Nadhani Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) lipo katika hali mbaya ya kifedha

Nadhani Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) lipo katika hali mbaya ya kifedha

Hlo shirika lilikuwa kiupigaji zaidi.....!!! Na kama hlo shirika lingefata sera yao nafkr watu wasingehangaika kujenga nyumba , but likageuzwa kuwa mradi wa watu wachache wa kupeana tenda , nyumba ya mil 25 inauzwa mil 85,....mwisho wakaamua kurundika maghorofa dsm ambayo sasa ni makaz ya popo
Wana minyumba Yao mighorofa uchwara kwenye miji mingi tz huwa haifanyiwi ukarabati au hata kujenga mpya imefanya miji mingi ionekane mikongwe na mibaya mfano ni mji wa bukoba,moshi,tabora nk
 
Umesikia (usidhani), usituaminishe kuwa umefanya uchunguzi na kuliona hilo, weka habari kama wote tulivyoisikia na chanzo chake si wewe.
Huhitaji kuwa na akili yoyote ukiliona gari limesimama.
Ukisema liko barabarani safarini huku liko juu ya mawe, basi inabidi upimwe akili.
 
Msechu walimuona kilaza wakapeana wakanda
Msechu na genge lake wameshiriki kikamilifu kulifikisha shirika katika hali mbaya kiuchumi, yeye alikuwa ananunua ardhi kwa bei mbaya na wazabuni wenye bei mbaya huku ubora wa nyumba ukiwa wa chini!! UFISADI umechangia kuchoka kwa shirika
 
Hili shirika la kujenga nyumba kwa wananchi, National Housing Corporation NHC, sasa imethibitika liko katika hali mbaya sana kifedha.

Hii ni licha ya kuambiwa uchumi wetu wa viwanda unakua kwa zaidi ya 7%.

Miradi iliyo mbele ya macho na inaonekana kila siku pale Morocco na Kawe, imesimama kabisa kwa miaka takriban minne sasa.
Hiyo ni dalili tosha kudorora kwa NHC.

Siyo siri, tutakachosikia punde ni shirika kushindwa kulipa mishahara ya wafanyakazi.
Siyo siri, shirikalikiendelea hivi litafilisika kibiashara ndani ya mwaka.
 
Hilo shirika lilianzishwa kuboresha hali ya makazi kwa wananchi wa kawaida hasa waishio maeneo ya mijini ikiwemo wafanyakazi, kwa kujenga hasa nyumba za kupangisha. Lilivyokuja kufufuka sasa wakadai wanajenga apartment za matajiri ili wakusanye pesa ndo wazitumie kujenga makazi ya makabwela. Kama hao matajiri waliowalenga ndo hawa wanaoitwa sasa mafisadi na wapiga dili basi hali ya shirika itaendelea kuwa mbaya ukizingatia kwamba mirija yao imebanwa.
 
Ila Nadhani huyu Jamaa alishawahi kupishana na mzee baba kwny anga zake enzi zile akiwa hajawa top boss.
Mchche yupo mitaani.
Lakini atalaumiwa kwa kuwa na bourgeouise vision ya shirika isiyoendana na hali halisi ya wanyonge.
 
Waliomuondoa Mchechu ...kwa maoni yangu naona walicheza faulu kubwa sana..Kama kunauwezekano...mimi ninashauri aombwe arudi kuokoa jaazi...Yaliopita amutumuachie Mungu...
 
Hili shirika la kujenga nyumba kwa wananchi, National Housing Corporation NHC, sasa imethibitika liko katika hali mbaya sana kifedha.

Hii ni licha ya kuambiwa uchumi wetu wa viwanda unakua kwa zaidi ya 7%.

Miradi iliyo mbele ya macho na inaonekana kila siku pale Morocco na Kawe, imesimama kabisa kwa miaka takriban minne sasa.
Hiyo ni dalili tosha kudorora kwa NHC.

Siyo siri, tutakachosikia punde ni shirika kushindwa kulipa mishahara ya wafanyakazi.
Nashukuru sana kama umeliona hili , napenda nikuhakikishie kwamba Hela zote zilizopangwa kwa miradi iliyosimama zimekombwa na kupelekwa " kunyumba "
 
Waliomuondoa Mchechu ...kwa maoni yangu naona walicheza faulu kubwa sana..Kama kunauwezekano...mimi ninashauri aombwe arudi kuokoa jaazi...Yaliopita amutumuachie Mungu...

mchechu ndie kaua shirika.. kwa kuzidisha sifuri kwenye ujenzi
 
Hlo shirika lilikuwa kiupigaji zaidi.....!!! Na kama hlo shirika lingefata sera yao nafkr watu wasingehangaika kujenga nyumba , but likageuzwa kuwa mradi wa watu wachache wa kupeana tenda , nyumba ya mil 25 inauzwa mil 85,....mwisho wakaamua kurundika maghorofa dsm ambayo sasa ni makaz ya popo
Hivi kwanini kila mradi, shirika au kampuni zinazoyumba katika awamu hii mnasema sababu ya kuyumba huko ni upigaji? Yaani mnataka kutuaminisha kwamba kila kitu katika nchi hii kilichokuwa kinastawi kabla ya awamu hii ni matokeo ya dili za ujanja ujanja na kwamba kwavile katika awamu hii dili hizo hazipo tena basi ndo sababu ya kuyumba.

Kwa maoni yangu huku ni kupotosha ukweli. Mathalani inawezekanaje kutuaminisha kuwa kulikuwa na dili za upigaji katika "kulistawisha" shirika la NHC wakati hakuna ripoti zinazoonesha upigaji huo iwe ya CAG, TAKUKURU au kamati yoyote ya Bunge? Mkurugenzi wa shirika hili Ndg Mchechu aliondolewa na Rais. Hata hivyo "mtumbuaji" hakueleza sababu ya kumuondoa mkurugenzi huyo kuwa ni ubadhirifu au utendaji usioridhisha kama afanyavyo kwa watumbuliwa wengine.

Lakini suala la msingi hapa siyo kujadili dili za upigaji za "watu wachache", bali ni ustawi wa shirika katika utawala huu. Hili ni shirika la umma, kwahiyo mwenye mamlaka na uwezo wa kuliendeleza au kiliua ni serikali. Itakuwa ni jambo la kushangaza sana kuona kwamba dili za upigaji za watu wacheche katika awamu zilizopita ziliweza kuliendeleza na kustawisha biashara za NHC, lakini mipango na mikakati halali ya serikali ya awamu ya tano inashindwa. Je, tulaumu dili za upigaji za watu wachache zilizostawisha shirika huko nyuma au tulaumu mipango na mikakati halali ya serikali ya awamu hii iliyoshindwa kustawisha shirika? Au tuseme shirika limetelekezwa na serikali ya awamu hii kwavile liliendelezwa kifisadi huko nyuma? Kama ni hivyo, je hatua hiyo ya kulitelekeza shirika ina tija gani kwa taifa?
 
Wakati mimi nataka kununua mwaka 2015, niliambiwa kuwa hizo za Morocco zingekamilika Dec 2017. Leo 2019 inayoyoma, halafu mnasema bado hazijakamilika! Wawe wanajenga kwanza wanakamilisha ndio wanauza. Mali kauli siyo nzuri. Sasa hivi kuna hatari ya kufilisi mabenki yetu kwa sababu ya tamaa zao.
NHC walikuja na mbwembwe sana mkuu.
Yale matangazo na uhamasishaji ukawapagawisha watu. Kwa vile kulikua na uhakika wa ile miradi kukamilika kwa wakati, mabenki na wateja wakaingia mkenge.
 
Wakati mimi nataka kununua mwaka 2015, niliambiwa kuwa hizo za Morocco zingekamilika Dec 2017. Leo 2019 inayoyoma, halafu mnasema bado hazijakamilika! Wawe wanajenga kwanza wanakamilisha ndio wanauza. Mali kauli siyo nzuri. Sasa hivi kuna hatari ya kufilisi mabenki yetu kwa sababu ya tamaa zao.


Hili ni janga
 
Hivi kwanini kila mradi, shirika au kampuni zinazoyumba katika awamu hii mnasema sababu ya kuyumba huko ni upigaji? Yaani mnataka kutuaminisha kwamba kila kitu katika nchi hii kilichokuwa kinastawi kabla ya awamu hii ni matokeo ya dili za ujanja ujanja na kwamba kwavile katika awamu hii dili hizo hazipo tena basi ndo sababu ya kuyumba.

Kwa maoni yangu huku ni kupotosha ukweli. Mathalani inawezekanaje kutuaminisha kuwa kulikuwa na dili za upigaji katika "kulistawisha" shirika la NHC wakati hakuna ripoti zinazoonesha upigaji huo iwe ya CAG, TAKUKURU au kamati yoyote ya Bunge? Mkurugenzi wa shirika hili Ndg Mchechu aliondolewa na Rais. Hata hivyo "mtumbuaji" hakueleza sababu ya kumuondoa mkurugenzi huyo kuwa ni ubadhirifu au utendaji usioridhisha kama afanyavyo kwa watumbuliwa wengine.

Lakini suala la msingi hapa siyo kujadili dili za upigaji za "watu wachache", bali ni ustawi wa shirika katika utawala huu. Hili ni shirika la umma, kwahiyo mwenye mamlaka na uwezo wa kuliendeleza au kiliua ni serikali. Itakuwa ni jambo la kushangaza sana kuona kwamba dili za upigaji za watu wacheche katika awamu zilizopita ziliweza kuliendeleza na kustawisha biashara za NHC, lakini mipango na mikakati halali ya serikali ya awamu ya tano inashindwa. Je, tulaumu dili za upigaji za watu wachache zilizostawisha shirika huko nyuma au tulaumu mipango na mikakati halali ya serikali ya awamu hii iliyoshindwa kustawisha shirika? Au tuseme shirika limetelekezwa na serikali ya awamu hii kwavile liliendelezwa kifisadi huko nyuma? Kama ni hivyo, je hatua hiyo ya kulitelekeza shirika ina tija gani kwa taifa?
Mkuu ume argue vizuri.
Mwenye mali ambaye ni serikali inaelekea hajui hasara inayomkabili.
 
Nachopenda mimi rais wetu ni msikivu , basi nilikuwa naomba ayo majengo wafanye kuyapeleka burigi kwa ajili ya kuongeza utalii kwenye mbuga yetu
 
Post namba 36 inafikirisha sana, Hongera X-bar kwa kuwaza deep..

Ukiisoma post hii namba 36, utajiuliza maswali yafuatayo pia, NSSF na PPF zilikuwa na projects nyingi sana za ujenzi wa majumba na vitega uchumi mbalimbali lakini iliweza kulipa wanachama wake FAO LA KUJITOA, NA PENSION BILA SHIDA, lakini wakati huu tunaona pia NSSF na PPF na hazina projects zozote lakini pia zinashindwa kulipa kabisa fao la kujitoa kwa watu wake, na pia hulipa watu pension kwa kusuasua - HAPA UNAAMBIWA PIA SHIDA NI AWAMU YA NNE na DR DAU walikuwa wapigaji na sasa tunanyoosha...

Ukiisoma post namba 36, utajiuliza maswali haya pia juu ya SEKTA YA OIL AND GAS.. Oil and gas iliifanya Mtwara na Lindi zianze kuja kasi na maisha kwa wakazi kuanza kuwa mazuri kiasi cha miji kuanza kujengwa kisasa na mzunguko wa hela kukua maradufu... Wahitimu wa PETROLEUM ENG walipata tegemeo kubwa sana juu ya uwepo wa makampuni mengi mtwara ya mafuta na gas lakini kwa sasa tuna mamia ya wahitimu hawana kazi wala mategemeo ya kazi.. OIL AND GAS Ilipoboom Mtwara na Lindi makampuni makubwa dunia yalivutika na kuweka base pale na ikawa faraja kwa wakazi na watanzania.. Makampuni zaidi ya kumi makubwa na maarufu kwenye oil and gas yaliweka kambi Mtwara na kuajiri mamia kwa maelfu ya watu na kuleta ahueni ya maisha kusini lakini leo hii yote hayapo - HAPO NAPO TUNAAMBIWA TATIZO NI UPIGAJI AWAMU YA NNE YA MZEE JK, lakini hatuoni chochote kikiendelea sasa..
 
Back
Top Bottom