Nahisi kuona vitu ambavyo vitanitokea, hii inatokana na nini ?

Nahisi kuona vitu ambavyo vitanitokea, hii inatokana na nini ?

wakuu sjui kama huu uzi ulishawahi kuletwa huku au bado ila kwa anayefahamu anaweza kunishauri.

Ninaweza nikawa nafanya kazi fulani, au niko mahali fulani au nakutana na watu fulani lakini huwa napata hisia halisi kabisa kwamba hicho kitu nilishawai kukifanya katika muda na mazingira yale yale hata kama ndio nafanya kwa mara ya kwanza. Au naweza nikakutana na watu ambao siwafahamu lakini akili inakuwa inalikumbuka hilo tukio kabisa yaani kama ilishawahi tokea kabla. Hii inanitokea katika mambo mengi na ni mara kwa mara. Kwa maana ya kwamba huwa nahisi kuona vitu ambavyo havijanitokea.

Kiukweli hali hii siipendi kwani inanipa hofu na kuumiza sana akili yangu kwa kutaka kujua kwa nini inakuwa hivyo. Mpaka naandika hapa imenitokea tena jana nilipoitwa kwa kiongozi wangu wa kazi na kunipa barua ya promotion, Yani lile tukio lilivyokuwa linatokea nikakumbuka mpaka maneno atayoongea mwishoni na ikawa hivyo,

Mwenye utaalamu na haya mabo tafadhali.

Mala zote nafsi hua inaweza kujua kijacho.Mungu ametuumba kwa namna ya mfano wake,akili yako inaweza kua na mambo mengi mpaka ikafuta kumbukumbu zote,lakini sio nafsi yako,unapoona mambo hayo inaonyesha uwezo ulio ndani yako kua ni mkubwa sana,tatizo hua ni jinsi gani utaweza kuchochea hiyo nguvu ikatenda kwa uhalisia zaidi ya hapo inapojionyesha na kwa akili zako zilizosongwa na mambo mengi isijue ni kitu gani kinaendelea,kiufupi usemacho ni nafsi iliwahi kujua kuna siku utapitia katika mambo kadhaa ambao ndio kama hayo,walioweza kutumia uwezo huo wapo kama vile wahubili na hata wasoma nyota ambao huitwa ni waongo na matapeli,lakini ukweli ni kwamba hutumia nguvu hizo kama ulizonazo,japo nakushauli ukitaka kujua vyema ni nini nafsi yako inaweza ikasema yajayo mshilikishe Mungu na si mwanadamu.hayo ni mawazo yangu kwa uelewa wangu,usiogope juu ya hilo,hiyo ni nafsi inakukumbusha kua iliwahi kukwambia utapitia hapo ila hukuweza kutunza kumbukumbu kwa sababu akili inabeba vitu vingi
 
Hiyo nyingine ya kusema af kitu kinatokea ni psych power na hiyo pia kila mtu anayo
But kwa sababu hatuidevelop professionally inakuja unconscious inakuwa Kama inatukera
Ukiona wazo limekuja af Ukaona ni baya bas likatae tu na wala halitotokea just kukataa tu bila hata kuingiza Imani yoyote coz hayo mambo ni Kazi ya akili tu


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mala zote nafsi hua inaweza kujua kijacho.Mungu ametuumba kwa namna ya mfano wake,akili yako inaweza kua na mambo mengi mpaka ikafuta kumbukumbu zote,lakini sio nafsi yako,unapoona mambo hayo inaonyesha uwezo ulio ndani yako kua ni mkubwa sana,tatizo hua ni jinsi gani utaweza kuchochea hiyo nguvu ikatenda kwa uhalisia zaidi ya hapo inapojionyesha na kwa akili zako zilizosongwa na mambo mengi isijue ni kitu gani kinaendelea,kiufupi usemacho ni nafsi iliwahi kujua kuna siku utapitia katika mambo kadhaa ambao ndio kama hayo,walioweza kutumia uwezo huo wapo kama vile wahubili na hata wasoma nyota ambao huitwa ni waongo na matapeli,lakini ukweli ni kwamba hutumia nguvu hizo kama ulizonazo,japo nakushauli ukitaka kujua vyema ni nini nafsi yako inaweza ikasema yajayo mshilikishe Mungu na si mwanadamu.hayo ni mawazo yangu kwa uelewa wangu,usiogope juu ya hilo,hiyo ni nafsi inakukumbusha kua iliwahi kukwambia utapitia hapo ila hukuweza kutunza kumbukumbu kwa sababu akili inabeba vitu vingi

Mkuu nafsi ndo roho?
 
Kitu chochote kabla ya kutendeka kwenye ulimwengu wa mwilini hutendeka katika ulimwengu wa rohoni. Mara nyingine mnachukuliwa rohoni na kuoneshwa mambo yajayo na Roho Mtakatifu lakini mnakuwa mmesahau kama mlichukuliwa na kuoneshwa rohoni. Jambo linapokuja kuthibitika kwenye ulimwengu wa mwilini ndio kama hivyo mnabaki mnashangaa.
Roho wa Mungu yuko katikati ya Watu wa Mungu kuwatendea mema na kuhakikisha wanakipata kile walicho andikiwa na Baba...
 
Mkuu Kawoli, Kuna mada moja nimezungumzia muda wa ulimwengu na matukio yake naona swali/mada yako linaendana na kipengele fulani cha future katika muda.

Kuna somo moja linapendekeza kuwa kutokana na jinsi tulivyoumbwa tunauona muda kama unakwenda mbele (flowing) na kwamba kuna past present na future. Past inaonekana kama imepita na haiwezi kubadilika na present inaonekana ndio au inahusishwa na reality alafu future ni kama vile haijatokea wala details zake hazijakuwepo. Flow ya muda ni illussion na ni matokeo ya jinsi ubongo wetu ulivyoumbwa.

Matukio yaliyo katika muda uliopita uliopo na unaokuja, yote yako katika mpangilio ambao una uwiano sawa na yaliyopita ni sawa na yanayokuja ila sisi binadamu kwa kawaida tunakumbuka yale yaliyopita (past) zaidi. Kutokana na ukweli huu wa kwa kawaida tunaweza kukumbuka past na siyo future hii inatujengea false impression kwamba muda unapita/unaenda kwa sababu kile ambacho hatukukijua (future) kimekuwa tunachokijua (past).

Kwakuwa future ni real na haiwezi kubadilishwa kama ilivyo past unahisi umekumbuka future? Kuna logical views nyingi zinazolezea kwa nini hatuwezi kukumbuka yale yaliyo mbele yetu ingawa yapo. Najiuliza je kama ungeamua kukataa promotion hiyo unadhani ungekuwa umeingilia mpangilio wa future? - kwa kuwa ulijua mpaka maneno ya mwisho yatakayosemwa na bosi wako.
 
Lakini mkae mkijua kuwa hiyo roho mnayozungumzia Ndio wewe mwenyewe


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
basi tuko wengi mie huwa naona na kila mikisemacho kama utan vile huja kuwa kweli?
mfano naweza kuona labda mtu fulan atakuja af kweli yule mtu huwa anakuja ama tukio fulan litatokea na kweli linatokea. cha ajabu zaid ni kwamba nikiona tukio la hatari af nikisema kwa mtu ama nikikemea lile tukio huwa halitokei lkn nisipo lisema kwa mtu ama kukemea linatokea.
sijipend na huwa naonaga kama ni aina fulan ya utambuzi ambayo pia siipendi


Hyo ndo nzuri ss
Na ukiwa umezama kiimani utakuwa unainyeshwa sn vitu!

Mi pia bt inani tokea kwa.kuota
 
Na Mimi inanitokea sana tu.tena baada ya tukio kumalizika ndio nakumbuka kwamba either niliwahi kuota ndoto kuhusu tukio lile au limewahi kunitokea before

Inshot ni hivi
Mungu huwa anasema na sisi kupitia Roho Mtakatifu
Shida ni kuwa hatuelewi coz hatujakaa na Mungu vzr
 
Ulimwengu wa Roho/usioonekana ni halisi.

Na kuna ulimwengu wa mwili huu ambao ni halisi.

Ss basi hakuna chochote kinachotokea kwenye ulimwengu wa mwili huu ambacho hakijaanzia kwenye ulimwengu wa roho.
msingi wa kila ki ni ulimwengu wa roho.

Mungu ni pendo.
Kabla chochote hakijatokea kwenye ulimwengu wa mwili hutujulisha kwanza kupitia ulimwengu wa roho. ..problem ni kuwa wengi bado hawaelewi wanajua ni ndoto za kawaida likitokea jambo anabaki anashangaa!

Bt satan ni baba wa uongo!

upande wa pili wana roho za utambuzi hawa ni waganga na wapunga pepo. ..

So u must b carefully na kumuomba Mungu akusaidie ucje ishia upande huo.

Nb sisi tunaemwabudu Mungu aliye hai ktk kristo Yesu huwa tunakemea au kuliombea jambo inategemea umeonyeshwa nn km mdau alivyosema yy huw anakemea
 
Mimi ilikuwa inanitokea Zamani...mfano nilienda shule boarding nikawa kama hiyo shule niliwahi kwenda before wakati ni first time....mostly ni vitu ulivyooteshwa ...na mostly ni vitu vizuri kwako...ndo maana wewe ulioteshwa promotion....inaaminika ni guardian Angel anakuotesha...
 
Yaani Umeandika Utafikiria Ni Mimi, Kuna Wakati Napigiwa Simu Na Mtu Mgeni Wa Sura Baadaye Naanza Kuvuta Picha Kuwa Mtu Huyu Atakuwa Yupo Hivi Na Hivi. Kweli Siku Nikija Kuonana Naye Namuona Yupo Vilevile Kama Nilivyo Muwaza.
 
Bora wewe una plan b ya kukemea mimi hii hali siipendi na sina plan b. nitajifunza kukemea

Hayo ni MAONO, na huonekana kwa watu wenye imani ya kweli. Ni wachache sana. Cha msingi simama katika imani, na uombe yaliyo mema na mungu atazidi kukufungulia, Na ukemee yaliyo mabaya na mungu atayafungia!
 
That is Called De Javu: Na hii ndo explanation :

De Javu ni hiyo hali ambayo wengi waliochangia wamesema wanaipataga...inaanza kutokea kwa mtu si chini ya miaka 9, ni stage ya brain development..jinsi mtu anavyokua ndo jinsi frequency ya kutokea huongezeka in teens and 20's ila as you get older inapotea (brain hai develop tena..ubongo unaanza ku depreciate..haha nimekosa neno..tuseme ubongo unaanza kuchakaa ndo maana usahaulifu unaanza etc)

Ok iko hivi..nielezee as simple as possible..in our brain kuna part ambayo ina process expirience zetu unconsciously (yani bila ufahamu wetu ) na kuna part nyingine ina process expirience zetu tukiwa na ufahamu kabisa..yani unaona au unahisi etc.

Tuanze na Visual System:

Wiley_Human_Visual_System.gif

Unapotazama kitu..ile image inapita kutoka nje then kwenye macho then kwenye organ kadhaa hapo katikati mwisho inafika kwenye occipital lobes ( hiyo sehemu ya njano hapo kwenye picha) hapo ndo image inatambulika..yani ikfika hapo wewe ndo utaweza kutambua ulichokitazama ni nini.
kumbuka nimesema image haitoki kwenye macho na kwenda direct kwenye occipital lobes..inapita sehemu nyingine hapo kwa ajili ya preliminary processing ....ila unakua hujaitambua..

NB: vipofu wengi ambao unaona wana macho mazima na wanatazama..mara nyingi wanakua na problems za occipital lobes..sio kwamba wakikuangalia hawakuoni...wanakuona ila wanashindwa kukutambua(this case is very interesting..we will discuss it next time).tuendelee

Inatokea ume expirience (kwa kuona in this case) say.. event A then B then C..then hizi ili uzitambue na zifikishwe kwenye conscious part ya ubongo inabidi zipite kwenye occipital lobe....ILA endapo occipatal lobe ita delay hata nusu sekunde... tuseme..ikapokea event A then B halafu ika delay kidogo...Event C itapelekwa kwenye Unconscious part..halafu occipital lobe sasa ikipokea event C na kuipeleka kwenye Consious part..wewe utahisi 'Mbona kama hili tukio nilishawai kuliona???' THAT IS IT..de Javu

Kwa Nyongeza:

1. kuna issue inaitwa Hypnogogic Jerk - unaweza kua una sinzia au muscles zime relax sana..au unalala halafu ghafla unashtuka (kwa nguvu)..au unakua kama umepigwa na shoti

2. Presque Vu - Unaweza kua uko familiar na kitu au mtu ..yani unakijua kabisa..kama ni movie labda umeiona mara 20 lakini ghafla tu unamsahau actor, au unakisahau kitu kabisaaaaa..na una uhakika una kijua vizuri tu etc..

Post yangu ishakua ndefu..ukitaka kujua more on that..kuna vitabu vya neuroscience vinaeleza kwa kina..au PM
 
basi tuko wengi mie huwa naona na kila mikisemacho kama utan vile huja kuwa kweli?
mfano naweza kuona labda mtu fulan atakuja af kweli yule mtu huwa anakuja ama tukio fulan litatokea na kweli linatokea. cha ajabu zaid ni kwamba nikiona tukio la hatari af nikisema kwa mtu ama nikikemea lile tukio huwa halitokei lkn nisipo lisema kwa mtu ama kukemea linatokea.sijipend na huwa naonaga kama ni aina fulan ya utambuzi ambayo pia siipendi
gfsonwin hata ile issue yetu tuliokuwa tunaidiscuss jana, ulishaiwaza kabla? ama ushaiona mwisho wake ukoje? hebu nisaidie dadangu, leo yamekuwa makubwa zaidi ya jana!
 
Last edited by a moderator:
hii hali inaitwa Deja Vu, ambayo inaelezwa hapa, someni tafadhali: "Have you ever visited -a store for the first time and had it feel eerily familiar? Or maybe you're deep in conversation with a friend and you suddenly get the feeling that you've had the exact conversation before, even though you know that you haven't. If you've ever found yourself in either of these situations, you've experienced déjà vu. Sixty to 70 percent of us admit to getting this feeling at least once in our lives. The sight, sound, taste or even smell of something makes us think that we've experienced it before, although we know that we couldn't have.

There are more than 40 theories as to what déjà vu is and what causes it, and they range from reincarnation to glitches in our memory processes. In this article, we'll explore a few of those theories to shed some light on this little understood phenomenon.
Déjà vu is a French term that literally means "already seen" and has several variations, including déjà vécu, already experienced; déjà senti, already thought; and déjà visité, already visited. French scientist Emile Boirac, one of the first to study this strange phenomenon, gave the subject its name in 1876.
There are often references to déjà vu that aren't true déjà vu. Researchers have their own definitions, but generally déjà vu is described as the feeling that you've seen or experienced something before when you know you haven't. The most common misuse of the term déjà vu seems to be with precognitive experiences -- experiences where someone gets a feeling that they know exactly what's going to happen next, and it does. An important distinction is that déjà vu is experienced during an event, not before. Precognitive experiences -- if they are real -- show things that will happen in the future, not things that you've already experienced. (However, one theory about déjà vu deals with precognitive dreams that give us a "déjà vu feeling" afterwards. See the Déjà Vu and Precognitive Dreams section.)
Hallucinations that are brought on by illness or drugs sometimes bring a heightened awareness and are confused with déjà vu. False memories that are brought on by schizophrenia can be confused with déjà vu as well. Unlike true déjà vu, which typically lasts from 10 to 30 seconds, these false memories or hallucinations can last much longer.

inapatikana zaidi hapa:

http://science.howstuffworks.com/science-vs-myth/extrasensory-perceptions/deja-vu.htm

Ni vema kuvumilia makala ndefu na kujifunza zaidi mambo tusiyoyajua.
 
hata mimi hali kama hiyo inanitokeaga, unakuta kuna tukio nimefanya au limetokea sasa hivi lakini nakumbuka kabisa nilishawaza au nilishalionaga muda flani kabla.

definitely...hii kitu ipo lakini ni ngumu sana kuielezea kitaalamu
ni aina za ndoto.
 
Back
Top Bottom