Nahitaji ndoa ya uke wenza

Hebu mkalishe kitako mdogo wako akueleze yanayomsibu, pengine ni makubwa kama dunia, si ndio mwenyewe asemavyo?
Hahahaaa!!! Hana lolote kaamua kunichemsha tu huyo.

Nimjuavyo angekuwa na makubwa wala asingeweza kuandika hapa. Saa hizi angekuwa Tanga kwa Maama na akiwa kule huwa hapatikani kirahisi.

Wajua tena Watanga tukikutana kwa stori hata simu hazishikwi yaani twaweka pembeni. πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Maasha Allah.

Allah awaongoe
 
Unajua watu wengine hupenda tu kufanya ushabiki. Mimi namfahamu Khantwe na najua analijua alilolimaanisha Marnah ila basi tu ushabiki
 
Umenikumbusha mbali Wallah Shadeeya! Maana Watanga hasa KE, wawe mabinti wadogo au wamama watu wazima, wakikutana wataongea kuanzia asubuhi, mchana, jioni na kama wanalala sehemu moja, basi na usiku pia watakesha hadi alfajiri wakiwa wanastorishana tu!

Wakiamka mwendo ni huohuo najiulizaga hivi yote wanayoongea yanakua ni ya kweli au mengine umbea tu?πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚. Lakini kwa vile hua hayanihusu nabakia kuwaangalia na kuwashangaa tuπŸ˜€... kawaida yao lakini Makorora kudekaπŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Hahahaaaa. Huwa hayaishi tamu mazungumzo yaani si ajabu basi hapo mkianza enhee wamjua mtoto wa mzee fulani hivi bado yupo pale akianza kuhadithia basi utauliza yuko wapi? Mama yake je? Na Mkaza fulani naye bado yupo pale pale?πŸ˜…πŸ˜… basi tafrani.

Ila tumejizoelea wenyewe hatuoni shida.
 
Alaa, kuumbee! Mwataka jua habari za kila mmoja, kuanzia yeye mwenyewe, watoto wake, wazazi wake, marafiki/mashosti zake, majirani zake kama kina Mzee Mabruki, wote aliosoma nao kuanzia chekechea hadi chuo! Hahahaaa ndio maana basi mambo hayeshi, ushanipa siri ya kambi sasa ShadeeyaπŸ˜€πŸ˜‚πŸ˜€πŸƒβ€β™‚οΈπŸƒβ€β™‚οΈπŸƒβ€β™‚οΈ
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…