama Jwtz,Polisi,Magereza nk
Hivyo tuna tuna wanajeshi wa jeshi la wananchi(jwtz) Wanajeshi wa jeshi la polisi(Polisi) Wanajeshi wa Jeshi la Magereza (Magereza) nk
Wote hao wanaitwa askari hivyo hakuna utambulisho unaitwa sijui mwanajeshi bali wanatambulika kwa kuitwa Maafisa/Askari.
Nikimaanisha Afisa ni askari mwenye cheo kuanzia single star begani na askari ni rank and file yani kuanzia Private/constable/Wdr mpaka Rsm kama sijakosea
Nimekupa elimu uelewe uelimishe na wengine Soma katiba ibara 147 na ibara zake ndogo zote
 
Okay, ila ikaishia hapo hapo. Wakati huo Mzee Waryoba alikuwa akihudumu; kwanza kama PM na baadaye Waziri wa TAMISEMI. Kwa hiyo kwenye utawala huo walianzisha kuitana Mtukufu, mbona anapiga kelele kuhusu Mheshimiwa?
Better late than never, sioni ubaya wowote hapo kwani alichosema ni jambo la maana.
 
Nakumbuka wakati wa Mwalimu hakukuwa na neno Mheshimiwa kwa mtu yeyote, viongozi wote walikuwa wakiitwa Ndugu kasoro Rais ambaye alikuwa pia akiitwa Mtukufu Rais! Baada ya Mwalimu Nyerere kutoka madarakani, ukaibuka mjadala Bungeni Wabunge wakitaka waitwe Waheshimiwa (Honorable). Mwalimu alipinga lakini wakamwambia mbona Uingereza wanaitwa Honorable. Wakapitisha sheria wakaanza kuitana Waheshimiwa. Siyo wakati wa akina Waryoba kweli?? Tafuta wazee watukumbushe. Ila wakati Waryoba ni PM Rais wake alikuwa akiitwa Mtukufu Rais, na Mzee sikumsikia akisema kitu kwa kuwa labda alikuwa na kitu.
Si kweli kuwa hapa Tanzania Rais alikuwa akiitwa Mtukufu! Ni Kenya Rais Mzee Kenyatta alikuwa akiitwa Mtukufu lakini hapa Tanzania tulimwita Ndugu Rais Nyerere.
 
Back
Top Bottom