Nadhani Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) lipo katika hali mbaya ya kifedha

Nadhani Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) lipo katika hali mbaya ya kifedha

Nyie ndo haters.
Mchechu alikuwa kiongozi wa 21st Century.
Vikwangua aga alivyobuni inabidi viendelezwe.

Nyie mnaoridhika kuishi maisha yasiyo na maendeleo huko mabonde kuinama nani atawaingilia?
Ni kweli NHC ilibadilika sana na kuwa shirika linalotaka kujiendesha kibiashara na kuweka uwekezaji mkubwa.
Lakini serikali-mwenye shirika haitaki hilo.
Serikali inataka shirika liendelee kujenga vijumba visivyolipa na bado haiingizi mtaji kwenye shirika.
 
Hili shirika la kujenga nyumba kwa wananchi, National Housing Corporation NHC, sasa imethibitika liko katika hali mbaya sana kifedha.

Hii ni licha ya kuambiwa uchumi wetu wa viwanda unakua kwa zaidi ya 7%.

Miradi iliyo mbele ya macho na inaonekana kila siku pale Morocco na Kawe, imesimama kabisa kwa miaka takriban minne sasa.
Hiyo ni dalili tosha kudorora kwa NHC.

Siyo siri, tutakachosikia punde ni shirika kushindwa kulipa mishahara ya wafanyakazi.

MAHAME YA KAWE BEACH

View attachment 1241869View attachment 1241870
Hela za mashirika yote - Bandari, NHC, Reli nk. - anakusanya Jiwe Halaf ananunulia ndege...

So Hakuna shirika linaweza kukamilisha miradi yake sasa!
 
Huhitaji kuwa na akili yoyote ukiliona gari limesimama.
Ukisema liko barabarani safarini huku liko juu ya mawe, basi inabidi upimwe akili.
Kama unalijua hilo kwanini unasema unadhani! Ukiona gari limesimama hudhani limesimama kwani limesimama.
 
Hivi mchechu ndio nasikia alikua anajilipa million 40 kwa mwezi na allowances za kufa mtu?
 
Hivi mchechu ndio nasikia alikua anajilipa million 40 kwa mwezi na allowances za kufa mtu?
Endelea kusikia lakini ukiwa na ka photocopy ka salary slip yake itakuwa vizuri zaidi.
Nyie ndo mnazusha vifo vya watu bila ushahidi.
 
Mchechu ndiye kaliua alikopa sana akitegemea mafisadi watanunua nyumba hizi za kimangumashu. Alipokuja JPM akaziba mashimo ya pannya pakadoda
M

kweli kabisa kinachoua mashirika ni ufisadi na si kingine.watu wamekuwa wabinafisi zaidi na hawajali hata maisha ya wengine.Mungu wamemweka kando wameegemea ya dunia as if wataishi duniani milele.Magu kawakomesha sasa hivi wamebaki vilio kila kona ati maisha magumu ,magumu wapi walizoea kuiba ndo maana wanasema magumu.mbona wengine wanaendelea na maisha kama kawaida lkn wao vilio kila kona.walikokuwa wanategemea kupiga kote kumezibwa sasa wamebaki na vilio tu.nchi sasa inaenda sawa sawa wacha nao wapigwe.
 
Kuna dhambi hii nchi ilikuwa inafanyiwa pole pole sasa naona Mungu kaingilia kati. Ni imani yangu kuwa ilikuwa ni dhuluma kwa Umma wa Watanzania kwa hili shirika kujenga nyumba kwenye prime areas na kuziuza kwa wenye kukopesheka kwa dhamana za vyeo. Hayo maeneo ndio yangeliingizia fedha shirika kama wangepangisha residential quarters lakini wao wanauziana wakubwa ili waje kuwa matajiri wa kudumu.
 
Kuna nyumba za shirika zinakaliwa na popo na panya..ukienda Kahama Kuna nyumba za NHC zimekosa watu zinachakaa tu.
 
Hivi kwanini kila mradi, shirika au kampuni zinazoyumba katika awamu hii mnasema sababu ya kuyumba huko ni upigaji? Yaani mnataka kutuaminisha kwamba kila kitu katika nchi hii kilichokuwa kinastawi kabla ya awamu hii ni matokeo ya dili za ujanja ujanja na kwamba kwavile katika awamu hii dili hizo hazipo tena basi ndo sababu ya kuyumba.

Kwa maoni yangu huku ni kupotosha ukweli. Mathalani inawezekanaje kutuaminisha kuwa kulikuwa na dili za upigaji katika "kulistawisha" shirika la NHC wakati hakuna ripoti zinazoonesha upigaji huo iwe ya CAG, TAKUKURU au kamati yoyote ya Bunge? Mkurugenzi wa shirika hili Ndg Mchechu aliondolewa na Rais. Hata hivyo "mtumbuaji" hakueleza sababu ya kumuondoa mkurugenzi huyo kuwa ni ubadhirifu au utendaji usioridhisha kama afanyavyo kwa watumbuliwa wengine.

Lakini suala la msingi hapa siyo kujadili dili za upigaji za "watu wachache", bali ni ustawi wa shirika katika utawala huu. Hili ni shirika la umma, kwahiyo mwenye mamlaka na uwezo wa kuliendeleza au kiliua ni serikali. Itakuwa ni jambo la kushangaza sana kuona kwamba dili za upigaji za watu wacheche katika awamu zilizopita ziliweza kuliendeleza na kustawisha biashara za NHC, lakini mipango na mikakati halali ya serikali ya awamu ya tano inashindwa. Je, tulaumu dili za upigaji za watu wachache zilizostawisha shirika huko nyuma au tulaumu mipango na mikakati halali ya serikali ya awamu hii iliyoshindwa kustawisha shirika? Au tuseme shirika limetelekezwa na serikali ya awamu hii kwavile liliendelezwa kifisadi huko nyuma? Kama ni hivyo, je hatua hiyo ya kulitelekeza shirika ina tija gani kwa taifa?
Nashukuru sana Mkuu kwa kuongelea vizuri upande ambao wengi hawauoni au hawaelewi kwa kutojua yanayoendelea nyuma ya pazia.
 
Back
Top Bottom