nilidhani unasema Milioni 13 kumbe milioni 1
Dodoma huku unapata eka moja porini kilomita 18 kutoka mjini kwa 1,3M, kiwanja kinafika 20m maeneo ya kujenga, ambayo joshua_ok anafananisha na KEREGE
mm nitafutieni kiwanja aua shamba iwe Kibaha, Chanika au Bunju najua barabara zipo
Ukienda usinisahau Dada
Mkuu uza hiyo gari tafuta Toyota hiace ya 15milion, Asubuhi unapokuja mjini beba abiria, unaporudi kerege pia beba abiria. weekend aamka asubuhi piga trip kazaa tegeta bagamoyo.. Hapo utakuwa umejiongezea kipato lakini pia utakuwa umepata hela ya mfuta kila siku ya kuendea kazini..
Umenena, yaan kwenye public transport ni unahisi kero mpaka, ukikanyagwa sasa!Yaani ukishazoea gari jamani kurudi kwenye daladala inabid wito haswa!
2 kwa siku? Uko vizuri mwayaKweli kila mtu anawaza ajuavyo yeye...yaan nipewe laki 2 kwa mwezi??hapana...!ila kuna biashara kichaa sana...labda ujenge nyumba ukopee mkopo mzuri benk...mwee huyo laki 2 mm naipata kwa siku 1!nah!
Wewe shukuru umejenga kibanda chako hata kama hukuwa umejipanga usicheze na maisha ya kupanga nduguWakuu enzi za Neema za Mkwere nilijenga maeneo ya Kerege sasa mambo yalipobana kodi ikanishinda Sinza nikahamia kwangu Kerege asee najuta maana hizo gharama za mafuta zinazidi kodi ya nyumba Sinza (400,000/=).
Bado sijaweka ukuta, vibaka kila mara wanavamia nikiwa kazini mjini nimejaribu kuuza nyumba haiuziki wanunuzi wengi wanadai huku uswahilini sana.
Funzo: Vijana msikimbilie kujenga kama hamjajipanga.
Jana nilikwenda huko Kinzudi asee kuna watu wanaishi mbali. Nikawaza mtu kama hana gari inakuwaje?Wakuu enzi za Neema za Mkwere nilijenga maeneo ya Kerege sasa mambo yalipobana kodi ikanishinda Sinza nikahamia kwangu Kerege asee najuta maana hizo gharama za mafuta zinazidi kodi ya nyumba Sinza (400,000/=).
Bado sijaweka ukuta, vibaka kila mara wanavamia nikiwa kazini mjini nimejaribu kuuza nyumba haiuziki wanunuzi wengi wanadai huku uswahilini sana.
Funzo: Vijana msikimbilie kujenga kama hamjajipanga.
Hhaaha ishakuwa soo!watanzania bwana!😊1 kwa siku? Uko vizuri mwaya
Kwani wakati unahamia hukujua umbali kutoka hapo hadi posta?Vibaka washabeba smart TV na laptop imebid nisinunue vingine mpaka ntakapoweka ukuta na electric fence
Kuna viwanja vinauzwa 1.3milion huko kisemvule na vikindu, huwa najiuliza kiwanja cha 1.3milion si kitakuwa mbali sana na mjini..yaani kila siku una drive 70km kwenda na kurud kazini..lakin hongera kwa kuwa na Nyumba
Hahahahahhhha nimeipenda hii... Hii ni formula nzuri kwenye maisha wengi wanaiogopa, usipunguze matumizi eti hali ngumu bali ongeza mbio uongeze kipato kucover matumizi yake..
hiyo sehemu inaitwa Mbalawala, Mpamatwa Mbande nk hakuna barabara ni njia za Baiskeli na pikipiki hatutarajii Mwendokasi ni mapori ya kukata mkaa, ndipo wazi km huko KeregeSawa lakini kerege kwenda posta ni karibu kilomet 40 au 50 sasa unafanya kazi Posta kwenda nakurudi km 70 au 80 bora hiyo dodoma km 18 tu na foleni hakuna
Ndivyo unavyofanyaga hivo?[emoji16]Panda gari yako, ukifika Tegeta Nyuki, acha gari Mahala... Chukua daladala... Utapunguza gharama..
Service ya gari si unaijua mzee..hiyo 14 haitaweza kuservice gari..otherwise labda kama umeamua tu kuwasaidia watuKivipi? Hakuna mlima, lami hadi anapofika anatembelea mchanga kama mita 150 tu! Anawashushia hapo Stesheni
Kifupi ingekuwa madai yako yanaukweli kwa muda aliotumia ingeshachoka!
Kikubwa gari ni service ya hali ya juu kwa kuangalia garage nzuri yenye vifaa na wataalam wenye weledi!
Dar moro masaa mawili hadi matatu kwa private ..lakini Posta Chanika inaweza chukua hadi saa tano kutegemeana na barabara ilivyo hiyo siku. So sijaelewa point yako unaongelea umbali au matumizi ya muda barabarani.Nimegundua wengi waliomshaul ni wanafunzi wa chuo wanaopenda maisha ya kwenye video, dume zima ukaona kerege mbali na watu wanakaa moro wanafanya kazi dar nimewazalau kwelikweli
Unaposema nunua kisha usubiri, unakuwa unamsubiria nani au unasubiri nini?!Tofautisha ardhi na nyumba. Thamani ya nyumba ni ardhi. Mbweni pale viwanja vya milioni 3 ulikuwa unakatiwa na halmashauri ya jiji.
Watu waliokuwa na hekari 10 Mbweni, wamepata faida sana.
Mleta mada kaongea point sana. Usijenge bila kujipanga. Nunua ardhi, subiri.
Yaan ukijenga huko ukiwa kijana ni lazima utarudi tu mjini!Kumbe wapo wengi nina ndugu yangu kajenga huko naye kakimbia amerudi mjini
Mmh [emoji849]Usalama ni changamoto isiyo na solution ya kuaminika. Kuna jamaa alikuwa maeneo hayo, ana uwezo, ameweka ukuta wenye nyaya za umeme na ving'ora na mbwa ndani lakini bado alikuwa target ya majambazi mara kwa mara. Mara wamtegeshee wakati anaingia kwenye geti au wakati mwingine waje mchana.