Naamini Mungu yupo ila nashindwa kuuelewa ukamilifu wake, labda muendelee kunifunza

Naamini Mungu yupo ila nashindwa kuuelewa ukamilifu wake, labda muendelee kunifunza

:::::MKUU MBAKASO NDIO MUNGU WA WABANTU MKUU.....!!!!TATIZO WABANTU MMEKIMBILIA DINI ZA WAGENI WAKOLONI
Kwani kila mbantu anasali? Mbona hatumsikii huyo mbakaso. Waafrica wamepotea sababu ya ulevi wa kupindukia bangi uzinzi kujifanya wajuaji ufisadi tamaa na ushirikina tu.
 
Hayo ni maneno tu, ndiyo maana huwezi hata kuthibitisha kwamba huyo Mungu yupo, achilia mbalia aliamuru chochote.

Ukibisha, thibitisha huyo Mungu yupo.
Kithibitisho ni jiangalie wewe hapo na mazingira yako nd unachoweza kupata mpagani. Ila watu wa Mungu wanamuona mbona na wanamthibitisha hata katika maisha yao ya kila siku ila dunia imewadeceive vitu mnvyopenda kuona nd vya maana.
 
Kithibitisho ni jiangalie wewe hapo na mazingira yako nd unachoweza kupata mpagani. Ila watu wa Mungu wanamuona mbona na wanamthibitisha hata katika maisha yao ya kila siku ila dunia imewadeceive vitu mnvyopenda kuona nd vya maana.
Hujathibitisha Mungu yupo. Unabwabwaja tu.

Mpagani anaamini Mungu, mimi siamini Mungu.

Wewe ni ngumbaru hata hujui mpagani ni nani.
 
Kwa hiyo Bora uamini Wikipedia ambao Ina magoli ya Ronaldo mpaka ya Jana. Au Bora uamini kitabu ambacho hujui kimeandikwa na Nani au lini, na kinatetea utumwa, uuaji, kinasema dunia ni flat, kinasema mvua Ni madirisha ya mbinguni kufunguliwa. Bora uamini kipi Sayansi ambayo ilimpeleka mzungu mwezini au dini aliyotumia kukutawala na yeye kaiacha huku waafrica wakiendelea kuumizana na kuibiana makanisani
Thibitisha kama dini ya kikristo imetetea utumwa kwa vifungu tuone hapa. Na wapi imeandikwa dunia ni flat. Wapi bible imesema tuibiane makanisani.
 
Hujathibitisha Mungu yupo. Unabwabwaja tu.

Mpagani anaamini Mungu, mimi siamini Mungu.

Wewe ni ngumbaru hata hujui mpagani ni nani.
Sasa kwenye bible mpagani ni mtu ambae haamini katika Mungu wa kweli na kajitengenezea miungu yake kwa mfano masanamu mali au hata maarifa yasio sahihi. Kwahyo hapo wewe ni mpagani kutokana na bible. Na ungeweza kutumia kauli ambayo kristo anataka kutojiona bora kuliko wenzio na kutowadharau ningeona una mantiki hivo inathibitishwa kuwa ukisoma bible vizuri utasafishika roho na kuweza kuwasaliana na jamii yoyote ile haijalishi mtazamo.
 
Sasa kwenye bible mpagani ni mtu ambae haamini katika Mungu wa kweli na kajitengenezea miungu yake kwa mfano masanamu mali au hata maarifa yasio sahihi. Kwahyo hapo wewe ni mpagani kutokana na bible. Na ungeweza kutumia kauli ambayo kristo anataka kutojiona bora kuliko wenzio na kutowadharau ningeona una mantiki hivo inathibitishwa kuwa ukisoma bible vizuri utasafishika roho na kuweza kuwasaliana na jamii yoyote ile haijalishi mtazamo.
Nakupeleka ignore list, hujafikisha viwango vya kujadiliana na mimi.

Wewe unaniona mimi mpagani, mimi nakuona wewe mburula ngumbaru guluguja gubegube.

Kuanzia hapa sitaona posts zako.
 
Duuh...mkuu kumjua Mungu kuna changamoto sana.

Hii ni kwa sababu hadithi nyingi za vitabu vitakatifu hazishabiliani kwa kiasi kikubwa(yaani kwenda sambamba).

Mfano : Biblia inamsema shetani kuwa alikuwa miongoni mwa malaika waliokuwa wanamwabudu Mungu mbunguni, lakini wewe unasema kwa mujibu Qur'an shetani alikuwa Jini na siyo malaika.

Kwa mujibu wa Biblia hakuna mahali panaelezea kuwa shetani aliomba msamaha bali inainesha tu kuwa yeye alikosea mara moja na kuhukumiwa pale pale wala hakuwa nafasi ya kujutia makosa, lakini wewe unasema kwa mujibu wa Qur'an shetani hakunyimwa fursa ya kutubu bali aliendelea kuwa na kiburi.

Mpaka hapo unaweza kuona namna gani vitabu vyetu vya dini vinatuambia stori tofauti kana kwamba kuna zaidi ya Mungu mmoja sijui ?

Sasa mimi nikuulize tena maswali haya mawili yafuatayo :

1.Kama shetani alikuwa akiishi Mbinguni na alikuwa akimwabudu Mungu kabla ya kuasi,Je ina maana tuseme makao ya majini huwa ni mbinguni siyo duniani na wao pia wamwchangamana na malaika wapo huko Mbinguni kumwabudu Mungu ?


2.Je, shetani akiamua hivi sasa aache kiburi na kurudi kwa Mungu kumwomba msamaha,inawezekana akasamehewa na jehanam kufutwa ?
vitabu vya dini vinafanya kua mfuasi wa dini na si kufahamu ukweli kila mmoja na stori zake.

Inabidi kutembea wenyewe kujionea haya masuala ya kwamba moto ulishuka ukafanyaje mara nini sijui.

MUNGU yupo na sipingani ila haya niko against hizi mambo zingine na nasoma biblia kama kitabu kuongeza maarifa na kufahamu ukweli zaidi na ningefahamu kiarabu quran ningekua nayo sambamba.
 
Ila kwenye story ya Job shetani alikuwa mbinguni na Mungu wakibet
Ndiyo alikuwa anaenda na baadhi ya malaika alikuwa ni rafiki yao mzuri tu na hawakuamini kam kiongozi wao kahasi mpaka alivofanya shambulio kwa masihi ndipo akanyang'anywa mamlaka zote na hawezi fika mbinguni tena. Lakini pia alikuwa akienda tu sio kwamba aliishi huko au kuwa na mamlaka maan alikuwa ashakula kipigo na Michael asingeweza mruhusu tena kule.
 
Nakupeleka ignore list, hujafikisha viwango vya kujadiliana na mimi.

Wewe unaniona mimi mpagani, mimi nakuona wewe mburula ngumbaru guluguja gubegube.

Kuanzia hapa sitaona posts zako.
Pole mkuu ungemjua Yesu usingekuwa na hasira na mitazamo ya watu kiasi hicho. Sasa upagani na matusi ulioandika ni kipi kibaya hapo. Mungu aje akufungue macho aisee.
 
Mwili wa Binadamu na nature ya viumbe hai Inaelezeka na evolution and origin of species. Hii mada ishamalizwaga. Ndo maana huwezi ona mtu wa dini anaongelea mwili watu wanaongelea uumbaji wa ulimwengu. Soma kitabu Cha Darwin utaelewa hizo system zote Ni mechanisms za nature.
Mbona hiyo nayo haiwezi kuthibitishika kwanini tuiamini kuliko dini?
 
Wakuu poleni kwa upambanaji.

Binafsi mimi kuna mda huwa nikitulizaga kichwa changu huwa naanza kujiuliza maswali mengi sana kuhusu mimi (binadamu) na ulimwengu kiujumla (Universe).

Maswali kama sisi (binadamu) ni kina nani,tumetoka wapi asili yetu, kwanini tupo (dhumuni la kuishi), mwisho wetu ama hatima yetu ni nini, Ulimwengu wa vitu je kama sayari, nyota, galaxies zimekuwepo vipi na nini hasa mwisho wake.

Hapo juu ni baadhi tu ya maswali ambayo huwa naiuliza sana akili yangu ikiwaga katika hali ya utulivu.

Lakini cha kusikitisha ni kwamba, katika maswali yote hayo ambayo huwa najiuliza, sijawahi kupata jibu la uhakika kuniridhisha kuhusu hayo maswali yangu.

Nimekuwa nikifanya bidii kubwa sana kupata majibu ya maswali yangu kupitia usomaji wa majarida au vitabu vihusuvyo historia,sayansi, dini na Falsafa lakini kote bado sijapata majibu ya kuniridhisha tofauti na kuambulia majibu ya kinadharia tu ambayo yana strength kiasi chake lakini pia yana weakness sehemu nyingi tu.

Na nikiri wazi tu kuwa katika usomaji wangu wa nadharia hizo zote (historia, sayansi, dini, falsafa) sehemu ambayo nimeanza kuiamini kunipa majibu ya maswali yangu ni kwenye DINI.

Nikiwa na maana nimeanza kuamini kwamba uwepo na sisi tuliohai na visivyo hai hapa ulimwenguni ni matokea ya Uumbaji ya nguvu kubwa sana inayoitwa MUNGU/ALLAH kama ambavyo dini nyingi zinaelezea nguvu hiyo.

Na leo maswali yangu yanajikita huko kwenye hiyo nguvu (Mungu) maana nimeanza kuiamini lakini pia kila nisomapo BIBLIA (mimi mkristo) inanipa maswali chungu nzima.

Sasa leo swali langu limejikita kwenye UKAMILIFU wa MUNGU.

Naombeni wasomaji mnielewe kuwa sina maana ya kukufuru (maana mara nyingi niulizapo maswali kuhusu MUNGU huwa naambiwa nakufuru) bali mimi nataka kujifunza zaidi kumuhusu huyu Mungu.

Dini nyingi (hasa Ukristo na uislamu) zimekuwa zikimwelezea Mungu kuwa ni Mkamilifu sana,mwenye nguvu nyingi sana, uwezo na akili zake hazichunguziki, hashindwi na chochote n.k.

Je hilo lina ukweli ? kupitia Biblia mimi nimeanza kudhani kwamba huenda kweli Mungu ana nguvu nyingi sana ila siyo zote, ana uwezo mkubwa sana ila siyo uwezo wote,ana maarifa mengi sana ila siyo maarifa yote, ana ukamilifu mwingi sana ila siyo ukamilifu wote n.k

Nasema haya ni kutokana na maswali yafuatayo :

1. Kama Mungu ana ukamilifu wote, kwanini sasa alimuumba malaika (Lucifer/shetani) alafu badae akaja kumuasi?
Kama Shetani/Lucifer aliasi maana yake ni kwamba Mungu alimuumba huyu kiumbe akiwa na madhaifu kadhaa na ndiyo maana alishindwa kuitii amri/mamlaka ya muumbaji wake.

Kama Mungu angelikuwa na ukamilifu wote, basi malaika wote wangelikuwa wameumbwa katika namna ya utii pekee, uasi usingetokea na huo uasi unadhihirisha kwamba Mungu aliwaumba hawa malaika wakiwa na udhaifu flani, hawakuwa na uimara wote.

2. Uumbaji wa Eva (Hawa) unaonesha kulikuwa na madhaifu pia.
Katika Biblia takatifu kwenye kitabu cha mwanzo, kuna mistari inaeleza kuwa "Mungu alimpa usingizi mzito Adam, alafu akabandua sehemu ya ubavu wake na kumfanya/kumuumba mwanamke (Hawa/Eva)".

Alafu Mungu akamwambia Adam kuwa huyu mwanamke atakuwa msaidizi wako

Lakini ni huyo huyo mwanamke ambae shetani (kwenye umbo la nyoka) alienda kumdanganya akachukua matunda ya mti walioambiwa asile yeye akala na akampelekea na mumewe (Adam) pia akala.

Lakini Mungu alivyomuuliza Adam kwanini umekula matunda ya mti ambao nilikwambia usile, Adam alijibu kuwa "Ni huyo mwanamke uliyenipa ndiye aliyeniletea nikala".

Tukio hili linadhihirisha kuwa Mungu alimpa Adam msaidizi (Hawa) ambae ni dhaifu sana na ndiyo maana alisababisha dhambi ikaenda hadi kwa Adam.

Na huenda kama Mungu angelikuwa amempa Adam msaidizi imara asiye na madhaifu basi ile dhambi ya kula tunda ingeepukika.

Uko wapi sasa ukamilifu wote wa Mungu ikiwa aliweza kuwaumba malaika dhaifu (ambao walikuja kumuasi) na pia bado akampa Adam msaidizi dhaifu kabisa ambaye alisababisha dhambi imwendee hadi Adam?

Kwa leo naombeni comment zenu zinifunze kuhusu hilo tu (La ukamilifu wa Mungu) alafu mengine nitauliza siku nyingine, na mengine nitakuwa nauliza humo humo kwenye comments zenu.

NB: Naamini Mungu yupo, kutokana na baadhi ya vitu ninavyoviona ulimwenguni (hasa uumbaji/creation) ambapo kuna baadhi ya vitu hasa sayansi inakosa majibu ya kuridhisha, ila shida yangu kubwa ni sifa za Mungu ambazo anapewa na wanadamu naona kama zinashindwa kujidhihirisha kwenye baadhi ya mambo.

Karibuni mnifunze.
Pole sana kiongozi
Pole kweli kweli
Endelea kujifunza utafikia ujuzi
 
Hata hao walioandika hayo mambo they were trying to explain the power that created the universe so they are not full correct.


Ila hayo mambo mengine ni kutishana tishana tu tena pengine ni kwa maslahi binafsi
Kwa maslahi ya nani wakati bible haijamkweza mtu wala kumshusha mtu. Ila binadamu wote ni sawa kwa kila nyanja. Kwanza unaelewa hata upendo maana ake nn.
 
Hatujui kwamba Mungu yupo. Kwa sababu zamani watu walisema upinde wa mvua Ni msamaha wa Mungu Ila Leo hii hata wewe unaweza tengeneza upinde wa mvua. Walisema mvua Ni maji yanayomwajika kutoka madirisha ya mbinguni. Lakini hata wewe ukipika unaweza una process ya condensation. In short kitu usichokijua ndo unampa Mungu. Inaitwa God of the Gaps. Na hizi gaps zinaendelewa kuwa filled kila siku na wanasayansi mwishowe utakosa pa kumficha huyo Mungu wako. Na jicho kuwa complex hainiambii kwamba Mungu Ni Allah na anataka nisali nikiangalia mji wa waarabu. Kusema Mungu yupo na Mungu Ni Allah au yahweh Ni vitu 26 tofauti.
Kwahyo kwasababu upinde wa mvua iliwekwa kama alama nd we unaona ina maanisha kuwa ulianzia siku hyo. Kwan mtu anavosema naweka jiwe la mpaka wa tanzania na kenya kweny kipande cha ardhi hichi hapa nd inamaanisha hicho kipande cha ardhi kimetokea siku hyo hyo? Hujui kwamba kila kitu kilishaumbwa tangu mwanzo kila unachokiona. Hujui Mungu anatoa maagizo na miujiza na maajabu kutokana na demand ya vizazi fulani.
 
Kama Mungu anapenda tumtii bila shuruti kwa nini alitupa uwezo wa kufanya mabaya na kutenda uovu ambao yeye unamchukiza?

Alishindwaje kutuumba tuwe tunafanya mema na mazuri tu kama atakavyo yeye??

Ana uwezo wa vyote kweli huyo Mungu??
Kujua kuhusi mabaya tulijitakia hujui kua Adam kabla ya kula tunda mema na mabaya alikuwa hajui lolote kuhusu mabaya. Mabaya ni adhabu ya kutomtii aliekuwa anajua mabaya ni shetani nd aliewashawishi wanadamu wale tunda la mema na mabaya.
 
it's said that kabla ya mtu kuumbwa mungu mwenyewe anakuwa anajua hatima ya kila mtu kuwa ni wa peponi au lah hata kabla hajaumbwa, si ndio?
Kwani mwalimu akijua kuna kilaza darasani akatoa mtihani na akajua fulani atafeli hyo ina tafsiri gani na influence ya mwalimu juu ya mwanafunzi huyo?
 
Sasa kwa nini hapendi wanaofanya mabaya?

Na uwezo wa kuyaondoa hayo mabaya alikua nao,

Utambuzi wa sisi kujua mema na mabaya ni dhahiri kwamba Mungu alipanga tufanye yote mema na mabaya.

Kama hapendi sisi tufanye mabaya asinge tupa utambuzi na ufahamu wa kutenda mabaya.

Labda useme kwamba anapenda mema na mabaya..
Hakupanga tujue mema na mabaya ndugu. Mema na mabaya ni adhabu ya uasi wa kwanza kuwa usile tunda la katikati ya mti.
 
Hayo mabaya kama hayapendi yeye si Mungu muweza wa vyote, Alishindwaje Kuto kuumba Dunia isiyo na mabaya??

Mabaya ambayo humsababisha mwanadamu ayafanye...
Mabaya ni adhabu kwa kuasi kwasababu mabaya yote adhabu yake ni kifo.
 
mimi nipo mwanza but i've got your point. Mkuu naongelea hatima ya mtu either jehanamu au peponi na kwa mfano wako umeongelea kupajua tu kwa majina na sio kufika au kupapitia


Kumbuka mungu ndio muumba sio tupo under him kabla hajakuumba anajua wewe ni wa jehanamu tu so huwezi change na ikitokea yeye alijua kuwa ni wa jehanamu ila ulipozaliwa ukatumia maombi kama ulivyodai ukaenda peponi hapo tunaiterm kama alikuwa hajui maana yeye kabla haujazaliwa alijua wewe ni wa jehanamu but umebadilisha ukawa wa peponi kwa maamuzi yako but something that's impossible


Hauwezi kuchange hatima anayoijua mungu since he is your designer you can never go beyond his expectations buddy!
Hapa kuna vitu viwili unachanganya kati ya view ya Mungu kwa wanadamu na view ya binadamu kwa Mungu. Kwa Mungu dini ni hukumu yako wewe yani ukiadhibiwa usije lalamika kuwa umeonewa(harsh but nd reality) ila kwa mwanadamu dini ni zawadi ya kuweza kumjua Mungu wa kweli na pia uwe na idea ya kitu gani utakutana nacho katika hukumu lakini hujui siri hiyo so inabidi ujifunze kufanya mema lakini bible imeweka wazi kuwa mtu muovu huongezewa uovu zaidi ili apotee it means kuwa destiny zetu Mungu anazijua. Sasa cha kufanya ni nini kama Mungu amekupa neema ya kufanya mema wewe jitahidi sana maan kuna watu it was over before it even started.
 
Lakini hamna kitu ambacho binadamu atafanya kinachostahili kuungua milele. Hii adhabu imewekwa na dini ili kuendesha watu. Hazikuwepo katika agano la kale. Ndo maana wanajua kwa hii adhabu wote mtakubali kuendeshwa na wanaosema dini imewafata wao
Swali ni je nani anatakiwa amuendeshe mwenzie according to bible? Usije ukachanganya interest za watu na mafundisho ya Mungu ndugu. There is no such thing kuendeshana kwenye neno la kweli nd maan Yesu mwenyew alikuwa masikini mtot wa fundi seremala(sio furniture ni seremala) hakuwa na gari wala meli za kisasa hakuwa na jumba la kifahali wala nyumba tu ya kuishi. Alikuwa anavaa nguo za kimasikini marafiki zake masikini ndugu zake masikini aliteswa na serikali na hakuwafanya chochote alijinyenyekeza mbele za watu wote leo hii unakuja kusema dini inataka maslahi ya watu emu lete vifungu hapa dini inambeba nani usilete story sijui za utumwa sijui nini sababu hao wakoloni hawakutumia dini peke ake. Kwann usiikatae sayansi pia ilitengeneza meli kubwa zinazoweza kufika vina vya kutisha kuzunguka dunia(Sayansi) , navigation systems( sayansi) silaha nzito( sayansi) baadae ndege(sayansi) kuna matumizi ya mawasiliano( sayansi) kuna uchimbaji madini(sayansi) kuna utengenezaji wa madini kwenye majengo yao kwa nakshi( sayansi) kuna kuweka masettelite ya kukusanyia data( sayansi) kuua wanyama wetu( sayansi) madawa ya kulevya( sayansi) mpaka mapinduzi ya technlojia simu janja ukoloni mpya( sayansi) kuchukua rasilimali watu zetu kwa kutamanisha mali zetu( sayansi) kuendeleza vita ya congo ili wapate madini ya kutengenezea simu na computer(sayansi) vita kubwa za dunia nuclear bombs na new technlogy zote(sayansi) uko hapa kushambulia maandishi kisa yamekukataza kuiba kuzini kusema uongo kusengenya kutukana wazazi na nyanja zote za kiujumla. Ushoga wenyewe ni zao la sayansi kupitia media za magharibi na siasa uchwara za shetani ila dini tu nd unaona imeiharibu africa. Sasa kwa akili hizo za mwafrica utalaumu dini kuwa kwann hujatoboa wakati hao unawasujudu wanahaha kuhakikisha watu hawafichui madudu yao yaliyojificha kweny hiyo mnaita sayansi. Muafrica umejitengenezea Mungu wako anaitwa pesa ambae nae huna nd maan unashadadia sayansi iliyokuvua nguo wewe na kuiacha dini iliyokuletea utu. Na kwa taarifa yako wamisionari sio wakoloni watu kama akina Paulo nchi kibao wameteswa kutangaza dini tu na watawala mbali mbali we chaganya mambo shetani akuchote. Endelea kushobokea sayansi iliyokuletea mashoga na uzinzi na uasherati(mitandao ya porn yote ni zao la sayansi) usengenyaji tamaa za kijinga sijui lamborghini sijui ferrari illusion tupu sijui story mwezini kwenye tambalo lako la utumwa linaitwa smart tv au smartphone mwisho wako ni moto tu.
 
Back
Top Bottom