Nahitaji kuwekeza Tsh. Milioni 170

Nahitaji kuwekeza Tsh. Milioni 170

Hivi kwanini sasa hivi kila mtu anawaza kuwekeza UTT na BOT, ina maana mazingira ya kufanya biashara Tanzania yamekuwa magumu sana au purchasing power ya raia imepungua sana? Yaani hakuna anayewaza hata kuhusu fursa za export.
Mazingiravya biashara tz ni risk sana hiyo ndio options pekee kwa wengi wasio na ideas za biashara na misukosuko yake..
 
Kaka sio simple kihivyo Ku shinda bid ya bond au treasury bill sio rahisi-unaweza ukawa na fedha zako na usipate hiyo nafasi ya kuzinunua.
Zina ushindani sana,kila MTU anataka kula kwa mrija.
KwanzA huwezi kaa mwaka mzima ukakosa chance kwenye annual calenda nzima

Pili, ukishindwa kuingia direct kwenye BONDS za serikali BOT tumia utt AMIS ana mfuko wa Bonds Hela zake Huwa anawekeza kwenye Kununua Bonds za serikali.

Nadhani umenielewa.
 
Kama uko interested nipigie 0714 122 011
Nikupe mpango wa Jenga uza,
Utapiga mchele wa kutosha,
Biashara ambayo haina hasara kabisa,
Kama faida inaweza kuwa milioni 3 mpaka 4 kwa mwezi kuanzia tunaanza kujenga mpaka tunaiuza,
Piga simu
Jenga uza sio rahisi kiivo boss huwezi pata mteja kirahisi kwa faida nzuri maana kila mwezi upate mteja wa kununua nyumba si rahisi abadan.
 
Toa ujinga wako hapa unasema wabongo eti hawajui kutafuta fursa. Umeitembea hii nchi uone wabongo wanavyochakarika! Kutafuta fursa ni Hadi kutoka nje ya nchi kwani. Nchi yetu Ina Kila kitu kwani ni vibaya mtu kukomaa na nchi yake.

Kipindi cha mwendazake kabla hajachafua soko la korosho ungeenda mtwara ukaona wabongo wanavyosambaza mabilioni kwenye korosho!

Usiongee vitu usivuojua.

Mutual funds ni uwekezaji sio biashara. Sio Kila binadamu anaiweza biashara. Sio Kila mtu anaweza compliance za TRA na regulatory bodies zingine za biashara kwanini asiweke Hela yake BOT au UTT AMIS. Kwani ni dhambi.


Huyo alieenda Kongo na Dola Laki 5 ni sawa na Bilion Moja. Hiyo Hela angepelea BOT akanunua BONDS za miaka 25 angekuwa anavuta milion 10+ Kila mwezi.


Na angeweza kutumia BOND certificate kama collateral kuchukulia mkopo bank hadi nusu kwa alichowekeza BOT. Maana yake bank wangeweza kumpa Hadi mkopo wa milion 500.

Hiyo milion 500 ya mkopo angeweza kuwekeza kujenga nyumba kadhaa Dar akapangisha. Kodi ya hizo nyumba ndio zingelipia mkopo. Na kama Kodi ingekuwa ndogo kwenye kulipa mkopo wa bank angetumia sehemu ya ile milion 10 ya riva ya BOT kusaidia kumalizia mkopo.

Mkopo ukiisha. Anakopa Tena bank Kwa kutumia collateral ya hizo nyumba kujengea hizo nyumba. Kumbuka ile Hela ya BOT milion 10 Iko pale pale.


Matajiri wote duniani hutumia Hela za masikini zihazokaa bank kufanyia projects zao. Wewe masikini unapeleka Hela bank MO DEWIJ anaenda kukopa ajengee ma-apartments.


Sio Kila mtu anaweza kuexport au kufanya biashara. Kila mtu afanye jambo Kwa personality yake. Biashara inahitaji roho ngumu , kujikana na kuwa tayari kwa lolote.

Ukiona huna hizo characters tafuta investment basi. Usione wanaoenda kuwekeza hawajielewi.
mjinga mwenyewe,hicho ulichoandika unafikiri nani asiye kijua, nafikiri hukuipata point yangu vizuri tangu mwanzo umedandia tuu mada, mimi sijapinga mtu ku invest niliuliza miaka hii ya karibuni watu wengi wanakimbizia mitaji yao kwenye mutual funds na bot ni kwamba mazingira ya kufanya biashara tanzania yamekuwa magumu au watu ni wavivu wa kutafuta fursa mpya.?
 
mjinga mwenyewe,hicho ulichoandika unafikiri nani asiye kijua, nafikiri hukuipata point yangu vizuri tangu mwanzo umedandia tuu mada, mimi sijapinga mtu ku invest niliuliza miaka hii ya karibuni watu wengi wanakimbizia mitaji yao kwenye mutual funds na bot ni kwamba mazingira ya kufanya biashara tanzania yamekuwa magumu au watu ni wavivu wa kutafuta fursa mpya.?
Kunguni wewe ulisoma comprehension kweli wewe.
 
Usijaribu kufanya biashara yoyote huku ukiwa huna uzoefu wowote ule. Bora ukafuata tu ushauri wa wadau hapo juu.

Kaweke hiyo hela kwenye hiyo biashara ya hati fungani, ukishindwa kabisa basi tafuta eneo lenye wasafiri/mzunguko mkubwa wa watu; jenga lodge yako standard! Halafu weka cctv cameras, weka usimamizi makini! Halafu uje ulete mrejesho.

Ukiingia tu kwenye biashara! Sijui ya madini, mazao, kilimo cha matikiti, nk. Hiyo hela yote itapukutika.
 
Kwamba rejesho dogo au kubwa sana?
Kariakoo kuna watu hawana mitaji(wanatafuta wateja wanachukua mzigo mali kauli wanamake at least 150 kwa siku - though kuna siku wanakosa lakini leo ukipata 150k, unakaa siku 4 pakavu, unapata 2m siku 1, unakaa wiki pakavu, anothe day unamake 700k ukija wastani wa mwezi unakuta una at last 150 daily) na wanamake zaidi ya 3m kwa mwezi wamejenga nyumba hawafanani nazo ukiwaona utajua wameachiwa kulinda, sasa huyu ana m170 anataka 2M huoni ni hajawa well informed, yaani huyu biashara akianza si ajabu akaangukia pua.
 
Za jioni wadau,

Naomba mchango wa mawazo yenu, nikiwa na milioni 170 za kitanzania naweza wekeza wapi pesa hii nikapata rejesho lenye tija?

Kwangu mimi rejesho lenye tija ni angalau milioni 2 kwa mwezi.

Natanguliza shukrani.
Jiunge na Niffer atakusaidia
 
Mkuu,
Kama kweli Upo Serious na Pesa Ipo Sio Kwenye Makaratasi nakucheck PM.Ila kwa Milioni 170 kutaka Faida ya 2 M kwa mwezi huhitaji kuumiza kichwa tembea kwenye Mabenki unaweza fanya Nao negotiation kidogo na risk ikawa Ndogo.Ila Kama Uko Serious Kabisa Nakucheck PM kuna maswali Nitakuuliza Then Huenda Ukaweza Kutengeneza Hadi 7,000,000 kwa Mwezi.
Kuna mtu anapigwa hapa. Kuwa makini kaka mwenye 170m
 
Kwahyo kwa pesa yako hiyo tunaweza kujenga nyumba mbili kali sana tukauza na kuziuza ndani ya miezi minne tushajenga nyumba mbili na kuziuza tayari(miezi miwili na nusu ujenzi mwezi mmoja na nusu kuuza)
Nyumba moja labda tunajenga kwa milioni 80 yaani kununua kiwanja na kujenga kilakitu tunakuja kuuza milioni 100 kwahyo unafaida ya milioni 20 kwa nyumba moja,
Kwa nyumba mbili unafaida ya milioni 40 kwa mtaji wa milioni 160,
Kumbuka nyumba hizi tumejenga zote na kuuza ndani ya miezi minne tuu,
Kwahyo ndani ya miezi minne tayari unafaida ya milioni 40 inamaana kwa mwezi unakuwa umetengeneza kama milioni 10 kwa mtaji wa milioni 160,
Kwa mwaka kutengeneza faida ya milioni 100 ni kawaida tuu,
Kumbuka mtaji wako unakua kwahyo kwa mwaka unaofata utatengeneza faida ya zaidi ya milioni 200 mwaka unaofata tena ni milioni 400 na kuendelea,
Aliekuwa serious apige simu tufanye kazi
Njoo tufanye kazi Boss [emoji3513] +255 714 122 011
Wewe huna akili.
 
Back
Top Bottom