Nadharia ya Usalama wa Taifa (TISS) ibadilike kuanzia sasa, Taifa lipo hatarini

Nadharia ya Usalama wa Taifa (TISS) ibadilike kuanzia sasa, Taifa lipo hatarini

Status
Not open for further replies.
Yericko tiss ilikuwa zamani sio sasa hivi ajira zake zinakwenda kwa vimemo, mtoto wa flani, nepotism nk. Nahisi sasa hata kagame ameshapenyeza watu wake pale sbb tuko vulnerable sana. zamani kuajiriwa pale mtu alikuwa vetted toka kijijini kwake alikozaliwa, shule aliyosoma na kila sehemu aliyopitia nk.

nakumbuka rafiki yangu mmoja aliajiriwa na tiss enzi hizo. kwanza yeye hakujua sbb kazi hii ilikuwa haiombwi na mhusika. watu walichujwa. jamaa kanambia kuwa alitumiwa ujumbe aende stand ya msamvu morogoro enzi hizo na kuwa ataikuta landrover ya kijivu saa sita mchana na akiikuta apande. baada ya hapo hakuonekana mwaka mzima na alivyorudi hakusema alikuwa wapi. lkn alitokea kuwa mmoja wa maofsa mahiri kitengoni.

hali ni tofauti na sasa. vuka tu pale ng'ambo ya makao makuu ya tiss kwenye bar ya SIMBA KAPAKATWA utawakuta wanakunywa pombe huku wakiongea mambo nyeti ya usalama wa nchi wakiwa njwiii. hakuna maadili wala secrecy ya masuala ya nchi. katiba mpya nadhani inaweza kuja na solution ya tatizo hili.

Nini kipimo cha ufanisi wa taasisi nyeti kama hii???? Nafikiri taasisi hii bado inafanya kazi japo kunawachache hawazingatii maadili. Hili la maadili sio kwa TISS tu ni kwa profesion zote, mwalimu anaeuza mtihani unamchukuliaje, dk anaeuwa au toa siri za wagonjwa, muhandisi anaesimamia kazi zake substandard(anajua jengo linahitaji 100 bags of cement yeye anajifanya kubalance, anaiba mifuko hamsini na anatumia hamsini baada ya muda jumba linaporomoka unamchukuliaje, mwanasiasa anaetumia na kupotosha ukweli ili apate madaraka kwa ngozi ya kondoo,ni mengi lakini niishie hapo halafu nije kwenye maada yenyewe.

Kulinganisha mambo wakati wa Nyerere na sasa kunawezekana si sawa, kwani zamani mlikua hamna uwezo wa kujadili TISS kama sasa, sasa kunauhuru mkubwa sana, ndio maana watu wengie humtukana hata rais wa nchi. Kwangu mimi utendaji wa TISS pengine ni bora kwa sababu za globalisation wameweza kuiweka nchi yetu kwenye usalama japo kuna pressure za hapa na pale. Mimi nafikri hawa mabwana wanatakiwa kuongeza umakini wa kazi zao.

Suala la maadili ni suala la taifa zima kwani kama mfumo wa taifa hauna maadili bora usitegemee kuwapata TISS wa maadili bora kiurahisi, tubadilikeni sote kuanzia ngazi ya familia muone kama hawatapatikana bora zaidi. Ofcourse chain yao ni kubwa manake wakati mwingine unatakiwa kuwa undercover wa vijiweni au wala dope, unategemea kuniteract kiulokole ili kudetect uhalifu waaina hiyo kweli??? Inabidi kujichanganya nao ilikujua japo ww hutovuta dope.

Nafikiri tusiwalaumu ukizingatia hatujui nijinsi gani wanafanya kazi zao ila wale wanaokiuka maadili waache ili taasisi isipakwe madoa. Mungu ibariki Tanzania.
 
yote uuyasemayo bwana kiranga ni sahihi kabisa na wajumbe wengi wanajaribu kuainisha maeneo mengi ambayo idara inaweza ku play part ili kuhakikisha kuwa nchi hii inakuwa salama wakati wote bila ya kuathiriwa na matatizo hayo ya nmdani. ninaamini kuwa jukumu hilo wanalitekeleza. shida kubwa iliyopo hapa ni kwa kiwango gani idara ishughulikie masuala hayo. nijuavyo mimi ni kuwa kila jambo hapa nchini kuna wizara ambayo inajukumu la kuweka mikakati ya kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika wizara husika. kwa issue ya food security, tuna wizara ya kilimo na chakula. kwa mujibu wa sheria ya idara ya usalama wa taifa ya mwaka 1996, ambayo mchangiaji mwenzetu ametusaidia ni kuwa iodara hii jukumu lake kuu ni kutoa ushauri kwa waziri husika. kwa vile hatuna waziri anayehusika na masuala ya usalama wa taifa, ninaamini kuwa jukumu hilo lipo mikononi mwa rais wa nchi. kwa maana hiyo ni kuwa consumer wa information za idara ni rais mwenyewe. huo ni mfumo ambao waliouandaa akina chenge wanajua lengo lake hasa lilikuwa nini. ila kwa mazingra ya sasa ni vigumu kwa informations zote wanazopata idara consumer akawa rais tu. bila shaka hapo idara itaendelea kulaumiwa. tatizo kubwa lililobainishwa na wachangiaji wengi ni la kisheria na si utendaji wa idara yenyewe

Usalama wa taifa ina tentacles wizara zote, si kazi kukuta mtu anafanya kazi wizara ya kilimo halafu ni mtu wa usalama wa taifa vilevile.Kwa sababu hii ni idara nyeti inayohitaji kuwa na habari zote.

Mimi nishaona washua wapo kwenye projects za misada ya kimataifa Tanzania, watu wa Usalama wa taifa.Lakini unamkuta mshua Engineer engineer kweli na anafanya kazi zote za kiinjinia, lakini na kazi za kukusanya data za usalama wa taifa anafanya pia. Na huko hata si serikalini per se, ni mi project ya misaada ya watu wa nje.

Hawa wapo kusikiliza habari mpaka kwenye uongozi wa vilabu vya mpira, mpaka wananifanya niwaone kama Stalinist Chekis sasa.

Kwa hiyo kama kuna failure hapa ni failure of imagination, sio failure of mandate/ access.
 
Tunachoshindwa kuelewana sisi sote ni juu ya haki na wajibu wetu,TISS si chombo cha kutegemea sana iwapo sisi sote tutatimiza hayo.


Huitaji wetu wa kisasa usitufanye kuingilia mipaka ya ambacho tunahisi eti ni sababu mojawapo ya uzembe wetu wa kutufanya kutokutimiza wajibu huko tuking'ang'ania haki.

TISS ni mimi,wewe,yule,wale wenye nia njema ya dhati ya kuhakikisha nchi inakuwa ni mahala salama na pazuri pa kuishi hata kama kuna machungu kwa kiasi gani kwa namna ya kuishi kwa wakati uliopo na ujao.
 
Nini kipimo cha ufanisi wa taasisi nyeti kama hii???? Nafikiri taasisi hii bado inafanya kazi japo kunawachache hawazingatii maadili. Hili la maadili sio kwa TISS tu ni kwa profesion zote, mwalimu anaeuza mtihani unamchukuliaje, dk anaeuwa au toa siri za wagonjwa, muhandisi anaesimamia kazi zake substandard(anajua jengo linahitaji 100 bags of cement yeye anajifanya kubalance, anaiba mifuko hamsini na anatumia hamsini baada ya muda jumba linaporomoka unamchukuliaje, mwanasiasa anaetumia na kupotosha ukweli ili apate madaraka kwa ngozi ya kondoo,ni mengi lakini niishie hapo halafu nije kwenye maada yenyewe.

Kulinganisha mambo wakati wa Nyerere na sasa kunawezekana si sawa, kwani zamani mlikua hamna uwezo wa kujadili TISS kama sasa, sasa kunauhuru mkubwa sana, ndio maana watu wengie humtukana hata rais wa nchi. Kwangu mimi utendaji wa TISS pengine ni bora kwa sababu za globalisation wameweza kuiweka nchi yetu kwenye usalama japo kuna pressure za hapa na pale. Mimi nafikri hawa mabwana wanatakiwa kuongeza umakini wa kazi zao.

Suala la maadili ni suala la taifa zima kwani kama mfumo wa taifa hauna maadili bora usitegemee kuwapata TISS wa maadili bora kiurahisi, tubadilikeni sote kuanzia ngazi ya familia muone kama hawatapatikana bora zaidi. Ofcourse chain yao ni kubwa manake wakati mwingine unatakiwa kuwa undercover wa vijiweni au wala dope, unategemea kuniteract kiulokole ili kudetect uhalifu waaina hiyo kweli??? Inabidi kujichanganya nao ilikujua japo ww hutovuta dope.

Nafikiri tusiwalaumu ukizingatia hatujui nijinsi gani wanafanya kazi zao ila wale wanaokiuka maadili waache ili taasisi isipakwe madoa. Mungu ibariki Tanzania.

sahihi sana amwanga. watu wanafikiri kuwa mtumishi wa idara basi atakuwa tofauti na mienendo ya watu wengine. tena mimi nawasifu sana hawa jamaa. wanaishi kwa kipato kidogo sana, hawana access na mabenki, hawana mikopo ya nyumba, wengi wanatembelea magari kuukuu. pamoja na hali hjiyo, bado wamebaki kuwa ni wazalendo ingawa wanapokea matusi kibao kwa watu wasioitakia mema idara hii na nchi kwa ujumla
 
Tunachoshindwa kuelewana sisi sote ni juu ya haki na wajibu wetu TISS si chombo cha kutegemea sana iwapo sisi sote tutatimiza hayo.


Huitaji wetu wa kisasa usitufanye kuingilia mipaka ya ambacho tunahisi eti ni sababu mojawapo ya uzembe wetu wa kutufanya kutokutimiza wajibu huko tuking'ang'ania haki.

TISS ni mimi,wewe,yule,wale wenye nia njema ya dhati ya kuhakikisha nchi inakuwa ni mahala salama na pazuri pa kuishi hata kama kuna machungu kwa kiasi gani kwa namna ya kuishi kwa wakati uliopo.

sure kaka. watu kutokana na uroho wao wa madaraka wanaiona idara kama ni kikwazo kwao. wengine huzusha uongo eti idara inawafuatilia kila waendAKO na wengine kudai kuwa wanatishiwa maisha. huo wote ni uongo na wanachotafuta ni huruma ya wananchi. ninaamini kuwa hata ndanio ya ccm kuna watu wengi wenye mtazamo kuwa idara ni kikwazo kwao hasa pale wanapoambiwa ukweli juu ya utendaji wao wa kazi usioridhisha
 
sahihi sana amwanga. watu wanafikiri kuwa mtumishi wa idara basi atakuwa tofauti na mienendo ya watu wengine. tena mimi nawasifu sana hawa jamaa. wanaishi kwa kipato kidogo sana, hawana access na mabenki, hawana mikopo ya nyumba, wengi wanatembelea magari kuukuu. pamoja na hali hjiyo, bado wamebaki kuwa ni wazalendo ingawa wanapokea matusi kibao kwa watu wasioitakia mema idara hii na nchi kwa ujumla
.

Atowele yani umenena sawiya, wengine hata basikeli hawana na wanafanya kazi bila kugoma, upo sawa kabisa asilimia kubwa ya hawa mabwana ni wazalendo. Wanauwezo wakutumia nafasi zao nakujipatia utajiri bwere lakini kwao kwanza nchi mengine baadae. Hata tusipo wasifia watafanya kazi zao kwa maslahi ya nchi yetu. Changamoto tuliyo nayo kwa idara hii ni teknolojia za kusaidia mambo mbalimbali ya usalama wa nchi, kwa mfano teknolojia za kilimo bora ambayo inatakiwa iwe initiated na kupata support kwa profesions na wao wakihakikisha hamna atakae zichezea.
 
Tiss imekuwa laini hadi inasikiliza order kutoka kwa prince riz one.
Kwa sasa tiss ni mali ya rais na familia yake chini ya usimamizi wa malkia salma.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

hawa ni walewale wenye uvivu wa kufikiri. nadhani hawa ni miongoni mwa wale walichora katuni za MESS na ZOMBI kwenye answer sheet za NECTA 2012. kama huna hoja waache wenye kuelewa mambo wachangie na wewe ufanye kazi ya kusoma tu post za watu pengine ipo siku utakuja kuelewa.
 
How dificult it is to deal with some one who is hugry, jamani unakua usalama wa taifa kwa nchi kama yakwetu unakutana na complex behavior za watu , ambao kutii sheria hawaelewi, lakini bado unaweza tekeleza majukumu yako bila kuwaadhiri. Msifanye mchezo jamani hata mngewaleta kina james bond wajekuwa wanausalama wa nchi yetu wangechemsha. TISS fanyeni kazi zenu kwa moyo wadhati na mtaendelea kufanikiwa.
 
mkuu, kumbuka idara inayozungumzwa humu ni hii TISS ambayo imeanzishwa kwa mujibu wa sheria ya mwaka 1996, mwaka mmoja tu baada ya rais mkapa kuwa rais wa nchi. kwachangiaji wengi wanaona kuwa sheria ndiyo kikwazo. kwanza napenda kuwapongeza viongozi wa Idara hii kwa kwa kutekeleza majukumu yao bila ya kukiuka misingi iliyowekwa ndani ya sheria hiyo. hao ni viongozi tunaowataka kwa vile wanaongoza kwa mujibu wa sheria za nchi. ninahakika kama viongozi wa tiss wangeamua kufanya mambo yao bila ya kuangalia sheria inasema nini, uwezo huo wanao na hakuna wa kuwazuia. ila kwa kuwa nchi hii inaongozwa kwa misiongi ya sheria na haki ndo maana leo hii tunapiga kelele na wengine kudiriki hata kuwatukana viongozi wa idara hii nyeti
Well, ni lazima uwapongeze viongozi wa idara na viongozi wa nchi kwamba wanaongoza nchi kwa mjibu wa sheria kwa kuwa na wewe ni mmoja wa wanausalama na haitakuwa rahisi kujiponda mwenyewe kwa kazi yako unayoifanya.

Wachangiaji wengi wameliangalia tatizo la ukosefu wa umakini katika utendaji wa TISS kwamba umetokana na sheria, na wanaiona sheria ni mbaya kwa kuwa inawaelezea TISS kuwa ni washauri tu, lakini mimi nasema tatizo siyo sheria peke yake, tatizo ni mfumo mzima wa TISS na serikali kwa ujumla wake.

TISS sasa hivi imekuwa ni kama kampuni ya watu binafsi, hata kama sheria ingewapa mamlaka yote, bado wangeyatumia mamlaka yao ku-abuse kazi zao. Nasema TISS imeoza ivunjwe, iundwe upya, na zaidi ya yote, napendekeza TISS isiwe mali ya Ikulu kama ilivyo sasa, bali iwe inawajibika pia kwa Bunge. Hii haimaanishi kwamba mambo ya TISS yajadiliwe bungeni, bali ina maanisha kwamba kamati ya bunge inayoshughulika na mambo ya ulinzi na usalama iwe na nafasi ya kuchukua hatua inapotokea kwamba kuna uovu au tishio la usalama ambalo TISS imeliriport ama kwa Rais au kwa waziri lakini wameshindwa kuchukua hatua.

Mimi sisemi TISS hawafanyi kazi kabisa, naamini kwa dhati kabisa kwamba kuna baadhi ya member wa TISS ambao ni waadilifu na wanafanya kazi kwa kufuata maadili, lakini wanakwamishwa na baadhi ya viongozi wa serikali ambao wanapuuza ushauri wanaopewa na TISS. Kama bunge litakuwa na mkono hapo, sitegemei kwamba kuna mtu atapuuza kirahisi tena. Kwa mawazo yangu, uongozi wa serikali na uongozi wa TISS wote una matatizo. Mfumo mzima wa utawala urekebishwe.
 
Asante sana mkuu, nilikuwa natafuta sana mawazo yako katika uzi huu, naaaam umetii kiu yangu na yawatanzania kabisa,

Mkuu umegusa maeneo yote nyeti kitaasisi. Bila shaka tutazidi kuwa begakwabega kuhimiza uhuishaji wa taasisi hii iendani na dunia ya leo iendavyo.

Asante sana mkuu.pamoja sana mkuu
 
Wadadisi wa masuala ya kiusalama wataungana nami kuwa TISS ndicho chombo pekee cha nchi hii kilichofanya kazi yake kwaufanisi mkubwa na kulifikisha taifa hapa lilipo,

Mathalani sheria hiyo inasema, "taasisi hii itahusika/itajihusisha na kutambua/kubaini na kutoa ushauri tu"

Kwani wakati ikifanya kazi yake kwa ufanisi mkubwa, ilikuwa inafanya kazi zaidi ya kutoa ushauri tuu?

Una maana kuwa sheria ilikuja kubadilishwa na kupunguza mamlaka ya hiyo taasisi kuliko ilivyokuwa huko nyuma?

Kwamba sheria ikibadilishwa basi taasisi hiyo itakuwa inafanya kazi yake kwa ufanisi mkubwa kuliko ilivyo sasa?

Kwamba tatizo ni sheria?
 
Tatizo lako unaangalia mambo katika mawazo mgando wakati dunia ina evolve.

Nilikuwa naongea na Balozi wa Tanzania Umoja wa Mataifa kipindi hicho, Dr. Augustine Philip Mahiga, mwanadiplomasia aliyebobea ambaye aliwahi kuwa mkuu wa usalama wa taifa kabla hata usalama wa taifa haujarasimishwa, enzi za Nyerere. Kuhusu challenges za usalama za ulimwengu, na Tanzania, hususan in the wake of 9/11.

Dr. Mahiga, mmoja kati ya ma dokta wa ukweli ninaowaamini Tanzania ambaye akiongea mtu unamjua huyu ni msomi hata kabla hajakuambia "mimi ni Balozi Dr. Mahiga", akaniambia mataifa makubwa yana ajenda zao za usalama na ajenda hizi si lazima ziwe sawa na ajenda za mataifa madogo katika suala la usalama.

Tukazungumza sana jinsi gani swala zima la "food security" linavyokosa kuongelewa vizuri Umoja wa Mataifa kwa sababu tu mataifa makubwa yamekazania "terrorism" in the context of Al-Qaeda and similar threats.

Akajenga hoja, ambayo sikuweza kuipinga, kwamba huku nchi masikini kwetu njaa inaweza kuwa "terror" kubwa kuliko Al-Qaeda, na at least inatubidi tuipe kipaumbele angalau sawa na hizo habari za Al-Qaeda, kama si zaidi.

Alielewa "food security" as a part of "national security".

Sasa wewe unakuja na one track mind kufikiri tu kwamba "usalama wa taifa ni mashushushu, kazi yao ni upelelezi na ujasusi". Period. Huwezi kuona kwamba hata "food security" ni sehemu ya usalama wa taifa.

Na kama tuna ukame periodically, Usalama wa taifa unatakiwa kuandaa contingencies za kuweza kukabili ukame wakati wowote.

Na kwamba sehemu yoyote kukiwa na ukame ni failure ya food security ambayo moja kwa moja ni failure ya national security, hata in the context ya "a hungry man is an angry man" tu. Mitatizo kibao ya wananchi kuchoma moto nyumba za wabunge na wakuu wa mikoa ukiiangalia kwa juu juu utaona ni masuala ya failure ya usalama wa taifa katika context ya usalama wa taifa kukosa kujua nini kinaendelea na ku project nini kitatokea, lakini ukiangalia zaidi utaona ni failure ya usalama wa taifa zaidi kwa sababu ina correlation na food security.

Njaa ni mafuta yanayosubiri cheche tu kulipuka na kutoa vurugu.Usalama wa taifa .

Njaa inaleta vishawishi hata mwananchi ahujumu nchi yake mwenyewe. Usalama wa taifa. Angalia Mali huko hajulikani nani raia nani Al-Qaeda, njaa tu hiyo.

You cannot talk about addressing national security if you cannot address food security.

Ndiyo maana nau indict "Usalama wa Taifa" kwa kushindwa kudhibiti njaa tu nchini. Je ukishindwa kudhibiti njaa tu nchini, utaweza kudhibiti Chinese, American and Iranian hackers wasiingilie computers za Ikulu?

Ikulu inatumia Yahoo emails, Yahoo hata hawatumii https, wanatumia http!

Usalama wa taifa unajua tofauti ya http na https?
Kiranga

Hiki kitu ulichoongea hapa hakieleweki si Tanzania tu ni Africa nzima ndiyo maana ukiongelea Economic Intelligence unaonekana unazingu au ukiongelea diplomasia ya uchumi unaonekana unaongelea lugha ya kigeni.

Kwa mfano majasusi watatumia maadui wetu wa ndani na maadui hawa tunawatengeneza wenyewe kutokana na sera zetu kwa mfano ajira,elimu,kilimo n.k

Watu wanadhani TISS ni umbea,majungu,au kutumia mitutu kumbe ni suala la brain na matumizi ya kisayansi na kiteknolojia tofauti na superstitious method
 
Last edited by a moderator:
Kiranga

Hiki kitu ulichoongea hapa hakieleweki si Tanzania tu ni Africa nzima ndiyo maana ukiongelea Economic Intelligence unaonekana unazingu au ukiongelea diplomasia ya uchumi unaonekana unaongelea lugha ya kigeni.

Kwa mfano majasusi watatumia maadui wetu wa ndani na maadui hawa tunawatengeneza wenyewe kutokana na sera zetu kwa mfano ajira,elimu,kilimo n.k

Watu wanadhani TISS ni umbea,majungu,au kutumia mitutu kumbe ni suala la brain na matumizi ya kisayansi na kiteknolojia tofauti na superstitious method

Precisely my point.
 
Hapa Tanzania hata kama tutatengeneza sheria nzuri kiasi gani hazitasaidia kama hatutabadili namna tunavyofikiri.

Sheria iliyounda TISS haina tatizo kwa mahitaji ya sasa. Lakini pale siasa inapochukua sehemu kubwa ndipo penye utata. Mlinganyo wa Rais kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na pia Mwenyekiti wa Kamati Kuu ya CCM inaipatia Kamati Kuu nguvu ya kupata taarifa za siri kuhusu vyama vingine na mengineyo(Dhana ya Wapinzani ni maadui). Bado hatujajiandaa kisaikolojia na kimfumo kuiondoa idara hii kutoka katika taasisi ya Urais.

Kuweza kuona ufanisi wa TISS inahitaji 'jicho la tatu' kwani shughuli nyingi hufanyika sirini.Kitengo ambacho ni maarufu zaidi ni kile cha Ulinzi wa Viongozi Wakuu(PPU).

Kumekuwepo na taarifa za baadhi ya maafisa wa idara hii kutokuwa na maadili lakini huo ni udhaifu wa binadamu. Kumbuka shughuli nyingi ni siri hivyo watu 'muhimu zaidi' huwezi kuwabaini kirahisi na si kila mfanyakazi wa TISS anajua kila kitu kinachoendelea.
 
Mungo Park

Ulichoongea ni sahihi kabisa mkuu,

Nilichojaribu kushawishi hapo ni kuwa taasisi hii ipewe mamlaka kamili kuliko kuwa nusu nusu,

Mfano, mwaka 2005 taasisi hii ilibaini wizi wa mamilioni kwenye EPA na ilifanya kazi yake kikamilifu kwa kuwapelekea ripoti wahusika/watawala, lakini matakwa ya kisiasa ya watawala hawa yalipingana na pendekezo la TISS, na ndio maana hata bunge lilipoazimia kuunda tume ya uchunguzi, mkuu wa taasisi hii aliluandikia barua bunge kusitisha uundanji wa tume hiyo, dhana kuu ya taasisi hii ikiwa ni kuwa hakuna cha maana kitakachofanywa na bunge hilo,

Pendekrzo kuu la taasisi lilikuwa ni kuleta wakaguzi wa nje ikiwa ushahidi na ushauri wao havikufanyiwa kazi.

Naam wote tulishuhudia kamupuni ya kigeni ya ukaguzi ikitua nchini na kufanikiwa kuweka wazi kila kitu.

Lakini hebu fikiria kama taasisi hii ingekuww na mamlaka ya moja kwa moja kwamaana ya kubaini,na kuzuia na si kutoa ushauri? Je yale mabilioni yangeteketea hivi hivi?
 
Last edited by a moderator:
Nilichojaribu kushawishi hapo ni kuwa taasisi hii ipewe mamlaka kamili kuliko kuwa nusu nusu,
Lakini hebu fikiria kama taasisi hii ingekuww na mamlaka ya moja kwa moja kwa maana ya kubaini,na kuzuia na si kutoa ushauri? Je yale mabilioni yangeteketea hivi hivi?

Kitu unachoshawishi kinawezekana lakini inatakiwa kwanza iwepo katiba ambayo ipo 'makini' vinginevyo utaipora taasisi ya urais hii idara kisha kuihamishia chini ya mtu au taasisi nyingine. Hii inaweza kutengeneza 'miungu watu' wanaoweza kudhoofisha nguvu za Rais na kutengeneza magenge ya ajabu ajabu - kumbuka akina John Edger Hoover(FBI).
 
Kitu unachoshawishi kinawezekana lakini inatakiwa kwanza iwepo katiba ambayo ipo 'makini' vinginevyo utaipora taasisi ya urais hii idara kisha kuihamishia chini ya mtu au taasisi nyingine. Hii inaweza kutengeneza 'miungu watu' wanaoweza kudhoofisha nguvu za Rais na kutengeneza magenge ya ajabu ajabu - kumbuka akina John Edger Hoover(FBI).
Hehee ni kweli kabisa, tunatakiwa kuanzia kwenye katiba makini,
 
Siku hizi mtu akiwa kwenye hiki kitengo basi atajisiifu,kila mtu atajua,moja ya sifa za hiki kitengo ni usiri na maadili ila vijana walivo daah! Ndo maana usalama wa hii nchi upo mashakani
 
hivi kama shirika hili likigeuzwa na kuitwa shirika la ujasusi la Tanzania itakuwaje?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom