"Mzoea vya kunyonga vya kuchinja Haviwezi". Hongera Halima Mdee na Makamanda wote kwa kugomea wito wa kienyejienyeji

"Mzoea vya kunyonga vya kuchinja Haviwezi". Hongera Halima Mdee na Makamanda wote kwa kugomea wito wa kienyejienyeji

KUTOKA OFISINI KWETU KIGOGO2014

👁️‍🗨️Baada ya kuwapasua na mipango yao ya maandamano kesho, jioni hili li Halima na kundi lake wameshauriwa na TISS kuwa waandike barua kuomba CC ya Chadema ipeleke muda mbele wa kuwasikiliza kwa siku 5 zaidi

👁️‍🗨️Mnyika, hawa dada zako wameshajipanga na TISS kwenda mahakamani jumatatu kuzuia msiwajadili na msiwafukuze mpaka miaka mitano ipite..
👁️‍🗨️Hizi ndizo habari za saa hii ikutoka ofisi ya Diwani na hayo ndiyo waliyoyapanga
👁️‍🗨️ Halima ni boya sana yaani mabarua yote 19 yametumwa mara moja, how come watu wote 19 mna kuwa na excuse moja ya kutokwenda kikaoni

👁️‍🗨️tuliwaambia nyie ni maarufu mkiwa ndani ya Chadema lakini nje ya chadema ninyini kama kima tu..
👁️‍🗨️yaani kikao kesho kiko palepale na ndo mtajua kama chama kina nguvu au hayo maujinga yenu na Diwani ndiyo yana maana
👁️‍🗨️Diwani ni bogus tu hajawahi kuwa smart nyie mnamsikiliza😁

Asa mzee pascal unawaita mataga wenzako makomando.. emb mwachie Lady jaydee tu hilo jina
Paskal mayala kaenda kwa mdee kuchukua pesa eti aje kuwatetea mitandaoni njaa mbaya sana
 
Waliosema samaki hukunjwa angali m'bichi hawakukurupuka wajomba..

Haya sasa lisamaki limeshakauka hilo hapo mkunje kama anakunjika tena.. Too late.
 
Hawatakiwi kwenda kwa sababu hawatatendewa haki. Tayari ishara za kutokutenda haki zinaonekana.
Wao wasiwe watabiri huko Bungeni mbona hawakutabiriwa walikwenda kama wachawi , nasikia juzi makada wa CCM walijilia mmoja wamepata wachumba wapya ccm hata Paskal mayala kalala kwa mdee ndiyo maana kaamua kuja na uzushi wake uliojaa mifano ya kipumbavu mitupu
 
Halima Mdee amesema hadharani kuwa wamepata baraka za Chama chini ya uongozi wa Mbowe. Lakini, Mbowe hajatoka hadharani kukanusha hilo. Kwahiyo, simple logic ni kuwa Mbowe anaunga mkono wabunge hawa kuapishwa.

Mengine yanayoendelea ni kuwalaghai tu wanaharakati. Ni sawa na kumuahidi mtoto peremende ili aache kulia.
Mbowe siyo CHADEMA
 
Chadema wakubali yaishe. Walishiriki uchaguzi ili wapate kura .Wamepata wabunge 20.Si haba wawape ushirikiano wawashe moto bungeni. Waendelee kujenga chama. Na waongee hoja bungeni. Maana huku nje wakiongea wanaitwa wachochezi.

Umenena logic sana mdogo wangu!
Wenyehekima watayaishi maono yako!
Hao watu ni wazuri kufikisha hoja za wananchi na kujadili mstakabali wa Taifa.

Sisi kama wanachama hatuo sababu ya kuendeleza malumbano yasiyo na tija.
Siasa ni ujira na wao washaula. Tuache roho za korosho
 
Umenena logic sana mdogo wangu!
Wenyehekima watayaishi maono yako!
Hao watu ni wazuri kufikisha hoja za wananchi na kujadili mstakabali wa Taifa.

Sisi kama wanachama hatuo sababu ya kuendeleza malumbano yasiyo na tija.
Siasa ni ujira na wao washaula. Tuache roho za korosho
Roho za korosho wanazo akina Mdee waliopora ubunge kwa njia za kihuni na kuwaacha list husika iliyokuwa imepitishwa na kamati kuu
 
Huu ni msemo wa Kiswahili kuwa Mzoea Vya Kunyonga, vya kuchinja haviwezi! Chadema ilizoea kuwanyonga wanachama wake kwa kuwafukuza kienyeji enyeji na kujinga jinga, nimeisoma taarifa hii kwa faraja.

Halima Mdee ni mwanamke shujaa, msomi na mwanasheria, anaijua katiba ya Chadema, na vikao vya mamlaka ya nidhamu ni kama ifuatavyo.
  • Kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA, ili kumvua mtu uanachama kuna mlolongo wa kanuni na taratibu za kufuatwa na miongoni mwake ni hizi nitakazo ziorodhesha hapa chini, jee zilifuatwa?
  • Kuandaa Hati ya Mashtaka kwa maandishi yenye tuhuma zote ambazo mtuhumiwa anakabiliwa nazo. Jee hati hizi za mashitaka kimaandishi ziliandaliwa?
  • Hati hiyo ya mashitaki kimaandishi inatakiwa ikabidhiwa kwa mtuhumiwa kwa "despatch" ili kuthibitisha imemfikia. Je, hili lilifanyika? Nimesikia kuna watu waliitwa kwa simu, je huu ndio utaratibu kwa jambo zito kama hili?
  • Mtuhumiwa atatakiwa kuzijibu tuhuma za mashitaka hayo ndani ya kipindi cha siku 14 tangu tarehe aliyopokea barua ile ili apate muda wa kutosha kutafakari, je hili litafanyika?
  • Baada ya majibu ya hati ile ya mashitaka kurejeshwa, ndipo mamlaka ya nidhamu ingepaswa kuitisha kikao rasmi kwa mujibu wa katiba na kumwalika mtuhumiwa kwa barua ili kuwapa nafasi ya kujieleza na kumsikiliza kabla ya kufikia maamuzi!. Jee this time Chadema itafuata taratibu?
Halima na genge lake they are very right, Chadema ilizoea kufanya mambo kienyeji, leo imekutana na kisiki cha mpingo!
Chadema sasa lazima ijifunze kufanya mambo kwa kufuata katiba yake, sheria, taratibu na kanuni!, kufanya mambo kwa kienyeji enyeji kwa mtindo wa zimamoto, sasa basi!

Hongera sana Kamanda Mhe. Halima Mdee na makamanda makomandoo wa kike kwa kuifunza nidhamu chama chenu cha Chadema.

Paskali
Kuna kitu kinaitwa pyrrhic victory.

Tuseme wakashinda yote hayo unayosema na wakabaki kuwa wabunge kwa juhudi za makada wa CCM na viongozi wa serikali watakuwa kweli na legitimacy ya kujiita wapinzani mbele ya kadamnasi? Baada ya miaka mitano kumalizika watarudi tena kuomba uteuzi wa chama chao walichokipigania kwa damu na machozi ili wapewe dola na kama itashindikana waweze kuisimamia serikali?

Mtu shupavu na mwenye mapenzi na chama chake angeendelea kupigania msimamo wao ndani ya chama chao. Hizo nafasi zingebaki wazi maana Spika na NEC hawana mamlaka ya kuteua watu kutoka kwenye vyama vingine. Kwa kufanya walivyofanya wameonyesha umma kuwa wao wanajiona wako juu ya chama chao kwa kuamini kuwa hamna ambacho wanaweza kufanywa. Aidha, wamewapora wanachama wenzao wa kike ambao walipigania nafasi hizo na walishinda na hivyo walistahili uteuzi kuliko baadhi ya hili genge.

Kwa kusema ukweli wameonyesha umimi uliopitiliza na wakae wakijua kuwa wale wanaowakumbatia wakati huu watawatema pale watakapoacha kuwahitaji. Na itakapotokea hivyo, hamna ambae alikuwa pamoja nao kwa hali na mali wakati wakipambana kutetea maslahi ya wananchi atakaewaonea huruma. Miaka mitano sio mirefu sana.

Amandla...
 
Chadema wakubali yaishe. Walishiriki uchaguzi ili wapate kura .Wamepata wabunge 20.Si haba wawape ushirikiano wawashe moto bungeni. Waendelee kujenga chama. Na waongee hoja bungeni. Maana huku nje wakiongea wanaitwa wachochezi.
CHADEMA wao wanajiona ndio machampioni wa haki za wanawake mpaka katika ilani waliwawekea kipengele cha kuwafunga jela waume halali wa ndoa kwa hoja kuwa wanabaka wake zao. Wawaache wakapiganie hizo haki za wanawake bungeni
 
Huu ni uchochezi kusema kweli. Hivi kwa nini watu hipenda nyumba ya jirani isiwe na amani au isiendelee?
Kama utaratibu umekiukwa na katibu mkuu kasimamia hii hoja ya ukiukwaji huo si ingekuwa jambo jema kujenga hoja kuwa utaratibu haukukiukwa kwa vigezo halali?
 
CHADEMA wao wanajiona ndio machampioni wa haki za wanawake mpaka katika ilani waliwawekea kipengele cha kuwafunga jela waume halali wa ndoa kwa hoja kuwa wanabaka wake zao. Wawaache wakapiganie hizo haki za wanawake bungeni
Haki za wanawake zipiganiwe na list ya wanawake waliokuwa wamepitishwa na kamati kuu siyo hiyo list ya kugushi iliyotengenezwa na mdee kihuni
 
Huu ni uchochezi kusema kweli. Hivi kwa nini watu hipenda nyumba ya jirani isiwe na amani au isiendelee?
Kama utaratibu umekiukwa na katibu mkuu kasimamia hii hoja ya ukiukwaji huo si ingekuwa jambo jema kujenga hoja kuwa utaratibu haukukiukwa kwa vigezo halali?
CCM inafagilia ukiukaji wa taratibu huko chadema ili kesho waje kusema chadema inaendeshwa kihuni katibu mkuu hana nguvu yupo chini ya Bawacha, kutetea uvunjifu wa Kanuni ni upumbavu ulioje
 
Back
Top Bottom