Nahisi kuona vitu ambavyo vitanitokea, hii inatokana na nini ?

Nahisi kuona vitu ambavyo vitanitokea, hii inatokana na nini ?

TAI DUME

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2014
Posts
9,748
Reaction score
26,238
wakuu sjui kama huu uzi ulishawahi kuletwa huku au bado ila kwa anayefahamu anaweza kunishauri.

Ninaweza nikawa nafanya kazi fulani, au niko mahali fulani au nakutana na watu fulani lakini huwa napata hisia halisi kabisa kwamba hicho kitu nilishawai kukifanya katika muda na mazingira yale yale hata kama ndio nafanya kwa mara ya kwanza. Au naweza nikakutana na watu ambao siwafahamu lakini akili inakuwa inalikumbuka hilo tukio kabisa yaani kama ilishawahi tokea kabla. Hii inanitokea katika mambo mengi na ni mara kwa mara. Kwa maana ya kwamba huwa nahisi kuona vitu ambavyo havijanitokea.

Kiukweli hali hii siipendi kwani inanipa hofu na kuumiza sana akili yangu kwa kutaka kujua kwa nini inakuwa hivyo. Mpaka naandika hapa imenitokea tena jana nilipoitwa kwa kiongozi wangu wa kazi na kunipa barua ya promotion, Yani lile tukio lilivyokuwa linatokea nikakumbuka mpaka maneno atayoongea mwishoni na ikawa hivyo,

Mwenye utaalamu na haya mabo tafadhali.
 
1.Unaonekana ni mtu mwenye msongo wa mawazo na hofu ya kupatwa na mabaya, pia unatumia muda mwingi kutafakari mustakabali wako binafsi kwa kulinganisha kile kilichokutokea na kile ulichokiwaza. Je ni kweli?
 
Hiyo kitu wanaita deja vu
Kila mtu anayo sio wewe tu
But hakuna scientific explanation inayotosheleza kueleza hiyo kitu
Wala usiogope
Pia Muda mwingine ni ndoto ulizozisahau af zinakuwa kweli


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
basi tuko wengi mie huwa naona na kila mikisemacho kama utan vile huja kuwa kweli?
mfano naweza kuona labda mtu fulan atakuja af kweli yule mtu huwa anakuja ama tukio fulan litatokea na kweli linatokea. cha ajabu zaid ni kwamba nikiona tukio la hatari af nikisema kwa mtu ama nikikemea lile tukio huwa halitokei lkn nisipo lisema kwa mtu ama kukemea linatokea.
sijipend na huwa naonaga kama ni aina fulan ya utambuzi ambayo pia siipendi
 
hata mimi hali kama hiyo inanitokeaga, unakuta kuna tukio nimefanya au limetokea sasa hivi lakini nakumbuka kabisa nilishawaza au nilishalionaga muda flani kabla.
 
sijui itakuwa ni kitu gani imewai kunitokea hata mimi ila ni mara chache sana,inatokea senario exactly kama ambavyo niliwai kuifikiria au kuiota
 
Na Mimi inanitokea sana tu.tena baada ya tukio kumalizika ndio nakumbuka kwamba either niliwahi kuota ndoto kuhusu tukio lile au limewahi kunitokea before
 
1.Unaonekana ni mtu mwenye msongo wa mawazo na hofu ya kupatwa na mabaya, pia unatumia muda mwingi kutafakari mustakabali wako binafsi kwa kulinganisha kile kilichokutokea na kile ulichokiwaza. Je ni kweli?

kuhusu msongo wa mawazo hapana kwani kuna muda hali hii hujitokeza hata nikiwa relaxed kiakili
 
mie huwa nikikumbuka kuwa mtu fulani sijawasiliana naye hasa anayenihusu, itapita intavo ya dk kama tano hv mara nakuta simu inaiita au sms imeingia ya yule niliyekuwa namfikiria.
 
basi tuko wengi mie huwa naona na kila mikisemacho kama utan vile huja kuwa kweli?
mfano naweza kuona labda mtu fulan atakuja af kweli yule mtu huwa anakuja ama tukio fulan litatokea na kweli linatokea. cha ajabu zaid ni kwamba nikiona tukio la hatari af nikisema kwa mtu ama nikikemea lile tukio huwa halitokei lkn nisipo lisema kwa mtu ama kukemea linatokea.
sijipend na huwa naonaga kama ni aina fulan ya utambuzi ambayo pia siipendi

Bora wewe una plan b ya kukemea mimi hii hali siipendi na sina plan b. nitajifunza kukemea
 
hata mimi hali kama hiyo inanitokeaga, unakuta kuna tukio nimefanya au limetokea sasa hivi lakini nakumbuka kabisa nilishawaza au nilishalionaga muda flani kabla.

mkuu yang kasema tusiogope
 
Last edited by a moderator:
mkuu......umepata shavu la unabii na utume...tafuta jengo ukodi upige Hela..au nenda kwa Gwajima ukapige matizi..

haha haha haa nikamate fursa sio? ngoja nikachukue maujuzi kwa mzee wa upako maana kule ndio naonaga tembo wakitolewa kwa wingi na wazi bila muda maalum ndio maana anaongeza tu muda wa ibada
 
mie huwa nikikumbuka kuwa mtu fulani sijawasiliana naye hasa anayenihusu, itapita intavo ya dk kama tano hv mara nakuta simu inaiita au sms imeingia ya yule niliyekuwa namfikiria.

Mkuu nahisi ukiwafikiria wanaokudai na bado huna cha kuwalipa utakuwa unachukia sana
 
Deja vu...
Google...
Ni kawaida kwa binadam
 
Back
Top Bottom