Naanza kupata hofu na stress sana, nina miaka 32 na familia haitaki nioe mwanamke mwenye mtoto

Naanza kupata hofu na stress sana, nina miaka 32 na familia haitaki nioe mwanamke mwenye mtoto

.... masikini kuzaa sio kwa kushinsana ila ni jambo jema TULIA na chagua mbegu na baba bora
 
Hapa umepuyanga masta.

Ilikuwa hekima ungemuuliza kwanza mwenye mada yake amewazalisha wangapi ndiyo umshauri yeye akawaoe.nadhani ilikuwa vizuri zaidi ungewashauri hao waliozalishwa kwenda kuolewa na waliowazalisha kuliko kutaka kuolewa na wengine na kwenda kuwavurugia maisha yao.
Bado hajapuyanga maana wanaowafanya binti kuwa na maisha ya kitanda hakizai haramu ndiyo huyu kijana hapa.

Mwenyewe kasema alikuwa na wapenzi wa kutosha na hapo hajasema yupi kamtimua nayo?.

Me wengi sana wamewapachika mimba binti na wanawake kibao ila ikija suala la kuoa mnadai hawafai. Pum na mber fhu sn.
 
Huko mtaani hali ni mbaya sana,asilimia 70 ya wasichana ambao wako kwenye umri wa kuolewa wana mtoto 1 au 2...
 
Oa mwanamke uliyejiridhisha kuwa utaishi naye, hii biashara ya kuachia familia maamuzi juu ya mwanamke wa kuoa sio poa aseeeee.

Ukumbuke ni wewe utakayeishi naye. Ukifuata Kila wanalokuamulia wanafamilia ipo siku maamuzi unayotakiwa kufanya wewe kama baba wa familia yako utaachia wanafamilia wakuamulie.

Mbinu mojawapo rahisi ya kujua mwanamke wa kuoa fuatilia undani wa maisha ya pale alipolelewa /kukuzwa. Ukiona mama mkwe dishi limeyumba basi ujue bintiye ana asilimia nyingi dishi limeyumba pia.

Usioe mwanamke ambaye mnala ni wa voda halafu network inasoma tigo.

Usioe mwanamke kwa kumuonea huruma utakuja kujuta siku huruma yako juu yake ikifikia kikomo
 
Mwaka huu nafikisha miaka 32 sina mke aisee.

Wapenzi nilishakuwaga nao huko nyuma tulishaachanaga kwa changamoto za mahusiano kila nikitaka kuoa nakutana na mwanamke ana mtoto yaani familia yangu imeshanionya kuoa mwanamke mwenye mtoto..

Yaani hapa sielewi kazi ninayo kipato cha kati ninacho..
Unaoaje mwanamke mwenye mtoto wakati wasichana wabichi wamejaa,sisi wenyewe wenye ndoa tuna michepuko mabinti ambao hawajazaa wewe unashindwa nn,tembelea vyuo vya juu na kati hautakosa kijana.
 
Mwaka huu nafikisha miaka 32 sina mke aisee.

Wapenzi nilishakuwaga nao huko nyuma tulishaachanaga kwa changamoto za mahusiano kila nikitaka kuoa nakutana na mwanamke ana mtoto yaani familia yangu imeshanionya kuoa mwanamke mwenye mtoto..

Yaani hapa sielewi kazi ninayo kipato cha kati ninacho..


Pole Ila jitahidi ufanye hivi.

Kuwa na mpango au mipango kinachoendelea hapo ni kukosa mipango katika swala mahusiano .

Ukitumia umri katika kuoa utakosa mwanamke sahihi , maana utakuwa unapambana Sana kukimbizana na umri na sio kukimbizana na malengo na kukimbizana na umri huwa ni kazi ngumu Sana.


Ushauri .

Tumia kanuni inaitwa "act like you don't need it"

Jifanye Kama hautaji kitu -maana yake tumia mkakati wa kutafuta mwanamke kipindi ambacho wewe binafsi hauna uhitaji naye

Hii itakufanya kukutana na mwanamke ambaye sio singo maza na ,ambaye sio rejected .

Mwisho
Msongo wa mawazo utaweza kuoondoa endapo utasahu kuhusu umri wako na utakumbuka kuhusu malengo yako .

Kanuni ya "Act like you don't need it " ndo kanuni bora .
 
Back
Top Bottom