MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 14,588
- 32,361
Huko kwenye viunga vya Instagram tayari Mchungaji wa taifa na nabii komandoo Mashimo ametamka wazi kwamba kijana na kada wa CHADEMA, kamanda Malisa GJ kuwa mrithi wa RC mstaafu Baba Keagan. Mimi kama mwanafunzi wa shule ya uongozi chini ya mwalimu mkuu Komredi POLEPOLE nimefurahishwa na tamko hili la kinabii.
Ikumbukwe Nabii Mashimo ametamka hayo wakati akimtakia heri ya kuzaliwa kamanda Malisa (Happy birthday to you). Nabii ameweka wazi kwamba kwa jinsi Malisa anavyojitolea maisha yake kusaidia watu wenye shida mbalimbali wanaomfikishia shida zao basi anapaswa kuitwa mrithi wa RC mstaafu Makonda ambaye enzi za uongozi wake alikuwa mstari wa mbele kuhakikisha kila shida inayopelekwa kwake basi inapatiwa ufumbuzi.
Mimi naunga mkono hii kauli ya kinabii kwa sababu wote ni mashahidi wa alama za upendo ambazo Baba Keagan aliziweka kwa watu wa mkoa wake kipindi chote cha uongozi wake. Malisa GJ nae anapita mulemule alikopita RC mstaafu. Huyu kijana kafanya mambo makubwa mno kwenye kugusa maisha ya wengine.
Nampongeza Mchungaji komandoo Mashimo kwa hili suala la kiroho alilopost. Nampongeza sana pia kamanda Malisa kwa moyo wake pia namtakia mema kwenye siku yake ya kuzaliwa. RC mstaafu nampongeza kwa kuonyesha njia.
Ikumbukwe Nabii Mashimo ametamka hayo wakati akimtakia heri ya kuzaliwa kamanda Malisa (Happy birthday to you). Nabii ameweka wazi kwamba kwa jinsi Malisa anavyojitolea maisha yake kusaidia watu wenye shida mbalimbali wanaomfikishia shida zao basi anapaswa kuitwa mrithi wa RC mstaafu Makonda ambaye enzi za uongozi wake alikuwa mstari wa mbele kuhakikisha kila shida inayopelekwa kwake basi inapatiwa ufumbuzi.
Mimi naunga mkono hii kauli ya kinabii kwa sababu wote ni mashahidi wa alama za upendo ambazo Baba Keagan aliziweka kwa watu wa mkoa wake kipindi chote cha uongozi wake. Malisa GJ nae anapita mulemule alikopita RC mstaafu. Huyu kijana kafanya mambo makubwa mno kwenye kugusa maisha ya wengine.
Nampongeza Mchungaji komandoo Mashimo kwa hili suala la kiroho alilopost. Nampongeza sana pia kamanda Malisa kwa moyo wake pia namtakia mema kwenye siku yake ya kuzaliwa. RC mstaafu nampongeza kwa kuonyesha njia.