Nadharia ya Usalama wa Taifa (TISS) ibadilike kuanzia sasa, Taifa lipo hatarini

Nadharia ya Usalama wa Taifa (TISS) ibadilike kuanzia sasa, Taifa lipo hatarini

Status
Not open for further replies.

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2010
Posts
17,005
Reaction score
20,425
Taasisi hii ambayo ndio uhai wa taifa letu imefanya mengi ya kutukuka na yasiyomithirika hata kwa chembe ya haradali. Wadadisi wa masuala ya kijasusi wataungana nami kuwa TISS ndicho chombo pekee cha nchi hii kilichofanya kazi yake kwaufanisi mkubwa na kulifikisha taifa hapa lilipo, Naelewa wengi watanishangaa na kuhamaki, kwanini naisifia taasisi hii ambayo wengi wapo nayo mlengo wakushoto.
Kama si uimara wa taasisi hii leo tungalikuwa tunanena kwa lugha yake kila mmoja wetu hapa nchini.

Pamoja na kusimama imara kwa taasisi hii, yapo mambo ya msingi yanayo takiwa kuwekwa sawa ili taasisi hii iendane na mageuzi ya dunia ya leo hasahasa kuelekea 2015, mahuisho katika chombo hiki muhimu ni lazima yaguse nyanja zote kuanzialeadership,watendaji,teknolojia na sheria.

Sheria iliyounda chombo hiki inamapungufu kwa sasa kulingana na mageuzi ya kifikra na kiteknolojia,

Sheria hii inaififisha tasisi hii huku ikiruhusu siasa kujipenyeza ndani ya chombo hiki adhimu na muhimu kwa uhai wa taifa letu,

Mathalani sheria hiyo inasema, "taasisi hii itahusika/itajihusisha na kutambua/kubaini na kutoa ushauri tu"

Kwamaneno hayo tu, TISS imenyimwa nguvu ya mojakwamoja, kama zilivyo taasisi za wenzetu huko ughaibuni tulikozoea kuakisi kila kitu.

Hii inatoa fursa kwa viongozi wa kitaifa (wakisiasa) kuingiza wazo lao lolote walipendalo, liwe jema kwa taifa ama jema kwao binafsi. Lakini hatari zaidi inakuja pale watawala wanapoingiza itikati zao za kisiasa katika chombo hiki,

Bunge la Tanzania linayofursa ya kuihuisha sheria hii ili taasisi hii ya Usalama wa Taifa iwe huru na iwe na meno, yaani (ibaini na kuzuia yenyewe), Hata hivyo nafikiri ihuishwe sheria hii imlazimishe kiongozi anayeshindwa kuchukua hatua kwa ushauri wa taarifa sahihi za usalama au anayechukua hatua zisizotakiwa wakati ana taarifa na ushauri sahihi wa taasisi hii hawajibike. Ili hii iwe na maana chombo hiki kinatakiwa kiimarishwe lakini pia kitenganishwe na siasa ya kivyama.

Kwa taifa ambalo ni imara,Usalama wa Taifa ni taasisi inayotakiwa kufanya kazi kwa weledi kuliko idara yoyote ile.Weledi wake hautakiwi kutiliwa shaka yoyote kwa viwango vya kitaifa,kiakanda(regional) au kimataifa kwa maana pana zaidi.TISS inatakiwa kutengeneza mfumo ambao ni more sophisticated katika kufanya information sharing wakati huo huo ikijaribu kuimarisha vitengo vilivyopo ili kutimiza malengo ya idara na taasisi kwa ujumla kama ilivyo mifumo ya mataifa makubwa kama mkakati wa ulinzi na usalama wa Marekani,Uingereza,Pakistan,Is rael,Afrika Kusini,China,India na Canada

Ingawa miakati mingi ya mataifa yaliyoendelea imekua sensitive zaidi kwenye maslahi yao ya kiuchumi na ushindani wa nguvu na mamlaka kimataifa(Power Interests) lakini kwa taifa lililofikisha umri wa miaka 50 ni lazima liwe na mtazamo imara na kwa kuanzia ni lazima tungeanza na kanda yetu ya Maziwa makuu,Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla, hii nikwakuwa Tanzania tumeingia kuwa taifa tajiri zaidi barani afrika kwa sasa baada ya ugunduzi wa GESI yakutosha inayokadiriwa kuweza kulihudumia bara la ulaya kwa miaka 100 bila kukoma.

Kwa mfano tuna washindani wetu kiuchumi na power struggle hapa east afica ambao ni Kenya.Hatujaweza vya kutosha kwenye Economic intelligence kule Kenya inagawa wao wamewekeza hapa kwetu.Leo hii Kenya ina-export TANZANITE,Wana-Export gold n.k.Balance of trade kati ya Tanzania na Kenya ni subject of Economic intelligence.tunapotunga sera zetu za kiuchumi tunatakiwa tutumie taarifa za kiinteligesnsia kwa kutumia wataalamu waliobobea na pia tuangalie possible scenarios na move za washindani wetu.Katika maofisa ubalozi wetu walioko Kenya tujiulize ni wangapi wenye uwezo kusimamia maslahi yetu ya kiuchumi hapa EAC au ukanda kupitia economic power house(Kenya) katika ukanda huu?

Kuna mgogoro kati ya dola na sarafu yetu.Je hakuna uwezekano kwamba dola zimekua zikinunuliwa kwa wingi na kuwa smuggled kwenda Kenya ili kuhujumu uchumi wetu na ku-frustrate fisical na monetary policy zetu?
Usalama wetu bado unahitaji mageuzi kutegemeana na matakwa ya kisheria na kuboresha malengo ya TISS ili iwe modern zaidi
Malengo ya TISS kulingana na trend ya dunia kwa sasa na mahitaji ya taifa tunakopitia kisiasa,kiuchumi na kiutamaduni yaegemee katika kutabiri(si utabiri wa majini/tunguri bali utabiri wa kisayansi),Kupenya,na kuwahi matukio ya hatari kwa maslahi na usalama wa taifa letu,na kuwasaidia wale wanaotekeleza sera yetu ya ulinzi na usalama,kulinda taifa na watu wake,utekelezaji wa sheria na kulinda maslahi na sera zetu kitaifa bila kuathiriwa na ushawishi au hatari yoyote kutoka ndani na nje ya taiafa letu na kulinda malengo yetu kama jamii kwenye Nyanja za kimataifa(jamii nyingine)


Malengo makuu yanatakiwa kujikita katika:

Mosi,Kuongeza nafasi na umuhimu wa idara ya mahakama na vyombo vya kutoa haki.Lengo hapa linatakiwa kuwa juu ya kuunganisha idara za mahakama,wizara ya mambo ya ndani na vitengo vyake kwa kuzingatia upeanaji wa taarifa huku haki za msingi za kiraia zikilindwa pamoja na uhuru wake tofauti na ilivyo sasa ambako TISS inatuhumiwa kutumika kuhujumu haki za kiraia kwa visingizio lukuki.Lengo kuu liwe kulinda haki na uhuru wa watu bila kuathiri maslahi ya jumla.Hili linahitaji ushirikiano kuanzia serikali kuu,mikoa,wilaya,majimbo ya uchaguzi,kata na hata ngazi ya mitaa pamoja na sekta binafsi

Pili,Utengenezwe utamaduni mpya wa kuahamasisha mawazo mbadala na matumizi ya weledi(professionalism/expertise):Kubadili utamaduni ndani ya TISS ni muhimu sana ili kuepuka mimosa ya kimkakati. It is necessary to create an intellectual culture that promotes discussion as well as dissenting opinion. It will require the use of collaborative technology, where subject expertise is maximized, increased cross-agency communication, and the exploration of alternative analysis

Tatu,Kurahisisha zaidi ukusanyaji wa taarifa za kintelijensia:TISS haina budi kuwa mbele katika matumizi ya teknolojia na pia ku-update wataalamu wake kitaaluma na katika matumizi ya zana za kisasa zaidi ili kurahisisha ukusanyaji huo kutoka Open-sources na kutoka Human-sources

Nne,Kuajiri watu kulingana na uwezo na taaluma zao na pia kuajiri watu ambao tayari wana ajira kwenye vitengo vingine lakini walipwe vizuri kwa ajili ya kazi ya usalama ili kupunguza gharama za kupachika watu wapya katika idara,mashirika na taasisi nyeti nchini.Pamoja na hili kitu cha muhimu watu hawa ni lazima wawe na sifa zinazofanana (common attributes) katika ujanja,uwezo wa hali ya juu na haraka katika utendaji huku maadili ya juu kabisa katika vigezo vya utendaji katika idara hii vikizingatiwa

Tano,TISS ibadili utamaduni wa kuhitaji-kujua kwenda Kuhitaji-kutoa taarifa(changing from the culture of need-to-Know to need-to-share):Ili kuongeza ushirikiano na ufanisi katika kila ngazi ni lazima mtazamo wa idara hii ubadilike na suala la kutoa taarifa liwe ndiyo njia kuu ya kufanikisha malengo ya idara katika ngazi zote kwa hiyo kuna haja ya kuangalia jinsi taarifa zinavyofika kwa ubora unaotakiwa,kwa usahihi na kwa muda muafaka na hili ni muhimu na litasaidia zaidi kuwa karibu na watunga sera(policy makers)

Sita,Kuimarisha na kupanua zaidi uhusiano kati ya TISS na washirika wa ndani ya nchi na vitengo vingine vya kijasusi vya mataifa ya nje:Hii ni kwa kuwa tunaweza kuwa na common threats kwenye uchumi,kiitikadi,kiutamaduni,k iulinzi n.kHata hivyo taarifa za kijasusi kutoaka kwa washirika wetu ni lazima ziangaliwe kwa umakini wa hali ya juu na pia tuwe na taarifa zetu ambazo tunaweza kulinganisha na taarifa za washrika wetu.Hizi kwa kijasusi zinaitwa ‘Corroboration codification’
Saba,kitengo kidogo kabisa cha mwisho ndichokinachotakiwa kuwa na acces ya taarifa nyeti lakini kitengo hicho kiwe scrutinized kwa hali na mali.Hata hivyo nitajadili kuhusu juu ya mfumo wetu mbovu wa counterintelligence

Nane,Kujenga mfumo ambao ni uniform zaidi katika utekelazi kisayansi na kiteknolojia,Ni lazima sasa idara iwe centralized katika kutoa maelekezo na iwe more decentaliced katika utekelezaji kwa mtindo ambao unaitwa ‘pyramid execution’.unified research itumike ili kuongeza ushirikiano na idara mbali mbali

Tisa,Mfumo wa kupongeza na kuzawadia utumike kuongeza performance

Kumi,mtindo wa kutumia miongo utumike lakini zaidi kwa haraka mtindo wa kutumia siku utumike badala ya miaka.Kwa mfano 720 days plan itumike badala ya miaka 2,180 days pla itumike badala ya 6 months plan kwa ajili ya monitoring na kuepuka urasimu na uvivu usio wa lazima

Pia ni vyema kutokana na power struggle ya ukanda tuunde vitengo vya ujasusi vya nje.kitengo hiki kifanane kwa muundo ingawa kutakua na marekebisho kidogo lakini kifanane na kitengo cha RAW cha india ambacho kiliundwa baada ya vita ya India na China.kabla ya hapo kulikua na kitengo cha IB ambacho kilikua na miaka 120 lakini hicho kilitumika kuchunguza watu zaidi na taasisi za kisaiasa.waingereza walikitumia kuwachunguza akina Mahatma Gandhi,Azad na Nehru zaidi.Kitengo cha RAW kinatumika kwa ajili ya military Intelligence na financial intelligence.Kuna haja ya kupima maofisa ubalozi wetu wanaopelekwa nje pamoja na Mwambata wa jeshi katika balozi zetu(defence attaché) kulingana na sera yetu.



Naiona hatari iliyombele yetu, hasa ya kisiasa, kiuchumi na machafuko ya kiroho.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki TISS.
 
Umenena mkuu, wanasiasa ni hatari sana kwa vyombo vyetu vya ulinzi kwani vinaweza kuzipa taasisi hizi wakati mgumu zinapotekeleza majukumu yake.
 
Sikuwa nafahamu kama TISS haina meno. Nadhani ndio maana yanajitokeza mambo mengi ambayo wengi tusiojua, tunajikuta tunahoji juu ya uwezo na utendaji wa TISS
 
Well said mkuu,wenye macho waliangalie hili kwa ukaribu sana na wenye masikio
wasikie kwa umakini wa hali ya juu.
 
Taasisi hii ambayo ndio uhai wa taifa letu imefanya mengi ya kutukuka na yasiyomithirika hata kwa chembe ya haradali.

Wadadisi wa masuala ya kiusalama wataungana nami kuwa TISS ndicho chombo pekee cha nchi hii kilichofanya kazi yake kwaufanisi mkubwa na kulifikisha taifa hapa lilipo,

Naelewa wengi watanishangaa na kuhamaki, kwanini naisifia taasisi hii ambayo wengi wapo nayo mlengo wakushoto.

Kama si uimara wa taasisi hii leo tungalikuwa tunanena kwa lugha yake kila mmoja wetu hapa nchini.

Pamoja na kusimama imara kwa taasisi hii, yapo mambo ya msingi yanayo takiwa kuwekwa sawa ili taasisi hii iendane na mageuzi ya dunia ya leo hasahasa kuelekea 2015.

Sheria iliyounda chombo hiki inamapungufu kwa sasa kulingana na mageuzi ya kifikra na kiteknolojia,

Sheria hii inaififisha tasisi hii huku ikiruhusu siasa kujipenyeza ndani ya chombo hiki adhimu na muhimu kwa uhai wa taifa letu,

Mathalani sheria hiyo inasema, "taasisi hii itahusika/itajihusisha na kutambua/kubaini na kutoa ushauri tu"
Hizo mbili mbona zinakinzana? kwa lugha nyepesi TISS kwa ushauri wake tu imeweza kusimamia mambo hadi kutuepusha na mengi sio?
 
usalama wa taifa wa kiukweli ulikuwa active under the late Mwalimu -- huu wa sasa unaegemea umekuwa kama usalama wa ccm.

Kwa mfano haya mambo ya rushwa za mabilioni , udini kuchinjana kwa imani za kidini, kuchoma makanisa, ukabila, ujangiri hadi watu wanatotosha twiga nje ya nchi, madawa ya kulevya, ushirikina (kuua maarubino) nk haya yanatakiwa yashughulikiwe na usalama wa taifa.

sasa ukiona vituko kama hivi unaweza kuhoji uwepo wa taasisi nyeti kama hii.
 
Yericko tiss ilikuwa zamani sio sasa hivi ajira zake zinakwenda kwa vimemo, mtoto wa flani, nepotism nk. Nahisi sasa hata kagame ameshapenyeza watu wake pale sbb tuko vulnerable sana. zamani kuajiriwa pale mtu alikuwa vetted toka kijijini kwake alikozaliwa, shule aliyosoma na kila sehemu aliyopitia nk.

nakumbuka rafiki yangu mmoja aliajiriwa na tiss enzi hizo. kwanza yeye hakujua sbb kazi hii ilikuwa haiombwi na mhusika. watu walichujwa. jamaa kanambia kuwa alitumiwa ujumbe aende stand ya msamvu morogoro enzi hizo na kuwa ataikuta landrover ya kijivu saa sita mchana na akiikuta apande. baada ya hapo hakuonekana mwaka mzima na alivyorudi hakusema alikuwa wapi. lkn alitokea kuwa mmoja wa maofsa mahiri kitengoni.

hali ni tofauti na sasa. vuka tu pale ng'ambo ya makao makuu ya tiss kwenye bar ya SIMBA KAPAKATWA utawakuta wanakunywa pombe huku wakiongea mambo nyeti ya usalama wa nchi wakiwa njwiii. hakuna maadili wala secrecy ya masuala ya nchi. katiba mpya nadhani inaweza kuja na solution ya tatizo hili.
 
Sikuwa nafahamu kama TISS haina meno. Nadhani ndio maana yanajitokeza mambo mengi ambayo wengi tusiojua, tunajikuta tunahoji juu ya uwezo na utendaji wa TISS

Mengi yatasemwa kuhusu Taasisi hiyo nyeti, lakini nadhani wengi hatujui inavyofanyakazi zake unajua jambo usilolijua ni kama usiku wa giza, nakumbuka kuna kipndi fulani jamaa mmoja aliposti Kitabu chake hapa JF akielezea namna ambavyo idara ya usalama wa taifa ilivyofanyakazi zake na akatahadharisha kuwa watu tusiojua namna ambavyo taasisi hiyo inafanyakazi tunaweza kufikiri kuwa imelala jambo ambalo si kweli. Binafsi nilipenda sana ile post, sijui yule jamaa yuko wapi ingefaa atuekee tena kile kitabu hapa ili tuwe angalau tunapata uwelewa badala ya kupaki tunalalama tu.
 
nakumbuka nikiwa mdogo, kuna chizi stand ya tabora alikuwa anaongea kingereza (sina uhakika kama kilikuwa kimenyooka) sasa tunaambiwa tusimsogelee jamaa ni usalama wa taifa, ni hatari. nikakariri usalama wa taifa mtu lazima ajifanye chizi kukusanya habari. ukisikia mtu ni usalama wa taifa bila hata kuwa na uhakika alikuwa anaogopwa kuliko hata mkuu wa majeshi.
 
yericko tiss ilikuwa zamani sio sasa hivi ajira zake zinakwenda kwa vimemo, mtoto wa flani, nepotism nk. nahisi sasa hata kagame ameshapenyeza watu wake pale sbb tuko vulnerable sana. zamani kuajiriwa pale mtu alikuwa vetted toka kijijini kwake alikozaliwa, shule aliyosoma na kila sehemu aliyopitia nk.

nakumbuka rafiki yangu mmoja aliajiriwa na tiss enzi hizo. kwanza yeye hakujua sbb kazi hii ilikuwa haiombwi na mhusika. watu walichujwa. jamaa kanambia kuwa alitumiwa ujumbe aende stand ya msamvu morogoro enzi hizo na kuwa ataikuta landrover ya kijivu saa sita mchana na akiikuta apande. baada ya hapo hakuonekana mwaka mzima na alivyorudi hakusema alikuwa wapi. lkn alitokea kuwa mmoja wa maofsa mahiri kitengoni.

hali ni tofauti na sasa. vuka tu pale ng'ambo ya makao makuu ya tiss kwenye bar ya SIMBA KAPAKATWA utawakuta wanakunywa pombe huku wakiongea mambo nyeti ya usalama wa nchi wakiwa njwiii. hakuna maadili wala secrecy ya masuala ya nchi. katiba mpya nadhani inaweza kuja na solution ya tatizo hili.

Nadhani suala la mtumishi kuongelea masuala ya ofisni kwake akiwa njwi ni HULKA ya mtu na sidhani kama ni hao wafanyakazi wa TISS pekee bali hata OFISI zingine ziwe za serikali na hata binafsi huwezi kuwakosa watu wa aina hiyo. Kuna mtaalam mmoja alisema ukiona mtu anaongea sana na kujifanya anajua ujue huyo ndo hajui kitu. Ni ukweli usiopingika kuwa watu wengi ambao wanajifanya kujua sana mambo mara nyingi wanakuwa ni waropokaji tu.
 
Hakuna taasisi inayoweza kuwa bora bila kufanya mabadiliko kwa kuendana na wakati,fikra na teknolojia.Ushauri wako ni mzuri kabisa kwani ni dhahiri tunahitaji Pentagon ya Tanzania

Yap. wanasiasa wangekuwa wanatoa ushauri kama huu pengine tungekuwa mbali, wao hubakia kulaumu tu.
 
mkuu yericko hebu kuwa wazi...
Tatizo ni leadership,watendaji,teknolojia duni au sheria?

Binafsi naona kama hawa jamaa kazi zao kutokuwa za wazi kama POLISI, JWTZ kunafanya wanachi tupotoshwe kuwa hawafanyazi kazi ipasavyo, japo pengine sheria nazo zinaweza kuwa tatizo.
 
nakumbuka nikiwa mdogo, kuna chizi stand ya tabora alikuwa anaongea kingereza (sina uhakika kama kilikuwa kimenyooka) sasa tunaambiwa tusimsogelee jamaa ni usalama wa taifa, ni hatari. nikakariri usalama wa taifa mtu lazima ajifanye chizi kukusanya habari. ukisikia mtu ni usalama wa taifa bila hata kuwa na uhakika alikuwa anaogopwa kuliko hata mkuu wa majeshi.

Tatizo nadhani ni kule kutofahamika kwao, hata POLISI wangekuwa hawafahamiki, lazima tungekuwa tunaambiwa kuwa chizi fulani ni Polisi, lakini tutambue pia kuwa maendeleo ya sayansi na technolojia lazima yaende sambamba na mabadiliko ya mbinu za kiutendaji. Hivi kweli inawezakana Usalama wa taifa wakaendelea kutumia mbinu walizokuwa wakizitumia zamani? Labda siku moja wangejitokeza wakatueleza wanavyokabiliana na changamoto hii ya kukua kwa kasi kwa sayansi na technolojia.,La sivyo tutaendelea kuamini kuwa kwa vile hatuwaoni tena machizi basi na usalama wa taifa haupo.
 
usalama wa taifa wa kiukweli ulikuwa active under the late Mwalimu -- huu wa sasa unaegemea umekuwa kama usalama wa ccm.

Kwa mfano haya mambo ya rushwa za mabilioni , udini kuchinjana kwa imani za kidini, kuchoma makanisa, ukabila, ujangiri hadi watu wanatotosha twiga nje ya nchi, madawa ya kulevya, ushirikina (kuua maarubino) nk haya yanatakiwa yashughulikiwe na usalama wa taifa.

sasa ukiona vituko kama hivi unaweza kuhoji uwepo wa taasisi nyeti kama hii.

Kwa hiyo uzuri wake ulikuwa kwa sababu Late Nyerere meaning that it is not capable on its own.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom