Nafasi za kazi Jeshi la Polisi Tanzania

Nafasi za kazi Jeshi la Polisi Tanzania

Usiogope mkuuu mambo Yana change muda mwingine jamaa amekata tamaaa na majeshi

Mimi nitatoa Tu General Experience na pia nitagusia Kada ya IT kwasababu Mimi pia ni IT.

Mwaka Juzi nilishiriki Usahili Hapo Barracks Kurasini, I mean intake waliomaliza hivi Karibuni CCP Moshi tulikuwa nao kwenye Usahili.

Kwa Idadi Degree Wotee Tulikuwa Kama 600+ hivi Ila upande wa IT kama 200+ Diploma na Cheti Hawakuwa Wengi Sanaa.

Kozi ambazo walipita kirahisi kwakuwa Hawakuwa Wengi Yaan nafasi zinazohitajika ni nyingii Watu Wachache ni ushonaji,udereva,na uimbaji.
Unapoenda Pale inatakiwa uwe full uende na Vyeti Vyako vyote halisia sio kopi na pia wanacheki ukakamavu wa mwili ni kama kwata flani hivi wanaangalia unavyopiga(hiyo ni Kwa Mtu mmoja moja) andaa pia hela ya vipimo sijajua Kwa mwaka Huu kama hiyo hela itakuwepo au lah ni buku 5 nadhani. Wanapima sanasana Macho, wanachukua na Damu(ukimwi na magonjwa mengine) pia lkn kuangalia kama ni Mwanaume Kamili au mwanamke Kamili. Na pia wanawapima urefuu kila MTU kujua urefuu wako ni futi Ngapi.
Upande wa Usahili Maswali wanauliza kulingana na Kada Yako na ni marahisi Sana hasa maswali ya oral Yako too general.

Mimi nilikuwa IT Lkn Usahili sikufanya wa IT Ile full hapana, walitukata vibangala pale nikawekwa upande wa forensic bureau Pale Pale Yan ilikuwa ni mtihani kidogo lkn walituelewesha tukaelewa (ingawa sio wote watu Wengine walikuwa ni wabishi Sana), kwahiyo hiyo forensic bureau walituchanganya coz zote za science hivyo oral ikawa ni moja(maswali ya oral huwa hayatabiriki Sana lkn ni too general labda unaweza kuulizwa kirefu cha Polisi au taja ma IGP baada ya Uhuru au utaje ranks za polisi au mission and vision ya Polisi Na maswali ni Kwa Kiingireza kama Kawaida kujieleza Kwa Kifupi swali la lazima kila MTU aliulizwa) lkn written ni Tofauti kulingana na Kada Yako Kwa Mfano Mimi IT nilipiga written ya IT, Mimi napiga Sana Mambo ya network kwahiyo walituclassify IT upande gani kama ni programming, network au database it's depends.
NB: Na walituclassify kila forensic bureau na kozi yake Kutokana Na malalamiko ya Baadhi ya Watu kuwa itakuwaje sasa Usahili wa kitu kigeni ambacho hujasomea afu Ndo wanakusahili ndo wakaamua Hivyo, ingawa Baadhi ya maaskari wakatuona tumezingua kwa kuwa hiyo ilikuwa ni Bonge La feva Kwetu wangetubebabeba Kwa kuwa ni kitu kipya Kwetu wengi hatujasomea.

Sasa nakumbuka pepa ya network ya written ilikuwa na kama maswali 50 na mengi ni ya kuchagua ya kujieleza Yalikuwa hayazidi matano na Maswali Mengi Sanaa waliyatoa kwenye Kitabu cha CCNA by Toddy Lammle hicho Kitabu kina maswali na Majibu yotee ya network. Ila Sisi watu wa forensic hatukufanya practical lkn watu wa IT walifanya ilikuwa ni Kawaida Sanaa masuala ya kusubnet na Nini Yani kama MTU umejiandaa Vizuri Usahili unatusua Vizuri Sanaa.

Trust me kwenye haya mapambano kila mmoja ana Siri yake ya Namna gani atapata hizi nafasi, unachokiamini Hicho hicho kishikirie usikiache Kama Ni Mungu, Au Mganga, Au Mbuyu kikubwa ni Kupambana Tuu ingawa Yotee juu ya yote Bado Mungu Ndo Kila Kitu.. Wapo Ambao Wametoboa Kwenye Ule Usahili Hawakuwa na Mbanga Wowote Ule. na nilichokiona watu wa degree competition Ni KUBWA Sanaa Usahili tulioitwa 600+ waliochaguliwa ni 70+, form four waliochaguliwa walikuwa ni Wengi Sanaa 1000+ huenda mwaka Huu degree wakaongeza Nafasi.

Tuzidi Kuombeana Wakuu Tusikate Tamaa Mungu Ni Wetu Sote.Hivyo Tu Wakuu Nisiwachoshe Sana..
Tangu nimeanza kufatilia huu uzi cham umeongea vitu kuntu sana aiseee ..... japo kwa uchache wake ila machamp wanatakiwa kuchukua notice hapa
 
Mungu atupambanie tutoboe na sisi , miaka mitano kitaa sio kitoto , hadi unajiuliza ulimkosea nini Mungu, na muda unaenda , nikikumbuka gharama nilizotumia kuomba pccb hadi kwenda interview Dodoma , mtaji wangu wote nilipita nao , kuanzia nauli na malazi huna ndugu na bado nikala ndoige mpaka kuna muda unakuwa na mgogoro wa nafsi kuhusu hz nafasi , kwamba hata ukiitwa usaili tena usiende kuna ndoige , ila hamna noma Mungu ni wa kwetu sote siku moja tutatoboa
Kaka mimi usail wa mwaka jana UT, nilikula za uso!! Mwaka huu jaman sijui itakuwaje daaah.... Mungu tufanyie wepesi sisi vijana wako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tangu nimeanza kufatilia huu uzi cham umeongea vitu kuntu sana aiseee ..... japo kwa uchache wake ila machamp wanatakiwa kuchukua notice hapa
Sure kukata tamaaa dhambi Sana mkuuu ....Wana walipiga mujibu wa sheria wakasoma chuo wakarudi kujitolea Kuna op ilitimua wote wenye elimu ya juuu Wana wakarudi home , wote watoto wa wakubwa wastaafu vyombo mifumo inazngua Wana wamepambana moja amekata tamaaa na mwambia always mfwende hiz Mambo swala majira ya Mungu tu yakifika. Hakuna wa kuzia Kuna mwana mzee wake Gen ana mkazia mshikaj ana mwambia aje imeenda ngumu kuzama mwana alikuwa na 27 mshua alisema mwamb age imesogea acheki Mambo mengine yakufanya hiz Mambo Mungu anajua hatima ya mtu iko wapi
 
Sure kukata tamaaa dhambi Sana mkuuu ....Wana walipiga mujibu wa sheria wakasoma chuo wakarudi kujitolea Kuna op ilitimua wote wenye elimu ya juuu Wana wakarudi home , wote watoto wa wakubwa wastaafu vyombo mifumo inazngua Wana wamepambana moja amekata tamaaa na mwambia always mfwende hiz Mambo swala majira ya Mungu tu yakifika. Hakuna wa kuzia Kuna mwana mzee wake Gen ana mkazia mshikaj ana mwambia aje imeenda ngumu kuzama mwana alikuwa na 27 mshua alisema mwamb age imesogea acheki Mambo mengine yakufanya hiz Mambo Mungu anajua hatima ya mtu iko wapi
Wazi sana champ
 
Haha hapana mkuu mimi napenda tu kufuatilia mambo ya majeshi ila sipo huko na sina connection boss
UNanikumbusha alipokamatwa Yesu, Petro aliulizwa wewe ni mmoja wao? Alikana sana, wakamwambia hata kuongea kwako unafanana na wanafunzi wa Yesu😅😅😅
Asomaye na ajue
 
Hzo link za juu,uhamiaji walitoa aptitude test kupitia maswali hayo,simple questions& math . civics ikukae kichwani ,immigration act& client service charter ikukae kichwani, na current issues zote nawasilisha. kwa mliofanya usaili mwaka jana mtuambie pia
Unyama Sana,mkuu
 
Back
Top Bottom