Naibu Waziri wa TEHAMA, Kundo Andrea ashauri TCRA kuanzisha mitandao yetu ya kijamii tuachane na Twitter, FB, YouTube n.k

Naibu Waziri wa TEHAMA, Kundo Andrea ashauri TCRA kuanzisha mitandao yetu ya kijamii tuachane na Twitter, FB, YouTube n.k

😁😁😁😁 uchumi wa social media kutoka uchumi wa viwanda.
 
Amenifurahisha sana hapo aliposema Facebook, twitter & YouTube zikiblockiwa hapa Bongo makampuni ya simu yatapata taabu sana.

Kumbe hata serikali kwa namna moja ama nyingine inategemea sana kodi inayopatikana kutokana na hii mitandao ya kijamii ya ubeberuni
 
Serikali inatoa go-ahead watu mnasema bangi sio nzuri.
Sasa aje mtu aongee umbea humu Ooh! I am a programmer, I have no life, mara Ooh Nimesoma IT naomba connection.


Mimi nitakuwa wa kwanza kukomenti kikatili juu ya mtu huyo.

Fanyeni Programming na mtuletee mitandao ya kijamii Kama Jamii Forum na mkapate mkate wenu huko.
 
Yani watu mnafunga ili Maxence wa JF mumpeleke jela, yani hapa kodi mpaka kuongea
 
Tunayo JF, itakayo anzishwa kama japo tu ikiwa na faragha kiwango cha facebook hata shetani atapongeza hatua hiyo kwani media na uhuru w a habari kwetu ni sumu.
 
Hiyo mitandao itakayoanzishwa na wanaccm watatumia wanaccm wenyewe.
 
Hivi hawa watu wana matatizo gani....
Lazima kuna tatizo mahali si bure...

kila siku tunasema wapumbavu ni wengi sana Tz hamwelewi ...yan waanzishe mashindano na magiant kama twita na fecbook ahahaha kazi ipo kwakweli
 
Nimemuelewa injinia. Ni kwamba:-

1. Mitandao ya nje wataishut down.

2. Kutakuwa na server ya aifa ambayo wataweza kui-access.

3. Hakuna kutumia majina yasiyo halisi.

4. Kuna ishu kaongea kuhusu innovation.

Big brother is watching you.
 
we think alike.
So far comments zote zimemponda nashangaa.

Mkuu yupo very wrong mzee hata kama kuna sehemu anapointi, yan its like wanataka waanzishe kitu kama tbc , yan kitu ambayo they will have full control in all the necessary means, sasa what are they trying to achieve?

Nimejaribu kuwaza motive yao nimeona ni vitu vya kipuuz tu, kama kuanzisha you tube channel tu mtu mpaka ulipie hela ivyo vingine itakuwaje ??

Kwanini hawa jamaa wa madarakan wanaogopa sana criticism ?

...Mkuu nakuhakikishia something somewhere is not okay...
 
Huyu waziri ni kama anachofikiri ni hiki tu, kwa mara nyingine amerudia tena maneno haya..yeye sasa ni consultant anaelekeza nini wengine wafanye, sifahamu kwa nini alishindwa kujaribu hayo anayoishauri TCRA wakati hajawa waziri..mara ya kwanza aliposema, nilidhani atajirekebisha baada ya kusoma hapa..
Mwambe mwenyewe ameshindwa hata kujibrush ule mwonekano wake angalau umpe haiba ya Leader, mfano afuge hata mandevu tu, au aache nywele ndefu aka afro...always looks like mwanachuo tena mwaka wa kwanza first degree, uongozi ni haiba pia, ule mwonekano wa nje ndio unajenga kuaminiwa kabla hujasema neno, lakini wakati mwingine tatizo si Mwambe, tatizo ni waliomuona na kumpa hizo nafasi hao ndio tatizo pengine kuliko hata Mwambe, factor wanazotumia kumsaidia mteuzi ni dhaifu sana, kama ufaulu wa chuo ndio kigezo, kwenye zama hizi basi bado tuna safari ndefu sana kupata watu wenye uwezo kutatua changamoto tulizo nazo...ni ajabu Mwambe kupewa uwaziri wa viwanda tena ni first timer bungeni wanaachwa kina Bashe ambao tayari walikuwa wameonyesha uwezo kwny wizara walizokuwa...tuna kasoro kubwa sana kwenye vetting process iliyopo. Inawezekana tanzania tu, mtu anateuliwa siku ya siku anashindwa kusoma kiapo, kapitishwa pitishwa kote huko...mara Uded, mara kagombea ubunge mara ya kwanza kashindwa, mara ya pili kashindwa tena lakini akabebwa, unaona kabisa kuna watu wana bebana bebana tu, juzi naibu waziri wa teknolojia, Kundo wa hii wizara mpya, anahojiwa na media kitu gani kwny teknolojia anadhani kina mchango kwny maendeleo yetu...anasema inabidi tuwe na Instagram kwa lugha yetu, tusitegemee za wenzetu, fikiria huyo ndio waziri anasema hivyo, kwake kitu cha maendeleo kinachotrend akilini mwake ni kuwa na instagram zetu wenyewe hiyo ndio priority kichwani mwake, waziri wake Dr. Ndugulile baada ya kushindwa kwenye wizara ya afya wakati akiwa naibu tena kwenye fani yake, leo unampa wizara mpya ambayo hata si fani yake, unawaacha kina Profesa Mbarawa waliofanya vizuri term iliyopita angalau...ni mengi ya hovyo kabisa kuyasikia, sema tu sisi watz akili yetu ni nyepesi sana siku zote haitaki kuangalia mambo yanayofanyika kwa kina kujua kama yanatufaa au hayatufai...tatizo lipo kwa wanaomsaidia mteuzi, wao kwanza ndio walipaswa kushughulikiwa kabla ya kuwalaumu wanaoteuliwa!
Hivi kila nchi ikianzisha social media zake hali itakuwaje? kwanza ni kwa kiwango kidogo sana sisi tunatumia social media kwa mambo ya maendeleo, mtu anayefahamu vzr IT kwa nchi kama yetu kipaumbele ni ku-leapfrog kwenye IT itusaidie kutatua changamoto nyingi kiuchumi, kijamii..afya, kodi, kilimo, elimu, sanaa nk, yote haya waziri hajui, anachojua ni kuanzisha twitter, whatsap, youtube za kwetu..aanzishe yeye kwanza kama anaona italeta maslahi kwa nchi na kwake.
 
Ndio mapungufu ya mfumo wa elimu ya Tanzania, kukusanya vyeti (vertical knowledge-elimu ya makaratasi) horizontal knowledge zero..hivi kweli mtu mwelewa anaweza amua ku-swim kwenye kina cha maji kimejaa mapapa damu imetapakaa akidhani anaweza kuogelea na kufika anakotaka kwenda? sijui..
 
...mnisaidie 4.10 zile nanilii maana yake nini? walimuacha Mzee Chenge bure tu, km mambo yenyewe ndio nanilii..
 
Kubadilisha vitabu vilivyoandikwa teyari na wazungu ila kazi yao iwe ni kunakili tu kutoka kiingereza kwenda kiswahili mpaka leo wanashindwa. Sasa ili ni nje ya uwezo wetu nafikiri.
 
Naunga mkono hoja!
Najua contractors wa facebook,Twitter, na instagram 'mnafuka moshi' kwenye uzi!
 
Back
Top Bottom