Naapa kuwa sirudii tena kumsaidia Mtanzania -- never!

Naapa kuwa sirudii tena kumsaidia Mtanzania -- never!

Habar zenu ndugu zangu. Ama baada ya salam ningependa kuendelea na kile kilichonifanya niandike uzi huu. Ndugu zangu kama ilivyo ada au kama tulivyofunzwa na misingi yetu ya Taifa kwamba watanzania popote tulipo haijalishi ni ndani au nje ya nchi, sisi ni watu wamoja. Kwahiyo kwa misingi hiyo sisi tulio nje huwa na desturi au utamaduni wa kusaidiana bila kujali tofauti zetu za kikabila, dini, rangi, jinsia au kanda ya mtu anayotokea ilimradi sote ni watanzania na tunatokea kwenye ardhi ya Tanzania basi ni ndugu.

Sasa basi miezi 3 iliyopita kuna kijana aliingia Kaburu akitokea bongo kwa lengo la kuja kutafuta maisha. Kijana anadai kuna rafiki yake wa kitaa, kwa sasa anaeishi Capetown ndio alimshawishi kuja maisha haya, lkn alipoingia tu "Kaburu" yule rafiki yake akamzimia simu na kumkosa kabisa online.

Kijana akachanganyikiwa asijue wapi pakwenda wala nini cha kufanya. Nikiwa katika mizunguko yangu mitaa ya park station Johannesburg, ghafla nikapita sehem na kumuona kijana akiwa kajiinamia na begi lake huku machozi yakimtoka. Nikamsogelea taratibu na kujaribu kumuuliza kwa lugha ya wenyeji, ghafla nikasikia jamaa akiongea kiswahili, hii ikanipa nguvu ya kumsogelea na kumuuliza zaidi baada ya kugundua kuwa naongea na mtu anaetoka nchini kwetu. Baada ya maongezi ya hapa na pale nikagundua kuwa jamaa ameingizwa cha kike na mwenyeji wake, kwahiyo nikachukua jukumu la kumsaidia.

Nikaondoka na jamaa hadi nyumban, akaoga, akala, baada ya kula nikampa sehem ya kupumzika akalala. Kwa kuwa mimi nina familia ikanibidi niende kuongea na homeboy fulan ambae ni single ili ampe hifadhi ya miezi kadhaa wakati nikiendelea na mchakato wa kumtafutia shughuli ya kufanya, mshikaji akakubali lkn kwa masharti ya kumsaidia kulipa rent.

Kwa kuwa nilikuwa nimeamua kumsaidia kijana, basi nikaona poa tu acha nimsadie kulipa rent ili aweze kuishi nae. Kijana tumekaa nae mwezi wa kwanza, wa pili na sometimes nilikuwa naenda nae kwenye mishe zangu ili kumzoesha mazingira ya nchi, na mishe za hapa na pale. Mwezi mmoja uliopita kuna rafiki angu Mkenya ambae tuliwahi kufanya nae kazi huko Gezina, Pretoria.

Mkenya alikuwa anatafuta mtu wa kumuachia saluni yake kubwa na ya kisasa iliyopo nje kidogo ya jiji la Pretoria huko Nellmapius, kwa malipo ya R600 kwa week (sawa na sh elfu 85 au elf 90) kula na kulala bure. Kwa vile nilikuwa na kijana na tayari alishanambia kuwa bongo kazi yake kubwa ilikuwa ni ukinyozi, nikaona YES maji ya mvua yameangukia juu ya mgongo wa bata. Nikampanga kijana, kesho yake mapema nikampeleka mpaka Pretoria kwa yule Mkenya na kumkabidhi.

Kweli bwana baada ya siku mbili kijana akaanza kazi huku Mkenya akiniomba nimtafutie vijana wengine ambao wataenda kusaidizana nae, maana saluni ni kubwa ilihitaji vinyozi zaidi ya watano, lkn pia kijana lugha ni tatizo, so alitaka ambao wangeweza pia kusaidiana hata katika mambo ya lugha za wenyeji ili kuwateka vizuri wateja wa kizawa.

Nikamuahidi jamaa kumtafutia hao vijana. Wakati namuacha kwa yule Mkenya kijana wang nilimuachia sim kwa ajili ya mawasiliano yetu, au ndugu zake wa bongo, au boss wake (Mkenya). Dogo tukawa tunawasiliana ananipa taarifa za kazi na mimi nampa mpa moyo kuwa akomae ili atimize malengo ya kile kilichomleta hapa nk. Siku tatu zilizopita sikumpata online, nikajua labda simu imepata tatizo ghafla.

Sasa jana yule rafiki angu Mkenya amenipigia simu na kuniambia kuwa jamaa amemuibia kila kitu cha saluni, na hela ambazo yule Mkenya anaendaga kuzichukua kwa week jamaa katimka nazo. Simu yake haipiti na hatujui tutamtoa wapi. Nilipotaka kumlipa yule Mkenya nusu ya hasara ya vitu alivyoiba jamaa, Mkenya amkataa amesema nisijali kwa vile sio kosa langu ni kosa la mtu mungine kwahiyo mimi sistahili kumlipa na ukizingatia na rafiki yangu.

Hiki kitendo cha huyu jamaa kimenisononesha na kunivunja nguvu. Imenifanya sasa niwachukie wabongo wenzangu, maana hii ni mara pili sasa nawasaidia wabongo afu wanaharibu na kutimkia kusikojulikana, japo kwa huyu sikutegemea hata kidogo kutokana na upole na muonekano wake.

Najua binadamu tunatakiwa tusamehe, lkn kwa mikasa hii sioni sababu ya kusamehe kwa lengo la kurudi kumsaidia mungine labda yule nimjuae A to Z. Ndugu zangu wabongo tubadilike, hii dunia tunapita tu. Kumuharibia mtu anaekusaidia sio ujanja bali ni ujinga wa mwisho. Hii ni tahadhari nimetoa kwa vijana wengine kuwa makini sana. Asanteni
Huyo atakuwa sio mtanzania wa asili.Itakuwa ni mchanganyiko na makabili ya wakimbizi,waliongia Tanzania.Watanzania ni waaminifu sana.Fikiria wapo waliofanyakazi kwa wahindi,wazungu na waarabu,na wanawachiwa nyumba zenye vitu vya thamani kubwa,na wenyewe wanasafiri nje ya nchi,hata mwaka mzima,wakirudi wanakuta kila kitu kiko,kama walivyokiwacha.Chunguza vizuri hao wasio waaminifu,watakuwa Wana asili ya wahamiaji,wakimbizi kutoka nchi nyingine.
 
Nyimyi watanganyika kazi zenu ni wizi na ujambazi ndio maana uaminifu kwenu ni zero tofauti na wazanzibar wanavoaminiwa ndani ya nchi yao mpaka njee ya nchi yao
Huyo sio mtanganyika. Mtanganyika ni mtu mwaminifu sana.Tatizo Tanganyika inapakana na nchi nyingi, huwa wanaingia wahamiaji,na wakimbizi kutoka nchi jirani, wakishazaana na kuloea, ukikutana naye kokote duniani ,wanajitambulisha ni Watanzania.
Watanganyika wameachiwa majumba, na wazungu, wahindi, waarabu, wakiwa safari nje ya Tanzania, wakirudi wanakuta lila kitu kiko kama walivyokiacha.
 
Huyo uliyekutana naye siye mtanganyika wa asili.Umekutana na watu wenye asili ya ukimbizi kutoka nchi jirani.Huwezi kupata mtu mwaminifu duniani kama mtanganyika.Wengi wanaachiwa majumba,mali za thamani,na wenye mali wakasafiri nje ya nchi,wakirudi mali,majumba yao,yako kama walivyoyaacha.
 
South Africa ya siku hizi ina watu wema hivyo? Yani umkute mtu analia uende kumuuliza analia nini unamsemesha kizulu then unagunduwa ni Mtanzania unampeleka kwako.

Konda tafadhali nishushe hapahapa nimefika, mwendo wa dereva ni hatarishi.
Teh teh teh teh...dah!...noma sana
 
Dah aisee niliposoma hapa nimeshtuka kidogo maana kwa jinsi ninavyomfahamu huyu jamaa sifikirii kama anaweza kufanya biashara hiyo. Kwa hapa South Africa biashara ya aina hiyo inaweza kuwa ngumu kidogo kuifanya, ila hata hivyo nashukuru kwa ushauri wako na nitajaribu kumpeleleza jamaa ili kujiridhisha na ushauri huu.
Kwa namna ulivojibu hapa unaonesha busara kubwa sana,nami niliposoma hapa niliwaza sana na nikangoja utajibu nini,binafsi nimeishi sana SA na hapo park station napajua kidogo ukweli ni kwamba watanzania hatuna sifa njema SA binafsi nilijulikana kama mrundi Capetown tangu naingia hadi naondoka
 
Labda atuelekeze hapo park station jamaa alikua kakaa analia kajiinamia. Labda sio SA
Absolutely his lie. Labda Kama Kuna code kwenye hili andiko lake
Labda code kwa mbali sana ni kuwa jamaa yuko SA ana roho nzuri na anaweza kukusaidia kukutafutia kazi ila kwa Park Station kumsaidia mtu na ukaenda nae hadi kwako na kuishi nae kama ndugu jamaa anastahili tuzo ya nobel
 
Pole sana mkuu kumbe tupo wengi tulio amua kusaidia wenzetu baadae wakatutenda vibaya, da nimeamini Allah (Mungu) mjuzi wa kila kitu Kama alivyotamka kwenye maandiko,

kwakuwa aliamua kutuumba binaadamu kisha akaumba moto akijua kabisa wapo Wapumbavu ambao adhabu yao ni kuwaingiza kwenye huo moto wa jehanamu kwa sababu ya yale maovu waliyo yatenda wakiwa duniani.

Kisha Mungu akasema kwa yule aliyetendewa mabaya na binaadamu mwenzake basi manung'uniko yake au huzuni alizopata baada ya kutendwa basi hayo manung'uniko yako ni Dua tosha itakayomfanya mtendaji asifike popote ikiwezekana kuangamia, mwisho wa kunukuu;
 
Mkuu nataka kuja SA naomba nisaidie ila mimi nakuja na kianzio ili nisiwe mzigo kwako nimejichanga changa nmepata 1.5M ya kiTz na hela ya nauli pemben ila nmekua mzito kuja huko maana sijawahi kufika huko na sina ninae juana nae huko na nmeskia wa Tz weng wa huko unaweza ukafikiri n msaada kumbe umejipeleka kwenye mdomo wa mamba ila ww nahisi utakua tofaut kutokana na moyo wa kusaidi nataka nianzishe hata kuuza matunda tu ila nahitaji masaada wako unipe muongozo tu.
Mkuu kuwa makini unaweza kupigwa pia...nenda Malawi bado wamelala ukiwa na hiyo hela utachanga bila pressure nenda Lilongwe au Brantire nadhani pale utaanza kuuza vitu kutoka SA wapo watanzania wanaenda kununua vitu SA ukiwa na mtaji uliosimama unaenda mwenyewe sasa hivi SA sio kuzuri kwa kutafutia maisha kama huna mwenyeji alieanza ila ni rahisi kwa kutokea kwa kuuza bidhaa zake Nchi zingine...
 
Kwa namna ulivojibu hapa unaonesha busara kubwa sana,nami niliposoma hapa niliwaza sana na nikangoja utajibu nini,binafsi nimeishi sana SA na hapo park station napajua kidogo ukweli ni kwamba watanzania hatuna sifa njema SA binafsi nilijulikana kama mrundi Capetown tangu naingia hadi naondoka
Shukran sana mkuu.. Ukweli ni kwamba kati ya watanzania watano basi watatu matapeli, afu wawili waliobaki ndio waaminifu.
 
Honestly speaking waTanzania wengi wanapenda shortcut

Siyo kwenye kazi
Kwenye biashara
Mpaka kwenye mambo ya kijamii

Kuna mmoja nilimpeleka godown fulani akapiga mzigo imekuja julikana too late na deni nikalibeba

Mimi nikisikia opportunity nakausha tu kuepuka lawama. Kisha utasikia waTanzania hatupendani.
Mungine alijifanya kunizoea akawa anakuja kila siku dukani nimuungie hela ya kula kwa madai kwamba anaumwa, hana nguvu za kufanya kazi. Siku moja akaniomba nimpe nauli arudi bongo maana kwa hali yake asingeweza kuendelea kuishi Kaburu. Nikaona wazo lake zuri, nikaingia masikani kuwachangisha wabongo wenzetu na baada ya week ikapatikana R1800, na mimi nikaongezea 1200 ikawa R3000. Nikamkatia ticket ya kutoka Kaburu hadi Zambia na pale Zambia nikampa maelekezo ya jinsi atapata usafiri wa kutoka pale Lusaka hadi Dar. Nikampa na vijichenji vilivyobaki kwa ajili ya kula, kunywa na mambo mengine madogo madogo njiani (hiyo ilikuwa kitambo kidogo kabla ya hili gonjwa corona) kwahiyo gharama za usafiri zilikuwa za chini sana. Siku hiyo nikamshindikiza jamaa hadi kwenye stand ya mabasi ya Zambia, tukaagana nikarudi mtaani. Baada ya week kama mbili kuna wana fulani kati ya wale waliomchangia wakaja kunambia kuwa msela wamemuona Durban anazurura tu (nahisi aliiuza ile ticket yake fasta fasta pale stand akajichenga kabla ya gari kuondoka), jamaa alipowaona wale washkaji akajifanya kujificha na wao wakampotezea kama hawakumuona vile. Hao ndio wabongo bwana. Ukitenda wema, wanalipa ubaya.
 
Mungine alijifanya kunizoea akawa anakuja kila siku dukani nimuungie hela ya kula kwa madai kwamba anaumwa, hana nguvu za kufanya kazi. Siku moja akaniomba nimpe nauli arudi bongo maana kwa hali yake asingeweza kuendelea kuishi Kaburu. Nikaona wazo lake zuri, nikaingia masikani kuwachangisha wabongo wenzetu na baada ya week ikapatikana R1800, na mimi nikaongezea 1200 ikawa R3000. Nikamkatia ticket ya kutoka Kaburu hadi Zambia na pale Zambia nikampa maelekezo ya jinsi atapata usafiri wa kutoka pale Lusaka hadi Dar. Nikampa na vijichenji vilivyobaki kwa ajili ya kula, kunywa na mambo mengine madogo madogo njiani (hiyo ilikuwa kitambo kidogo kabla ya hili gonjwa corona) kwahiyo gharama za usafiri zilikuwa za chini sana. Siku hiyo nikamshindikiza jamaa hadi kwenye stand ya mabasi ya Zambia, tukaagana nikarudi mtaani. Baada ya week kama mbili kuna wana fulani kati ya wale waliomchangia wakaja kunambia kuwa msela wamemuona Durban anazurura tu, alipowaona akajifanya kujificha na wao wakampotezea kama hawakumuona vile. Hao ndio wabongo bwana. Ukitenda wema, wanalipa ubaya.

Kuna mmoja alizimiwa simu na mshkaji wake akabakia airport basi simu huku Simu kule akapata mwenyeji alikaa kwa mwenyeji wake baada ya mwezi anataka kumtomb…a mke wa mwenyeji wake akatimuliwa.



Lunatic [emoji2957][emoji2957][emoji2957]
 
Watanzania kichomi mimi nimenyosha mikono juu

Rafiki yangu kipenzi baada ya kusikia natafuta mtu wa kuniwekea nguzo ( alama za kiwanja ) aliniletea jamaa yake anayemtumia kwenye kazi mbalimbali. Kwa jinsi nilivyokuwa namwamini rafiki yangu ikapelekea nimwamini hata yule jamaa, nikampa 90K cash za nguzo lakini mpaka Leo hakuna nguzo wala kurudisha pesa.

Mzee mmoja aliniuzia kiwanja hivyo nikamwamini mwanae kwa kumpa pesa asafishe hadi leo shamba halikusafishwa na pesa ikapigwa.

Mwingine alilia shida vibaya sana nimkopeshe 1.5M basi nikaamua kumsaidia cha ajabu mwaka sasa pesa yangu haijalipwa karibu tunapelekana mahakamani.


KAMWE SIJI KUMWAMINI MTANZANIA ...NEVERR
 
Sister.. ma gape kama haya tuna watu wana uhitaji nayo sana sana, nikuombe usikate tamaa kwa ajili ya watu wachache unaweza ukawa msaada kwa watu wengi sana

Mie tena?

Hapana kwa kweli

Mtu anakuchafulia na kukushushia reputation kwa watu wa faida
 
Konda anamroga dereva ili aachiwe gari.
House girl anatamani kuwa mama mwenye nyumba.
Ukimpa mchongo wa kazi, asipokuibia, kukuchafulia cv au kukuumiza basi atataka awe boss wako.

Roho za kimaskini tabu sana.
 
Back
Top Bottom