Nahisi wapo watu wana ugomvi na Waziri Mkuu wetu mchapa kazi hodari

Crocodiletooth

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2012
Posts
20,561
Reaction score
24,428
Nimekuwa nikipita humu mara kwa mara na threads nyingi zimekuwa zikimtakia au kumuombea mabaya Waziri wetu Mkuu mchapa kazi hodari mzalendo wa kweli asiyependa uzembe utokee popote, amekuwa akipigwa Vita na vya kimtandao wa kumuombea mabaya yamfike.

Nadhani pengine hili linatokea baada ya pengine mirija yao ya upigaji kuzibwa aidha wanaona amekuwa kikwazo kwao kwa namna moja au nyingine.

Kassim Majaliwa ndiye Waziri Mkuu anayeifaa Tanzania yetu kwa nyakati hizi, ni mkali kidogo, anapofika mahala jasho huanza kuwatoka wabadhirifu.

Naoimba CCM na vikao vyake na mamlaka zake kutokana na hayo yanayoendelea mitandaoni isiyafuate, Majaliwa anaifaa Tanzania yetu kwa nyakati hizi.

Jumatano kareem.
 
Allah atamlinda na mahsuda na awapeperushe kama karatasi!
 
Kabisa !!
 
Waziri Mkuu wenu sio mchapa kazi bali ni fisadi mkubwa. Kajenga uwanja wa mpira na kumiliki timu ya mpira kwa pesa za ufisadi. Ni mpigaji mkubwa wa pesa za umma
 
Naunga mkono hoja, kuna watu wana wivu wa kike na Majaliwa!.
P
 
Waziri Mkuu wenu sio mchapa kazi bali ni fisadi mkubwa. Kajenga uwanja wa mpira na kumiliki timu ya mpira kwa pesa za ufisadi. Ni mpigaji mkubwa wa pesa za umma
"Amefisadi akajenga uwanja wa mpira unaotumiwa na umma wa watanzania wote!"
Tafakuri......!
Siamini kama ni mmiliki wa timu bali naweza kuamini kama mfadhili na msaidizi.
 
Kundi la Msoga,halipendezewi kumuona Majaliwa akiwa karibu na Samia!
 
Hilo ni kundi la watu wapumbavu sana!

Wanafikiri Majaliwa asipokuwa waziri mkuu watakuwa wamemkomoa marehemu na pia wao machadema sasa watakuwa wameenda ikulu kwa kishindo!

Ni utaahira wa hali ya juu sana
 
Hilo ni kundi la watu wapumbavu sana!

Wanafikiri Majaliwa asipokuwa waziri mkuu watakuwa wamemkomoa marehemu na pia wao machadema sasa watakuwa wameenda ikulu kwa kishindo!

Ni utaahira wa hali ya juu sana
Hii ni Vita ya ndani kwa ndani chadema haipo hapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…