Nadandia kwa mbele hoja ya Rais kuhusu bima ya afya kuwekeza kwenye viwanda vya madawa

Nadandia kwa mbele hoja ya Rais kuhusu bima ya afya kuwekeza kwenye viwanda vya madawa

Madawa mpaka yaingie sokoni research inacost billions of money, production not so much .....
Unafikiri viwanda vingi vya dawa hapa Afrika vinafanya tafiti za kutengeneza dawa mpya?
Nyingi zinanua hakimiliki ya kutengeneza dawa iliyo maarufu tayari sokoni.

Coca Cola tanzania hawapo kwenye kubuni soda mpya bali kuzalisha under license products za nje.
Nadhani hata ukifuatilia hivi viwanda vitengo vyao vya tafiti vinafanya tafiti nyingi kama sio zote za masoko tu.

Tena hii viwanda hakuna haja sana ya kuingiza pesa nyingi kwenye tafiti za dawa mpya wakati kuna taasisi kama NIMR.
Wanaenda kuomba vibali vya kutumia matokeo ya tafiti za hizi taasi tu.

Huko NIMR kuna pesa za wahisani kibao zinawekwa, na hata NHIF ikianzisha kiwanda itakuwa sio faida kiuchumi kama wataenda kupoteza pesa kwenye tafiti ambazo NIMR wanafanya tayari.
 
Siungi mkono NHIF kuwa na viwanda, maana viwanda ni mzigo wa misumari. Kukiyokea hivyo madawa hayatakuwa na viwango kwani hakuna ushindani wa tafiti. Nhif bado kuna mchwa anatafuna matoleo, hilo bado wanashindwa kulitatua wataweza la viwanda? Ndio mwanzo wa kuchomekea madawa feki
 
Kwa hiyo pesa za wanachama wa NHIF mkiziwekeza kwenye viwanda vya madawa,wanachama ambao pesa zao zinakatwa mtawagawia hisa?
Wamezoea na mazoea hujenga tabia.Tumeyaona yaliyotokea kwa NSSF,PPF,LAPF na Kidogo GEPF ya wakubwa.Hii mifuko inafahamika ni ya wanachama kisheria lakini maamuzi na faida za uwekezaji ni Government na kuinusuru kufilisika wakaiunganisha.Mapato na raslimali kama faraja LA Kigamboni,majengo na kiwanda cha sukari yamekuwa ya wanachama?
 
Wamezoea na mazoea hujenga tabia.Tumeyaona yaliyotokea kwa NSSF,PPF,LAPF na Kidogo GEPF ya wakubwa.Hii mifuko inafahamika ni ya wanachama kisheria lakini maamuzi na faida za uwekezaji ni Government na kuinusuru kufilisika wakaiunganisha.Mapato na raslimali kama faraja LA Kigamboni,majengo na kiwanda cha sukari yamekuwa ya wanachama?
Embu fungukeni kidogo kimtazamo..
Hizo taasisi ulizotaja ukiwekeza pesa yako kuna huduma unapewa kupitia pesa yako kwa maana hiyo tayari unafaidika na pesa yako.
Lakini ukinunua hisa kwenye PLC kama mabenki au taasisi nyingine za kibiashara hakuna faida unapata zaidi ya kusubiria gawio lako la faida kutokana na hisa zako.

Kwa hivyo ukitaka faida ya uwekezaji wa michango yako kwenye hii mifuko uliyotaja utakuwa unataka kupata faida mara mbili zaidi.

Jambo jingine la msingi mnasahau kuna huduma za kijamii mnapata bila kujali umechangaia nini.
Mfano, huduma za miundo mbinu, elimu, ulinzi, n.k.
Huku ndio gawio lenu linaenda kutumika.

Kwani wewe unajua umma ndio akina nani kama sio wewe na mimi?
Kwa hivyo viwanda vitamilikiwa na wewe na mimi isipokuwa hatutapewa pesa taslimu (cash) kama faida ya uwekezaji wetu. Tutapewa huduma za kijamii mbadala wake.
 
Unafikiri viwanda vingi vya dawa hapa Afrika vinafanya tafiti za kutengeneza dawa mpya?
Nyingi zinanua hakimiliki ya kutengeneza dawa iliyo maarufu tayari sokoni.

Coca Cola tanzania hawapo kwenye kubuni soda mpya bali kuzalisha under license products za nje.
Nadhani hata ukifuatilia hivi viwanda vitengo vyao vya tafiti vinafanya tafiti nyingi kama sio zote za masoko tu.
Hio ilikuwa second point kwamba production sio gharama kama research, point ya kwanza ni kwamba, kwanini hizo private sectors zisianshishe hivyo viwanda wakati soko lipo kuliko kusubiri pesa za wachangiaji ndio uwe mtaji wa wao kuingia sokoni ili waendelee kuwauzia hao hao wachangiaji..., si waingie sokoni kuanzia sasa...
 
Hio ilikuwa second point kwamba production sio gharama kama research, point ya kwanza ni kwamba, kwanini hizo private sectors zisianshishe hivyo viwanda wakati soko lipo kuliko kusubiri pesa za wachangiaji ndio uwe mtaji wa wao kuingia sokoni ili waendelee kuwauzia hao hao wachangiaji..., si waingie sokoni kuanzia sasa...
Kwani ukisikia "Government empowerment programs" unajua ndio nini mfano wake?
Zina faida gani hizo program?
 
Embu fungukeni kidogo kimtazamo..
Hizo taasisi ulizotaja ukiwekeza pesa yako kuna huduma unapewa kupitia pesa yako kwa maana hiyo tayari unafaidika na pesa yako.
Lakini ukinunua hisa kwenye PLC kama mabenki au taasisi nyingine za kibiashara hakuna faida unapata zaidi ya kusubiria gawio lako la faida kutokana na hisa zako.

Kwa hivyo ukitaka faida ya uwekezaji wa michango yako kwenye hii mifuko uliyotaja utakuwa unataka kupata faida mara mbili zaidi.

Jambo jingine la msingi mnasahau kuna huduma za kijamii mnapata bila kujali umechangaia nini.
Mfano, huduma za miundo mbinu, elimu, ulinzi, n.k.
Huku ndio gawio lenu linaenda kutumika.

Kwani wewe unajua umma ndio akina nani kama sio wewe na mimi?
Kwa hivyo viwanda vitamilikiwa na wewe na mimi isipokuwa hatutapewa pesa taslimu (cash) kama faida ya uwekezaji wetu. Tutapewa huduma za kijamii mbadala wake.
Wasio kuwa wanachama wa NHIF nao wamewekeza wapi?Hivi unafahamu kuwa wachangiaji wa Bima hawaugui wote,na wanaougua pia wana limitations za huduma wanazostahili kupata?Vile vile ni walipa kodi ya PAYE na VAT through purchase of goods & services?Tuache kushabikia kila wasemacho wanasiasa.
Mifuko ya Pension inakusanya fedha kutoka kwa watumishi,hizo fedha zao zikiwekezwa walitakiwa wapewe faida kupitia uwekezaji husika.
 
Mbona naona pumba tupu hapa. No mkusanyiko wa maneno na sentensi lakini hakuna la maana.
 
Wasio kuwa wanachama wa NHIF nao wamewekeza wapi?Hivi unafahamu kuwa wachangiaji wa Bima hawaugui wote,na wanaougua pia wana limitations za huduma wanazostahili kupata?Vile vile ni walipa kodi ya PAYE na VAT through purchase of goods & services?Tuache kushabikia kila wasemacho wanasiasa.
Mifuko ya Pension inakusanya fedha kutoka kwa watumishi,hizo fedha zao zikiwekezwa walitakiwa wapewe faida kupitia uwekezaji husika.
Kwani ukiwekeza pesa yako kwenye biashara kwa mfumo wa hisa hiyo biashara hailipi kodi?
Au ukiwekeza bank na ukifungua account bank hiyo hiyo haulipi kodi za miamala na nyinginezo?

Kwanini haudai double dividend?

Hivi haufahamu sio kila anaelipia bima ya gari lazima gari inapata ajali na kuitumia pesa yake aliyo lipia bima?
Kwanini haudai watu wa bima ya gari wakupatie gawio la faida kama fedha mnayolipia wateja wanawekeza ktk biashara nyingine kama kukopesha fedha na kupata faida?

Ikiwa kila anaelipia bima lazima akutwe na shida inayolipiwa na bima hadi pesa zake ziishe basi hiyo haitakuwa bima.
Na shirika husika la bima litafilisika, kwanza hilo shirika halitastahili kupewa leseni ya kufanya shughuli za bima sababu itakuwa limefanya vibaya hesabau zake.

Bima lazima kuwe na kuchangiana kwa namna moja au nyingine, na pia lazima mmfuko/shirika lazima liwekeze pesa inayo kusanya ili kuweza kupata fedha ya kulipia fedha za ziada walizo lipiwa/lipwa wateja. Vinginevyo basi ungelipiwa mwisho sawa na kiasi ulicho changia tu.
 
Hayo yalitokea enzi hizo taarifa za kumuwezesha mtu kukopa hazikuwa sahihi na rushwa iliwawezesha wakopaji kama hao kufanikisha kupata mikopo wasiyo stahili.

Sasa hivi vyombo vya dola vinasimamia vizuri kwenye udanganyifu kama huu usitokee, nani anapenda kesi ya uhujumu uchumi isiyo kuwa na dhamana?
siafiki NHIF kujitosa kwenye viwanda hela itazama na madawa mengi ni trade mark za nje gharama za kulipia royalities na kadhalika ni kubwa mno tena kwa pesa za kigeni.

serikali ikilitaka hlilo ianzishe kampuni separate iipe mtaji usitoke NHIF .lakini serikali ilishakuwa nayo na ilikufa.

mfuko ubaki kama mfuko usiguswe

sekta binafsi viwanda vya madawa vipo mfano mansoor daya nk wao hukopa kwenye mabenki ,yeyote wa sekta binafsi anayetaka kuanzisha kiwanda chochote kiwe cha madawa au la aende benki za biashara akakope huko pesa ya NHIF ibaki ilivyo
 
siafiki NHIF kujitosa kwenye viwanda hela itazama na madawa mengi ni trade mark za nje gharama za kulipia royalities na kadhalika ni kubwa mno tena kwa pesa za kigeni.

serikali ikilitaka hlilo ianzishe kampuni separate iipe mtaji usitoke NHIF .lakini serikali ilishakuwa nayo na ilikufa.

mfuko ubaki kama mfuko usiguswe

sekta binafsi viwanda vya madawa vipo mfano mansoor daya nk wao hukopa kwenye mabenki ,yeyote wa sekta binafsi anayetaka kuanzisha kiwanda chochote kiwe cha madawa au la aende benki za biashara akakope huko pesa ya NHIF ibaki ilivyo
Kama soko au mahitaji ya madawa ni kubwa sana kuliko viwanda vilivyopo na serikali imeona pesa nyingi sana ipo kwenye akaunti ya NHIF kwanini isiwekezwe kiasi na kikabakizwa kiasi ambacho mzunguko wa shughuli za mfuko hazitakwama?

Kwanini tunawaza lazima hakutakuwa na faida kwa shirika binafsi likiendesha biashara hiyo?
Kwanini unafikiri lazima pesa yote ya mradi itatoka NHIF?
Hapa yakaribishwe hadi mashirika ya nje lakini kwa ubia na wenyeji.

Kuna uwezekano wa mkopaji kukopa sehemu zaidi ya moja, na mojawapo ya hizo sehemu ni NHIF na nyingine zinaweza kuwa benki za kibiashara au AFDB na taasisi zingine.
Kama gharama za kulipia royalties kwa wenye haki miliki ya madawa flani zingekuwa kubwa hivyo kiasi cha kuhesabu hasara tu basi akina Mansoor Day na Shelys wasingekuwepo sokoni.

Nimeshauri makusudi sekta binafsi zikopeshwe pesa na kufanya hii biashara sababu ya ufanisi wa hizo taasisi, najua serikali itashindwa mapema sana kama tunavyo ona kwenye miradi mingine ya kibiashara inayo milikiwa na serikali.

Tatizo letu watanzania kuamini kila kitu ni aghali sana na sisi hatukiwezi.
 
Nimewahi kufanya kazi na moja ya taasisi ya bima. Of course sio Bima ya Afya. Taasisi za bima zinapata fedha nyingi sana kupitia makusanyo (premium) na kazi yao kubwa ni kulipa madai (claims) ikiwamo bima ya AFYA.

In most cases claims huwa ni chache kuliko makusanyo (premium) kwa hiyo kinachobaki mashirika haya huwa yanaweka bank. Bank wanakopesha yeyote atakae.

Dhani ya JPM na mtoa hoja ni nzuri sana tu.Badala ya NHIF kupoesha hospitali kujenga majengo, na baaada ya hapo kurejeshwa, dhana hiyo hiyo ya mkopo bora tupewe Watanzania wenye investment projects za kuwekeza kwenye vifaa tiba.

Kwa takwimu zisozo rasmi, Tanzania tuna less than 10 pharmaceutical factories. Kati ya hizo billions 200+ ambazo zinawekwa kununua madawa na vifaa tiba, ni busara tungekopeshwa na NHIF ili kuwekeza, kwa soko ambalo ni ready made na linazidi kukua; eventually NHIF angepata fedha zake, bila shaka staff wa kiwanda nao wangekuwa wanachama wa NHIF hivyo angepata wanachama pia, nchi ingepunguza imports na bila shaka ajira kwa vijana.

Ngoma, ipo kwenye who knows who ili who andiko lake lifanyiwe kazi??

Kuna wakati Rais aliwahi hata kuwataka waandishi wa habari waanzishe projects za kuwa kwenye value chain ya miradi ya ujenzi; nani amjuae Fred au Kusiga, au Matomora au Manka ili kweli akiwa na genuine project aifanyie kazi kwa maslahi (ku-endorse ipate hela za kunua machineries) mapana ya taifa?

Tukitoboa hapo, Tanzania itafika kwa haraka kwenye njozi ya Tanzania ya viwanda yenye kukuza middle class earners.
 
Kwanini tunawaza lazima hakutakuwa na faida kwa shirika binafsi likiendesha biashara hiyo?
Kwanini unafikiri lazima pesa yote ya mradi itatoka NHIF?
Hapa yakaribishwe hadi mashirika ya nje lakini kwa ubia na wenyeji.


Kama gharama za kulipia royalties kwa wenye haki miliki ya madawa flani zingekuwa kubwa hivyo kiasi cha kuhesabu hasara tu basi akina Mansoor Day na Shelys wasingekuwepo sokoni.
hao wana ubia na makampuni ya madawa ya kimataifa na wana sole manufacturing license kwenye madawa mengi tu .Wewe ukiingia wamiliki license watakwambia Kwa Tanzania tunaye mansoor daya au shellys hatutoi leseni kwa mwingine hawakupi leseni ya kuzalisha hao wabia wao.


sio rahisi kama unavyofikiri.Mfano mdogo ukitaka ku import dawa Tanzania uwe distributor hupati ma sole distributor wengi wa dawa Africa mashariki wapo kenya.Wenye kiwanda watakwambia kanunue kupitia kwa agents wao kenya

Ndio maana watanzania wengi ni wauza maduka tu ya reja reja ya madawa hata ukikuta anauza jumla ni ki stock kidogo tu

ndio maana napinga sekta binafsi kukopeshwa hela za NHIF wakakope benkii zikizama wajuane na benki sio zizame pesa za wanachama
 
pesa za bima hazitakiwi kuwekezwa kwenye miradi hata siku moja zinakiwa kuwekwa kwenye dhamana za serikali,au fixed deposits za benki ili wakati wowote zikitakiwa kwa ajili ya malipo ziwepo

wazo la kuwekeza kwenye miradi kama viwanda haliko sahihi Litaua mfuko.
 
hao wana ubia na makampuni ya madawa ya kimataifa na wana sole manufacturing license kwenye madawa mengi tu .Wewe ukiingia wamikiki license watakwambia Kwa Tanzania tunaye mansoor daya au shellys hatutoi leseni kwa mwingine

yupo ma hawakupu leseni ya kuzalisha hao wabia wao.


sio rahisi kama unavyofikiri.Mfano mdogo ukitaka ku import dawa Tanzania uwe distributor hupati ma sole distributor wengi wa dawa Africa mashariki wapo kenya.Wenye kiwanda watakwambia kanunue kupitia kwa agents wao kenya

Ndio maana watanzania wengi ni wauza maduka tu ya reja reja ya madawa hata ukikuta anauza jumla ni ki stock kidogo tu

ndio maana napinga sekta binafsi kukopeshwa hela za NHIF wakakope benkii zikizama wajuane na benki sio zizame pesa za wanachama
Nashukuru kwa mchango wako mzuri sana.
Kwa hivyo hitimisho wazo la pesa ya NHIF kuwekeza kwenye viwanda vya madawa halifai kabisa hata zile drip za maji(IV sijui)?
 
Ni yeye mwenyewe ndio alisema ashahuriki, yeye ni Jiwe na dereva wa Lori. Mie nimekupa fact. Tafiti za wataalamu wapi huyu bwana amekuwa kiongozi kwa muda mrefu na ni predictable katika matendo yake, hasa yale mazuri yenye kuboresha maisha ya watu na sekta binafsi ana allergy nayo ungeshauri kujenga daraja usingetumia msuli, as long as umetupa fursa tuchangie utuwie radhi wengine tunafikiri tofauti.
Sawa mkuu, inabidi tu niheshimu mawazo yako.
 
Nashukuru kwa mchango wako mzuri sana.
Kwa hivyo hitimisho wazo la pesa ya NHIF kuwekeza kwenye viwanda vya madawa halifai kabisa hata zile drip za maji(IV sijui)?
halifai watu binafsi wanaoweza wakope banki watengeneze hizo drip wauzie mahospitali bima ya afya ilipie wagonjwa tukuenda kienyeji hivi itafika Imahali hata hospitali zitatakiwa ziwe na viwanda vya drip au gloves!!!! kisa wanapata hela za wagonjwa .Huduma zitadorora hosputalini.Hospitali zibaki kama hospitali,bima za afya zibaki kama bima za afya ,na viwanda vya dawa vibaki kama viwanda vya dawa vinavypjitegemea visivyo chini ya bima ya afya wala visivyotumia pesa za bima ya afya kama mtaji wake
 
Mimi nilikuwa na ombi moja ktk kuboresha wazo lako. Naomba NHIF itangaze kupokea miradi ya watu au taasisi binafsi zinazo taka kuwekeza kwenye viwanda vya madawa kwa lengo la kupata mikopo kama mtaji wa miradi yao.
Sijui nikuchangie kifupi au kirefu mada yako hii nzuri mkuu Titicomb.

Ngoja nijaribu, nitakapoishia ndio hapo, iwe kirefu au kifupi.

Historia ya Tanzania kuwa nauwezo wa kutengeneza madawa yake kwa matumizi yake na biashara ilipamba moto sana kwenye miaka ya 60; hapo ndipo serikali ikishirikiana na UNIDO (United Nations Industrial Development Organization) ilipoombwa kutengeneza ramani ya namna kazi hiyo itakavyotekelezwa.

Bila shaka Wizarani (Afya) mafaili hayo bado yapo.

Huo ndio uliokuwa mwanzo wa mafunzo ya wataalam katika utengenezaji wa madawa. Chuo cha mafamasia Muhimbili kikianzishwa maksudi 1975 (?) nadhani kwa lengo hilo.

Chuo hicho madhumuni yake hayakuwa kupata wauza maduka ya dawa. Lengo mhimu lilikuwa ni kupata watengeneza dawa.

Na ni wakati huo huo, viwanda kama Keko, na Arusha vilijengwa na kuanza kufanya kazi

Hiyo ni historia bila kugusa ni vipi tulishindwa kwenda mbele tokea hapo. Sababu zipo.

Wewe umegusia habari ya serikali kutoweza kufanya kazi inayoweza kufanikishwa na sekta binafsi. Mimi hili sikubaliani nalo, nikikupa mfano wa China.

Serikali zetu hizi zinaposhindwa kufanya kazi vizuri, tusiwe wepesi wa kukimbilia sababu rahisi rahisi kama unazoziangukia wewe. Tunakosa nidhamu inayotakiwa kwa watumishi kuwa nayo ili kufanikisha kazi hizo. Na hapa tunaweza kujadili kirefu kwa nini inakuwa hivyo. Sasa hivi siendi huko.

Kwa hiyo nihitimishe kwa hili kwa kusema kuwa sio kweli kabisa kwamba serikali haina nafasi yake katika viwanda vya namna hiyo.

Utengenezaji madawa una sehemu nyingi sana unazoweza kuzichambua. Baadhi ya hizo serikali hasa ndiyo yenye jukumu ya kuzisimamia.

Mfano mmoja ni huo wa kuwaandaa wataalam katika nyanja hiyo.
Kwa hiyo, unapomshauri rais, mwambie aweke mkazo zaidi na zaidi kuwapata wataalam walioiva vizuri katika utengenezaji madawa hayo.
Curriculum (kiswahili chake kimegota) iliyopo hapa nchini siku hizi katika eneo hilo inakazia zaidi katika kuhudumia wagonjwa mahospitalini; kuuza madawa madukani. Utengenezaji kwa sehemu kubwa umetupiliwa mbali.

Hilo ni moja linaloweza kufanywa na kusimamiwa naserikali kwa lengo maalum.

Kama serikali inavyosimamia baadhi ya mambo mhimu yanayoihusu nchi, serikali inaweza ikasimamia, tena kwa ufanisi kabisa kuanzisha viwanda vya 'Chemical Industry' ambako ndiko mali ghafi inakotokea. Nchi kama Taiwani wamethubutu na wakaweza. Nasi tukidhamiria tutaweza tu. Eneo hili ukisubiri "private sctor" wakujengee, utasubiri sana, kwa sababu zinazoeleweka kabisa.
Hilo ni la pili.

Utengenezaji wa dawa ulioukazia wewe, ni huo wa 'kuchanganya chemikali mbalimbali na kutoka na kidonge, sindano au mafuta ya kupaka n.k. Eneo hili hao "Binafsi" wanalipenda sana, ndio maana unawaona hao walioko Nyerere Road, karibu na uwanja wa ndege kule, na sehemu zinginezo.
Lakini hata katika eneo hili, serikali ingetaka, na ikawa na nia kweli ya kuifanya hiyo kazi ipasavyo, hakuna sababu yoyote ya kuzuia isiweze kuifanya kazi hiyo. Ni swala la nidhamu tu, hata nidhamu ya shurti ikilazimu, why not?
Maeneo haya ndio mimi binafsi ningependa aelekeze ukali wake rais bila ya kupepesa macho, hata mimi ningemuunga mkono.

Yooote niliyoeleza hapo juu, hii ni kazi za kizamani. Watu wamekwishaingia sasa kwenye viwanda tofauti kabisa na tunavyovizungumzia hapa. Watu wpo sasa kwenye "individualized treatment" - Biotechnology na Genetic engineering.

Viini alivyonavyo mgonjwa, tuseme kwenye damu yake, vinakusanywa kwenye 'testtube' na kutengenezwa kuwa dawa; vinarudishwa tena mwilini mwake vinapambana na ugonjwa unaomsumbua.
Usiseme sisi hatuwezi sasa hivi kujiandaa kwenda huko. Huo mfuko unaweza kuanza kupanda mbegu, na kama tunayo 'discipline' kama ninavyokazia hapa, miaka mitano hadi kumi hutatambua kwamba tulikuwa hatuna chochote tulipoanzia.

Ngoja nimalizie kwa kusema haya.

Nguvu kazi yetu mhimu tokea kianzishwe kile chuo pale Muhimbili ni kama tuliipoteza bure tu. Wale walioanza kwenye programu ile, wengi wao watakuwa wamestaafu au wamo njiani kustaafu. Elimu waliyoipata hawakuitumia ipasavyo. Ni kama unajenga barabara nzuri, halafu usiitumie, liwe pambo tu!

Ungekuwa ni mshauri wa Rais kama unavyosema hapo juu, ungeweza hata kumshauri awakusanye baadhi ya hawa watu awaweke kambini kama akitaka na kuwapa jukumu la kuhakikisha katika miaka miwili watoke na mpango kabambe wa namna ya kuanzisha viwanda vyetu vya dawa hapa nchini- si hivyo tu, hata waanze wao, kama kundi la wataalamu, au kama kazi wanayoifanyia serikali.

Hilo la kusema "serikali ikiwekewa vikwazo", umelivuruga. Tanzania ikiwekewa vikwazo ni pamoja na sekta binafsi iliyomo ndani yake.

Sasa niambie, hii ni "Kifupi au Kirefu"? Mimi naona ni kifupi!
 
Back
Top Bottom