Nahisi kuona vitu ambavyo vitanitokea, hii inatokana na nini ?

Nahisi kuona vitu ambavyo vitanitokea, hii inatokana na nini ?

Inaamina dunia ilishaisha sasa wale watu walio ishi ndo wanakumbukia maisha so hata hapo unapoishi ni unakumbukakia tu kama mm ninauwezo wa kuona cku nzima ya leo nikiwa nimelala
 
Hata bange sometimes huleta maono ya jinsi hii

Lakini kwa bange au hallucinogen nyingine inafanya mtu awe completely anaamini Ndio ukweli Ila experience hizi zinatokea mtu akiwa aware


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Daah Mimi huwa zaidi ni ndotoni alafu likija kunitokea nakumbuka picha nzima.sasa hivi huwa Nina naandika kwenye kitabu harafu huwa linatokea kweli daah mbaka naogopa .Kuna jamaa yangu kaniambia kwamba sisi binadamu ni wa toleo jipya kwa hiyo roho zetu zilikuwepo kwa watu wengine wanaofanana kila kitu na wewe uliye sasa wao walikufa matendo yanayojirudia ni yaleyale ijapokuwa ktk mazingira tofauti

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Hii hali inaitwa deja vu. Binadamu wengi huwapata. Hata mimi huipata mara nyingi. Uki google neno deja vu imeelezewa sana na vyanzo mbalimbali. Kifupi nilivyoielewa hali hiyo ni kwamba uki ona,gusa,nusa,lamba au sikia kitu,kile kitu hakiendi moja kwa moja ubongoni kwa tafsiri. Huanza kupita sehemu iitwayo subconcious mind na kisha kwenda ubongoni kwa tafsiri. Sasa kuna wakati ike taarifa huwa inapitiliza na kwenda ubongoni moja kwa moja(ambako mara moja itatafsiriwa),kisha inarudishwa subconcious area. Hili likitokea,kwa sababu ubongo utakua ulisha tafsiri,utaletewa tafsiri nyingine na subconcious mind kwamba kitu hicho au hali hiyo ulisheiona! Sababu tayari ilisha tafsiriwa na kuhifadhiwa ubongoni. Kwa walioona filamu ya matrix,mfano wa deja vu umeoneshwa. Leo ambaye ni main character alimuona paka wa rangi ileile,size ileile,akikatisha eneo lilelile kwa wakati uleule. Mwenzake akamwambia'hiyo ni deja vu'lakini kwa pale haikuwa hivyo,ilikuwa real thing kwani walikua wana deal na matrix system!
 
Hata mimi nilikuwa nayo...sasa bab kubwa ni moja niliyopaa na kupelekwa mpaka jehanam na kuona watu wanavyoungua moto
 
wewe unaonekana unavuta sana bangi na kuwatamani dada zako....
 
Inaamina dunia ilishaisha sasa wale watu walio ishi ndo wanakumbukia maisha so hata hapo unapoishi ni unakumbukakia tu kama mm ninauwezo wa kuona cku nzima ya leo nikiwa nimelala

HAPA KUNA AINA FULANI YA UKWELI...IS VERY COMPLICATED KWA MANAKE MPAKA LEO HAKUNA KITU KINACHOWEZA KU PROVE KISAYANSI NDOTO INGAWA KILA MTU ANAOTA....TOKA ENZI ZA NDOTO ZA YUSUFU AMBAZO NAZO ZILIKUJA KUTOKEA....KUANZIA HAPO NDO mUNGU PEKEE ANAWEZA JUA.....
 
Mimi ilinitokea siku moja kabla ya kujifungua,nilikua nimekaa nyumbani mchana kikaanza tu kuimagine nimepata uchungu,nakwenda hospital na baada ya kufika hospital nkajifungua mtoto wa kike then mume wangu akaja na kibegi cha nguo za mtoto,heee cha ajabu siku iliyofuata nilipatwa na uchungu,the whole situation niliyoiona kwenye imagination ndio ilikua inatokea for real,hakuna kilichobadilika,mume wangu alipokuja hospitali kweli alileta kibegi cha nguo na nilipifungua ndani zilikua nguo ambazo niliziona katika imagination,ikabidi nianze kumsimulia mume wangu,nae akabaki anashangaa
 
wakuu sjui kama huu uzi ulishawahi kuletwa huku au bado ila kwa anayefahamu anaweza kunishauri.

Ninaweza nikawa nafanya kazi fulani, au niko mahali fulani au nakutana na watu fulani lakini huwa napata hisia halisi kabisa kwamba hicho kitu nilishawai kukifanya katika muda na mazingira yale yale hata kama ndio nafanya kwa mara ya kwanza. Au naweza nikakutana na watu ambao siwafahamu lakini akili inakuwa inalikumbuka hilo tukio kabisa yaani kama ilishawahi tokea kabla. Hii inanitokea katika mambo mengi na ni mara kwa mara. Kwa maana ya kwamba huwa nahisi kuona vitu ambavyo havijanitokea.

Kiukweli hali hii siipendi kwani inanipa hofu na kuumiza sana akili yangu kwa kutaka kujua kwa nini inakuwa hivyo. Mpaka naandika hapa imenitokea tena jana nilipoitwa kwa kiongozi wangu wa kazi na kunipa barua ya promotion, Yani lile tukio lilivyokuwa linatokea nikakumbuka mpaka maneno atayoongea mwishoni na ikawa hivyo,

Mwenye utaalamu na haya mabo tafadhali.

kwakweli hili unaloliandika hata nami huwa linanitokea
 
Una kipaji Mkuu ulichojaliwa na Mungu cha kuyaona yatakayojiri siku za usoni kama ni mazuri hamna neno kama ni mabaya basi inatisha, kukukosesha raha na kukuweka katika wasiwasi mkubwa.
 
Kinachotokea hapo ni delay kati ya macho after kukiona ki2 na brain kuinterprete Hilo 2kio. So unakuwa ushaliona 2kio na kusikia kilichosemwa then wakati brain inainterprete unakuwa unaona kama 2kio linajirudia. Hakikisha unapata mda Mzur wa kupumzika na kupumzisha akili yako.
 
Hiyo kitu wanaita deja vu
Kila mtu anayo sio wewe tu
But hakuna scientific explanation inayotosheleza kueleza hiyo kitu
Wala usiogope
Pia Muda mwingine ni ndoto ulizozisahau af zinakuwa kweli


Sent from my iPhone using JamiiForums

Me mara nying ndoto au kama alivo sema Huwa kit kama nimewah kukifanya
 
Mkuu Kawoli, Kuna mada moja nimezungumzia muda wa ulimwengu na matukio yake naona swali/mada yako linaendana na kipengele fulani cha future katika muda.

Kuna somo moja linapendekeza kuwa kutokana na jinsi tulivyoumbwa tunauona muda kama unakwenda mbele (flowing) na kwamba kuna past present na future. Past inaonekana kama imepita na haiwezi kubadilika na present inaonekana ndio au inahusishwa na reality alafu future ni kama vile haijatokea wala details zake hazijakuwepo. Flow ya muda ni illussion na ni matokeo ya jinsi ubongo wetu ulivyoumbwa.

Matukio yaliyo katika muda uliopita uliopo na unaokuja, yote yako katika mpangilio ambao una uwiano sawa na yaliyopita ni sawa na yanayokuja ila sisi binadamu kwa kawaida tunakumbuka yale yaliyopita (past) zaidi. Kutokana na ukweli huu wa kwa kawaida tunaweza kukumbuka past na siyo future hii inatujengea false impression kwamba muda unapita/unaenda kwa sababu kile ambacho hatukukijua (future) kimekuwa tunachokijua (past).

Kwakuwa future ni real na haiwezi kubadilishwa kama ilivyo past unahisi umekumbuka future? Kuna logical views nyingi zinazolezea kwa nini hatuwezi kukumbuka yale yaliyo mbele yetu ingawa yapo. Najiuliza je kama ungeamua kukataa promotion hiyo unadhani ungekuwa umeingilia mpangilio wa future? - kwa kuwa ulijua mpaka maneno ya mwisho yatakayosemwa na bosi wako.

Kiukweli mkuu kumbe elimu hainaga mwisho. nilikuwa siyajui kabisa haya uliyoyaweka hapa. Nitaisaka hiyo mada mkuu
 
Daah Mimi huwa zaidi ni ndotoni alafu likija kunitokea nakumbuka picha nzima.sasa hivi huwa Nina naandika kwenye kitabu harafu huwa linatokea kweli daah mbaka naogopa .Kuna jamaa yangu kaniambia kwamba sisi binadamu ni wa toleo jipya kwa hiyo roho zetu zilikuwepo kwa watu wengine wanaofanana kila kitu na wewe uliye sasa wao walikufa matendo yanayojirudia ni yaleyale ijapokuwa ktk mazingira tofauti

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

duu bora me ingeniingia roho ya biligeti
 
wewe unaonekana unavuta sana bangi na kuwatamani dada zako....
rolla wengi humu wamekubalina na hii hali huwa inawatokea, kwaio wote hawa wanavuta bhange kuwatamani da/kaka zao?
 
Last edited by a moderator:
Si binafsi hali hii nime experience kwa miaka mingi mpaka sasa,na sijui ni kwanini?
 
Back
Top Bottom