Najuta kuhamia kwangu Kerege

Najuta kuhamia kwangu Kerege

Wakuu enzi za Neema za Mkwere nilijenga maeneo ya Kerege sasa mambo yalipobana kodi ikanishinda Sinza nikahamia kwangu Kerege asee najuta maana hizo gharama za mafuta zinazidi kodi ya nyumba Sinza (400,000/=).

Bado sijaweka ukuta, vibaka kila mara wanavamia nikiwa kazini mjini nimejaribu kuuza nyumba haiuziki wanunuzi wengi wanadai huku uswahilini sana.

Funzo: Vijana msikimbilie kujenga kama hamjajipanga.
Hongera kwa kujenga itakuja kukuaa hata mbele huko, kama kazi/mishe mjini kati jaribu kupanga maeneo ya karibu yenye bei nafuu ila pawe poa,tena mengi tu. Mafuta na kukesha barabarani utazeeka kabla ya umri wako.
 
Wakuu enzi za Neema za Mkwere nilijenga maeneo ya Kerege sasa mambo yalipobana kodi ikanishinda Sinza nikahamia kwangu Kerege asee najuta maana hizo gharama za mafuta zinazidi kodi ya nyumba Sinza (400,000/=).

Bado sijaweka ukuta, vibaka kila mara wanavamia nikiwa kazini mjini nimejaribu kuuza nyumba haiuziki wanunuzi wengi wanadai huku uswahilini sana.

Funzo: Vijana msikimbilie kujenga kama hamjajipanga.
Nyie ndo mnatubana bana huku Kerege.
Rudi mjini tuachie shamba.
 
Hujaelewa kumbe... Anaweza kuwa na kiwanja huko lakini sio kukaa huko
yupi sasa ? km ttunayemzungumzia mbona post#1 imejieleza, p/se anza mwanzo ndipo utaelewa mtiririko
1573479932046.png

post: 33428902 said:
Wakuu enzi za Neema za Mkwere nilijenga maeneo ya Kerege sasa mambo yalipobana kodi ikanishinda Sinza nikahamia kwangu Kerege asee najuta maana hizo gharama za mafuta zinazidi kodi ya nyumba Sinza (400,000/=).
 
Mwezi Ulopita, Baada ya Biashara kuchanganya vizur.
Nmenunua Kiwanja kizur zaidi Ukubwa ule ule pale pale maili 1 kwa 85mil kikiwa na tofali 219 za block
Ila Sijutii, maana kimenunuliwa mda muafaka kabisa kwa ajili ya kukitumia.
Jamaa angu, Biashara zake zimeyumba.
Hana bajeti tena ya kupaendeleza.
Kiwanja chake nakiona bado kipo tu kinaendelea tu kusubiri mteja mwezi wa 3 sasa maana katangaza Anauza 75mil.
jamani tenganisheni UKWELI na UONGO
enzi za Mkwere mwenzako kajenga sasa hali ni ngumu hata mpangaji hapati
Eti wewe una sema leo biashara imechanganya, ni ipi hiyo? maana hata ya kutakatisha pesa, ngada na mashuzi zote HAZITOKI Chinga wote wanalia, wewe ukanunue kiwanja 85m bila taarifa TRA
Tafuta waraka wa fedha kuhusu zaidi ya 10M popote ni lazima uitolee maelezo (huwezi nikubandikie sasa hivi uisome)
wewe unasema mwezi uliopita, hata aliyekuuzia angeshajieleza kwanini KODI hamjalipa
Mleta Mada kasema ukweli tuliobaki ni matajiri nyuma ya keybody
 
Unajidanganya, maisha ya kuamka saa 10 usiku ili saa moja asubuhi ndio ufike mjini kati huu ni uwendawazimu kwa Tanzania, kuna nchi nimeishi train za umeme ndio usafiri wa kwenda makazini na mtandao wa reli umepita kwenye makazi mengi, ukikaa mbali na mjini hakuna tatizo lakini si kwa Tanzania acha kudanganya wenzanko.
Watu wenye busara akiwa na million 50 ananunuwa nyumba karibu na town unang'arisha then unaenjoy maisha.
Unakaa sehemu hata kuhudhuria harusi huwezi unawaza stress za muda wa kurudi usiku, disco huwezi kwenda haya ni maisha gani sasa?
Ardhi ni mali Mkuu hata iwe mashambani, wenzetu jirani tu hapo wanaithamini kuliko sisi tunaoona Kerege hapafai
Huko Kaskazini Nchini mwetu sio WEHU mtu anaamka Mwika, Marangu na hata Rombo anafanya kazi KIA au Arusha kwenda na kurudi kwanini asitoke mgombani akapange Sombetini Arusha
Fika huko siku moja uone Mini bus zinavyojaza wakati Treni za umeme hakuna Mkuu, watu hawalali labda hapo Posta Dar hamtaki kuamka
 
Una vimelea vya utumwa na umaskini, niulize nikufundishe kitu
Wakuu enzi za Neema za Mkwere nilijenga maeneo ya Kerege sasa mambo yalipobana kodi ikanishinda Sinza nikahamia kwangu Kerege asee najuta maana hizo gharama za mafuta zinazidi kodi ya nyumba Sinza (400,000/=).

Bado sijaweka ukuta, vibaka kila mara wanavamia nikiwa kazini mjini nimejaribu kuuza nyumba haiuziki wanunuzi wengi wanadai huku uswahilini sana.

Funzo: Vijana msikimbilie kujenga kama hamjajipanga.
 
nyumba za NHIF [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Inawezekana wewe umekomaa vigimbi lakini siyo akili,

Nyumba ya million 50 ni Dar na kwa taarifa yako Mimi real estate ndio fani yangu.

Kutoka harusini saa 8 usiku kudrive km 50 huu nao ni zaidi ya uwendawazimu.

Kama umezaliwa kijijini Nyalugusu ni lazimà ushangae swala LA outing, kila MTU na hobby take mwingine disco mwingine live band mwingine matamasha.
Tatizo mtu umri ukienda anahisi kudrop vitu vya kumpa starehe ndio kukua eti...wenzetu wazungu wana afya njema muda mwingi sababu wanajua nini maana ya kujipa raha, beach utakuta wazee wa kutosha, club wamoo, ilimradi wanapata furaha...sada bongo ili uonekane umekua ni kujifungia ndani na kuinamisha bichwa chini all the time.
Tusiambukizane lifestyle kwa nguvu
 
Mzee wangu alikuwa anakaa mjini kati.

Wakati nipo kidato cha kwanza akahama mjini anakaenda nje ya mji kisa ng'ombe wake wanakosa majani.

Kimbembe kilianzia hapa;

1. Wakati wa likizo nilikuwa nasoma tuition mchikichini, akawa ananiamsha saa 4:00 alfajiri tunaondoka wakati anaenda kazini ananiacha kkoo majira ya saa 6:30 asubuhi (hapo vibaka wanamalizikia kwenda makwao).

2. Ananiachia na 5000 ya kulipia vipindi, lunch na nauli ya kurudi nyumbani. Hiyo ni kila siku. Kwa siku 5 ni sawa na 25,000/- (hii ni zaidi ya miaka 15 iliopita) na hapo usafiri ulikuwa shida si mchezo. Unapanda magari hata matatu kurudi nyumbani. Au wakati mwingine namsubiri wakati anarudi pale fire nidandie lift.

3. Weekends tulikuwa tunakutana UDSM kwa ajili ya discussion na washkaji. Lazima anipe 5000 ya nauli na chakula.

4. Yeye mwenyewe alikuwa anafanya kazi posta, alikuwa anaweka full tank kila jumatatu.

Nilikuwa nachoka sana na yeye mwenyewe alikuwa anachoka sana.

Hadi namaliza ilikuwa kimbembe. Wakati nahama nikatafuta nyumba katikati ya mji.

Naenda sehemu yeyote, muda wowote.
 
Nina rafiki zangu wawili. Wote hawajaoa.

1. Mmoja ni dokta, anafanya kazi muhimbili na sehemu nyingine kama part time. Amepanga nyumba upanga. Analipa kodi 600,000. Anaenda kazini kwa miguu wakati mwingine na gari. Akiweka full tank anakaa hata week 3 au mwezi kabisa. Weekends ndo anatoka mjini kuja nje ya mji kula bata.

2. Wa pili ni engineer, ofisi ipo posta, wakati wa JK akapiga deal akapata kama 80M. Akakimbilia kununua kiwanja huko mbele ya bunju akajenga fastafasta. Kimbembe kikaja muda anaotumia toka nyumbani hadi ofisini. Anakaa njiani almost masaa 3 hadi 4 kila siku ya ofisi. Anatumia mafuta ya 400,000 kila mwezi. Baada ya mwaka akaifunga nyumba akatafuta apartments za NHC ilala anakaa huko sasa. Ile nyumba anafikiria kuiuza.

Msimamo wangu binafsi; nitakaa nje ya mji kama nataka kustaafu. Mizunguko nimeipunguza zaidi ya 90%.
 
Mkuu binafsi si kushauri hiyo nyumba uuze hata kidogo ,bora ww umejenga kerege mimi nimejenga kiromo na nimehamia huko na shughuli zangu zinaenda ,fikiria mtu anaekaa mlandizi anapiga mishe town au anayekaa chalize na kila siku asubuhi yuko town na jioni anageuka ,
Usiuze nyumba mkuu ,utakuja juta usawa huu ,
Watanzania tunapoteza muda mwingi kizembe sana ....just imagine huyo anaeishi mlandizi na kufanya shughuli zake kkoo ni muda gani anaupoteza akiwa njiani kila siku?

Ukipiga hesabu unaweza kuta kwa mwaka anatumia miezi mitatu akiwa barabarani.
 
Wakuu enzi za Neema za Mkwere nilijenga maeneo ya Kerege sasa mambo yalipobana kodi ikanishinda Sinza nikahamia kwangu Kerege asee najuta maana hizo gharama za mafuta zinazidi kodi ya nyumba Sinza (400,000/=).

Bado sijaweka ukuta, vibaka kila mara wanavamia nikiwa kazini mjini nimejaribu kuuza nyumba haiuziki wanunuzi wengi wanadai huku uswahilini sana.

Funzo: Vijana msikimbilie kujenga kama hamjajipanga.
Hiyo ndio nyumba uliyojenga au ni banda LA uani
 
Back
Top Bottom