Naishauri serikali Kesho isije Ikatumia mabavu, iache CHADEMA wafanye maandamano yao kwa Amani

Naishauri serikali Kesho isije Ikatumia mabavu, iache CHADEMA wafanye maandamano yao kwa Amani

Kwema Wakuu!

Nimeona nami kwa nafasi yangu hata kama ni ndogo, niishauri serikali kuhusu haya maandamano ya hawa ndugu zetu wa CHADEMA.

Hakuna haja ya kutumia mabavu na ubabe kuzuia CHADEMA kuonyesha hisia za Maumivu ya ndugu zao waliouawa na kutekwa. Ni wanachama wenzao.

Mimi acha nipumzike Sasa. Tutasimama upande wenye HAKI.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam
Naunga mkono hoja,
Hata mimi, kwanza nimeyaunga mkono haya maandamano Kufuatia Umuhimu wa Maandamano ya UKUTA: Nimehamasika, Nitashiriki, Tujitokeze kwa Wingi! Ila...!
na nikalishauri jeshi letu la polisi Jeshi la polisi likifanya vyema, lipongezwe, hongera FFU kusambaratisha maandamano bila virungu, mabomu ya machozi, risasi za moto, bila maafa! na kuwasisitiza polisi wetu Ombi Muhimu Kwa Jeshi Letu Kakamavu na Adilifu la La Polisi."Nyinyi ni Wenzetu, Kwenye Maandamano Yetu, Please Msigeuke. Gestapo au Makaburu!"
P
 
Kikawaida Maandamano ni njia ambayo inatumika baada ya mazungumzo ya kawaida kushindikana.

Samia Must Go ingekuwa wakati wa uchaguzi yaani Mwakani ingekuwa na Mantiki kwa sababu ni wakati sahihi ambapo chama chochote hata CCM yenyewe inaweza kuitumia hiyo Kauli mbiu ya Samia Must Goo kama hawajamkubali Mwenyekiti wao. Lakini kwa Sasa Kauli hiyo sio sahihi kabisa.

Ni kutaka kuiangusha serikali ya Samia ambayo tunajua kuwa mpaka dakika hii ni serikali Halali hata kama ingekuwa inafanya mambo haramu

..wakati wote vyama vinawaza kubaki madarakani, na vingine vinawaza kuingia madarakani.

..hivi tunavyozungumza kuna watu wanawa " Samia must stay" , na wengine wanawaza " Samia must go. "

..sasa unaweza kuwazuia watu wasiseme, Je utawazuia kuwaza " Samia must go. "

..Mimi nadhani sio busara hivi tunavyokwenda kupangiana hata nini cha kusema.

..Zaidi nadhani wananchi wakiwa HURU kuzungumza ndivyo ambavyo serikali utajua kama inafanya vizuri, au vibaya.
 
..wakati wote vyama vinawaza kubaki madarakani, na vingine vinawaza kuingia madarakani.

..hivi tunavyozungumza kuna watu wanawa " Samia must stay" , na wengine wanawaza " Samia must go. "

..sasa unaweza kuwazuia watu wasiseme, Je utawazuia kuwaza " Samia must go. "

..Mimi nadhani sio busara hivi tunavyokwenda kupangiana hata nini cha kusema.

..Zaidi nadhani wananchi wakiwa HURU kuzungumza ndivyo ambavyo serikali utajua kama inafanya vizuri, au vibaya.

Kuzungumza sio tatizo wala sio kosa.
Lakini kuandamana na kusema Samia Must Goo kidogo haijakaa sawa.
 
Mkuu serikali ya CCM kikawaida ni serikali ya vitisho. Ajabu ni kuwa Watanzania wengi ndio wanapenda serikali za namna hiyo.

Ushahidi wa hili tuliona kwenye serikali ya Magufuli, Moja ya mambo yaliyofanya Jpm apendwe ni aina ya siasa zake za vitisho mbali na uchapakazi wake.

Watanzania wengi ni watu wa aina ya ajabu sana. Usipotumia vitisho wao huamini kuwa huwezi kuongoza.

Embu Muangalie Makonda, siasa za Makonda zinapendwa na Watanzania wengi ukichunguza kwa undani utagundua sababu ni kufanya siasa za vitisho na Ubabe.

Watanzania wengi ni kama wanyama yaani hawana utashi wenye afya. Sio ajabu hupenda Kuona siasa za vitisho au pengine ni athari za kisaikolojia walizozipata.

Juzi tuu hapa Rais Samia alitoa hotuba ambayo kwa sisi wengine tuliona ametoa Boko kwa sababu hotuba Ile iliandikwa na kusomwa kwa hisia Kali huku akili iliyotulia ikitumika kidogo.
Lakini Mimi nilifuatilia mitandaoni nikaona Watanzania wakijaribu kumpongeza Ati kuwa ameanza kuwa kama JPM. Na wakaonyesha tumaini la kumkubali
Imenibidi nicheke tu baada ya kusoma andiko lako hili.
Sina shaka yoyote huko ndiko unakolalia mwenyewe na kufanya iwe hivyo kwa wingi wa waTanzania.
Wahenga husema," tunda halidondoki mbali na mti ulio lizaa"; sasa sijui kama utauelewa vizuri msemo huu.

Ngoja na mimi nikupe ninapo simamia katika hali hiyo uliyo ielezea wewe mara kwa mara kuhusiana na tabia za waTanzania na viongozi wa aina ya Magufuli.

Siamini hata mara moja kwamba waTanzania walipenda mambo machafu aliyokuwa akifanya Magufuli; lakini naamini walipenda baadhi ya misimamo aliyo kuwa nayo juu ya nchi hii, Tanzania. Ni muhimu kutofautisha hayo mawili.

Ndiyo, hata mimi namtaka sana kiongozi asiyefanya masihala na mambo muhimu ya nchi. Kama watu maofisini ni kufanya kazi na kulipwa haki ya kazi zao, kuna kipi hapo cha kuchekeana na kubembelezana. Ndiyo, kama kiongozi hana uvumilivu na ufujaji wa mali za umma, kwa nini nisimuunge mkono mtu huyo kama anayo yafanya yamo ndani za taratibu zinazofahamika (kisheria). Ndiyo, kwa nini nisimkubali kiongozi ambaye maamuzi yake yanaonekana ni kwa manufaa ya nchi na wananchi wake; na bila kuonyesha kuwa anajitafutia sifa zisizokuwa na msingi wowote?

Nisichotaka kwa kiongozi ni uigizaji, kama huo wa Samia, Makonda, na hata Magufuli katika baadhi ya mambo.. Nataka kiongozi mkweli, anaye tumia akili, za kuchambua anayo shauriwa na wengine. Sitaki kiongozi mpenda sifa kama Magufuli. Sitaki kiongozi mwonevu kwa wengine kwa sababu tu hawakubaliani na baadhi ya mambo yake. Sitaki kiongozi anayetumia madaraka yake vibaya na kujichukulia sheria mkononi kwa sababu tu anayo madaraka na vyombo vya dola

Sasa basi, tuache kuwasingizia waTanzania kuwa na sifa hizo unazo zielezea wewe za kupenda tu kiongozi yeyote mradi anafoka na kukandamiza watu. Hili silikubali hata mara moja.

Kuna sababu muhimu sana kwa nini unafikiri waTanzania wanashindwa kuachana na CCM, pamoja na ubovu ilioufikia nyakati hizi; na kwa nini inakuwa vigumu kwao kukubali vyama vingine kama CHADEMA. Mchambuzi mzuri wa maswala haya anatakiwa aainishe kwa nini hali iko hivyo, siyo kukimbilia tu kuwalaumu waTanzania kirahisi rahisi.
Hata hivyo, ni wazi sasa CCM yenyewe Samia kaimaliza, kama hapatatokea watu makini wa kuirudishia uimara wake iliowahi kuwa nao.
CHADEMA wamejiweka katika nafasi nzuri ya kuanza kuwavuta waTanzania kama mbadala iwapo kama wataachana na baadhi ya mambo yaliyokuwa yakiwadidimiza siku za nyuma.

Sijui kama nitakuwa na muda tena wa kuendeleza majadiliano haya katika hali hii ya sasa.
 
Kwema Wakuu!

Nimeona nami kwa nafasi yangu hata kama ni ndogo, niishauri serikali kuhusu haya maandamano ya hawa ndugu zetu wa CHADEMA.

Hakuna haja ya kutumia mabavu na ubabe kuzuia CHADEMA kuonyesha hisia za Maumivu ya ndugu zao waliouawa na kutekwa. Ni wanachama wenzao.

Haitakuwa HAKI.
Nilikuwa najaribu kujishawishi kuwa Wanachadema wasifanye maandamano na niwe upande wa serikali lakini nimeona Sina hoja ya kupinga maandamano hayo.

Ikiwa lengo kweli ni kuomboleza, kukemea na kuitaka serikali ichukue hatua kwa HAKI za wanachama wao na Watanzania wengine waliotekwa na kuuawa na kutojulikana walipo, sioni tatizo la maandamano.

Mimi napinga Kauli ya "Samia Must Goo" kwani hiyo ni nje ya utaratibu wa sheria zetu. Hiyo wasubiri Mwakani 2025.

Wanahaki kwa sababu:

1. Waliotekwa na kuuawa ni wanachama wenzao. Kutochukua hatua zozote itaashiria kuwa chama chao hakiwezi kupigania Haki za Wanachama wenzao.

Hata hivyo ilitakiwa maandamano haya yafanywe na wananchi wote wa Tanzania.
Lakini kwa vile sisi sio kitu kimoja hiyo haitawezekana.

2. Wanahaki kwa Sababu wenye wajibu ambao ni serikali imeshindwa kufanya sehemu yake kutafuta wanaofanya hayo matukio u mauaji na UTEKAJI.

Hii inawafanya wao wenyewe kutetea haki za wanachama wenzao. Hii itamaanisha kuwa kuwa mwananchi wa chama cha Demokrasia Hauna Haki na hata ukiuawa hautakuwa n tofauti na sungura au panya Buku. Tena Bora sungura huko TANAPA wanalinda wanyamapori.

NINI KINAJENGEKa IKIWA SERIKALI HAITACHUKUA HATUA STAHIKI NA IKITUMIA MABAVU;

1. Chuki na Visasi vitajengeka.
Chuki baina ya wanachama wa CHADEMA na serikali(CCM) itazidi kukua.

Mtu anaweza kusamehe Makosa mengi lakini kosa la kumuua mzazi wake au Mtoto wake ni kosa ambalo kikawaida halitakiwi kusamehewa. Ni kosa la kulipa Kisasi. Na ni HAKI Kisasi kilipwe ikiwa Haki ya kawaida haikutendeka.

Inaweza kuwa, kwa vile wanaotendewa hayo wakadharauliwa kwa sababu ni Wachache na hawana nguvu lakini mambo ya Haki hayaendagi hivyo. Tusifanye watu waichukie nchi yao na wananchi wao.

Kwa sababu kama wananchi watakaa kimya wakati watu wenzao wanauawa itahesabika kuwa waliungana na WAUAJI kufanya uhalifu huo.

Hiyo ni sababu ya matendo mabaya ya kigaidi yanayoendelea Duniani. Ni hatari sana.

2. Nchi kupasuka na kukosa utulivu.

Matendo haya kikawaida hayawezi kufurahisha viongozi wote waliopo kwenye vyombo vya Dola.
Wapo viongozi ambao huweza kuingia na moyo wa Imani na Kuona kinachoendelea sio chema. Hii hupelekea Dola kupasuka na nchi kukosa utulivu.

Tunaona nchi kama Libya kwa Hayyati Gadafi, Iraq kwa Sadamu Hussein. Yanapotokea matukio ya ukandamizaji wa kundi Fulani ni rahisi kwa adui kuivuruga nchi.

Kwa sisi watibeli tunajua, matokeo ya uovu.

Yuda alipomsaliti Yesu akamuuza kwa vipande vya fedha baadaye aligundua kuwa Ile fedha Haina maana yoyote, matokeo yake akaona airudishe kisha akaenda kujiua sababu ya Hatia.

Hatia ndio huifarakanishaga watawala. Linazuka tuu kundi linaona yanayoendelea sio sawa na jingine linaona sawa alafu Kuna kuwa na uwiano wa kinguvu. Mwishowe nchi inapasuka au kuchafuka.

3. Wasio na vyama ambao ni sisi nasi tutachoka Kuona kundi Fulani likiumizwa.

Watanzania wengi hawana vyama lakini hiyo haimaanishi hawafuatilii siasa. Hatutaki chama au kundi Fulani lionewe. Makundi na vyama vyote vipewe HAKI sawa.
Hatutaki Dini Fulani ionewe au ipendelewe tunataka Dini zote na wasio na Dini wapewe HAKI sawa.

Sisi tusio na upande ambao ndio wengi tunataka mfanye mambo yenu bila kuoneana na kufanyiana dhulma.

Hatutaki nchi yetu ichafuke. Hatutaki nchi yetu ipasuke vipande vipande au kugawanyika kama Sudan kaskazini na Sudani Kusini.

Tunataka nchi Moja. Na nchi Moja ni Ile ambayo Kuna usawa na Haki baina ya watu na makundi yao. Hakuna chama chenye mamlaka au Haki zaidi ya vyama vingine.

Kukosekana umoja na kundi linalotaka kujipendelea na kukandamiza makundi mengine ndilo litahesabika kama linaloivuruga Amani ya nchi hii. Kila kundi linalohaki ya kujilinda na kutetea HAKI zake ikiwa litaona kuwa linaonewana kudhulimiwa.

Serikali, mambo haya hayahitaji nguvu na mabavu. Hatutaki Kuona watu wanapigana na kumwagana Damu na ubongo bila sababu ya msingi.

Akili kazi yake ni kutafuta suluhu kwa njia isiyoumiza. Akili hizo ninaamini viongozi mnazo sema mnataka kufanya Makosa ya kiufundi kwa kutumia nguvu zisizohitajika.

Wewe kiongozi utakayezuia maandamano kabla hujafanya hivyo lazima ujiulize;

Wewe Baba yako au Mtoto wako ndio angekuwa ameuawa au kutekwa na hajulikani alipo usingeandamana?
Yaani assume hao watoto wako ambao wako salama au huyo Babaako unayempenda aliyesalama angetokea mtu akamuua kwa kifo cha kikatili au akatekwa usingeandamana?

Au fikiria wewe ndio umeuawa, au umetekwa uko matekani kwa watesi wako. Alafu ukasikia watoto na watu wanaandamana kwaajili yako ungejisikiaje? Ungewachukuliaje Wananchi wenzako?
Ungeionaje nchi yako?

Hata kama ungekufa au usiporudi ungefarijika na ungekufa kwa amani kwa kuhisi kuwa watu wa nchi yako walikuwa wanakupenda, taifa lako lilikuwa linakupenda.

Tunahitaji haya mambo kuyaweka Sawa kabla maji hayajazidi UNGA.

Tunaushahidi wa kutosha kuwa ubabe haujawahi kuwa suluhu linapokuja swala la mambo ya uhai. Tunaona huko Gaza.

Chondechonde SERIKALI na vyombo vya Dola. Shughulikieni hilo jambo kwa akili, UPendo, na HAKI.

Soma Pia:

Mambo ya kusema sijui ubabe sijui nani mkubwa hiyo haitasaidia nchi yetu. Zaidi sana tutawapa adui zetu nafasi. Adui tunaowajua na wale tusiowajua.

Mimi acha nipumzike Sasa. Tutasimama upande wenye HAKI.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam
Jf Waendelee kukupa tuzo ya ujinga tuu 😂😂😂😂

Vibaraka Wameshughulikiwa ipasavyo

View: https://x.com/Kipanga1986/status/1838195046467645818?t=MAu17qF7lsVEEn9Iw90tcQ&s=19
 
  • Nzuri
Reactions: Tui
Ushauri wako umepuuzwa na utawala wa kidikteta
 
Kwema Wakuu!

Nimeona nami kwa nafasi yangu hata kama ni ndogo, niishauri serikali kuhusu haya maandamano ya hawa ndugu zetu wa CHADEMA.

Hakuna haja ya kutumia mabavu na ubabe kuzuia CHADEMA kuonyesha hisia za Maumivu ya ndugu zao waliouawa na kutekwa. Ni wanachama wenzao.

Haitakuwa HAKI.
Nilikuwa najaribu kujishawishi kuwa Wanachadema wasifanye maandamano na niwe upande wa serikali lakini nimeona Sina hoja ya kupinga maandamano hayo.

Ikiwa lengo kweli ni kuomboleza, kukemea na kuitaka serikali ichukue hatua kwa HAKI za wanachama wao na Watanzania wengine waliotekwa na kuuawa na kutojulikana walipo, sioni tatizo la maandamano.

Mimi napinga Kauli ya "Samia Must Goo" kwani hiyo ni nje ya utaratibu wa sheria zetu. Hiyo wasubiri Mwakani 2025.

Wanahaki kwa sababu:

1. Waliotekwa na kuuawa ni wanachama wenzao. Kutochukua hatua zozote itaashiria kuwa chama chao hakiwezi kupigania Haki za Wanachama wenzao.

Hata hivyo ilitakiwa maandamano haya yafanywe na wananchi wote wa Tanzania.
Lakini kwa vile sisi sio kitu kimoja hiyo haitawezekana.

2. Wanahaki kwa Sababu wenye wajibu ambao ni serikali imeshindwa kufanya sehemu yake kutafuta wanaofanya hayo matukio u mauaji na UTEKAJI.

Hii inawafanya wao wenyewe kutetea haki za wanachama wenzao. Hii itamaanisha kuwa kuwa mwananchi wa chama cha Demokrasia Hauna Haki na hata ukiuawa hautakuwa n tofauti na sungura au panya Buku. Tena Bora sungura huko TANAPA wanalinda wanyamapori.

NINI KINAJENGEKa IKIWA SERIKALI HAITACHUKUA HATUA STAHIKI NA IKITUMIA MABAVU;

1. Chuki na Visasi vitajengeka.
Chuki baina ya wanachama wa CHADEMA na serikali(CCM) itazidi kukua.

Mtu anaweza kusamehe Makosa mengi lakini kosa la kumuua mzazi wake au Mtoto wake ni kosa ambalo kikawaida halitakiwi kusamehewa. Ni kosa la kulipa Kisasi. Na ni HAKI Kisasi kilipwe ikiwa Haki ya kawaida haikutendeka.

Inaweza kuwa, kwa vile wanaotendewa hayo wakadharauliwa kwa sababu ni Wachache na hawana nguvu lakini mambo ya Haki hayaendagi hivyo. Tusifanye watu waichukie nchi yao na wananchi wao.

Kwa sababu kama wananchi watakaa kimya wakati watu wenzao wanauawa itahesabika kuwa waliungana na WAUAJI kufanya uhalifu huo.

Hiyo ni sababu ya matendo mabaya ya kigaidi yanayoendelea Duniani. Ni hatari sana.

2. Nchi kupasuka na kukosa utulivu.

Matendo haya kikawaida hayawezi kufurahisha viongozi wote waliopo kwenye vyombo vya Dola.
Wapo viongozi ambao huweza kuingia na moyo wa Imani na Kuona kinachoendelea sio chema. Hii hupelekea Dola kupasuka na nchi kukosa utulivu.

Tunaona nchi kama Libya kwa Hayyati Gadafi, Iraq kwa Sadamu Hussein. Yanapotokea matukio ya ukandamizaji wa kundi Fulani ni rahisi kwa adui kuivuruga nchi.

Kwa sisi watibeli tunajua, matokeo ya uovu.

Yuda alipomsaliti Yesu akamuuza kwa vipande vya fedha baadaye aligundua kuwa Ile fedha Haina maana yoyote, matokeo yake akaona airudishe kisha akaenda kujiua sababu ya Hatia.

Hatia ndio huifarakanishaga watawala. Linazuka tuu kundi linaona yanayoendelea sio sawa na jingine linaona sawa alafu Kuna kuwa na uwiano wa kinguvu. Mwishowe nchi inapasuka au kuchafuka.

3. Wasio na vyama ambao ni sisi nasi tutachoka Kuona kundi Fulani likiumizwa.

Watanzania wengi hawana vyama lakini hiyo haimaanishi hawafuatilii siasa. Hatutaki chama au kundi Fulani lionewe. Makundi na vyama vyote vipewe HAKI sawa.
Hatutaki Dini Fulani ionewe au ipendelewe tunataka Dini zote na wasio na Dini wapewe HAKI sawa.

Sisi tusio na upande ambao ndio wengi tunataka mfanye mambo yenu bila kuoneana na kufanyiana dhulma.

Hatutaki nchi yetu ichafuke. Hatutaki nchi yetu ipasuke vipande vipande au kugawanyika kama Sudan kaskazini na Sudani Kusini.

Tunataka nchi Moja. Na nchi Moja ni Ile ambayo Kuna usawa na Haki baina ya watu na makundi yao. Hakuna chama chenye mamlaka au Haki zaidi ya vyama vingine.

Kukosekana umoja na kundi linalotaka kujipendelea na kukandamiza makundi mengine ndilo litahesabika kama linaloivuruga Amani ya nchi hii. Kila kundi linalohaki ya kujilinda na kutetea HAKI zake ikiwa litaona kuwa linaonewana kudhulimiwa.

Serikali, mambo haya hayahitaji nguvu na mabavu. Hatutaki Kuona watu wanapigana na kumwagana Damu na ubongo bila sababu ya msingi.

Akili kazi yake ni kutafuta suluhu kwa njia isiyoumiza. Akili hizo ninaamini viongozi mnazo sema mnataka kufanya Makosa ya kiufundi kwa kutumia nguvu zisizohitajika.

Wewe kiongozi utakayezuia maandamano kabla hujafanya hivyo lazima ujiulize;

Wewe Baba yako au Mtoto wako ndio angekuwa ameuawa au kutekwa na hajulikani alipo usingeandamana?
Yaani assume hao watoto wako ambao wako salama au huyo Babaako unayempenda aliyesalama angetokea mtu akamuua kwa kifo cha kikatili au akatekwa usingeandamana?

Au fikiria wewe ndio umeuawa, au umetekwa uko matekani kwa watesi wako. Alafu ukasikia watoto na watu wanaandamana kwaajili yako ungejisikiaje? Ungewachukuliaje Wananchi wenzako?
Ungeionaje nchi yako?

Hata kama ungekufa au usiporudi ungefarijika na ungekufa kwa amani kwa kuhisi kuwa watu wa nchi yako walikuwa wanakupenda, taifa lako lilikuwa linakupenda.

Tunahitaji haya mambo kuyaweka Sawa kabla maji hayajazidi UNGA.

Tunaushahidi wa kutosha kuwa ubabe haujawahi kuwa suluhu linapokuja swala la mambo ya uhai. Tunaona huko Gaza.

Chondechonde SERIKALI na vyombo vya Dola. Shughulikieni hilo jambo kwa akili, UPendo, na HAKI.

Soma Pia:

Mambo ya kusema sijui ubabe sijui nani mkubwa hiyo haitasaidia nchi yetu. Zaidi sana tutawapa adui zetu nafasi. Adui tunaowajua na wale tusiowajua.

Mimi acha nipumzike Sasa. Tutasimama upande wenye HAKI.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam

"Njia pekee ambayo Wananchi wataitumia katika kuzungumza au kujadiliana na Watawala wao ambao ni madikteta ili kufikia muafaka wenye maslahi kwa pande zote mbili ni kwa kupitia mtutu wa bunduki."

Jeff's O'Brien.
 
Ndio maana nikaandika watumie AKILI
Kujua na Kuona na kutofautisha nyakati ni sehemu ya AKILI.
Zamani watu walikuwa wanaogopa Polisi siku hizi hawaogopi.

Ninachoandika ni kuweka mambo sawa ili yasiharibike sana
Aya yako ya pili inasemaje,?Wangeandamana waone kama wanatania.Ulete uchochezi wa kuchochea vurugu uachwe.Rwanda walianza hivi hivi kuwakejeli wengine kwa lugha za kichochezi na tunajua kilichotokea.Hakuna kucheka na mchochezi.
 
Aya yako ya pili inasemaje,?Wangeandamana waone kama wanatania.Ulete uchochezi wa kuchochea vurugu uachwe.Rwanda walianza hivi hivi kuwakejeli wengine kwa lugha za kichochezi na tunajua kilichotokea.Hakuna kucheka na mchochezi.

Mambo yameisha kwa utulivu.

Serikali ifuatilie hoja za wananchi wake(hao Wanachadema)
 
Kuzungumza sio tatizo wala sio kosa.
Lakini kuandamana na kusema Samia Must Goo kidogo haijakaa sawa.

..watu wanapoandamana mara nyingi huwa wana jambo lililowakera. Katika mazingira hayo lazima kutakuwepo na kauli zinazo akisi machungu ya waandamanaji.

..Na maandamano ya Chadema chanzo chake ni watu wao kutekwa, kuteswa, na kuuwawa, na watu wanaodhaniwa ni askari Polisi. Sijui kwanini tunashangaa kusikia kauli za kuwalaani Polisi, au Raisi, ambaye ni kiongozi Mkuu wa vyombo vya dola.

..Resilience ktk 4R ni pamoja na kuwavumilia wale wasioridhishwa na utendaji wa Rais Samia wanapoeleza hisia zao. Wanaosema Samia must go wana haki zilezile na sawa na wanaosema Mama anaupiga mwingi, Nani kama Mama,...
 
Back
Top Bottom