Naibu Rais Gachagua augua ghafla na kupelekwa hospital Muda mfupi kabla hajaanza kutoa ushahidi

Naibu Rais Gachagua augua ghafla na kupelekwa hospital Muda mfupi kabla hajaanza kutoa ushahidi

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Katika hali isiyotarajiwa, Naibu wa Kenya Rais Rigathi Gachagua ameripotiwa kuzidiwa na kupelekwa hospitalini zikiwa zimebaki dakika chache kabla ya kutoa ushahidi wake.

Wakili wake, Paul Muite, aliwaambia Maseneta kuwa Gachagua alizidiwa baada ya chakula cha mchana wakati akisubiri kesi ya kumwondoa madarakani iendelee .

Ikumbukwe kuwa leo, Maseneta walitarajiwa kupiga kura juu ya mashtaka 11 yanayomkabili Gachagua.

Muite alisema, “Ukweli mchungu ni kwamba Naibu Rais wa Jamhuri ya Kenya ameugua sana, na anapokea matibabu hospitalini."

Muite hakufichua ni hospitali gani Naibu Rais amepelekwa wala aina ya ugonjwa unaomsumbua.
Gachagua alitarajiwa kutoa ushahidi wake mwenyewe katika kesi hiyo ya kumvua madaraka yake kama Naibu Rais

Spika Kingi alisema,

“DP alitarajiwa kutoa ushahidi. Nilitangaza mpango uliotakiwa kufanyika mchana, na nikaeleza kuwa tutautekeleza mpango kwa umakini ili tumalize jambo hilo leo. Wakili Paul Muite alisema hawezi kumfikia mteja wake, lakini hilo si jukumu la Bunge. Seneti inamngoja Naibu Rais, hakuna Seneta mwingine atakayechukua nafasi hiyo."

Nation.png

Source: Nation Africa

Pia, soma: Yanayojiri katika Kesi ya kumuondoa Madarakani Naibu Rais wa Kenya, Rigathi Gachagua leo Oktoba 17, 2024
 
Hiyo ndio breaking news

Wakati Baraza la seneti linaahirishwa saa 7:15 ilitangazwa watakaporejea saa 8:30 Naibu Rais Gachachagua ataanza kujitetea Kwa muda wa dakika 120

Lakini ndio hivyo tena 🐼
Mkuu hayo mashtaka yote ni kumbambikia. Ni mfumo umemkataa tu. Hayo maneno aliyosema wanasiasa wa Afrika wanayasema kila kukicha. Magufuli mwenyewe alikuwa anayasema kila siku. Ila tumejifunza kuwa mabunge yote ya Kenya ni kama wanafunzi wa vyuo vikuu na mabunge ya kwetu (bara na wawakilishi) ni kama chekechea.
 
Leo mchana muda wa saa nane na dakika 20 ulikuwa mahsusi kwa Naibu Rais wa Kenya Mh Rigathi Gachagua kutoa utetezi wake. Lakini Cha kushangaza wakili wake Mr Paul Muite akadai hapatikani. Ila baada ya muda wakili wake huyo akadai amewasiliana naye na kwamba yupo hospitalini kalazwa. Inakuaje kalazwa muda wa kutoa ushahidi wake?

Kuna kitu kakiona kaona aingie mitini?. Kwa Sasa seneti inajadili maamuzi ya namna watakavyoendelea na hili suala.
 
Mkuu hayo mashtaka yote ni kumbambikia. Ni mfumo umemkataa tu. Hayo maneno aliyosema wanasiasa wa Afrika wanayasema kila kukicha. Magufuli mwenyewe alikuwa anayasema kila siku. Ila tumejifunza kuwa mabunge yote ya Kenya ni kama wanafunzi wa vyuo vikuu na mabunge ya kwetu (bara na wawakilishi) ni kama chekechea.
Kweli kabisa
 
Wakati Baraza la seneti linaahirishwa saa 7:15 ilitangazwa watakaporejea saa 8:30 Naibu Rais Gachagua ataanza kujitetea Kwa muda wa dakika 120.

Hata hivyo baada ya kurejea hakuonekana. Kwa mujibu wa maelezo ya wakili wake, naibu huyo wa rais wameugua ghafla hivyo amepelekwa hospitalini kwa matibabu.

Baada ya majadiliano, Spika wa Bunge la Seneti amesitisha kikao na kuamuru kirejee saa 11 kamili jioni ili kujua kama Gachagua atakuwa sawa ili kutoa ushahidi au la kwani mchakato huu umefungwa na muda wa kisheria.
Hiyo ndio faida ya kusoma elimu ya falaq!
 
Sarakasi Zinaendelea huku..., Mambo Lukuki yapo at a Standstill...., Bima za Afya.., Huku Airport na Mikataba na Adani haijulikani nini ni nini as well as Umeme nao kuna Mikataba yenye Sintofahamu...

Wao wapo kwenye Drama....., Kweli Politics kwa sasa Duniani ni full of Maigizo...
 
Back
Top Bottom