Nadharia ya Usalama wa Taifa (TISS) ibadilike kuanzia sasa, Taifa lipo hatarini

Nadharia ya Usalama wa Taifa (TISS) ibadilike kuanzia sasa, Taifa lipo hatarini

Status
Not open for further replies.
Yericho, tatizo la msingi kwenye hii taasisi sio la kisiasa bali la wanausalama wenyewe. Ukichunguza kwa umakini utagundua kuwa tatizo lake la msingi linaanzia kwenye recruitment yaani usahili. Badala ya kutumia utaratibu aliuacha Mwl. Nyerere ambao unatumika pia na mataifa mengine ambayo taasisi kama hizi zinanguvu. Utaratibu ni kwamba usaili sio zoezi la siku moja bali la miaks kazaa.

Mtu anachunguzwa kuanzia familia yake, primary, secondary hapo kama wamelizika wanamchukua na wengine walikuwa wanachunguzwa mpaka level ya chuo na ndiyo wanachukuliwa lakini sasa hivi wanausalama wenyewe wanashangaana kuwa huyu wa tabia hii ameingiaje humu? Kuna ukabira, udini, ushost, na mpaka ubazazi katika kupata kazi huko. Watu wameona ndiyo sehemu ya kuficha ndugu zao wasio na sifa.

Pamoja na kupewa meno na bunge lazima wabadilishe utendaji wao na ndiyo jamii itawapa heshima yao sitahiki. Vinginevyo watapewa meno na watayatumia kuuma watu wasio na hatia na kuwaacha wenye hatia wakijinafasi kama zilivo sekta nyingine za kutoa haki.
 
You guys are missing a fundamental principle kwenye national intelligence services - intelligence policy. Hivi mmewahi kujiuliza intelligence policy ya Tanzania ni nini? Hivi mnajua sera ya CCM kuhusu Intelligence ni nini?
 
Naomba kuelimishwa usalama wa taifa ni nini?
Kama mmoja wa raia wa Tanzania una haki ya kujua usalama wa Taiafa nini?Kwa miaka ipatayo 51 sasa toka tumepata uhuru mtanzania wa kawaida ajajua maana ya usalama wa Taifa ina maana lengo kuu la Usalama wa Taifa halijatimizwa ilivyopaswa kwa uhalisia na uhakika usio tiliwa shaka na raia yoyote yule mwenye ufahamu wa kawaida [normal citizen] achilia mbalia raia mwenye upeo wa juu wa ujuzi wa mambo ya binadamu na mahusiano yake na viumbe wengine na mazingira yake [intellectual citizen].

Ipo kazi kweli kweli, na hiki ndio kilio kuwa usalama pamoja na majukumu yao ya kazi nzito kwa dhati mambo mengi ya yanaonekana kuibua maswali kuwa kweli tunaenda na nyakati sisi wa Tanzania katika na kujipanga kuwakabili maadui wa ndani na wa nje.Nikitizima mpambano wa marekani na china kwenye swala la vita baridi ya wizi wa taarifa za kiitelenjesia kupitia mtandao napata hofu Je sisi tuna hali gani,japo tunawatanzania wenye vipaji vya juu sana angle hizo lakini naona sijui hata watatumika vipi kulilinda Taifa,wakati hata Mtanzania wa kawaida hajui usalama wa Taifa ni nini?!!!!!Sio kosa lako mkuu!!!na siku Mkuu UMucha...laumu kwa kuwa naamini ni wajibu wa wahusika tajwa kuwa walishapaswa kua wameelimisha umma kwa ujumla wake na kuwapa raia zake haki ya ufahamu juu ya kulilinda Taifa lao kwa kushirikiana na taasisi hsuika.
 
Taasisi hii ambayo ndio uhai wa taifa letu imefanya mengi ya kutukuka na yasiyomithirika hata kwa chembe ya haradali........

Mathalani sheria hiyo inasema, "taasisi hii itahusika/itajihusisha na kutambua/kubaini na kutoa ushauri tu"

Kwamaneno hayo tu, TISS imenyimwa nguvu ya mojakwamoja, kama zilivyo taasisi za wenzetu huko ughaibuni tulikozoea kuakisi kila kitu.

Hii inatoa fursa kwa viongozi wa kitaifa (rais) kuingiza wazo lao lolote walipendalo, liwe jema kwa taifa ama jema kwao binafsi. Lakini hatari zaidi inakuja pale watawala wanapoingiza itikati zao za kisiasa katika chombo hiki,

Bunge la Tanzania linayofursa ya kuihuisha sheria hii ili taasisi hii ya Usalama wa Taifa iwe huru na iwe na meno, yaani (ibaini na kuzuia yenyewe)

Naiona hatari iliyombele yetu, hasa ya kisiasa na machafuko ya kiroho.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki TISS.
Mkuu hii issue ilishapita huku tukajadiliana.Ni kweli TISS inamchango mkuu uliotukuka,lakini msimamo wa mbio za vijiti usiozingatia umahili wa kitaahasisi na nyakati hakika usalama wa Taifa kama jina lilivyo utakuwa shakani.
Binafsi nilichangia na kutoa mada kwenye angle ya TISS humu jamvini na nikasema umefika wakati TISS watoke kuwa IDARA [Department] wawe Taasisi timilifu [INSTITUTIONAL] yenye kujitosheleza na idala yake.Kwa kupewa nafasi ya kuwa Taasisi haki sheria unayo lia nayo tayari itakuwa imekufa kifo cha pekee yake na matamanio ya kuiona taasisi [by now department] yenye meno itakuwa imetimia.

Kwa TISS kuwa taaisisi matamanio yangu kwaweza kuzaliwa idara madhubuti zenye kwenda na nyakati kama idara
1: Ulinzi wa Viongozi
2: Elimu na Mambo ya Sayansi na Technolojia
3: Ujasusi ndani na wa kimataifa
4: Siasa za Ndani [Tanzania Bara na Visiwani] na Mahusiano Ya Kimataifa
5: Maliasili watu na mahusiano ya jamii [Administration and Public Relation]
6: Uchumi na Fedha
7: Maliasili za Taifa

Kwa hayo hakika tunaweza kufika mbali na kuwa na kamati maalumu ambayo pia nayo itakuwa mlinzi wa jicho la mwenendo mzima wa TISS [Watchdog] isiwe ile misemo ya the court break become the court breaker!!inapata nafasi ya kutumika. Ina maana kwa TISS kuwa taasisi itwajibika kwa Wananchi kupitia Bunge! Na DG wao atateuliwa na Rais lakini atapitishwa na Bunge. Na Kamati ikishateuliwa inawajibika kwa bunge kutoa maoni na mwazo huru kuhusu mwenendo mzima wa taasisi hiyo ya umma yenye jukumu kubwa la kulinda Nchi ndani na nje ya mipaka ya Taifa letu. Na wao TISS kuwa na meno ya kutenda na kutoa ushauri wenye TIJA kwa TAIFA.Na makosa yao yatakayo sababisha hasara au uzembe kwa Taifa yawajibishwe kwa wale wote wenye dhamana [vested] ya kitaasisi kwa wakati huo.

Hakika kunatakiwa mageuzi makubwa na elimu kubwa itolewa kwa umma kuwa usalama wa Taifa sio uhuaji au utishaji dhidi ya raia wema. Mtanzania ajisikie raha na huru kusaidia Taasisi hiyo popote pale anpoona panastahiki kwa mujibu wa elimu aliyonayo juu ya taasisi hiyo. Leo ukiwawauliza Wamerekani FBI na CIA ni nini hakika haraka sana watakwambia nini, na raia wa Tanzania leo hii wanajua kazi za CIA na FBI kuliko wanavyojua taarifa za Usalama wa Taiafa lao.

Information is Power,kitendo cha raia wa kawaida kuelimisha kazi za Usalama kuwa ni Ulinzi wa Taifa lake kwa ushirikiano wake hakika hata upatikanaji wa taarifa zao wigo wake utapanuka.
 
usalama wa taifa wa kiukweli ulikuwa active under the late Mwalimu -- huu wa sasa unaegemea umekuwa kama usalama wa ccm.

Kwa mfano haya mambo ya rushwa za mabilioni , udini kuchinjana kwa imani za kidini, kuchoma makanisa, ukabila, ujangiri hadi watu wanatotosha twiga nje ya nchi, madawa ya kulevya, ushirikina (kuua maarubino) nk haya yanatakiwa yashughulikiwe na usalama wa taifa.

sasa ukiona vituko kama hivi unaweza kuhoji uwepo wa taasisi nyeti kama hii.
Rejea maandiko ya Yericko "taasisi hii itahusika/itajihusisha na kutambua/kubaini na kutoa ushauri tu"
 
You guys are missing a fundamental principle kwenye national intelligence services - intelligence policy. Hivi mmewahi kujiuliza intelligence policy ya Tanzania ni nini? Hivi mnajua sera ya CCM kuhusu Intelligence ni nini?
binafs naona policy yao ni kuwashughulikia wanaowakosesha usingizi,na wanafanikiwa japo kwa shida.:tape2:
 
yericho, tatizo la msingi kwenye hii taasisi sio la kisiasa bali la wanausalama wenyewe. Ukichunguza kwa umakini utagundua kuwa tatizo lake la msingi linaanzia kwenye recruitment yaani usahili. badala ya kutumia utaratibu aliuacha mwl. Nyerere ambao unatumika pia na mataifa mengine ambayo taasisi kama hizi zinanguvu. Utaratibu ni kwamba usaili sio zoezi la siku moja bali la miaks kazaa.

Mtu anachunguzwa kuanzia familia yake, primary, secondary hapo kama wamelizika wanamchukua na wengine walikuwa wanachunguzwa mpaka level ya chuo na ndiyo wanachukuliwa lakini sasa hivi wanausalama wenyewe wanashangaana kuwa huyu wa tabia hii ameingiaje humu? Kuna ukabira, udini, ushost, na mpaka ubazazi katika kupata kazi huko. Watu wameona ndiyo sehemu ya kuficha ndugu zao wasio na sifa.

Pamoja na kupewa meno na bunge lazima wabadilishe utendaji wao na ndiyo jamii itawapa heshima yao sitahiki. Vinginevyo watapewa meno na watayatumia kuuma watu wasio na hatia na kuwaacha wenye hatia wakijinafasi kama zilivo sekta nyingine za kutoa haki.
nao wamekuja na utaratibu wao si mbaya
 
nao wamekuja na utaratibu wao si mbaya

Utaratibu wao ndoo umetufanya tufike hapa. Miongozo mbalimbali ukianzia na dira, sera mpaka sheria zinaleta maana pale ambapo watu mliomo mnaamini katika miongozo hiyo. Kama hamuamini miongozo hiyo hata kama ikiwa mizuri kiasi gani humuendi mahali. kwa mfano hapa Tanzania tunayo sheria inayoshughulikia masuala ya wizi wa mali za umma. Lakini kwa kuwa viongozi wetu hawaamini katika sheria hiyo ndiyo maana watu wa EPA walishikwa na fedha za wizi toka BOT badala ya kupelekwa mahakamani wakaambiwa warudishe na hawajapelekwa mahakamani mpakal leo. Na waliopelekwa baaadaye wakarudisha kiasi kesi zao zinasuasua ukiondoa Maranda na ndg yake ambao walikiuka "makubaliano ndiyo wapo jela kwa muda sasa. Jiulize kesi zingine ziko wapi? Mbona ya Maranda ilienda kasi?
Hivyo Mzee wangu Mwanakijiji hoja hapo sio upungufu wa kisera na kisheria ila aina ya watu wenyewe. Kuboresha sera na sheria kutasaidia endapo nao watabadilika kimtazamo
 
Mkuu Yericko umeleta hoja nzurri sana na inastahili pongezi kwa kujaribu kuchungua nini hasa tatizo la TISS.

Hata mkuu Ben Saanane ameelezea vizuri kuhusu mambo ambayo yanakosekana kwenye ufanisi kiutendani wa taasisi hiyo.

Lakini Mkuu mwanakijiji nae amehoji kama hata tunayo sera kuhusu usalama wa taifa kwamba hafahamu kama CCM inayo sera hiyo.

Haya ni mambo ya msingi sana kufahamu kwani badala ya TISS kuanza kuwinda wale wanaojaribu kuikosoa kwa makosa ya kiutendani wanayoyafanya, kiongozi wa idara hii angezingatia zaidi ubunifu mpya wa mikakati ya idara hii huko tuelekeako ambako ni kugumu zaidi kwa wananchi maskini na kuzuri kwa waitakiayo mabaya nchi yetu.

Hayati mwalimu Nyerere aligusia jambo la utandawazi kwamba litatumeza kabisa na tutashindwa kuuza hata papai nje ya nchi kwani nchi matajiri wao wanakazania kujiimarisha na kuzuia wengine wasiwafikie pale walipo na ndio maana tunaona vita vya chinichini kwenye mitandao baina yao ikiwemo China, Iran, na watu wengine.

Hii idara sio siri kwamba baada ya miaka kumi iliyopita imeharibiwa kabisa na mfumo mbovu wa kuajiri watumishi wake na utendaji wake wa kazi umeharibiwa na mfumo mbovu wa serikali ambao umeruhusu hata watu wasiostahili kufanya kazi TISS nao wawemo humo.

Kutokana na hali hiyo ndio tunaona watu wanatishiwa maisha yao hata kama wanaishi nje ya nchi kama ndugu yetu Ulimboka na juzijuzi bwana Chahali na gazeti la Raia Mwema.

Ukianza kufanya hivyo unaonyesha kutojiamini na kutokuwa mshindani wa kimaendeleo.

TISS inahitaji kiongozi ambae ana muono mpya na wenye kutoa mikakati mipya juu ya nchi yetu inakokwenda na kutokana na hivyo tunapata mtu ambae heshima yake inashuka mpaka kwa shushushu ambae anauza miwa.

Hakuwezi kuwepo sera ya usalama wa nchi kama hakuna hata baraza la usalama wa nchi ambalo kazi yake ni kumshauri raisi juu ya hali ya usalama wa nchi katika kila idara iwe mazingira, hali ya hewa, usafiri wa anga, uchumi na biashara na hata uhamiaji.

Kunakuwepo baraza la usalama la nchi ambalo linahusisha wadau wote- mkuu wa majeshi, waziri wa ulinzi, waziri wa fedha, washauri wa raisi wa masuala ya usalama.

Pia humo kwenye baraza kuna washauri wa raisi wa masuala ya uchumi, ulinzi, na idara zingine nyeti kama usafiri wa anga na hali ya hewa wanakuwemo humo.

Baraza la usalama wa nchi litatoa muelekeo wa hali ya usalama wa nchi na kumshauri raisi juu ya hali ya usalama wa nchi na pia kupitia sera ya mambo ya nje ya nchi.

Hapo hata kwenye suala la mgogoro na nchi jirani ya Malawi ungeweza kutatuliwa kiufundi zaidi kama wajumbe wa kama hiyo wangetoa mawazo yao ya kitaalam kuhusu namna na kutatua tatizo hilo.

Sasa sifahamu kama tunalo baraza la usalama wa nchi ila ipo kamati ya bunge ya ulinzi na usalama ambayo inawajibika kwa bunge kupitia ugunduzi wa jambo lolote linalohatarisha usalama wa taifa.

Kukiwepo baraza la usalama wa nchi linakuwa ni independent ingawa ni lazima lipitishwe na bunge na utendaji wake ujulikane kwa ofisi ya raisi.

Hivyo ni muhimu kwa raisi ajae baada ya uchaguzi wa 2015 kuangalia muundo wa TISS na sheria inayoingoza idara hii viwe ni kioo cha kuifanya idara hii ijijengee heshima yake iliyokuwa nayo miaka ya nyuma.
 
You guys are missing a fundamental principle kwenye national intelligence services - intelligence policy. Hivi mmewahi kujiuliza intelligence policy ya Tanzania ni nini? Hivi mnajua sera ya CCM kuhusu Intelligence ni nini?
Mkuu Mwanakijiji umegusa jambo muhimu sana,

Hilo nalo ni moja ya tatizo kuu, hata watawala wetu hawajui hili jambo,
 
Mkuu hii issue ilishapita huku tukajadiliana.Ni kweli TISS inamchango mkuu uliotukuka,lakini msimamo wa mbio za vijiti usiozingatia umahili wa kitaahasisi na nyakati hakika usalama wa Taifa kama jina lilivyo utakuwa shakani.
Binafsi nilichangia na kutoa mada kwenye angle ya TISS humu jamvini na nikasema umefika wakati TISS watoke kuwa IDARA [Department] wawe Taasisi timilifu [INSTITUTIONAL] yenye kujitosheleza na idala yake.Kwa kupewa nafasi ya kuwa Taasisi haki sheria unayo lia nayo tayari itakuwa imekufa kifo cha pekee yake na matamanio ya kuiona taasisi [by now department] yenye meno itakuwa imetimia.

Kwa TISS kuwa taaisisi matamanio yangu kwaweza kuzaliwa idara madhubuti zenye kwenda na nyakati kama idara
1: Ulinzi wa Viongozi
2: Elimu na Mambo ya Sayansi na Technolojia
3: Ujasusi ndani na wa kimataifa
4: Siasa za Ndani [Tanzania Bara na Visiwani] na Mahusiano Ya Kimataifa
5: Maliasili watu na mahusiano ya jamii [Administration and Public Relation]
6: Uchumi na Fedha
7: Maliasili za Taifa

Kwa hayo hakika tunaweza kufika mbali na kuwa na kamati maalumu ambayo pia nayo itakuwa mlinzi wa jicho la mwenendo mzima wa TISS [Watchdog] isiwe ile misemo ya the court break become the court breaker!!inapata nafasi ya kutumika. Ina maana kwa TISS kuwa taasisi itwajibika kwa Wananchi kupitia Bunge! Na DG wao atateuliwa na Rais lakini atapitishwa na Bunge. Na Kamati ikishateuliwa inawajibika kwa bunge kutoa maoni na mwazo huru kuhusu mwenendo mzima wa taasisi hiyo ya umma yenye jukumu kubwa la kulinda Nchi ndani na nje ya mipaka ya Taifa letu. Na wao TISS kuwa na meno ya kutenda na kutoa ushauri wenye TIJA kwa TAIFA.Na makosa yao yatakayo sababisha hasara au uzembe kwa Taifa yawajibishwe kwa wale wote wenye dhamana [vested] ya kitaasisi kwa wakati huo.

Hakika kunatakiwa mageuzi makubwa na elimu kubwa itolewa kwa umma kuwa usalama wa Taifa sio uhuaji au utishaji dhidi ya raia wema. Mtanzania ajisikie raha na huru kusaidia Taasisi hiyo popote pale anpoona panastahiki kwa mujibu wa elimu aliyonayo juu ya taasisi hiyo. Leo ukiwawauliza Wamerekani FBI na CIA ni nini hakika haraka sana watakwambia nini, na raia wa Tanzania leo hii wanajua kazi za CIA na FBI kuliko wanavyojua taarifa za Usalama wa Taiafa lao.

Information is Power,kitendo cha raia wa kawaida kuelimisha kazi za Usalama kuwa ni Ulinzi wa Taifa lake kwa ushirikiano wake hakika hata upatikanaji wa taarifa zao wigo wake utapanuka.
Asante sana mkuu kwamchango wako murua, hakika taifa linaweza kufanya mageuzi makubwa ya taasisi hii
 
yote uuyasemayo bwana kiranga ni sahihi kabisa na wajumbe wengi wanajaribu kuainisha maeneo mengi ambayo idara inaweza ku play part ili kuhakikisha kuwa nchi hii inakuwa salama wakati wote bila ya kuathiriwa na matatizo hayo ya nmdani. ninaamini kuwa jukumu hilo wanalitekeleza. shida kubwa iliyopo hapa ni kwa kiwango gani idara ishughulikie masuala hayo. nijuavyo mimi ni kuwa kila jambo hapa nchini kuna wizara ambayo inajukumu la kuweka mikakati ya kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika wizara husika. kwa issue ya food security, tuna wizara ya kilimo na chakula. kwa mujibu wa sheria ya idara ya usalama wa taifa ya mwaka 1996, ambayo mchangiaji mwenzetu ametusaidia ni kuwa iodara hii jukumu lake kuu ni kutoa ushauri kwa waziri husika. kwa vile hatuna waziri anayehusika na masuala ya usalama wa taifa, ninaamini kuwa jukumu hilo lipo mikononi mwa rais wa nchi. kwa maana hiyo ni kuwa consumer wa information za idara ni rais mwenyewe. huo ni mfumo ambao waliouandaa akina chenge wanajua lengo lake hasa lilikuwa nini. ila kwa mazingra ya sasa ni vigumu kwa informations zote wanazopata idara consumer akawa rais tu. bila shaka hapo idara itaendelea kulaumiwa. tatizo kubwa lililobainishwa na wachangiaji wengi ni la kisheria na si utendaji wa idara yenyewe

Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa anaripoti kwa Waziri wa Utawala bora
 
Watu wanakosa imani na chombo hicho hicho kwa sbbu mengi mabaya yanayosemwa juu ya viongozi wetu hayachukuliwi hatua hasa wanasiasa viongozi ngazi za juu, kama chombo hicho ni kutafta na kuhakiki ukweli wa mambo tunataka tuoni report/vidhibitisho hizo mahakamani watu mafisadi/majizi/wahujumu uchumi wanahukumiwa ,no body is above the law
 
Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa anaripoti kwa Waziri wa Utawala bora

Who told you that? Yani nafuu Kidogo ungesema PM Sio Mkuchika. Operational Level anaripoti Magogoni moja kwa moja. Utawala bora ni parent ministry kwa ajili ya sera pekee.
 
Sizani kama tuko na usalama wa TAIFA bali ni usalama wa wachache wenye hela zao Tz.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom