Naibu waziri wa Mambo ya Ndani Hamad Masauni na Ramadhani Kailima watinga TAKUKURU kuhojiwa

Naibu waziri wa Mambo ya Ndani Hamad Masauni na Ramadhani Kailima watinga TAKUKURU kuhojiwa

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni amefika Ofisi za TAKUKURU Dodoma,  ( 640 X 640 ).jpg


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani nchini Tanzania, Ramadhani Kailima ( 640 X 640 ).jpg


Baadhi ya wadau walikuwa wanajiuliza kwamba kama Waziri wa Mambo ya ndani na Katibu wake wameng'olewa mbona wasaidizi wao hawajaguswa ?

Jibu laweza kupatikana baada ya Naibu Waziri wa mambo ya ndani Hamad Masauni na Naibu Katibu Mkuu Ramadhan Kailima kutinga TAKUKURU kwa mahojiano .

Dodoma. Naibu katibu mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Ramadhan Kailima leo asubuhi Februari Mosi, 2020 amefika katika ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mjini Dodoma kuhojiwa.

Kailima amefika katika ofisi hizo kuhitimisha idadi ya walioondolewa kwenye wizara hiyo na wanaoendelea na majukumu yao kuhojiwa na taasisi hiyo kwa agizo la Rais John Magufuli.

Jana alihojiwa aliyekuwa waziri wa wizara hiyo, Kangi Lugola, Meja Jenerali Jacob Kingu (alikuwa katibu mkuu) pamoja na aliyekuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye.

Mbali na Kailima, naibu waziri wa wizara hiyo, Hamad Masauni naye atahojiwa leo.
Wote wanatuhumiwa kuhusika katika mkataba wa jeshi la Zimamoto unaotajwa kuwa na harufu ya ufisadi. Rais Magufuli ndio aliibua kasoro katika uingiaji wa mkataba huo na kuwataja jinsi walivyohusika.

Magufuli amesema Kailima alihusika kuanzia mwanzo hadi mwisho wa mchakato wa kuingia mkataba huo wa kununua ndege zisizo na rubani kwa ajili ya kuzima moto. Kiongozi mkuu huyo wa nchi amesema Kingu aliandika barua ya kujiuzulu na kuiridhia. Kingu ameteuliwa kuwa balozi.

Kailima amewasili Takukuru saa 2:52 asubuhi katika gari aina ya Toyota Land Cruiser.

Huku akiwa amevaa tisheti ya mistari ya rangi nyeupe na damu ya mzee na suruali nyeusi, alikuwa ameambatana na msaidizi wake aliyekuwa amebeba begi jeusi.

Baada ya kushuka katika gari hilo, aliingia ndani kupitia mlango mdogo wa ofisi hizo, baada ya muda alitoka na kupita katika mlango mkubwa ambao ndani kuna eneo la mapokezi.

“Jamani salama,” amesema Kailima wakati akipishana na waandishi wa habari waliopo ndani na nje ya jengo hilo lililopo mtaa wa Jamhuri.

Pia soma: Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola adaiwa kuwa chini ya ulinzi
 
View attachment 1343363

View attachment 1343364

Baadhi ya wadau walikuwa wanajiuliza kwamba kama Waziri wa Mambo ya ndani na Katibu wake wameng'olewa mbona wasaidizi wao hawajaguswa ?

Jibu laweza kupatikana baada ya Naibu Waziri wa mambo ya ndani Hamad Masauni na Naibu Katibu Mkuu Ramadhan Kailima kutinga TAKUKURU kwa mahojiano .

Wameenda kuhadaa watanzania kuwa kuna la maana. Hiyo Takukuru ni taasisi ya kusafishia wezi.
 
Mapicha picha mengi nadhani ni matangazo ya biashara?
 
Jiwe ana maigizo ya ajabu sana kibali Cha kina Lugola kwenda nnje ya nchi nani aliwapa ? Na wsliandika sababu zipi za kwenda nnje ya nchi.
 
Ndivyo ilivyokuwa leo makao makuu ya Takukuru jijini Dodoma kwamba Naibu waziri na Naibu katibu mkuu wamehojiwa kila mmoja kwa masaa zaidi ya mawili.

Masauni na Kahilima baada ya mahojiano hawakuweza kuongea lolote na waandishi wa habari bali walikimbilia kwenye magari yao na kuondoka kwa kasi.

Source ITV habari

My take; Hawa wawili hawakupaswa kukaa pembeni kupisha uchunguzi?!
 
Nakumbuka katika lile sakata la mkataba wa kununua vifaa vya kuzima moto lililopelekea kutumbuliwa Kangi Lugola na Kamishna Thobias Andengenye, Mheshimiwa Rais Magufuli alisema Naibu Waziri alishaandika barua ya kuachia ngazi mapeema na hata akashangaa Waziri alipataje guts za kuhudhuria kwenye mkutano wake.

Leo nilikua napitia magazeti katika mtandao nikakutana na habari za Masauni akiwaagiza polisi huko Zanzibar kuwaachia kwa dhamana watuhimiwa wenye makosa ya kudhaminika ili kujikinga na maambukizi ya virusi ya korona.

Sikumbuki kusikia kauli ya kumrudisha kwenye nafasi yake lakini nikiri pia sikuwahi kumsikia Mheshimiwa Rais akisema amekubaliana na barua ya kujiuzulu la Masauni

Kwa muktadha huo najiuliza je Bwana Masauni sio miongoni mwa waliofanya kazi ya kum snitch Kangi na Thobias huku ikionekana na yeye naye yupo kwenye hot soup lakini kiuhalisia yeye ndio kauza wenzie?

20200410_071017.jpg
 
mbona Rais alisema Masauni hakuhusika na hiyo dili na yeye ndio aliofanya ajue huu uozo

Sent using Jamii Forums mobile app
Sikuwahi kuiskia hiyo kauli mkuu. Ninachokumbuka siku ile kwenye ile hafla ya polisi pale kurasini Rais alisema Naibu Waziri alisha achia ngazi kwa kupeleka barua ya kujiuzulu na akawa anamshangaa Kangi kwa ujasiri wa kuhudhuria hafla ile kwani hakutarajia kumkuta pale! Sikumbuki kumsikia akisema amekataa kujiuzulu kwa Masauni
 
Sikuwahi kuiskia hiyo kauli mkuu. Ninachokumbuka siku ile kwenye ile hafla ya polisi pale kurasini Rais alisema Naibu Waziri alisha achia ngazi kwa kupeleka barua ya kujiuzulu na akawa anamshangaa Kangi kwa ujasiri wa kuhudhuria hafla ile kwani hakutarajia kumkuta pale! Sikumbuki kumsikia akisema amekataa kujiuzulu kwa Masauni
Aliyeandika barua ya kujiuzulu alikuwa ni Katibu Mkuu wa Wizara ambaye ni mjeda, na siyo Masauni.
 
Aliyeandika barua ya kujiuzulu alikuwa ni Katibu Mkuu wa Wizara ambaye ni mjeda, na siyo Masauni.
Mkuu kama utakumbuka vizuri Rais alisema KM alimfuata akamueleza uozo unaoendelea pale Wizarani kuhusiana na huo mkataba na hakutaka kua sehemu ya huo uchafu na akaomba kujiuzulu na Rais akasema atamuheshimu sana kwa uamuzi wake huo

Kuhusu Naibu Waziri, Mheshimiwa alisema tu "Ameshaandika barua ya kujiuzulu na hapa hayupo, nashangaa kukuona hapa Waziri!"

Ila nikiri pia sikumbuki kama katika walioitwa kuhojiwa TAKUKURU na NW alikuwepo
 
Back
Top Bottom