Najuta kumkaribisha demu wangu JF

Najuta kumkaribisha demu wangu JF

Mkuu uanogopa nini na kwanini ujute huoni kwamba kwa kumruhusu kuwa kwenye mtandao kumekufanya umtambue kabla hujaweka nadhiri za milele.
 
Demu wangu hakuwa hata anajua kama duniani kuna jukwaa la JF,

Nikamshawishi ajiunge na akajiunga, tokea ajiunge wanajukwaa wengi wa kiume wamekuwa wakimsumbua sana kwa pm, wakipiga mistari,

Wengine wamefikia hatua hadi ya kumtumia namba za simu, nikitembelea profile yake nakuta vistors kibao wa kiume.

Kama mnavyojua miluzi mingi humpoteza mbwa, ninahofu anaweza nipotea kwa mtindo huu, kinachonitisha zaidi niliamua kutengeneza ID asiyoijua nami nikaanza kumtongoza, kanitumia namba yake na ninachat naye sana na ameshaonesha dalili zote za kunikubali, mtihani ni kuonana naye, naogopa kuweka appointment halafu kweli atokee, nitazimia.

Okay…
Hebu nipe ID yake tuone…
 
Back
Top Bottom