Naitwa Analyse, na hii ndio safari yangu ya maisha...

Naitwa Analyse, na hii ndio safari yangu ya maisha...

Jf nimejiunga siku nyingi,nashangaa hz story zilinipita,ila nakumbuka 2019 nilkuwa kwenye msoto wa shule ya afya na jf nilkuwa naingia mara moja moja sana,visa vyako ni vikali sana,ile thread ya mwanamke uliezaa nae ndo imenileta mpaka huku
 
Aisee dingi alikuwa na akili sana,ila ana mambo ya kikauzu sana ila kuna muda yanachekesha
 
Jf nimejiunga siku nyingi,nashangaa hz story zilinipita,ila nakumbuka 2019 nilkuwa kwenye msoto wa shule ya afya na jf nilkuwa naingia mara moja moja sana,visa vyako ni vikali sana,ile thread ya mwanamke uliezaa nae ndo imenileta mpaka huku
[emoji28][emoji28][emoji28] msoto ndio ulisababisha usione Uzi mkuu
 
Aisee dingi alikuwa na akili sana,ila ana mambo ya kikauzu sana ila kuna muda yanachekesha
Mzee jembe sana yule. Namtakia maisha marefu yenye amani siku zote [emoji120][emoji120]
 
SEHEMU YA 2:

Inaendelea.....


...Mwenyeji wangu hakupatikana hadi kunakucha. Usiku huo ilibidi nijilaze mle mle stand ya mkoa. Na hata asubuhi nilipomtafuta, alipongundua ni mimi, mtandao ukaanza kuzingua. Mara hanisikii vizuri. Simu hakupokea tena, na mimi nikaamua kuachana nae.

Nilitoka nje ya stand,nikawa natembea tembea tu bila kujua naenda wapi. Mida ya mchana nikajakustukia nipo eneo linaitwa Tabata. Njaa kali, sina hela. Kiufupi sina kitu chochote cha thamani. Nikaingia kwa mama ntilie, nikamlilia shida nione kama atanisaidia, akagoma. Nikamwambia hata nifanye kazi yoyote nipate hata ukoko. Akanijibu, kazi zipo, ila msosi wote una order yani hadi huo ukoko. Nikaishia kunywa maji kisha nikaondoka.

Usiku ukapita bila kula chochote zaidi ya maji. Kesho yake ikakata tena bila chochote. Kwanza sina sehemu maalumu, natembea tu bila kujua naenda wapi, cha msingi naenda mbele. Ilipofika siku ya pili usiku, nikaona kabisa hapa nakufa. Maana mwili haukuwa na nguvu hata kidogo, ukiomba msaada unaishia kupewa maji, tena na yenyewe ni baada ya kuulizwa maswali kibao.

Sijui akili au ujasiri ulitoka wapi, ila nakumbuka kuna sehem inaitwa Vingunguti, njiani niliokota kava la simu jeusi. Baada ya kuwa na lile kava, nikatafuta kiroba cha unga kilocho tupu, ndani nikakiweka mawe kadhaa na mabox, alaf nikaingia kwa mama ntilie. Nikauliza chai ipo? Akasema ipo, chapati nazo zipo? Akajibu zipo. Huku natetemeka na moyo unadunda kuliko maelezo, nikamwambia " Naomba chai ya maziwa na chapati 5"

Zikaletwa, nikazipiga, nikaongeza na chai. Chapati zilipoisha na chai ipo nusu. Nikatoa kava la simu na kujifanya naongea na simu huku nasogea nje ya kibanda, hapo ule mzigo wangu nimeuacha pale ndani. Nikasimama mlangoni huku naongea "Me nishafika, na mzigo ninao hapa, njoo na usafiri unichukue maana nataka kuondoka"... Nilipoona yule mama ntilie hanifatilii, nikazidi kusogea mbele, nilivyokata kona tu, nilitoka mbio sio za nchi hii. Sijui kule ilikuwaje,na sikuwahi kurudi tena.

Kulipokucha nikaendelea kutafuta kibarua. Nikafanikiwa kupata kwa wale wafyatua tofali kwa mashine. Zikifyatuliwa tu,unabeba fasta na kwenda kupanga sehemu. Speed,uzito wa tofali,inama inuka jumlisha kuwa sijapata msosi wa uhakika kwa siku kadhaa...nilipatwa na kizunguzungu nikaanguka na tofali la watu. Bosi aliwaka kichizi. Akasema nimlipe. Sina hela,ikabidi nimwambie kwa uungwana akate hela yake ktk posho yangu alaf anipe iliyobaki ambayo nastahili kupata kwa kazi ambayo nishafanya. Boss akasema makubaliano ni ufanye kazi siku nzima,kwa muda huu mchache uliofanya sina cha kukulipa,kwanza ushanitia hasara,SEPA.


Ikabidi niondoke.

•••••••••• ••••••••••••• •••••••••••••• •••••••••••••••••

Mungu si Athumani, katika kuendelea kujielezea kwa watu niliokuwa nakutana nao nilibahatika kupata kazi ya kusimamia ng'ombe wa mzee mmoja maeneo ya tabata. Dar majani hakuna, unayatafuta kwa tabu sana, alafu mzee akawa anasumbua malipo. Sema hakuna jinsi, si nilikimbia kusoma Vishazi?.

Nakumbuka siku moja katika pita pita natafuta sehemu ya kukata nyasi, nikakuta Don mmoja bomba la maji limepasuka nje ya fensi yake, na maji yanavuja sana. Akaniita na kuniuliza kama namfahamu fundi bomba yoyote maeneo yale.. Bila kuvunga ikabidi nijifanye fundi bomba. Yule Don akaniambia sasa hapa inabidi uwe na konekta , tunazipataje? Nikaropoka "itabidi tununue, moja inauzwa 7000" ila kiukweli hata sikuelewa hizo konekta ndio nini na bei sijui. Jamaa akasema mbona unataja bei kubwa hivyo? Ngoja nikuelekeze sehemu wanapouza kwa 6000. Akanielekeza kisha akanipatia hela. Ila kabla sijaondoka akaniuliza ninapokaa. Nikamuelekeza akapajua.

Baada ya kununua zile konekta, nikarudi, nikachimba sehemu iliyopasuka. Ili niweze kupaunga, ikabidi nikate bomba. Presha na wingi wa maji vikanizidia, nikaanza kutetemeka pale. Kila nikitaka kuziba, maji hayo. Yule Don ikabidi aniulize "Hivi ww ni fundi kweli?.. Na jibu nini kwa mfano? Bahati nzuri simu yake ikaita, aliongea kidogo alaf akaondoka eneo lile. Hapo na mm akili ikarudi, maana kusimamiwa kulinitoa mchezoni. Nikapata wazo la kutumia moto kutanua bomba, alaf nikayazungushia na mifuko ya nailoni, mwisho nikabana na mpira . Maji yakaacha kutoka,zile konekta nikaweka mfukoni maana sikuzitumia. Nikafukia, nikamuita yule Don, akapaangalia na kuridhishwa ila akasema hela nifate kesho ili aangalie kama kweli zoezi limefanikiwa kwa 100%.

Kesho yake mapema sana, yule Don akaja home pale kumuulizia fundi bomba (mimi). Inaonekana usiku presha ya maji ilizidi pakafumuka. Sasa yule mzee ninayekaa nae anashangaa mimi kuitwa fundi bomba. Ikabidi amwambie ukweli yule Don kuwa mimi sio fundi. Hapo nishasemwa sana. Ikabidi aitwr fundi kweli, nikawarudishia konekta zao. Sema yule Don akaniambia ukiwa na shida unasema, sio unajitwika majukumu sio yako utakuja kupata matatizo mjini hapa, akanipa elfu 5 nikasepa..

Nikaendelea na kazi ya kulisha mifugo kwa yule mzee. Ila mkewe alikuwa na nongwa sana. Ukiacha kazi za mifugo,alikuwa ananipa kazi ya kufulia nguo wanae, kudeki, kumwagilia bustani, kusafisha mtaro uliokuwa nje ya nyumba. Pia kuna siku akataka nimfulie nguo zake yeye sidiria, nguo za kulalia na tight. Niligoma kufua, akaongea sana. Na kumbuka akatoka kwa hasira. Sijui alisahau nini ndani , akarudi na kunikuta napiga deki, nilipomuona na mm ndio nikamwaga sabuni ya unga na maji kwenye zile malumalu. Kaja na hasira, alipiga mwereka sio wa nchi hii,alijibamiza chini hadi nikamuonea huruma. Usiku wa siku hiyo ndio ilikuwa siku ya mwisho mimi kufanya kazi na kulala kwenye nyumba hiyo...
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Tuendelee sasa..


.....Maana yule Mzee aliporudi, kabla hata sijamsalimia aliniuliza namdai kiasi gani? Tukapigiana hesabu akanipa changu alaf akaniambia "Fanya haraka utoke nataka kufunga geti tulale"

Sikujifikiria sana, kama niliweza kuondoka kwetu sembuse hapa? Nikabeba vyangu nikatoka. Hapo ilikuwa majira kama ya saa tatu usiku. Nikajichanganya mtaani. Niwe muwazi, pamoja na kukaa sana Dar ila watu wake sijawahi kuwaelewa. Kila mtu ni mjanja mjanja na anajua kila kitu,hakuna siku niliyotoka nje usiku nikakuta watu wamelala,mda wote wanapirika pirika tu. Pia hata mtu usiyemdhania anaweza akakuibia au kukudhurumu. Nasema hivi kwasababu ya kilichonikuta nilivyorudi mtaani. Nilikuwa natembea mdogo mdogo lengo ikiwa nielekee sehemu inaitwa Kariakoo maana niliambiwa huko kuna kila kitu japo sikuwahi fika. Kutokana na kubana bajeti sikutaka kupanda gari maana hela yenyewe ya ngama.

Kuna sehemu kule Dar panaitwa kwa Mnyamani. Maeneo yale nilikutana na watu kama wa 5 wakiwa wameshika fimbo, wanajiita sungusungu. Walinisimamisha na kuanza kunihoji, muda ule. Nikajaribu kutoa maelezo yangu, ila hawakutaka kunielewa. Watu wa Dar wanaongea haraka haraka sana hadi wakaanza kunichanganya. Naongea neno moja, wao washao gea 10.

Sijawahi kuona sungusungu anamsachi mtu, wala kumpiga mtu. Wakachukua hela zangu, bahati nzuri sikuziweka zote pamoja, nikabaki na kiasi kidogo. Waliponiacha, nikatembea hadi sokoni buguruni, nilipoona watu wengi wengi, nikaweka kambi pale kwa mzee aliyekuwa anauza kahawa. Kulipokucha nikapata kibarua cha kushusha matikiti. Hapo kidogo nikapata vijihela. Sikwenda tena kariakoo, nikaweka kambi hapo. Mida ya mchana, kazi hakuna ikabidi nitulie kwenye kijimgahawa cha mama mmoja hivi huku nakunywa soda maana hawaruhusu kukaa bure. Wakati nainywa soda yangu taratibu ili isiishe, kwenye tv kulikuwa na kipindi cha maswala ya shule (nishakisahau jina) ila channel ni Star Tv. Yani kile kipindi cha siku hiyo kama kilinilenga mimi, maana somo lilikuwa Kiswahili, maswala ya sentensi sentensi. Yule ticha alikuwa anafundisha maswala ya kutunga sentensi za "...nge..." Mara nikamsikia ametoa mfano "Ningejua, nisingeondoka" . Ile sentensi ikanishtua sana. Nikamwambia yule mama mwenye mgahawa abadili channel "Maliza soda uende" ilo ndio jibu alilonipa

Kimoyo moyo nikafikiria " Ningeenda kidato cha tano, nisingekuwa hapa" Nikajikuta napakumbuka nyumbani kwa wazee. Ikanipelekea kulikumbuka tukio moja ambalo lilitaka kuwagombanisha mama na baba. Ilikuwa ni kama wiki mmoja baada ya kudondosha kibox cha kondom darasani, kwavile nilipewa suspension ya wiki 3. Nilivyorudi nyumbani mzee alisema kwa wiki 3 zote itakuwa zamu yako kuchunga mbuzi.

Sasa siku hiyo tuko machungoni na na watoto wengine, tukaokota kiberiti cha gesi. Kule machungoni tukawa tunawasha majani alafu tunazima kwa kukanyaga. Sasa kuna muda tukawasha, ile tunazima, kukanyaga jani likapeperushwa na upepo, moto ukawaka na kwingine. Kila tukijitahidi kuzima, moto unapepea. Moto ukatanda kote, mbuzi zikaanza kukimbia ovyo. Kuona vile na sisi tukakimbia kuzifata mbuzi huku tunarudi nyumbani. Wanakijiji wakaitana, wakaushambulia moto na kufanikiwa kuuzima japo ulishaunguza eneo kubwa kiasi. Mzee mzima nikarudi nyumbani, moja kwa moja chumbani nikazuga kulala. Kumbe wakati tunakimbia na mbuzi kuna bibi mmoja alikuwa anaokota kuni alituona. Kwenye mkutano wa kijiji akatutaja tuliosababisha moto. Siku hiyo mzee alinipiga fimbo sio za nchi hii. Baadae namsikia anamuuliza mama " Hivi mama nanii, huyu ni mwanangu kweli??" Bi mkubwa nae akawaka "Nitolee wehu wako hapa, angalia lipua la mwanao alaf nenda kajiangalie kwenye kioo kama hujawahi kujiangalia" faza akawa mpole, maana kama ni pua tu, kweli tunazo.

Pia wakati nasubiria majibu ya kidato cha nne, kuna demu nilikuwaga nae ila akaja kunipiga chini baada ya kumpata mwenye hela. Miezi kadhaa akadaka mimba, ila yule jamaa akaikana. Kijiji chote kilikuwa kinanionaga na yule dem, habari zikasambaa mimba yangu. Demu nae akashikiria pale pale kuwa mimba yangu. Nilijitahidi sana kukataa , ila watu akiwemo faza hawakunielewa. Japo baadae sana ilikuja kugundulika kuwa mimba haikuwa yangu.

Hayo matukio yote nilikuwa nayakumbuka wakati nipo kwenye ule mgahawa pale buguruni. Nikamalizia soda nikatoka.

** ** ***** ***** *****

Nilikomaa sana pale buguruni kwa muda mrefu, nafanya kazi pale na kujiegesha mule mule. Nakumbuka siku moja nilikuwa nimekaa na wabeba mizigo wenzangu tunapiga story. Akatokea jamaa akawa anatupa story za migodini, kuwa unafanya kazi kwa tabu ila ukitusua unasahau msoto. Jamaa alikuwa anafanyia kwenye migodi za Msumbiji, kuna eneo linaitwa Mtipweshi (kama sijakosea kulitamka). Story yake ilinivutia, nikajisemea, sibebi mizigo tena hapa, naenda Msumbiji


...............
Daah! Mwanangu Upo Vizuri sana kwenye Kusimulia
 
.... Tofauti na wengi wanafikiria, leo hii ukiniuliza shujaa wangu ni nani katika dunia hii,au ni nani namkubali sana katika ulimwengu huu, kwa kujivunia kabisa nitasema "BABA YANGU" . Huko mbele nitakwambia kwanini au hata wewe utagundua sababu.

Msimu wa kilimo ulipofika, sikuwa na hela ya kutosha kusema iniwezeshe kulima eneo kubwa sana. Nilifanya ushirikiano na jamaa mwingine mmoja, kwa pamoja tukafanikisha kulima heka tano za mbaazi. Shamba tulipata eneo moja lipo manispaa ya Songea, linaitwa Mlilayoyo. Tuliweka juhudi zote na usimamizi wa hali ya juu. Zao lilistawi vizuri sana. Naweza sema kati ya watu wote tuliokuwa tumelima maeneo ya pale, mimi na jamaa ndio tulikuwa na matokeo mazuri. Nakumbuka wakati tunaanza kilimo, bei ya mbaazi ilikuwa juu na nzuri. Kilo moja kuna sehemu ilikuwa inafika hadi 2500.

Msimu wa mavuno wakati unakaribia, ndio zikaja zile tetesi za kushuka kwa mbaazi. Tetesi zikawa kweli, soko likapotea. Ikafika kipindi kisado kinauzwa shillingi 500. Tukashauriana na jamaa tusivune, tusubirie hadi soko likae vizuri kwanza. Siku zikaenda, soko halikai sawa, mpaka mbaazi zetu zikakutana na msimu mpya wa kilimo. Gharama ya kuzivuna ilikuwa kubwa kuliko hata hela ambayo ingepatikana baada ya kuuza, achilia mbali gharama za kuendesha shamba mpaka kufikia hapo.

Mwenye shamba lake anatuuliza, tunampango gani msimu ujao? Tunalikodi tena shamba lake au la? Kama hatukodi, basi tuvune mbaazi tumuachie ardhi yake. Mshirika wangu ananiuliza, tunafanyaje? Nikamwambia me sina cha kufanya , we amua chochote utakachoona nakuachia shamba lote, siwezi kuingia tena gharama za kuvuna. Jamaa nikatemana nae kwa mtindo huo. Nikarudi ghetto pale moonlight.

Kwavile hela niliingiza zote kwenye kilimo, nikawa nimefulia tena. Hapo nilipata somo kuwa kama bajeti ya unachotaka kufanya ni laki 3,alaf na wewe una laki 3 hiyo hiyo, acha. Tulia kwanza mpaka upate hela ya ziada walau mara mbili ya hiyo au hata nusu yake, vinginevyo utakuja kuona watu wanakuchawia huko mbeleni.

Nilianza upya vibarua, hapo nipo choka mbaya. Baada ya kudunduliza na kupata hela kadhaa, sikutaka kujiuliza mara mbili wala kuzurura sana mitaani maana naweza nikakutana na mtu mwingine akanipa fursa. Nikaamua kurudi nyumbani.


* ** ** ** ****

Nilifika nyumbani majira ya usiku. Kabla sijaingia kwenye himaya ya nyumbani kabisa, nilipaangalia kwa muda mrefu sana. Kwa muonekano palikuwa panavutia na maisha hayakuwa mabaya. Nikagonga mlango baada ya kuvuka fensi ya maua na geti kubwa la mbao. Baba ndio alifungua mlango, alivyoniona akaniambia karibu. Yani hakuonesha kama ameshangaa, amefurahi au kushtuka, kiufupi alichukulia kama nilienda dukani sasa ndio narudi.

Asubuhi ya siku hiyo, naskia mama alijichoma na msumali wakati anapalilia maua pale nyumbani, toka hapo hakuweza kukanyaga vizuri chini, alikuwa anachechemea, ila aliponiona nahisi alipata ganzi ya mguu, maana sio kunikumbatia tu, bali pamoja na ndevu zangu alinibeba. Nikapata faraja niliyoitaka, faza nikampotezea. Pale mezani alikuwa ndio anamtengea mzee chai na maandazi (siku zote baba hupenda kunywa chai usiku hata awe ameshiba vipi). Basi ile chai akanipa mimi, Mzee anauliza vipi mbona unagawa chai yangu? Mama hana hata habari nae. Mara kaniletea hiki, mara kile, ilimradi ukarimu. Nilipoenda kulala, kila mara anakuja kunichungulia. Sina uhakika kama yeye alilala usiku ule.

Asubuhi ndio tuliweza kuongea vizuri kama familia. Hapo mama ameshawaambia ndugu zangu wote kuwa nimerudi. Baada ya chai ndio niliweza kukaa na kuongea na mzee. Kitu cha kwanza kuniuliza "Umefata ada?". Nikamwangalia kwa mshangao, ila kilichonishangaza zaidi nilipogundua kuwa hakuwahi kuwaambia nyumbani kuwa tulikutana Madaba, Songea. Ilo lilinishangaza.

Ila aliniambia, "Ulitaka nimwambie mama yako kuwa baada ya kupotea miaka mingi tulikutana ukiwa kibarua ambae maisha bado yamekupiga? Au baada ya miaka mingi kutoonekana, tumeonana ila bado ukaniomba hela? . Nilijua hutorudi ndio maana sikumwambia chochote mama yako kwa kipindi kile, na pia sitoshangaa kama utaondoka tena. Najua tulipoachana maisha yako yaliendelea kuwa magumu na ndio maana hata hela niliyokutumia wala hukunirudishia. Nikajiuliza hela gani alinitumia huyu mzee? Nahisi alijua ninachowaza, akaniambia siku tuliyoachana alichukua namba yangu toka kwa wale vibarua niliokuwa nafanya nao, na alipoona imepita zaidi ya miezi 6 sijaonekana nyumbani alinitumia laki 3 kwenye simu. Nikakumbuka kuna siku iliingia hela, nikajua mtu kakosea kutuma, nikaitoa kwa wakala alaf nikakausha. Mtumaji nae hakunicheki tena. Niliona aibu kichizi.


Baba akaniambia "Ikitokea leo hii Mama yako aseme nyie wote 7 sio wanangu, nitakubaliana nae kwa hao 6 wengine lakini wewe nina uhakika wa asilimia zote ni mwanangu. Mimi na wewe ni mapacha tuliozaliwa katika miaka tofauti, kwa kifupi ww ni mimi". Maneno ya mzee yalinigusa sana kwa mbali machozi yakawa yananilenga hivi. Faza akaniambia "Kama unalia nenda jikoni kwa mama yako" . Mzee wangu kauzu kichizi yani,kwanza toka nakua sijawahi kumuona anasikitika. Nikabaki nashangaa tu maneno yake. Akazidi kuniambia " Tofauti ya ww na mimi, ni kwamba mimi nilirudi baada ya safari yangu kuelekea mwishoni,nilirudi nikiwa shujaa. Wewe ni shujaa lakini safari yako haijaisha,umerudi ikiwa kati"

Kuna mengi sana hatuyajui kuhusu wazazi wetu ambayo yangetufunza na kutujenga, hii inatokana na kwamba tuko bize sana kiasi tunakosa muda wa kuzungumza nao. Misukosuko tunayokutana nayo leo hii, majibu yote yapo kwenye maisha waliyopitia wazazi wetu. Tunatafutaga majibu, lakini majibu sahihi yapo tulipotoka. Baba yangu ni Shujaa wangu,Mimi ni Baba yangu,na Baba yangu ni Mimi, unajua kwanini? Ni kutokana na stori fupi ya safari ya maisha yake aliyonisimulia.


* * * * * *

Kwa ufupi tu ilikuwa hivi. Anasema "Sikuwa na uwezo mkubwa wa kuelewa darasani, shule niliishia elimu ya msingi hata mtihani wa mwisho sikufanya, nilifukuzwa kwa kosa la kuchoma ofisi ya walimu. Tokea hapo nilikuwa naonekana kama mtoto mtukutu nyumbani, babu yako aliniwekea zamu ya kuchunga kila siku, alaf nyumbani sikuwa napewa upendeleo wowote. Kuna siku nilienda kuchunga,jioni nikarudisha ng'ombe ila nikasepa na mbuzi wote. Nikauza na kufanya mtaji. Heri yako unaondoka nyumbani umepewa hela, tena tukijua kuwa utaondoka. Sijui msoto uliopitia ww, lakini msoto niliopitia mimi baba yako ndani ya miaka minne ya mwanzo nadhani ww ungekufa. Ndani ya hiyo miaka minne ya mwanzo kuna siku niliamua kabisa kurudi kwa babu yako nikaombe msamaha, nilifika mpaka pale, nikaiangalia sana nyumba ila nikaona siwezi kurudi nikiwa hivi, nikageuza na kuondoka. Ndio maana sikuile tuliyokutana Songea, nilijisemea kimoyo moyo, kama huyu ni mwanangu hatorudi nyumbani.

Tokea ile siku niliyogeuza, nilijituma sana kiasi kwamba siku niliyorudi nyumbani, nilirudi na idadi ile ile ya mifugo niliyoondoka nayo ila badala ya mbuzi nilirudi na ng'ombe. Ila pamoja na hayo babu yako aligoma kunisamehe hadi kikafanyika kikao na wazee wa kijiji, ndio nikasamehewa,tena baada ya kuchapwa bakora pamoja utu uzima wangu.

Aliendelea kunisimulia vitu vingi sana, hapo ndio nikajua nilidhani nimesota na kupitia tabu nyingi sana, kumbe ningezifananisha na za mzee, basi zangu zingekuwa ni utangulizi tu. Mgodini niliposhindwa kwenda, yeye alishaenda na alishawahi kufukiwa hadi na kifusi. Baba yangu akitembea huwa anachehemea,mguu mmoja ni kama mfupi. Ananiambia ule ulishavunjika mara mbili kutokana na mbilinge za migodini.

Tokea siku hiyo, kila nnapopitia ugumu wowote, lazima nijiangalie kwenye kioo. Baba yangu ni kioo changu.

* ** * * ****

Kurudi kwangu kulirudisha furaha sana nyumbani. Usiku kabla ya kulala, mshua aliniuliza "Una watoto wa ngapi mpaka sasa? Nikamjibu mmoja wa kiume. Akasema namuhitaji, fanya mpango aje hapa nyumbani.

Najua kuna wadau watashangaa kuona nimesema nina mtoto mmoja wa kiume, wakati katika stori yote sijawahi kuongelea ili swala. Katika hii stori ya safari yangu, nimegusa baadhi ya matukio ya kwenye maisha yangu ila sio yote. Na sijagusia mapenzi kwasababu yamenitesa kichizi, nadhani mwanaume akiwa hana hela mwenendo wake wa mapenzi unajilikana tu,mapenzi yanatesa sana Me kuliko Ke. Kuna msemo mmoja nimeuona juzi kuwa "Mwanaume kama huna hela, kazi ya kulinda mahusiano yako muachie Mungu" hii ni kweli kwa asilimia zote. Kwa ufupi kwenye hii safari yangu, mtoto ninae tena wa kiume.


Nikafanya mpango na taratibu zote, nikapewa yule mtoto. Sasa hivi anaishi na babu yake.

Siku ambayo mtoto alifika pale nyumbani, kesho yake mzee aliniita tukawa na mazungumzo ya hapa na pale. Kisha akatoa bahasha na kunikabidhi, kuhesabu ni milioni mbili. Nikamuuliza za nini. Akasema "Babu yako alinipokea baada ya kufanya kikao na wazee kisha nikachapwa bakora,nimekupokea nyumbani ila sitokuchapa...Safari yako bado haijaisha, nenda kapambane". Nilimwangalia yule mzee sikummaliza.

Wiki moja badae nilikuwa ndani ya bus naelekea Songea. Nikarudi rasmi kwenye kilimo. Safari hii nikalima tangawizi..

Nitarudi kukwambia jambo zuri lililotokea. Katika maisha,Baraka za wazazi ni kila kitu.

....

Analyse #Baharia wa nchi kavu.
Had machozi yananilenga mkuu
 
Back
Top Bottom