Titicomb
JF-Expert Member
- Jan 27, 2012
- 12,823
- 21,210
Mh. Raisi J.P. Magufuli nakusalimu na kukupongeza kwa wazo au ushauri wako kwa Mfuko wa Taifa wa bima ya Afya (NHIF) wa kuwekeza makusanyo yao ya michango ya wateja kwenye sekta ya afya hasa kwenye viwanda vya madawa n.k.
Mimi nilikuwa na ombi moja ktk kuboresha wazo lako. Naomba NHIF itangaze kupokea miradi ya watu au taasisi binafsi zinazo taka kuwekeza kwenye viwanda vya madawa kwa lengo la kupata mikopo kama mtaji wa miradi yao.
Ipo wazi kabisa kama tukisema NHIF ndio imiliki hii miradi hakika haitakuwa na ufanisi. Sababu ya kuzidiwa mzigo wa majukumu na pia uzoefu unaonesha taasisi za serikali nyingi hazina ufanisi sana zinapokuwa zinajiendesha kibiashara.
Na hii pia inatokana na mzunguko mrefu wa taratibu za kutekeleza mipango flani. Urasimu(Bureaucracy) ni adui wa biashara , timing is everything, kitu kizuri kikifanyika nje ya muda wake kinakuwa hakifanikishi lengo na huenda kinasababisha hasara kibiashara.
Naomba NHIF ikopeshe miradi binafsi lakini ifuatilie kwa ukaribu na ihakikishe pesa yao haipotei kwa mikopo chefu chefu.
Nahisi mahali pa kuanza kujifunza kuhusu ufanisi wa sekta za uwekezaji za umma uanzie kwenye mradi kama wa kiwanda cha maji cha Suma JKT. Je unafanya vizuri kwa kasi kama ya viwanda binafsi vilivyo anzishwa muda unao fanana au vilivyo fuata baada ya mradi huo wa SUMA?
Kuna wakati kutokana na vita vyetu vya kiuchumi tunaweza kujikuta sisi kama nchi tunawekewa vikwazo flani hasa taasisi za kibiashara zinazo milikiwa na umma. Mfano wa hili ni sakata la HUAWEI na vikwazo vya kibiashara vya USA dhidi ya CHINA.
Sasa tukiwa tunahitaji masoko ya nje au mali ghafi za kemikali za hivi viwanda toka nje tunaweza kukuta vikawekwa kwenye orodha ya taasisi zilizo kwenye vikwazo.
Lakini kama zikiwa chini ya umiliki wa sekta binafsi zinaweza kukwepa vikwazo hivi na bado vikatuokoa kwenye pato letu la taifa kipindi cha hali ngumu ikitokea tatizo kama hilo.
Mwisho nakutakia kazi njema Mh. Raisi J.P. Magufuli.
Wadau wengine wa JF naomba mmchangie hoja zaidi huenda Mh. raisi atasoma hapa yeye mwenyewe au wasaidizi wake.
Watu wa itifaki: Mkimshauri Mheshimiwa juu ya hili nipeni credit huko huko kwa kumuambia imetoka wapi. Wala msije hapa JF kunipa credit na wala msiniambie kama ameona ushauri wangu, wala sihitaji teuzi, it's just a love for my country.
Mimi najua akijua kuna ushauri unapatikana JF basi haitafungwa kwa makosa ya wachache wanao tumia vibaya jukwaa hili.
TANZANIA MBELE DAIMA, TANZANIA KWANZA.
Mimi nilikuwa na ombi moja ktk kuboresha wazo lako. Naomba NHIF itangaze kupokea miradi ya watu au taasisi binafsi zinazo taka kuwekeza kwenye viwanda vya madawa kwa lengo la kupata mikopo kama mtaji wa miradi yao.
Ipo wazi kabisa kama tukisema NHIF ndio imiliki hii miradi hakika haitakuwa na ufanisi. Sababu ya kuzidiwa mzigo wa majukumu na pia uzoefu unaonesha taasisi za serikali nyingi hazina ufanisi sana zinapokuwa zinajiendesha kibiashara.
Na hii pia inatokana na mzunguko mrefu wa taratibu za kutekeleza mipango flani. Urasimu(Bureaucracy) ni adui wa biashara , timing is everything, kitu kizuri kikifanyika nje ya muda wake kinakuwa hakifanikishi lengo na huenda kinasababisha hasara kibiashara.
Naomba NHIF ikopeshe miradi binafsi lakini ifuatilie kwa ukaribu na ihakikishe pesa yao haipotei kwa mikopo chefu chefu.
Nahisi mahali pa kuanza kujifunza kuhusu ufanisi wa sekta za uwekezaji za umma uanzie kwenye mradi kama wa kiwanda cha maji cha Suma JKT. Je unafanya vizuri kwa kasi kama ya viwanda binafsi vilivyo anzishwa muda unao fanana au vilivyo fuata baada ya mradi huo wa SUMA?
Kuna wakati kutokana na vita vyetu vya kiuchumi tunaweza kujikuta sisi kama nchi tunawekewa vikwazo flani hasa taasisi za kibiashara zinazo milikiwa na umma. Mfano wa hili ni sakata la HUAWEI na vikwazo vya kibiashara vya USA dhidi ya CHINA.
Sasa tukiwa tunahitaji masoko ya nje au mali ghafi za kemikali za hivi viwanda toka nje tunaweza kukuta vikawekwa kwenye orodha ya taasisi zilizo kwenye vikwazo.
Lakini kama zikiwa chini ya umiliki wa sekta binafsi zinaweza kukwepa vikwazo hivi na bado vikatuokoa kwenye pato letu la taifa kipindi cha hali ngumu ikitokea tatizo kama hilo.
Mwisho nakutakia kazi njema Mh. Raisi J.P. Magufuli.
Wadau wengine wa JF naomba mmchangie hoja zaidi huenda Mh. raisi atasoma hapa yeye mwenyewe au wasaidizi wake.
Watu wa itifaki: Mkimshauri Mheshimiwa juu ya hili nipeni credit huko huko kwa kumuambia imetoka wapi. Wala msije hapa JF kunipa credit na wala msiniambie kama ameona ushauri wangu, wala sihitaji teuzi, it's just a love for my country.
Mimi najua akijua kuna ushauri unapatikana JF basi haitafungwa kwa makosa ya wachache wanao tumia vibaya jukwaa hili.
TANZANIA MBELE DAIMA, TANZANIA KWANZA.