Nakanusha: Hospitali za Umma hazipendi kutoa huduma mbovu isipokuwa majukumu yanawalemea

Nakanusha: Hospitali za Umma hazipendi kutoa huduma mbovu isipokuwa majukumu yanawalemea

Naungana na wewe mkuu , wahudumu wa Afya serikalini Kwanza niwape pongezi Sana , mnafanya kazi ngumu ya kuogofya mno , mazingira magumu ya kazi , mnakuwa overwhelming na idadi ya wagonjwa , wakat mwingine mgonjwa anakufia mkononi sio kwamba ni uzembe Ila vifaa hamna, unaweza Lia kabisa but nothing you can do....

Serikali yetu hi worst na terrible Sana upande wa Afya ....!!! Inashangaza hii ndo Wizara ambayo ingetakiwa kuongoza Kwa kuwa na ukubwa wa bajeti lakini hata kwenye top 5 nafkri hata haimo wakat ndo imebeba uhai wa raia ...

Watu wengi wanafariki Kwa kukosa matibabu stahiki , kiuhalisia daktari hawez fanya lolote kama mazingira sio wezeshi
Point tupu
 
serikali inalijua hilo lakini ipo kimya, zahanati huko vijijini zinaemdeshwa na mtumishi mmoja, mda mwingine hata yeye anachoka anafunga anajificha, ndo maisha yanavyoenda ivyo

lawama waipelekee CCM sio watu wasiohusika
Very good tena mtumishi mwenyewe unakuta ni medical attendant
 
Unataka wananchi walalake kwa Nani?

Na kwa nini mmekubali muwe wachache ili hali wenye taaluma hiyo wapo tu na vyeti vyao mitaani.?

Kama mmekaa kwa kutulia ili hali mnajua mko watoa huduma wachache, basi mnao huo uwezo wa kuhudumia

Msilalamike, chapeni kazi!

Lkn pia, Mwendazake aliwezaje kuwafanya mpunguze haya malalamiko ya wananchi.?
Wao ndiyo wanaajili?
 
Bro umetumia nguvu kubwa kueleza mambo yaliyo wazi(hongera)
Kwa mtanzania mkaazi anaelewa jinsi sekta zote za umma zilivyo choka mbaya.Ukiondoa mtima nyongo,kila mwenye roho safi juu ya watumishi haya anayajua.Mimi niseme 'wananchi wa Tanzania mara nyingi hujenga chuki dhidi ya watumishi wa umma bila sababu!
Siyo huko tu,watu wanaenda kazini lakini anaja anaenda kutimiza baadhi ya majukumu na mengine anajua hatashughulika nayo kwani yapo juu ya uwezo wake.
Niulize tu swali,
NI SEKTA/IDARA GANI HAPA TANZANIA INAFANYA VIZURI NA KULETA MATOKEO BORA?
Nijijibu,HAMNA! maana hata saccos 'CCM' imeshindwa ku-deliver!!
 
Mfumo mbovu wa Ujamaa alioujenga Nyerere ndiyo umetukwamisha kiuchumi. Uchumi ukikwama, hata huduma za afya zinakuwa mbaya. Ndiyo maana vigogo wakiugua wanaenda kutibiwa nje ya nchi.
V8 ya mwigulu ambayo ingeweza kununua vifaa Kibao vya maabara, napo lawama kwa nyerere.
 
Utawasikia wanasema kasomee afya kazi zake ni za heshima na malipo mazuri ila ukiwaona wamepauka sana kuliko sisi Administrators wa Taasisi za Serikali.
Suala la kupauka halina uhusiano wowote na afya wala elimu wala huo uadministrator wako, kukuza kipato ni weledi tu wa mtu, wapo darasa la 7 wana maisha mazuri kuliko degree holders
 
Duh, muhimbili pale na ukubwa wote nimekaa jam kuanzia 12 asubuh mpaka 12 jion na Bado, majibu Sasa inakaribia wiki Sasa Bado, yaan unachoka hoi
 


Amtaki hao mkiletewa watu wenye uwezo wa kupigana kubadili tabia za wahudumu na kufahamu regulations za huduma mnaanza kuwatukana.

Si mlikuwa mnamtaka ‘Ummy Mwalimu’ haya sasa kila mtu apambane na hali yake kutokana na mfuko wake, ukiona vipi nenda Kenya au South Africa kama matajiri wanavyofanya.
 
MODS USUNGANISHE UZI, NATAKA WATANZANIA WAELEWE CHANGAMOTO TUNAZOPITIA

Kuna mdau amelalamika sana kwamba ameenda hospitali ya Umma akakuta huduma ni mbovu na wagonjwa ni wengi sana ila watumishi wanapiga tu story mpaka wagonjwa wengine wanazidiwa mapokezi.

Amedai mgonjwa anapokelewa saa mbili ila hadi saa nne hajapata huduma yoyote!

Naomba nikanushe na nijibu tuhuma za mdau.

Mimi nimefanya kazi hospitali zaidi ya moja, tatizo kubwa linalosababisha huduma zizorote hospitali za Umma ni ufinyu wa wafanyakazi wala sio kwamba ni wazembe.

Mfano nautolea kuna hospitali zinahitaji watu zaidi ya 30 lakini unakuta wahudumu ni kumi tu.

Mfano hospitali ya kanda ya mtwara kiuhalisia inatakiwa kuwa walau na wafanyakazi 200 lakini mpaka sasa wapo chini ya 50 idadi ambayo haiendani kabisa na jumla ya wagonjwa wanaokuja hapo.

Nimefanya kazi hospitali moja yenyewe ni kituo cha wanafunzi kufanya mafunzo kwa viitendo, ile hospitali ni kama imetelekezwa wahudumu ni wanafunzi tupu.

Hospitali za vijijini mpaka raia wanaitwa wasaidie kutoa huduma, imagine zahanati nzima muhudumu mmoja, hana off hana masaa ya kazi hata saa saba usiku anaamshwa akazalishe anazalisha mtu saa kumi usiku, halafu asubuhi anatakiwa kazini! haya mambo yapo na tunayapitua sio story,
wahudumu wa afya wanafanya kazi kubwa sana tusiwabeze.

Mfano mwingine mdau amelalamika kua unaenda hospitali saa mbili hadi saa saba hakuna huduma yyte.

Kuna hospitali kubwa tu lakini unakuta ina maabara mbili tu, au moja kiasi kwamba watu zaidi ya 200 wanasubiri majibu toka maabara moja kwa wakati mmoja.

Muiambie serikali ya CCM iboreshe huduma za afya musisingizie kua watumishi ni wazembe.

Wodi moja usiku mmoja unakuata ina muuguzi mmoja! Mnataka afanyeje?

Mhudumu mmoja wagonjwa 70 unategemea huduma gani bora hapo?

Tusidanganyane hapa wala tusilaumu wwatumishi wa afya

Kuna hospitali niliwai kushangaa usiku mzima nesi ni mmoja wodi nzima tena ni mwanafunzi

Narudia tena tatizo sio sisi watumishi tatizo ni serikali yenu.

Shida inakuja pale mgonjwa yuko wodi A anaona hapati huduma anashangaa kuona watumishi wengine wako nje wanazunguka ambao hata huwenda hawahusikibna hyo wodi.

Mtu akiwa na mgonjwa akiona mhudumu yoyote anataka amhudumie bila kujua hospitalini kuna vitengo mbalimbali.

Hata watumishi wa umma wanatamani wawahudumie vizuri kama private tatizo ni kulemewa na majukumu private watumishi wengi, wagonjwa wachache.

Umma watunishi wachache sana wagonjwa wengi!

Msilaumu watumishi mpk kuwatukana wanafanya kazi nzuri sana

serikali inabidi iongezeje bajeti wizara ya afya wajenge miundombinu inayoendana na idadi ya watu pia waongeze watumishi, muone kama huduma zitakua za hovyo

Mungu ibariki Tanzania na watumishi wa Afya
Private ndio zinawahudumu tosherezi?
 
Unataka wananchi walalake kwa Nani?

Na kwa nini mmekubali muwe wachache ili hali wenye taaluma hiyo wapo tu na vyeti vyao mitaani.?

Kama mmekaa kwa kutulia ili hali mnajua mko watoa huduma wachache, basi mnao huo uwezo wa kuhudumia

Msilalamike, chapeni kazi!

Lkn pia, Mwendazake aliwezaje kuwafanya mpunguze haya malalamiko ya wananchi.?
Elewa mada kwanza ndugu yangu
 
Duh, muhimbili pale na ukubwa wote nimekaa jam kuanzia 12 asubuh mpaka 12 jion na Bado, majibu Sasa inakaribia wiki Sasa Bado, yaan unachoka hoi
huwenda mnaosubiri majibu mpoa hata 600
 
MODS USUNGANISHE UZI, NATAKA WATANZANIA WAELEWE CHANGAMOTO TUNAZOPITIA

Kuna mdau amelalamika sana kwamba ameenda hospitali ya Umma akakuta huduma ni mbovu na wagonjwa ni wengi sana ila watumishi wanapiga tu story mpaka wagonjwa wengine wanazidiwa mapokezi.

Amedai mgonjwa anapokelewa saa mbili ila hadi saa nne hajapata huduma yoyote!

Naomba nikanushe na nijibu tuhuma za mdau.

Mimi nimefanya kazi hospitali zaidi ya moja, tatizo kubwa linalosababisha huduma zizorote hospitali za Umma ni ufinyu wa wafanyakazi wala sio kwamba ni wazembe.

Mfano nautolea kuna hospitali zinahitaji watu zaidi ya 30 lakini unakuta wahudumu ni kumi tu.

Mfano hospitali ya kanda ya mtwara kiuhalisia inatakiwa kuwa walau na wafanyakazi 200 lakini mpaka sasa wapo chini ya 50 idadi ambayo haiendani kabisa na jumla ya wagonjwa wanaokuja hapo.

Nimefanya kazi hospitali moja yenyewe ni kituo cha wanafunzi kufanya mafunzo kwa viitendo, ile hospitali ni kama imetelekezwa wahudumu ni wanafunzi tupu.

Hospitali za vijijini mpaka raia wanaitwa wasaidie kutoa huduma, imagine zahanati nzima muhudumu mmoja, hana off hana masaa ya kazi hata saa saba usiku anaamshwa akazalishe anazalisha mtu saa kumi usiku, halafu asubuhi anatakiwa kazini! haya mambo yapo na tunayapitua sio story,
wahudumu wa afya wanafanya kazi kubwa sana tusiwabeze.

Mfano mwingine mdau amelalamika kua unaenda hospitali saa mbili hadi saa saba hakuna huduma yyte.

Kuna hospitali kubwa tu lakini unakuta ina maabara mbili tu, au moja kiasi kwamba watu zaidi ya 200 wanasubiri majibu toka maabara moja kwa wakati mmoja.

Muiambie serikali ya CCM iboreshe huduma za afya musisingizie kua watumishi ni wazembe.

Wodi moja usiku mmoja unakuata ina muuguzi mmoja! Mnataka afanyeje?

Mhudumu mmoja wagonjwa 70 unategemea huduma gani bora hapo?

Tusidanganyane hapa wala tusilaumu wwatumishi wa afya

Kuna hospitali niliwai kushangaa usiku mzima nesi ni mmoja wodi nzima tena ni mwanafunzi

Narudia tena tatizo sio sisi watumishi tatizo ni serikali yenu.

Shida inakuja pale mgonjwa yuko wodi A anaona hapati huduma anashangaa kuona watumishi wengine wako nje wanazunguka ambao hata huwenda hawahusikibna hyo wodi.

Mtu akiwa na mgonjwa akiona mhudumu yoyote anataka amhudumie bila kujua hospitalini kuna vitengo mbalimbali.

Hata watumishi wa umma wanatamani wawahudumie vizuri kama private tatizo ni kulemewa na majukumu private watumishi wengi, wagonjwa wachache.

Umma watunishi wachache sana wagonjwa wengi!

Msilaumu watumishi mpk kuwatukana wanafanya kazi nzuri sana

serikali inabidi iongezeje bajeti wizara ya afya wajenge miundombinu inayoendana na idadi ya watu pia waongeze watu
mishi, muone kama huduma zitakua za hovyo

Mungu ibariki Tanzania na watumishi wa Afya
View attachment 2279137
Wengi wanaoropoka huko mitandaoni wanashindwa kuelewa ukweli kwamba hospital za serikali zimezidiwa na wagonjwa, upungufu wa dawa na vifaa tiba,kukosa wataalamu au upungufu,vifaa tiba nk..

Hao hao ndio utakuta wanapinga hata ujenzi mpya unaendelea , watakwambia majengo sio huduma sasa sijui huduma zitafanyika chini ya miti au vipi..

Rais anapambana kutatua upungufu ambapo zaidi ya wahudumu wa Afya 15,000 wanaingia kazini mwesi huu,ikumbukwe Miaka ya hapo kuna watu waliokuwa hawaajiri kwa visingizio vya kujenga sgr and such nonsense..
 
V8 ya mwigulu ambayo ingeweza kununua vifaa Kibao vya maabara, napo lawama kwa nyerere.
Nyerere angetuachia mfumo wa demokrasia, ingekuwa rahisi kumdhibiti huyo Mwigulu na wenzake. Lakini Nyerere alikataa demokrasia.
 
Fikiria ni Mara ngapi Ummy Mwalimu amepiga ngonjera bungeni juu ya bima ya afya kwa wote!. Utasikia bunge lijalo serikali italeta mswada wa bima ya afya kwa wote; bunge likianza maigizo ni yaleyale ya bunge lijalo serikali italeta mswada wa bima ya afya kwa wote!.

Kwa hiyo, kwa hiyo, kwa hiyo (narudia,kwa hiyo) kinacholeta shida katika nchi hii hata katika sekta ya afya sio wahudumu/ wataalamu wa afya bali siasa imeharibu kila kitu. Tunao madakatari wenye weledi na utaalamu wa kiwango cha kustahili lakini hawahusishwi katika mipango na maamuzi katika sekta ya afya bali maamuzi yanatolewa na mtu ambae hata hana utaalamu wowote kwenye sekta ya afya.

Madakatari na wahudumu wengine wa sekta ya afya wanafanya kazi kubwa Sana ya kututibu sisi ila kikwazo kipo kwa wanasiasa ambao wanasema bungeni hawaendi kubeba zege bali kuchanganya maneno tu yawe ya kweli au ya uongo (nikimrejea Augustino Lyatonga Mrema).

Sisi tunaambiwa elimu bure; haya tafuteni watoto wa wanasiasa Kama mtawakuta kwenye hizo zinazoitwa elimu bure Kama sio mtawakuta Feza boys/girls, Casmiri, Marian boys and girls. Haya, tuendelee kushangilia elimu bure wakati darasani Mwalimu hawezi kupata nafasi ya kudhibiti wanafunzi wapiga kelele waliopo pale backbench.

Matatizo ya nchi hii yanaanzishwa na kusababishwa na wanasiasa forehence no room of blaming civil servants unless proved viz scientific research.
 
Back
Top Bottom