Najuta kuoa Single mother, kila nikimtazama huyu mtoto wake Moyo wangu Unaumia kwa machungu makali. Nahitaji msaada

Acha ufala Kijana, ungekuwa mwanangu ningekugonga ngumi za uso ili akili yako ikawe sawa, badala ya kumshughulikia mkeo apate ujauzito unaleta habari za kijinga. Usitupotezee muda pambana ukishindwa omba msaada kwa marijali wakusaidie.

Samahani kama nimekukwaza ila nimekuambia ukweli mchungu.
 
Huu ushauri umeuandika kiutani ila ni mkubwa sana kwa maana umejikita zaidi kwenye madhara yanayoweza kujitokeza pindi hiyo hali itakapozidi.
 
Umeoa au umesogeza?

Kuoa namaanisha kama ulifuata taratibu zote za kisheria.

Kama umeoa, wazazi wako hasa mama aliridhia?

Mkeo ushawahi kumpeleka kwenu?

Mzazi mwenzake wa huyo mtoto unamfahamu?

Wazazi wako walimpokeaje?

Kama ulisogeza ni kitu gani kinakufanya ujute na kuanza kulialia, kwamba umeshindwa kumtema kwa kutumia tu uongo kidogo kabla unyumba wenu haujaota mizizi, hadi utumie ushauri wa watu?

Una umri gani kwani!

Mkuu mada tukiikandamiza maswali hii, naiona eti kama inaelea haina uzito wowote kama puto ama kwa lugha nyingine 'chai jaba'?
 
IPO ivi mdg wangu utoto Bado unakusumbua huja mature kiakili, nilidhan labda umekuta mke wako Wana mawasiliano chanya na huyo baba wa mtoto ila kumbe ni unajutia maamuzi ulioyafanya apo umefeli, unapomsaidia mtu yeyote usi demand kulipwa fadhira Fanya kama unatoa sadaka kanisani, Mimi baba angu alinifukuza home kipindi nasoma na nilipokua shule nikipata rafiki mchaga akaenda kuwaeleza kwao kua nna matatzo na anaomba nikae kwao,


Akanikubalia nikaenda kukaa kwa yule mchaga ambae sina undugu nae hata tone alinilea kama mwanae wa kuzaa kwa kunipa mahitaji yote muhimu na kipindi hiko baba ni mfanyakazi serikalini na huyu bwana ni mfanyabiashara

mpk Namaliza shule naamua kuondoka kwake sijawah kumlipa hata sent kuhusu kunilea

Na hajawahi kunilaum wewe kulea mtoto wa mwenzio unaona ni kazi,, kwa hyo ata watoto wako utawalea uki demand watakuja kukulipa??


Lea kama unavoweza kumlea mtoto uliemuokota mtaani au kama mwanao au kama mtoto wa ndg yako acha ufala
 
Nimetongoza mtu na mama yake wote wamejaa kwenye kumi na nane halafu wameolewa,
 
Huyo mtoto Hana kosa mkuu usimchukie tafafhari..
Kaa chini na Mama yake akubali mtoto akaishi kwa baba yake kama Bado yupo hai au kwa Bibi.
 
Nikajua labda tatizo ni mawasilino kati ya mkeo na mzazi mwenzake, kumbe ni huyo mtoto! Unatia aibu, mtoto ni malaika, ulivyoamua kumlea mwanzo ulitakiwa kufikiria yote pamoja na huyo mtoto.

Kama mama yake hakusumbui, lea mtoto, ni sadaka unatoa. Huyo mpuuzi aliyeacha damu yake bila kuiangalia wala usimfikirie.
 
Huna mamlaka naye
1. Kifamilia
2. Kisheria
3. Hata kiroho.
 
Uwongo mtupu huu. Na sina hata haja ya kutoa maelezo

Huu ni muendelezo wa wakataa ndo na wanyanyasaji wa Ma single mother.

Uwongo na upuuzi mtupu huu
 
Hiyo option ya 1 Nimemwambia afanye hivyo amekataa Mkuu. Option ya 2 ndiyo nafikiria kufanya hivyo aisee..
 
Yani mwanaume una 28 yrs kijana mbichi kabisa unaenda kuoa mwanamke aliyezalishwa na mwanaume mwingine kweli??,hivi huwa mnafikiri kwa kutumia akili au??
Wanawake wenyewe wa kitanzania suala la uaminifu kwao ni zero,kesho ukimkuta anawasiliana na mzazi mwenzake utajisikiaje??,suo ndio chanzo cha migogoro na hatimae kifo.

Achana na huyo mwanamke,tafuta mwanamke ambaye hajazaa uoe.Kila mtu ahukumiwe na maamuzi ya maisha yake-yeye alichezea maisha yake kwa kuzaa mapema basi akae bila kuolewa afaidi matunda ya maamuzi yake.
 
Mpende huyo mtoto na umhudumie kama ulivyoazimia. Siku utakapomgusa huyo mtoto asiwe sehemu ya familia yako ndoa yako itakuwa imefikia mwisho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…