Naapa kuwa sirudii tena kumsaidia Mtanzania -- never!

Naapa kuwa sirudii tena kumsaidia Mtanzania -- never!

South Africa ya siku hizi ina watu wema hivyo? Yani umkute mtu analia uende kumuuliza analia nini unamsemesha kizulu then unagunduwa ni Mtanzania unampeleka kwako.

Konda tafadhali nishushe hapahapa nimefika, mwendo wa dereva ni hatarishi.
Mkuu hata majambazi watano wakija kwako, juwa kwamba kati ya wale watano kuna mmoja au wawili ambao watakuwa na moyo wa huruma kwako. Ndio pale unapokuta unapigwa na kuelekezewa mdomo wa bunduki kichwani kwako kwa lengo la kutaka utaje zilipo hela au mali au chochote wanachohitaji ndipo hapo utashangaa kati yao anatokea mmoja au wawili kumsihi yule anaepanga kukuuwa asikuuwe

Na hii ndio husababisha mtu anaibiwa kila kitu na kuachwa hai bila kupigwa au kuuwawa, japo unakuta wenyewe walikwenda pale kwa malengo mawili ya kuiba na kuuwa ili kupoteza ushahidi, ila mmoja kati yao anazuia mauaji ya muibiwaji na kusababisha wenzake wanaondoka bila kuuwa. Kwahiyo binadamu wote hatuwezi kuwa sawa, kuna wema na wabaya. Hapo sasa utaamua mwenyewe mimi uniweke katika kundi la wema au wabaya ila nilitumia utu kumsaidia na sikujua yatakayotokea mbele.
 
Pole sana, mungu atakuongezea ulipo pungukiwa. Saudia lkn uwe unawaacha wapatane wenyewe, na lazima useme wazi , hunjui.
Shukran kwa ushauri mkuu, hii imenipa funzo ambalo sikuwahi kujifunza hapo kabla.
 
Kuna thread pia humu ya biashara Commoro naskia wakijua wewe ni mtanzania wanakuogopa maana wanajua ni tapeli tu.
Wakomoro wapo tayari kufanya biashara na mkomoro mwenzao lakini sio mbongo.....

Nenda bandarini pale wanaofanya biashara comoro ni wacomoro wenyewe
 
Mr Dudumizi huyo mshikaji uliyemsaidia kupata kazi kauawa kwa kutolewa kafala/biashara ya viungo, na mkenya kasingizia kamuibia. Huyo mkenya hiyo itakuwa ni side business kwa ajili ya viungo etc. Muepuke huyo Mkenya hata wewe atakuja akuue auze viungo.
Dah aisee niliposoma hapa nimeshtuka kidogo maana kwa jinsi ninavyomfahamu huyu jamaa sifikirii kama anaweza kufanya biashara hiyo. Kwa hapa South Africa biashara ya aina hiyo inaweza kuwa ngumu kidogo kuifanya, ila hata hivyo nashukuru kwa ushauri wako na nitajaribu kumpeleleza jamaa ili kujiridhisha na ushauri huu.
 
Mtu haanzi wizi mkubwa hivyo mara moja tena nchi ya ugeni huwa wanaogopa. Jina lake ni nani? Weka na picha yake hapa. Na police taarifa mmetoa wakasemaje? Kama kweli imetokea huyo ni jambazi mkubwa sana na mwisho wake ni kifo tu. Hata hio story utakuta alitunga. Alikuwa south africa muda mrefu akakulia njari akijua ww ni mtz nk. Dunia ina mambo ya ajabu sana.
Huyu dogo alinambia yeye kwao ni kijitonyama opposite na sinza, jina lake ni Frank anadai kitaani alikuwa anatumia jina la chagosi. Picha sikuweza kumpiga kwani sikufikiria kuwa atayafanya aliyoyafanya. Jamaa alishatoa taarifa police, kwahiyo anatafutwa. Na kama kweli ni mgeni ninaamini atakamatwa tu maana atafika sehem ata stuck asijue pa kuelekea.
 
Habar zenu ndugu zangu. Ama baada ya salam ningependa kuendelea na kile kilichonifanya niandike uzi huu. Ndugu zangu kama ilivyo ada au kama tulivyofunzwa na misingi yetu ya Taifa kwamba watanzania popote tulipo haijalishi ni ndani au nje ya nchi, sisi ni watu wamoja. Kwahiyo kwa misingi hiyo sisi tulio nje huwa na desturi au utamaduni wa kusaidiana bila kujali tofauti zetu za kikabila, dini, rangi, jinsia au kanda ya mtu anayotokea ilimradi sote ni watanzania na tunatokea kwenye ardhi ya Tanzania basi ni ndugu.

Sasa basi miezi 3 iliyopita kuna kijana aliingia Kaburu akitokea bongo kwa lengo la kuja kutafuta maisha. Kijana anadai kuna rafiki yake wa kitaa, kwa sasa anaeishi Capetown ndio alimshawishi kuja maisha haya, lkn alipoingia tu "Kaburu" yule rafiki yake akamzimia simu na kumkosa kabisa online.

Kijana akachanganyikiwa asijue wapi pakwenda wala nini cha kufanya. Nikiwa katika mizunguko yangu mitaa ya park station Johannesburg, ghafla nikapita sehem na kumuona kijana akiwa kajiinamia na begi lake huku machozi yakimtoka. Nikamsogelea taratibu na kujaribu kumuuliza kwa lugha ya wenyeji, ghafla nikasikia jamaa akiongea kiswahili, hii ikanipa nguvu ya kumsogelea na kumuuliza zaidi baada ya kugundua kuwa naongea na mtu anaetoka nchini kwetu. Baada ya maongezi ya hapa na pale nikagundua kuwa jamaa ameingizwa cha kike na mwenyeji wake, kwahiyo nikachukua jukumu la kumsaidia.

Nikaondoka na jamaa hadi nyumban, akaoga, akala, baada ya kula nikampa sehem ya kupumzika akalala. Kwa kuwa mimi nina familia ikanibidi niende kuongea na homeboy fulan ambae ni single ili ampe hifadhi ya miezi kadhaa wakati nikiendelea na mchakato wa kumtafutia shughuli ya kufanya, mshikaji akakubali lkn kwa masharti ya kumsaidia kulipa rent.

Kwa kuwa nilikuwa nimeamua kumsaidia kijana, basi nikaona poa tu acha nimsadie kulipa rent ili aweze kuishi nae. Kijana tumekaa nae mwezi wa kwanza, wa pili na sometimes nilikuwa naenda nae kwenye mishe zangu ili kumzoesha mazingira ya nchi, na mishe za hapa na pale. Mwezi mmoja uliopita kuna rafiki angu Mkenya ambae tuliwahi kufanya nae kazi huko Gezina, Pretoria.

Mkenya alikuwa anatafuta mtu wa kumuachia saluni yake kubwa na ya kisasa iliyopo nje kidogo ya jiji la Pretoria huko Nellmapius, kwa malipo ya R600 kwa week (sawa na sh elfu 85 au elf 90) kula na kulala bure. Kwa vile nilikuwa na kijana na tayari alishanambia kuwa bongo kazi yake kubwa ilikuwa ni ukinyozi, nikaona YES maji ya mvua yameangukia juu ya mgongo wa bata. Nikampanga kijana, kesho yake mapema nikampeleka mpaka Pretoria kwa yule Mkenya na kumkabidhi.

Kweli bwana baada ya siku mbili kijana akaanza kazi huku Mkenya akiniomba nimtafutie vijana wengine ambao wataenda kusaidizana nae, maana saluni ni kubwa ilihitaji vinyozi zaidi ya watano, lkn pia kijana lugha ni tatizo, so alitaka ambao wangeweza pia kusaidiana hata katika mambo ya lugha za wenyeji ili kuwateka vizuri wateja wa kizawa.

Nikamuahidi jamaa kumtafutia hao vijana. Wakati namuacha kwa yule Mkenya kijana wang nilimuachia sim kwa ajili ya mawasiliano yetu, au ndugu zake wa bongo, au boss wake (Mkenya). Dogo tukawa tunawasiliana ananipa taarifa za kazi na mimi nampa mpa moyo kuwa akomae ili atimize malengo ya kile kilichomleta hapa nk. Siku tatu zilizopita sikumpata online, nikajua labda simu imepata tatizo ghafla.

Sasa jana yule rafiki angu Mkenya amenipigia simu na kuniambia kuwa jamaa amemuibia kila kitu cha saluni, na hela ambazo yule Mkenya anaendaga kuzichukua kwa week jamaa katimka nazo. Simu yake haipiti na hatujui tutamtoa wapi. Nilipotaka kumlipa yule Mkenya nusu ya hasara ya vitu alivyoiba jamaa, Mkenya amkataa amesema nisijali kwa vile sio kosa langu ni kosa la mtu mungine kwahiyo mimi sistahili kumlipa na ukizingatia na rafiki yangu.

Hiki kitendo cha huyu jamaa kimenisononesha na kunivunja nguvu. Imenifanya sasa niwachukie wabongo wenzangu, maana hii ni mara pili sasa nawasaidia wabongo afu wanaharibu na kutimkia kusikojulikana, japo kwa huyu sikutegemea hata kidogo kutokana na upole na muonekano wake.

Najua binadamu tunatakiwa tusamehe, lkn kwa mikasa hii sioni sababu ya kusamehe kwa lengo la kurudi kumsaidia mungine labda yule nimjuae A to Z. Ndugu zangu wabongo tubadilike, hii dunia tunapita tu. Kumuharibia mtu anaekusaidia sio ujanja bali ni ujinga wa mwisho. Hii ni tahadhari nimetoa kwa vijana wengine kuwa makini sana. Asanteni


Pole sana mkuu

Walimwengu ndivyo walivyo. Yaliwahi kunikuta hayo kwa cousin yangu kabisa niliyemtaftia kazi sehemu niliyokua nasimamia.

Baada ya kuwataftia na wengine ambao anawafahamu yeye alianza kutoka na na watu tofautitofauti pale na kuwaambia huyu dada kila anayemtaftia kazi hapa ni ndugu yake kasoro mimi☺☺☺

Mambo ya kijinga yakaanza, anonymous mails ziliandikwa hq kunichafua ila uzuri policy ilikua inasema wazi ajira izingatie watu wanajulikana na watu wa ndani, na walioniajiri waliniamini

Nakumbuka niliapa kutomtaftia tena mtu yoyote kazi!!! Ila baadae niligundua roho ya mtu haibadilishwi na ubaya aliotendewa

Kikubwa tenda wema uende zako

Usiache kusaidia watu10 wenye shida na wasio na ubaya sababu ya mtu mmoja aliyeamua kuwa mjinga
 
Mimi siyo mnafiki na wala simwogopi mtu.

Lazima niseme ukweli.

Mbona hapo nimesema wakenya ni wezi na hujalalamika.
Sasa angalia muktadha wa uzi.. jamaa amewashutumu watanzania wote, wewe umekimbilia moja kwa moja kwenye wachaga ni wezi.. Totaly nje ya point
 
Sijui tunakwama wapi sifa zetu ni mbaya sana
Aliyetupumbaza alikuwa ni the late mwalimu na sera zake za ujamaa na kukumbatia lugha ya kiswahili kuwa ya Taifa
Ujamaa ni sera rahisi sana kuzalisha wavivu kama Raia hawakupewa elimu.
Watanzania tuna desturi ya kuchukulua poa , ndo maana unaweza kumsaidia mtu kwa nia njema tu ,na yeye akajiaminisha kuwa msaada huo ni haki yake kupewa
 
Habar zenu ndugu zangu. Ama baada ya salam ningependa kuendelea na kile kilichonifanya niandike uzi huu. Ndugu zangu kama ilivyo ada au kama tulivyofunzwa na misingi yetu ya Taifa kwamba watanzania popote tulipo haijalishi ni ndani au nje ya nchi, sisi ni watu wamoja. Kwahiyo kwa misingi hiyo sisi tulio nje huwa na desturi au utamaduni wa kusaidiana bila kujali tofauti zetu za kikabila, dini, rangi, jinsia au kanda ya mtu anayotokea ilimradi sote ni watanzania na tunatokea kwenye ardhi ya Tanzania basi ni ndugu.

Sasa basi miezi 3 iliyopita kuna kijana aliingia Kaburu akitokea bongo kwa lengo la kuja kutafuta maisha. Kijana anadai kuna rafiki yake wa kitaa, kwa sasa anaeishi Capetown ndio alimshawishi kuja maisha haya, lkn alipoingia tu "Kaburu" yule rafiki yake akamzimia simu na kumkosa kabisa online.

Kijana akachanganyikiwa asijue wapi pakwenda wala nini cha kufanya. Nikiwa katika mizunguko yangu mitaa ya park station Johannesburg, ghafla nikapita sehem na kumuona kijana akiwa kajiinamia na begi lake huku machozi yakimtoka. Nikamsogelea taratibu na kujaribu kumuuliza kwa lugha ya wenyeji, ghafla nikasikia jamaa akiongea kiswahili, hii ikanipa nguvu ya kumsogelea na kumuuliza zaidi baada ya kugundua kuwa naongea na mtu anaetoka nchini kwetu. Baada ya maongezi ya hapa na pale nikagundua kuwa jamaa ameingizwa cha kike na mwenyeji wake, kwahiyo nikachukua jukumu la kumsaidia.

Nikaondoka na jamaa hadi nyumban, akaoga, akala, baada ya kula nikampa sehem ya kupumzika akalala. Kwa kuwa mimi nina familia ikanibidi niende kuongea na homeboy fulan ambae ni single ili ampe hifadhi ya miezi kadhaa wakati nikiendelea na mchakato wa kumtafutia shughuli ya kufanya, mshikaji akakubali lkn kwa masharti ya kumsaidia kulipa rent.

Kwa kuwa nilikuwa nimeamua kumsaidia kijana, basi nikaona poa tu acha nimsadie kulipa rent ili aweze kuishi nae. Kijana tumekaa nae mwezi wa kwanza, wa pili na sometimes nilikuwa naenda nae kwenye mishe zangu ili kumzoesha mazingira ya nchi, na mishe za hapa na pale. Mwezi mmoja uliopita kuna rafiki angu Mkenya ambae tuliwahi kufanya nae kazi huko Gezina, Pretoria.

Mkenya alikuwa anatafuta mtu wa kumuachia saluni yake kubwa na ya kisasa iliyopo nje kidogo ya jiji la Pretoria huko Nellmapius, kwa malipo ya R600 kwa week (sawa na sh elfu 85 au elf 90) kula na kulala bure. Kwa vile nilikuwa na kijana na tayari alishanambia kuwa bongo kazi yake kubwa ilikuwa ni ukinyozi, nikaona YES maji ya mvua yameangukia juu ya mgongo wa bata. Nikampanga kijana, kesho yake mapema nikampeleka mpaka Pretoria kwa yule Mkenya na kumkabidhi.

Kweli bwana baada ya siku mbili kijana akaanza kazi huku Mkenya akiniomba nimtafutie vijana wengine ambao wataenda kusaidizana nae, maana saluni ni kubwa ilihitaji vinyozi zaidi ya watano, lkn pia kijana lugha ni tatizo, so alitaka ambao wangeweza pia kusaidiana hata katika mambo ya lugha za wenyeji ili kuwateka vizuri wateja wa kizawa.

Nikamuahidi jamaa kumtafutia hao vijana. Wakati namuacha kwa yule Mkenya kijana wang nilimuachia sim kwa ajili ya mawasiliano yetu, au ndugu zake wa bongo, au boss wake (Mkenya). Dogo tukawa tunawasiliana ananipa taarifa za kazi na mimi nampa mpa moyo kuwa akomae ili atimize malengo ya kile kilichomleta hapa nk. Siku tatu zilizopita sikumpata online, nikajua labda simu imepata tatizo ghafla.

Sasa jana yule rafiki angu Mkenya amenipigia simu na kuniambia kuwa jamaa amemuibia kila kitu cha saluni, na hela ambazo yule Mkenya anaendaga kuzichukua kwa week jamaa katimka nazo. Simu yake haipiti na hatujui tutamtoa wapi. Nilipotaka kumlipa yule Mkenya nusu ya hasara ya vitu alivyoiba jamaa, Mkenya amkataa amesema nisijali kwa vile sio kosa langu ni kosa la mtu mungine kwahiyo mimi sistahili kumlipa na ukizingatia na rafiki yangu.

Hiki kitendo cha huyu jamaa kimenisononesha na kunivunja nguvu. Imenifanya sasa niwachukie wabongo wenzangu, maana hii ni mara pili sasa nawasaidia wabongo afu wanaharibu na kutimkia kusikojulikana, japo kwa huyu sikutegemea hata kidogo kutokana na upole na muonekano wake.

Najua binadamu tunatakiwa tusamehe, lkn kwa mikasa hii sioni sababu ya kusamehe kwa lengo la kurudi kumsaidia mungine labda yule nimjuae A to Z. Ndugu zangu wabongo tubadilike, hii dunia tunapita tu. Kumuharibia mtu anaekusaidia sio ujanja bali ni ujinga wa mwisho. Hii ni tahadhari nimetoa kwa vijana wengine kuwa makini sana. Asanteni
Kusema kwamba utafikiria mara mbili mbili kabla ya kumsaidia mtu mwenye tatizo kutokana na uliyojifunza ni sawa kabisa. Lakini si sawa kuwaweka Watanzania wote kwenye kapu moja kutokana tu na Mtanzania mmoja alivyokufanyia. Huyu mmoja si kipimo cha Watanzania wote. Huko huko Kusini mwa Bara letu la Afrika niliwahi kumsaidia Mkenya (japo si vikubwa kama wewe) akanilipa kwa mabaya. Siwezi kuwasema Wakenya wote kwa sababu tu ya huyu mmoja.
 
Kuna thread pia humu ya biashara Commoro naskia wakijua wewe ni mtanzania wanakuogopa maana wanajua ni tapeli tu.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Dah Park Station umenikumbusha mbali sana. Nilikuwa nachukua Combi hapo ili kwenda Manzini/Swaziland kabla sijafulia.
Niliwahi kukabwa na majita hapo park station , mbele ya gari ya polisi, tena saa moja asubuhi .
Kumbe polisi wanapaki gari halafu wanaenda kulewa na kuchukua malaya diplomat bar , gari linakuwa kama boya tu na majita wanalijua hilo
 
Mr Dudumizi huyo mshikaji uliyemsaidia kupata kazi kauawa kwa kutolewa kafala/biashara ya viungo, na mkenya kasingizia kamuibia. Huyo mkenya hiyo itakuwa ni side business kwa ajili ya viungo etc. Muepuke huyo Mkenya hata wewe atakuja akuue auze viungo.
Hakika kabisaaa yaan, naamini hili.
 
Back
Top Bottom