Nadharia ya Usalama wa Taifa (TISS) ibadilike kuanzia sasa, Taifa lipo hatarini

Nadharia ya Usalama wa Taifa (TISS) ibadilike kuanzia sasa, Taifa lipo hatarini

Status
Not open for further replies.
TISS bado inaweza kuwa na meno, ufanisi, wao unategemea sana msimamo wa bosi mkuu yaani raisi wa nchi, maana wanadhani kuna baadhi ya habari anazipenda na atazifanyia kazi na zingine hapendi kuzisikia na hata kama zina maslahi kwa nchi,... ndio hapa hata zipata....

wakati Idara hiyo inafanya kazi kweli kweli, aliyekuwa top man alikuwa muelewa, alipokea kila achopelekwewa, alikifanyia kazi bila kukipuuzia na alikitolea maanuzi au kukiacha kama aligundua kuwa hakina ukweli au maslahi kwa taifa....

Baada ya kubadilisha mfumo wetu wa siasa kutoka chama kimoja kwenda vyama vingi, nadhani kitengo hiki cha Usalama wa taifa kilitakiwa kufanya mabadiliko makubwa ya kimtazamo

Ninaposema mabadiliko ya kimtazano....wakati wa miaka ya 1980, World Bank na IMF, walikuja na Adjusted Struactual Programme, ambazo rais wa kwanza hayati Mwl, aliwashauri aliowaachia nchi juu ya kuwa makini katika kupekea mapendekezo hayo...noja lilikuwa nai kuacha na mfumo wa chama kimija cha siasa na kwenda vyama vingi, sidhani kama walikuwa wanasaidi sana waafrika, maana walijua viongozi wengi wa africa ni walafi wa daraka na hawata kubali kutoka madarakani kwa kura, viongozi hao meitumia sana ofisi hii ya usalama wa taifa kutumia hela nyingi sana ya nchi kuhakikisha chama tawala kinabaki madarakani, wakaacha kazi ya kulinda maslahi ya nchi, maana sidhani kama kazi ya usalama wa taifa ni kuwalinda watawala, maana ndio kazi pekee wanayoifanya na kwa madaha kwa sasa...maana ninashindwa kuelwa wanashindwaje kujua wizi wa pesa za umma mabilioni kwa mabilioni, mikataba mibovu, hujuma za wizi bandari, hujuma kwa shirika la reli n.k, wakati kwa sasa kuna vijana wasomi wengi zaidi ya wakati wa awamu ya kwanza......

Tunahitaji madadiliko ya kimtazamo, wajue kwamba kazi yao sio kusimama nyuma ya viongozi, kama wanafanya kazi vizuri, usalama wa viongozi unakuwa mbubwa kama watanzania wanakuwa wameshiba, wanapata huduma za afya kwa gharama nafuu...lakini kama hawa wana-njaa, basi hata kila kiongozi awe na walizi 1,000 hamta wedha kuwazuia wakitaka kundhuru

Taasisi hii ambayo ndio uhai wa taifa letu imefanya mengi ya kutukuka na yasiyomithirika hata kwa chembe ya haradali.

Wadadisi wa masuala ya kiusalama wataungana nami kuwa TISS ndicho chombo pekee cha nchi hii kilichofanya kazi yake kwaufanisi mkubwa na kulifikisha taifa hapa lilipo,

Naelewa wengi watanishangaa na kuhamaki, kwanini naisifia taasisi hii ambayo wengi wapo nayo mlengo wakushoto.

Kama si uimara wa taasisi hii leo tungalikuwa tunanena kwa lugha yake kila mmoja wetu hapa nchini.

Pamoja na kusimama imara kwa taasisi hii, yapo mambo ya msingi yanayo takiwa kuwekwa sawa ili taasisi hii iendane na mageuzi ya dunia ya leo hasahasa kuelekea 2015.

Sheria iliyounda chombo hiki inamapungufu kwa sasa kulingana na mageuzi ya kifikra na kiteknolojia,

Sheria hii inaififisha tasisi hii huku ikiruhusu siasa kujipenyeza ndani ya chombo hiki adhimu na muhimu kwa uhai wa taifa letu,

Mathalani sheria hiyo inasema, "taasisi hii itahusika/itajihusisha na kutambua/kubaini na kutoa ushauri tu"

Kwamaneno hayo tu, TISS imenyimwa nguvu ya mojakwamoja, kama zilivyo taasisi za wenzetu huko ughaibuni tulikozoea kuakisi kila kitu.

Hii inatoa fursa kwa viongozi wa kitaifa (rais) kuingiza wazo lao lolote walipendalo, liwe jema kwa taifa ama jema kwao binafsi. Lakini hatari zaidi inakuja pale watawala wanapoingiza itikati zao za kisiasa katika chombo hiki,

Bunge la Tanzania linayofursa ya kuihuisha sheria hii ili taasisi hii ya Usalama wa Taifa iwe huru na iwe na meno, yaani (ibaini na kuzuia yenyewe)

Naiona hatari iliyombele yetu, hasa ya kisiasa na machafuko ya kiroho.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki TISS.
 
Hiyo sheria isiyoipa meno TISS ilianzishwa lini? Tangu wakati wa Nyerere hiyo sheria ilikuwa hivyo hivyo ilivyo na bado usalama wa taifa walifanya mambo makubwa yenye tija kwa taifa, hata kuipelekea Tanzania kuwa nchi ya mfano katika suala zima la amani na usalama wa raia.

Nionavyo mimi, tatizo si sheria, ila tatizo ni mfumo wa serikali, hasa hii ya Kikwete kuendesha mambo kishikaji na kwa maslahi binafsi. Wakati zamani mtu alikuwa anaingia kwenye idara ya usalama wa taifa kutokana na maadili yake na pia uwezo wake wa kuchambua mambo na akili za darasani pia, siku hizi unaingia usalama wa taifa kupitia wazazi, ndugu na marafiki. Usalama wa taifa imekuwa ni ajira on its own, mzazi ambaye mtoto wake amefeli shule anampeleka usalama wa taifa. Zamani mtu anaweza kuwa mwalimu by profession lakini anafanya kazi za usalama wa Taifa, ndivyo ilivyokuwa wakati wa Nyerere. Lakini siku hizi usalama wa Taifa wanakaa ofisini. Nawafahamu usalama wa Taifa waliokuwa wanachoma chips pale Ilula miaka hiyo, lakini miaka ya leo ni usalama wa taifa gani atakayekubali kwenda kuchoma chips?

La pili, zamani usalama wa taifa ulikuwa unafanya kazi kwa maslahi ya taifa, sasa hivi usalama wa taifa, wanapokea rushwa! Kwa hiyo kwenye dili kama hizi za wizi wa pembe za ndovu usalama wa taifa wanakula cha kwao na kuwasaidia wezi kupitisha pembe za ndovu. Na sababu kubwa ya hili ni huu mtindo mpya wa kupeana nafasi za usalama wa taifa kwa misingi ya undugu na kujuana badala ya ule utaratibu wa zamani wa kumwandaa mtoto tangu yupo shule ya msingi kutokana na maadili na umakini wake katika utendaji wa mambo. Siku hizi wezi wanawapigia simu usalama wa taifa kuomba wapitishe mzigo wa wizi, zikiwemo nyara za taifa. Sasa hawa ukiwapa full authority si watafagia kila kitu?

Na lingine, viongozi wa serikali ni wababe wa kutetea maslahi yao binafsi na wasio na uwezo wa kuchukua hatua dhidi ya ubadhirifu wa mali za umma. Watu kama akina Pinda hata wakiletewa taarifa yenye ushahidi wote kwamba Illunga ametangaza waislam waue maaskofu, ataanza ....nafikiri nafikiri tumpe kwanza muda tuone kama ataendelea. Watu wanahamisha hela mchana kweupe kupeleka nje ya nchi, lakini taarifa hizi zikifika kwa akina Kikwete wanampigia simu mwizi na kumwambia niwekee na mimi kiasi fulani kwenye akaunti yangu ya UK ili nikulinde. Katika hapo huwezi kutalajia ufanisi wowote.

Kwa mawazo yangu, badala ya kufikiria kubadilisha sheria, tubadilishe viongozi wa nchi pia tubadilishe mfumo wa kuwaajiri hawa usalama wa taifa ili wawe hakika kwa ajili ya maslahi ya taifa na si vinginevyo. Kwa mfano wazo la kubadili hiyo sheria linaweza kuwa ni la hovyo sana katika wakati huu ambapo usalama wa taifa wanakula rushwa na wanafanya kazi kwa maslahi ya watu na chama fulani. Hivi niambie usalama wa taifa wakiwa na mamlaka kamili na wana rungu la kuitetea CCM au kuhalalisha rushwa ya uchaguzi unafikiri kuna kitu kitatoka salama hapo?

Mimi naona wabaki kama washauri lakini wawe na mahali pengine pa kusemea. Kwa mfano wawe na opportunity ya kushare mambo yao na kamati ya bunge ya ulinzi na usalama. Hii itasaidia kuwapa habari wananchi iwapo kuna mambo ya hatari kwa taifa ambayo Rais ameambiwa lakini hajataka kuchukua hatua. Kwahiyo wakiona Rais amewapuuza basi wapeleke habari kwenye kamati ya bunge ya ulinzi na usalama kwa ajili ya hatua zaidi. Hili kidogo linaweza kusaidia kuliko wao wenyewe kuchukua hatua. Na hasa pale ambapo siasa zinaingilia mfumo wa usalama wa taifa.

Nafikiri turudishe nchi yetu kwenye mfumo na maadili yanayokubalika ya uongozi. Na kwa mtizamo wangu, kama nilivyowahi kushauri wakati fulani, ni kwamba kama ataingia kiongozi mwenye maadili mema ni vema avunje kabisa hili jeshi la usalama wa Taifa na aanze kuliunda upya. Hili lililopo sasa lipo totally polluted. Na uongozi wa serikali ndiyo ten times polluted, full utilization ya usalama wa taifa kwa maslahi ya watu na maslahi ya chama fulani. Usalama wa taifa wa sasa uvunjwe, uundwe upya, kwa kuzingatia miiko, maadili na maslahi mapana ya taifa.
 
Sijui kwanini hawakumpa ole Terere,ukurugenzi wa TISS.jamaa hanaga utani kwenye kazi.
 
Kwa taifa ambalo ni ambitious,Usalama wa Taifa ni taasisi inayotakiwa kufanya kazi kwa weledi kuliko idara yoyote ile.Weledi wake hautakiwi kutiliwa shaka yoyote kwa viwango vya kitaifa,kiakanda(regional) au kimataifa kwa maana pana zaidi.TISS inatakiwa kutengeneza mfumo ambao ni more sophisticated katika kufanya information sharing wakati huo huo ikijaribu kuimarisha vitengo vilivyopo ili kutimiza malengo ya idara na taasisi kwa ujumla kama ilivyo mifumo ya mataifa makubwa kama Mkakati waq ulinzi na usalama wa Marekani,Uingereza,Pakistan,Israel,Afrika Kusini,China,India na Canada

Ingawa miakati mingi ya mataifa yaliyoendelea imekua sensitive zaidi kwenye maslahi yao ya kiuchumi na ushindani wa nguvu na mamlaka kimataifa(Power Interests) lakini kwa taifa lililofikisha umri wa miaka 50 ni lazima liwe ambitious na kwa kuanzia ni lazima tungeanza na kanda yetu ya Maziwa makuu,Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla.

Kwa mfano tuna washindani wetu kiuchumi na power struggle hapa east afica ambao ni Kenya.Hatujaweza vya kutosha kwenye Economic intelligence kule Kenya inagawa wao wamewekeza hapa kwetu.Leo hii Kenya ina-export TANZANITE,Wana-Export gold n.k.Balance of trade kati ya Tanzania na Kenya ni subject of Economic intelligence.tunapotunga sera zetu za kiuchumi tunatakiwa tutumie taarifa za kiinteligesnsia kwa kutumia wataalamu waliobobea na pia tuangalie possible scenarios na move za washindani wetu.Katika maofisa ubalozi wetu walioko Kenya tujiulize ni wangapi wenye uwezo kusimamia maslahi yetu ya kiuchumi hapa EAC au ukanda kupitia economic power house(Kenya) katika ukanda huu?

Kuna mgogoro kati ya dola na sarafu yetu.Je hakuna uwezekano kwamba dola zimekua zikinunuliwa kwa wingi na kuwa smuggled kwenda Kenya ili kuhujumu uchumi wetu na ku-frustrate fisical na monetary policy zetu?
Usalama wetu bado unahitaji mageuzi kutegemeana na matakwa ya kisheria na kuboresha malengo ya TISS ili iwe modern zaidi
Malengo ya TISS kulingana na trend ya dunia kwa sasa na mahitaji ya taifa tunakopitia kisiasa,kiuchumi na kiutamaduni yaegemee katika kutabiri(si utabiri wa majini/tunguri bali utabiri wa kisayansi),Kupenya,na kuwahi matukio ya hatari kwa maslahi na usalama wa taifa letu,na kuwasaidia wale wanaotekeleza sera yetu ya ulinzi na usalama,kulinda taifa na watu wake,utekelezaji wa sheria na kulinda maslahi na sera zetu kitaifa bila kuathiriwa na ushawishi au hatari yoyote kutoka ndani na nje ya taiafa letu na kulinda malengo yetu kama jamii kwenye Nyanja za kimataifa(jamii nyingine)

Malengo makuu yanatakiwa kujikita katika

Mosi,Kuongeza nafasi na umuhimu wa idara ya mahakama na vyombo vya kutoa haki.Lengo hapa linatakiwa kuwa juu ya kuunganisha idara za mahakama,wizara ya mambo ya ndani na vitengo vyake kwa kuzingatia upeanaji wa taarifa huku haki za msingi za kiraia zikilindwa pamoja na uhuru wake tofauti na ilivyo sasa ambako TISS inatuhumiwa kutumika kuhujumu haki za kiraia kwa visingizio lukuki.Lengo kuu liwe kulinda haki na uhuru wa watu bila kuathiri maslahi ya jumla.Hili linahitaji ushirikiano kuanzia serikali kuu,mikoa,wilaya,majimbo ya uchaguzi,kata na hata ngazi ya mitaa pamoja na sekta binafsi

Pili,Utengenezwe utamaduni mpya wa kuahamasisha mawazo mbadala na matumizi ya weledi(professionalism/expertise):Kubadili utamaduni ndani ya TISS ni muhimu sana ili kuepuka mimosa ya kimkakati. It is necessary to create an intellectual culture that promotes discussion as well as dissenting opinion. It will require the use of collaborative technology, where subject expertise is maximized, increased cross-agency communication, and the exploration of alternative analysis

Tatu,Kurahisisha zaidi ukusanyaji wa taarifa za kintelijensia:TISS haina budi kuwa mbele katika matumizi ya teknolojia na pia ku-update wataalamu wake kitaaluma na katika matumizi ya zana za kisasa zaidi ili kurahisisha ukusanyaji huo kutoka Open-sources na kutoka Human-sources

Nne,Kuajiri watu kulingana na uwezo na taaluma zao na pia kuajiri watu ambao tayari wana ajira kwenye vitengo vingine lakini walipwe vizuri kwa ajili ya kazi ya usalama ili kupunguza gharama za kupachika watu wapya katika idara,mashirika na taasisi nyeti nchini.Pamoja na hili kitu cha muhimu watu hawa ni lazima wawe na sifa zinazofanana (common attributes) katika ujanja,uwezo wa hali ya juu na haraka katika utendaji huku maadili ya juu kabisa katika vigezo vya utendaji katika idara hii vikizingatiwa

Tano,TISS ibadili utamaduni wa kuhitaji-kujua kwenda Kuhitaji-kutoa taarifa(changing from the culture of need-to-Know to need-to-share):Ili kuongeza ushirikiano na ufanisi katika kila ngazi ni lazima mtazamo wa idara hii ubadilike na suala la kutoa taarifa liwe ndiyo njia kuu ya kufanikisha malengo ya idara katika ngazi zote kwa hiyo kuna haja ya kuangalia jinsi taarifa zinavyofika kwa ubora unaotakiwa,kwa usahihi na kwa muda muafaka na hili ni muhimu na litasaidia zaidi kuwa karibu na watunga sera(policy makers)

Sita,Kuimarisha na kupanua zaidi uhusiano kati ya TISS na washirika wa ndani ya nchi na vitengo vingine vya kijasusi vya mataifa ya nje:Hii ni kwa kuwa tunaweza kuwa na common threats kwenye uchumi,kiitikadi,kiutamaduni,kiulinzi n.kHata hivyo taarifa za kijasusi kutoaka kwa washirika wetu ni lazima ziangaliwe kwa umakini wa hali ya juu na pia tuwe na taarifa zetu ambazo tunaweza kulinganisha na taarifa za washrika wetu.Hizi kwa kijasusi zinaitwa 'Corroboration codification'
Saba,kitengo kidogo kabisa cha mwisho ndichokinachotakiwa kuwa na acces ya taarifa nyeti lakini kitengo hicho kiwe scrutinized kwa hali na mali.Hata hivyo nitajadili kuhusu juu ya mfumo wetu mbovu wa counterintelligence

Nane,Kujenga mfumo ambao ni uniform zaidi katika utekelazi kisayansi na kiteknolojia,Ni lazima sasa idara iwe centralized katika kutoa maelekezo na iwe more decentaliced katika utekelezaji kwa mtindo ambao unaitwa 'pyramid execution'.unified research itumike ili kuongeza ushirikiano na idara mbali mbali

Tisa,Mfumo wa kupongeza na kuzawadia utumike kuongeza performance

Kumi,mtindo wa kutumia miongo utumike lakini zaidi kwa haraka mtindo wa kutumia siku utumike badala ya miaka.Kwa mfano 720 days plan itumike badala ya miaka 2,180 days pla itumike badala ya 6 months plan kwa ajili ya monitoring na kuepuka urasimu na uvivu usio wa lazima

Pia ni vyema kutokana na power struggle ya ukanda tuunde vitengo vya ujasusi vya nje.kitengo hiki kifanane kwa muundo ingawa kutakua na marekebisho kidogo lakini kifanane na kitengo cha RAW cha india ambacho kiliundwa baada ya vita ya India na China.kabla ya hapo kulikua na kitengo cha IB ambacho kilikua na miaka 120 lakini hicho kilitumika kuchunguza watu zaidi na taasisi za kisaiasa.waingereza walikitumia kuwachunguza akina Mahatma Gandhi,Azad na Nehru zaidi.Kitengo cha RAW kinatumika kwa ajili ya military Intelligence na financial intelligence.Kuna haja ya kupima maofisa ubalozi wetu wanaopelekwa nje pamoja na Mwambata wa jeshi katika balozi zetu(defence attaché) kulingana na sera yetu.

Kwa bahati mbaya sera yetu ya mambo ya nje tumeipigia kelele sana ifumuliwe.Naamini Mungu akitupa uhai CHADEMA itakuja na sera bora zaidi ya mambo ya nje specifically kwa regions na strategic partners
 
Ben Saanane,

Asante sana mkuu, nilikuwa natafuta sana mawazo yako katika uzi huu, naaaam umetii kiu yangu na yawatanzania kabisa,

Mkuu umegusa maeneo yote nyeti kitaasisi. Bila shaka tutazidi kuwa begakwabega kuhimiza uhuishaji wa taasisi hii iendani na dunia ya leo iendavyo.
 
Last edited by a moderator:
Yote ni muhimu yakatazamwa, lakini muhimu zaidi ni sheria na teknolojia

hivi kwa upande wa sheria unataka kusema miaka kadhaa ya nyuma performance ya TISS iliathiriwa na sheria hii?
Kuhusu technolojia,mbona inasemekana matumizi ya tecknolojia yamepunguza usiri wa kazi hii?
 
TISS ni zaidi ya muijuavyo,msione mambo yanakwenda kama yalivyo mkajua hawajui kitu au wamelala,si kweli.
 
hivi kwa upande wa sheria unataka kusema miaka kadhaa ya nyuma performance ya TISS iliathiriwa na sheria hii?
Kuhusu technolojia,mbona inasemekana matumizi ya tecknolojia yamepunguza usiri wa kazi hii?
Miaka ya nyuma utendaji kazi wa taasisi hii haukuarithiriwa sana na mapungufu ya sheria hii, hilo lilitokana na mfumo wa siasa ya nchi hii kuwa ya chama kimoja, na uimara wa viongozi waliopita hasa kwa weledi na uadilifu,

Kiteknolojia bado tupo nyuma sana tena sana, hivyo tunahitaji mageuzi yaendayo kasi sawa na dunia iendavyo sasa leo,
 
yaani humu ndani watu wenye uzalendo wa kweli utawajua tu kwa post zao. lakini wengine wapo kishabiki mno. badala ya kujadili mfumo mzima wa utendaji kazi wa idara yetu wengine wanaanza kumshambulia mtu. kumbukeni nchi haijengwi kwa kutukanana bali kwa kutoa mawazo chanya.
 
What is this? Mental dyslexia?

unajua kiranga, kuna watu nafikiri wana utindiwa wa ubongo. badala ya kuchangia hoja za msingi wanaanza kuiona idara dhaifu eti kwa sababu kuna njaa nchini. badala ya kuanza kuangalia nini chanzo cha kuwepo kwa tatizo la njaa mtu anapita njia ya mkato ya kuilaumu idara. hata matokeo ya form four 2012 yalivyokuwa mabaya kuna watu nimewasikia wanaigusia idara
 
Taasisi hii ambayo ndio uhai wa taifa letu imefanya mengi ya kutukuka na yasiyomithirika hata kwa chembe ya haradali.

Wadadisi wa masuala ya kiusalama wataungana nami kuwa TISS ndicho chombo pekee cha nchi hii kilichofanya kazi yake kwaufanisi mkubwa na kulifikisha taifa hapa lilipo,

Naelewa wengi watanishangaa na kuhamaki, kwanini naisifia taasisi hii ambayo wengi wapo nayo mlengo wakushoto.

Kama si uimara wa taasisi hii leo tungalikuwa tunanena kwa lugha yake kila mmoja wetu hapa nchini.

Pamoja na kusimama imara kwa taasisi hii, yapo mambo ya msingi yanayo takiwa kuwekwa sawa ili taasisi hii iendane na mageuzi ya dunia ya leo hasahasa kuelekea 2015.

Sheria iliyounda chombo hiki inamapungufu kwa sasa kulingana na mageuzi ya kifikra na kiteknolojia,

Sheria hii inaififisha tasisi hii huku ikiruhusu siasa kujipenyeza ndani ya chombo hiki adhimu na muhimu kwa uhai wa taifa letu,

Mathalani sheria hiyo inasema, "taasisi hii itahusika/itajihusisha na kutambua/kubaini na kutoa ushauri tu"

Kwamaneno hayo tu, TISS imenyimwa nguvu ya mojakwamoja, kama zilivyo taasisi za wenzetu huko ughaibuni tulikozoea kuakisi kila kitu.

Hii inatoa fursa kwa viongozi wa kitaifa (rais) kuingiza wazo lao lolote walipendalo, liwe jema kwa taifa ama jema kwao binafsi. Lakini hatari zaidi inakuja pale watawala wanapoingiza itikati zao za kisiasa katika chombo hiki,

Bunge la Tanzania linayofursa ya kuihuisha sheria hii ili taasisi hii ya Usalama wa Taifa iwe huru na iwe na meno, yaani (ibaini na kuzuia yenyewe)

Naiona hatari iliyombele yetu, hasa ya kisiasa na machafuko ya kiroho.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki TISS.

Mkuu,

Tatizo siyo sheria ila tatizo ni watu.
Kama huna watu wenye mawazo ya kujenga taifa bora katika taasisi nyeti kama hii, usitegemee lolote la maana hata kama una sheria nzuri kiasi gani.
Kutunga sheria ni jambo moja na kusimamia matumizi ya sheria hiyo ni jambo lingine linalotegemea sana watendaji, na hili la mwisho ndilo la muhimu zaidi.
Kwa sheria moja inayotumika kwa wakati huo mawaziri kama Magufuli, Mwakyembe na mwingine yeyote anayeweza kufananishwa nao wanafanya mambo mazuri ya faida kwa nchi lakini waziri bogus atasingizia sheria kuwa ni mbaya inahitaji kubadilishwa!
Tunahitaji kuweka maslahi ya uma mbele kuliko kuwa watumwa wa sheria!
 
unajua kiranga, kuna watu nafikiri wana utindiwa wa ubongo. badala ya kuchangia hoja za msingi wanaanza kuiona idara dhaifu eti kwa sababu kuna njaa nchini. badala ya kuanza kuangalia nini chanzo cha kuwepo kwa tatizo la njaa mtu anapita njia ya mkato ya kuilaumu idara. hata matokeo ya form four 2012 yalivyokuwa mabaya kuna watu nimewasikia wanaigusia idara

Tatizo lako unaangalia mambo katika mawazo mgando wakati dunia ina evolve.

Nilikuwa naongea na Balozi wa Tanzania Umoja wa Mataifa kipindi hicho, Dr. Augustine Philip Mahiga, mwanadiplomasia aliyebobea ambaye aliwahi kuwa mkuu wa usalama wa taifa kabla hata usalama wa taifa haujarasimishwa, enzi za Nyerere. Kuhusu challenges za usalama za ulimwengu, na Tanzania, hususan in the wake of 9/11.

Dr. Mahiga, mmoja kati ya ma dokta wa ukweli ninaowaamini Tanzania ambaye akiongea mtu unamjua huyu ni msomi hata kabla hajakuambia "mimi ni Balozi Dr. Mahiga", akaniambia mataifa makubwa yana ajenda zao za usalama na ajenda hizi si lazima ziwe sawa na ajenda za mataifa madogo katika suala la usalama.

Tukazungumza sana jinsi gani swala zima la "food security" linavyokosa kuongelewa vizuri Umoja wa Mataifa kwa sababu tu mataifa makubwa yamekazania "terrorism" in the context of Al-Qaeda and similar threats.

Akajenga hoja, ambayo sikuweza kuipinga, kwamba huku nchi masikini kwetu njaa inaweza kuwa "terror" kubwa kuliko Al-Qaeda, na at least inatubidi tuipe kipaumbele angalau sawa na hizo habari za Al-Qaeda, kama si zaidi.

Alielewa "food security" as a part of "national security".

Sasa wewe unakuja na one track mind kufikiri tu kwamba "usalama wa taifa ni mashushushu, kazi yao ni upelelezi na ujasusi". Period. Huwezi kuona kwamba hata "food security" ni sehemu ya usalama wa taifa.

Na kama tuna ukame periodically, Usalama wa taifa unatakiwa kuandaa contingencies za kuweza kukabili ukame wakati wowote.

Na kwamba sehemu yoyote kukiwa na ukame ni failure ya food security ambayo moja kwa moja ni failure ya national security, hata in the context ya "a hungry man is an angry man" tu. Mitatizo kibao ya wananchi kuchoma moto nyumba za wabunge na wakuu wa mikoa ukiiangalia kwa juu juu utaona ni masuala ya failure ya usalama wa taifa katika context ya usalama wa taifa kukosa kujua nini kinaendelea na ku project nini kitatokea, lakini ukiangalia zaidi utaona ni failure ya usalama wa taifa zaidi kwa sababu ina correlation na food security.

Njaa ni mafuta yanayosubiri cheche tu kulipuka na kutoa vurugu.Usalama wa taifa .

The Roman poet Juvenal was no fool when he said "food and circuses" as the ultimate tools of pacifying the hoi polloi. Trouble is, we are not getting even the bread, much less any worthy circus!

The Arab spring in Egypt was caused as much by Mubarak's oppressive regime as by the rise in the price of bread, a staple there. I can remember the exact day I was reading a NYT article about the rise of the price of bread in Egypt and concluding that it was only a matter of time before something momentous was going to happen there. And this was before the Tunisian vegggie vendor suicide.

Njaa inaleta vishawishi hata mwananchi ahujumu nchi yake mwenyewe. Usalama wa taifa. Angalia Mali huko hajulikani nani raia nani Al-Qaeda, njaa tu hiyo.

You cannot talk about addressing national security if you cannot address food security.

Ndiyo maana nau indict "Usalama wa Taifa" kwa kushindwa kudhibiti njaa tu nchini. Je ukishindwa kudhibiti njaa tu nchini, utaweza kudhibiti Chinese, American and Iranian hackers wasiingilie computers za Ikulu?

Ikulu inatumia Yahoo emails, Yahoo hata hawatumii https, wanatumia http!

Usalama wa taifa unajua tofauti ya http na https?
 
Hiyo sheria isiyoipa meno TISS ilianzishwa lini? Tangu wakati wa Nyerere hiyo sheria ilikuwa hivyo hivyo ilivyo na bado usalama wa taifa walifanya mambo makubwa yenye tija kwa taifa, hata kuipelekea Tanzania kuwa nchi ya mfano katika suala zima la amani na usalama wa raia.

Nionavyo mimi, tatizo si sheria, ila tatizo ni mfumo wa serikali, hasa hii ya Kikwete kuendesha mambo kishikaji na kwa maslahi binafsi. Wakati zamani mtu alikuwa anaingia kwenye idara ya usalama wa taifa kutokana na maadili yake na pia uwezo wake wa kuchambua mambo na akili za darasani pia, siku hizi unaingia usalama wa taifa kupitia wazazi, ndugu na marafiki. Usalama wa taifa imekuwa ni ajira on its own, mzazi ambaye mtoto wake amefeli shule anampeleka usalama wa taifa. Zamani mtu anaweza kuwa mwalimu by profession lakini anafanya kazi za usalama wa Taifa, ndivyo ilivyokuwa wakati wa Nyerere. Lakini siku hizi usalama wa Taifa wanakaa ofisini. Nawafahamu usalama wa Taifa waliokuwa wanachoma chips pale Ilula miaka hiyo, lakini miaka ya leo ni usalama wa taifa gani atakayekubali kwenda kuchoma chips?

La pili, zamani usalama wa taifa ulikuwa unafanya kazi kwa maslahi ya taifa, sasa hivi usalama wa taifa, wanapokea rushwa! Kwa hiyo kwenye dili kama hizi za wizi wa pembe za ndovu usalama wa taifa wanakula cha kwao na kuwasaidia wezi kupitisha pembe za ndovu. Na sababu kubwa ya hili ni huu mtindo mpya wa kupeana nafasi za usalama wa taifa kwa misingi ya undugu na kujuana badala ya ule utaratibu wa zamani wa kumwandaa mtoto tangu yupo shule ya msingi kutokana na maadili na umakini wake katika utendaji wa mambo. Siku hizi wezi wanawapigia simu usalama wa taifa kuomba wapitishe mzigo wa wizi, zikiwemo nyara za taifa. Sasa hawa ukiwapa full authority si watafagia kila kitu?

Na lingine, viongozi wa serikali ni wababe wa kutetea maslahi yao binafsi na wasio na uwezo wa kuchukua hatua dhidi ya ubadhirifu wa mali za umma. Watu kama akina Pinda hata wakiletewa taarifa yenye ushahidi wote kwamba Illunga ametangaza waislam waue maaskofu, ataanza ....nafikiri nafikiri tumpe kwanza muda tuone kama ataendelea. Watu wanahamisha hela mchana kweupe kupeleka nje ya nchi, lakini taarifa hizi zikifika kwa akina Kikwete wanampigia simu mwizi na kumwambia niwekee na mimi kiasi fulani kwenye akaunti yangu ya UK ili nikulinde. Katika hapo huwezi kutalajia ufanisi wowote.

Kwa mawazo yangu, badala ya kufikiria kubadilisha sheria, tubadilishe viongozi wa nchi pia tubadilishe mfumo wa kuwaajiri hawa usalama wa taifa ili wawe hakika kwa ajili ya maslahi ya taifa na si vinginevyo. Kwa mfano wazo la kubadili hiyo sheria linaweza kuwa ni la hovyo sana katika wakati huu ambapo usalama wa taifa wanakula rushwa na wanafanya kazi kwa maslahi ya watu na chama fulani. Hivi niambie usalama wa taifa wakiwa na mamlaka kamili na wana rungu la kuitetea CCM au kuhalalisha rushwa ya uchaguzi unafikiri kuna kitu kitatoka salama hapo?

Mimi naona wabaki kama washauri lakini wawe na mahali pengine pa kusemea. Kwa mfano wawe na opportunity ya kushare mambo yao na kamati ya bunge ya ulinzi na usalama. Hii itasaidia kuwapa habari wananchi iwapo kuna mambo ya hatari kwa taifa ambayo Rais ameambiwa lakini hajataka kuchukua hatua. Kwahiyo wakiona Rais amewapuuza basi wapeleke habari kwenye kamati ya bunge ya ulinzi na usalama kwa ajili ya hatua zaidi. Hili kidogo linaweza kusaidia kuliko wao wenyewe kuchukua hatua. Na hasa pale ambapo siasa zinaingilia mfumo wa usalama wa taifa.

Nafikiri turudishe nchi yetu kwenye mfumo na maadili yanayokubalika ya uongozi. Na kwa mtizamo wangu, kama nilivyowahi kushauri wakati fulani, ni kwamba kama ataingia kiongozi mwenye maadili mema ni vema avunje kabisa hili jeshi la usalama wa Taifa na aanze kuliunda upya. Hili lililopo sasa lipo totally polluted. Na uongozi wa serikali ndiyo ten times polluted, full utilization ya usalama wa taifa kwa maslahi ya watu na maslahi ya chama fulani. Usalama wa taifa wa sasa uvunjwe, uundwe upya, kwa kuzingatia miiko, maadili na maslahi mapana ya taifa.

mkuu, kumbuka idara inayozungumzwa humu ni hii TISS ambayo imeanzishwa kwa mujibu wa sheria ya mwaka 1996, mwaka mmoja tu baada ya rais mkapa kuwa rais wa nchi. kwachangiaji wengi wanaona kuwa sheria ndiyo kikwazo. kwanza napenda kuwapongeza viongozi wa Idara hii kwa kwa kutekeleza majukumu yao bila ya kukiuka misingi iliyowekwa ndani ya sheria hiyo. hao ni viongozi tunaowataka kwa vile wanaongoza kwa mujibu wa sheria za nchi. ninahakika kama viongozi wa tiss wangeamua kufanya mambo yao bila ya kuangalia sheria inasema nini, uwezo huo wanao na hakuna wa kuwazuia. ila kwa kuwa nchi hii inaongozwa kwa misiongi ya sheria na haki ndo maana leo hii tunapiga kelele na wengine kudiriki hata kuwatukana viongozi wa idara hii nyeti
 
Taasisi hii ambayo ndio uhai wa taifa letu imefanya mengi ya kutukuka na yasiyomithirika hata kwa chembe ya haradali.

Wadadisi wa masuala ya kiusalama wataungana nami kuwa TISS ndicho chombo pekee cha nchi hii kilichofanya kazi yake kwaufanisi mkubwa na kulifikisha taifa hapa lil)lewa wengi watanishangaa na kuhamaki, kwanini naisifia taasisi hii ambayo wengi wapo nayo mlengo wakushoto.

Kama si uimara wa taasisi hii leo tungalikuwa tunanena kwa lugha yake kila mmoja wetu hapa nchini.

Pamoja na kusimama imara kwa taasisi hii, yapo mambo ya msingi yanayo takiwa kuwekwa sawa ili taasisi hii iendane na mageuzi ya dunia ya leo hasahasa kuelekea 2015.

Sheria iliyounda chombo hiki inamapungufu kwa sasa kulingana na mageuzi ya kifikra na kiteknolojia,

Sheria hii inaififisha tasisi hii huku ikiruhusu siasa kujipenyeza ndani ya chombo hiki adhimu na muhimu kwa uhai wa taifa letu,

Mathalani sheria hiyo inasema, "taasisi hii itahusika/itajihusisha na kutambua/kubaini na kutoa ushauri tu"

Kwamaneno hayo tu, TISS imenyimwa nguvu ya mojakwamoja, kama zilivyo taasisi za wenzetu huko ughaibuni tulikozoea kuakisi kila kitu.

Hii inatoa fursa kwa viongozi wa kitaifa (rais) kuingiza wazo lao lolote walipendalo, liwe jema kwa taifa ama jema kwao binafsi. Lakini hatari zaidi inakuja pale watawala wanapoingiza itikati zao za kisiasa katika chombo hiki,

Bunge la Tanzania linayofursa ya kuihuisha sheria hii ili taasisi hii ya Usalama wa Taifa iwe huru na iwe na meno, yaani (ibaini na kuzuia yenyewe)

Naiona hatari iliyombele yetu, hasa ya kisiasa na machafuko ya kiroho.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki TISS.
Hakuna ubishi kwamba taasisi hii imefanya mengi katika historia ya nchi yetu. Jambo la kusikitisha ni jinsi utendaji wa asasi hii ulivyoporomoka ghafla katika awamu mbili ambapo kumefanyika uhalifu dhidi ya taifa bila ya wao kuchukua hatua. Yaelekea wanasiasa wamefaulu kuwachakachua na sasa wana behave kama watumishi wa mtu Binafsi.
 
Tatizo lako unaangalia mambo katika mawazo mgando wakati dunia ina evolve.

Nilikuwa naongea na Balozi wa Tanzania Umoja wa Mataifa kipindi hicho, Dr. Augustine Philip Mahiga, mwanadiplomasia aliyebobea ambaye aliwahi kuwa mkuu wa usalama wa taifa kabla hata usalama wa taifa haujarasimishwa, enzi za Nyerere. Kuhusu challenges za usalama za ulimwengu, na Tanzania, hususan in the wake of 9/11.

Dr. Mahiga, mmoja kati ya ma dokta wa ukweli ninaowaamini Tanzania ambaye akiongea mtu unamjua huyu ni msomi hata kabla hajakuambia "mimi ni Balozi Dr. Mahiga", akaniambia mataifa makubwa yana ajenda zao za usalama na ajenda hizi si lazima ziwe sawa na ajenda za mataifa madogo katika suala la usalama.

Tukazungumza sana jinsi gani swala zima la "food security" linavyokosa kuongelewa vizuri Umoja wa Mataifa kwa sababu tu mataifa makubwa yamekazania "terrorism" in the context of Al-Qaeda and similar threats.

Akajenga hoja, ambayo sikuweza kuipinga, kwamba huku nchi masikini kwetu njaa inaweza kuwa "terror" kubwa kuliko Al-Qaeda, na at least inatubidi tuipe kipaumbele angalau sawa na hizo habari za Al-Qaeda, kama si zaidi.

Alielewa "food security" as a part of "national security".

Sasa wewe unakuja na one track mind kufikiri tu kwamba "usalama wa taifa ni mashushushu, kazi yao ni upelelezi na ujasusi". Period. Huwezi kuona kwamba hata "food security" ni sehemu ya usalama wa taifa.

Na kama tuna ukame periodically, Usalama wa taifa unatakiwa kuandaa contingencies za kuweza kukabili ukame wakati wowote.

Na kwamba sehemu yoyote kukiwa na ukame ni failure ya food security ambayo moja kwa moja ni failure ya national security, hata in the context ya "a hungry man is an angry man" tu. Mitatizo kibao ya wananchi kuchoma moto nyumba za wabunge na wakuu wa mikoa ukiiangalia kwa juu juu utaona ni masuala ya failure ya usalama wa taifa katika context ya usalama wa taifa kukosa kujua nini kinaendelea na ku project nini kitatokea, lakini ukiangalia zaidi utaona ni failure ya usalama wa taifa zaidi kwa sababu ina correlation na food security.

Njaa ni mafuta yanayosubili cheche tu kulipuka na kutoa vurugu.Usalama wa taifa .

Njaa inaleta vishawishi hata mwananchi ahujumu nchi yake mwenyewe. Usalama wa taifa.

You cannot talk about addressing national security if you cannot address food security.

yote uuyasemayo bwana kiranga ni sahihi kabisa na wajumbe wengi wanajaribu kuainisha maeneo mengi ambayo idara inaweza ku play part ili kuhakikisha kuwa nchi hii inakuwa salama wakati wote bila ya kuathiriwa na matatizo hayo ya nmdani. ninaamini kuwa jukumu hilo wanalitekeleza. shida kubwa iliyopo hapa ni kwa kiwango gani idara ishughulikie masuala hayo. nijuavyo mimi ni kuwa kila jambo hapa nchini kuna wizara ambayo inajukumu la kuweka mikakati ya kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika wizara husika. kwa issue ya food security, tuna wizara ya kilimo na chakula. kwa mujibu wa sheria ya idara ya usalama wa taifa ya mwaka 1996, ambayo mchangiaji mwenzetu ametusaidia ni kuwa iodara hii jukumu lake kuu ni kutoa ushauri kwa waziri husika. kwa vile hatuna waziri anayehusika na masuala ya usalama wa taifa, ninaamini kuwa jukumu hilo lipo mikononi mwa rais wa nchi. kwa maana hiyo ni kuwa consumer wa information za idara ni rais mwenyewe. huo ni mfumo ambao waliouandaa akina chenge wanajua lengo lake hasa lilikuwa nini. ila kwa mazingra ya sasa ni vigumu kwa informations zote wanazopata idara consumer akawa rais tu. bila shaka hapo idara itaendelea kulaumiwa. tatizo kubwa lililobainishwa na wachangiaji wengi ni la kisheria na si utendaji wa idara yenyewe
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom