Mzee Zahiri Ally Zoro Akiwa Na Watoto Wake

Ila hiyo picha ya kuchora kwenye background mmmmh! Nadhani ni mchoro tu,vinginevyo ningehisi Mzee ni devil worshiper.
 
Namkumbuka sana akiwa na band ya JK Kimulimuli jazz ikiwa Mafinga, Iringa then alikuja Dar wakiwa na babu Seya na band yao ya Orchestra Sambulumaa, sijui hi picha na wanae ni enzi akiwa Iringa au Dar. Long live brother Zahil Alli Zorro, tukiwa wadogo tulikuaga tunashindwa kutamka jina lako la Zahir badala yake tulikua tunaita Zaire Ali, nilijuaga wewe ni Mzaire (sasa Congo ya Kinshasa ) kumbe wewe ni Mmanyema/Muha wa Kigoma.
 
By the way,Wamanyema asili yao ni Congo.

Ule mtaa wa Manyema uliopo jijini Dsm uliitwa hivyo maana ulijaa Wamanyema,wengi wao walikuwa ni watumwa/wapagazi kutoka Congo. Si unajua kuna mtaa pia unaitwa Congo street jirani kabisa na Manyema street?

Diamond Platnumz naye ni Mmanyema na ndo maana Diamond alipofanya 'collabo' na Koffi Olomide ,Mama Dangote (mamaye Diamond) alisema kwamba hiyo ni collabo ya mtu na mjomba'ake,akimaanisha wao pia kihistoria wanatoka Congo.

Originally,Zahir A. Zorro is from Congo. A home of music.Kule ambako waasi hubeba bunduki mkono wa kulia na gitaa mkono wa kushoto.
 
SIFA ZA KIJINGA.
 
Thanks brother for the nice history, gained something, this is JF bwana.
 
Huyu Mzee sugu namkubali sana.Hasa ule wimbo wake 'Photo album' akiwa na Kimulimuli Jazz Band.

Ananifurahisha zaidi anapoutaja mji wa Mwanza na viunga vyake (Nyamanoro,nk). Nikiusikiliza huwa napakumbuka sana nyumbani.
Hiv nyimbo za Kimulimuli zipo youtubes? Najua za Sambulumaa zipo na nime download kadhaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…