Nakodisha shamba kwa wajasiriamali wadogo wanotaka kujaribu Vitunguu

Nakodisha shamba kwa wajasiriamali wadogo wanotaka kujaribu Vitunguu

Nyamgluu

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
3,160
Reaction score
1,726
Habari wakuu, wajenga Taifa na wachukuia mafisadi na ufisadi.

Kutokana na mipangilio yangu ya kikazi nimeamua kutokulima vitunguu kwenye shamba langu la Ruaha Mbuyuni mwaka huu. Nina eka 50 kandokando ya mto ruaha, ila ambazo nilishapanda vitunguu na kuvuna mwaka juzi na jana ni ekari 15 hivi. Kwa maana hio ni kwamba hizo eka 15 zinamiundo mbinu tayari ya upandaji vitunguu na hivyo kumpunguzia yeyote gharama za maandalizi ya shamba kama ambavyo ataamua kuanza shamba jipya kabisa.

Gharama za kukodisha eka 1 ya shamba ni shillingi laki 2 na nusu (Ths 250,000/=) hii gharama ni pamoja na kutumia machine yangu ya kumwagilia ambapo kama watumiaji ni zaidi ya mmoja basi umwagiliaji ni wa zamu.

Kwa wale wageni wa hii kazi mtaji unaohitajika kwa eka moja kuanzia ununuzi wa mbegu,mbolea,palizi,mafuta ya kumwagilia na uvunaji ni 1,700,000/= mpaka 2,000,000/=.

Na kama kila kitu kikifanywa kwa usahihi na mother nature na mwenyezi Mungu asiwe kagadhabika na chochote unao uwezo wa kutoa gunia 60 mpaka 80.

Mimi sitalima kipindi hichi kwasababu nataka nielekeze nguvu zangu kwenye shamba jingine na sababu sina uwezo wa kusimamia sehemu kadhaa effectively nikaona bora nikodishe hili lingine aidha lote au kwa vipande vipande.

Natanguliza shukrani wadau.

ANGALIZO: Ukitaka mafanikio kwenye kilimo, usimamizi wako binafsi wewe mtoa hela ni muhimu sana. LABDA uwe na bahati ndogo kama punje ya mchanga bahari kumpata ndugu au mtu mwaminifu na mwenye usimamizi maridadi wa mali zako. Hivyo zingatia hilo.
 
Tatizo tupo mbali mzee na usimamizi wa remote control ni hatari hatari!
 
Habari wakuu, wajenga Taifa na wachukuia mafisadi na ufisadi.

Kutokana na mipangilio yangu ya kikazi nimeamua kutokulima vitunguu kwenye shamba langu la Ruaha Mbuyuni mwaka huu. Nina eka 50 kandokando ya mto ruaha, ila ambazo nilishapanda vitunguu na kuvuna mwaka juzi na jana ni ekari 15 hivi. Kwa maana hio ni kwamba hizo eka 15 zinamiundo mbinu tayari ya upandaji vitunguu na hivyo kumpunguzia yeyote gharama za maandalizi ya shamba kama ambavyo ataamua kuanza shamba jipya kabisa.

Gharama za kukodisha eka 1 ya shamba ni shillingi laki 2 na nusu (Ths 250,000/=) hii gharama ni pamoja na kutumia machine yangu ya kumwagilia ambapo kama watumiaji ni zaidi ya mmoja basi umwagiliaji ni wa zamu.

Kwa wale wageni wa hii kazi mtaji unaohitajika kwa eka moja kuanzia ununuzi wa mbegu,mbolea,palizi,mafuta ya kumwagilia na uvunaji ni 1,700,000/= mpaka 2,000,000/=.

Na kama kila kitu kikifanywa kwa usahihi na mother nature na mwenyezi Mungu asiwe kagadhabika na chochote unao uwezo wa kutoa gunia 60 mpaka 80.

Mimi sitalima kipindi hichi kwasababu nataka nielekeze nguvu zangu kwenye shamba jingine na sababu sina uwezo wa kusimamia sehemu kadhaa effectively nikaona bora nikodishe hili lingine aidha lote au kwa vipande vipande.

Natanguliza shukrani wadau.

ANGALIZO: Ukitaka mafanikio kwenye kilimo, usimamizi wako binafsi wewe mtoa hela ni muhimu sana. LABDA uwe na bahati ndogo kama punje ya mchanga bahari kumpata ndugu au mtu mwaminifu na mwenye usimamizi maridadi wa mali zako. Hivyo zingatia hilo.

Ntakutafuta mkuu
 
Habari wakuu, wajenga Taifa na wachukuia mafisadi na ufisadi.

Kutokana na mipangilio yangu ya kikazi nimeamua kutokulima vitunguu kwenye shamba langu la Ruaha Mbuyuni mwaka huu. Nina eka 50 kandokando ya mto ruaha, ila ambazo nilishapanda vitunguu na kuvuna mwaka juzi na jana ni ekari 15 hivi. Kwa maana hio ni kwamba hizo eka 15 zinamiundo mbinu tayari ya upandaji vitunguu na hivyo kumpunguzia yeyote gharama za maandalizi ya shamba kama ambavyo ataamua kuanza shamba jipya kabisa.

Gharama za kukodisha eka 1 ya shamba ni shillingi laki 2 na nusu (Ths 250,000/=) hii gharama ni pamoja na kutumia machine yangu ya kumwagilia ambapo kama watumiaji ni zaidi ya mmoja basi umwagiliaji ni wa zamu.

Kwa wale wageni wa hii kazi mtaji unaohitajika kwa eka moja kuanzia ununuzi wa mbegu,mbolea,palizi,mafuta ya kumwagilia na uvunaji ni 1,700,000/= mpaka 2,000,000/=.

Na kama kila kitu kikifanywa kwa usahihi na mother nature na mwenyezi Mungu asiwe kagadhabika na chochote unao uwezo wa kutoa gunia 60 mpaka 80.

Mimi sitalima kipindi hichi kwasababu nataka nielekeze nguvu zangu kwenye shamba jingine na sababu sina uwezo wa kusimamia sehemu kadhaa effectively nikaona bora nikodishe hili lingine aidha lote au kwa vipande vipande.

Natanguliza shukrani wadau.

ANGALIZO: Ukitaka mafanikio kwenye kilimo, usimamizi wako binafsi wewe mtoa hela ni muhimu sana. LABDA uwe na bahati ndogo kama punje ya mchanga bahari kumpata ndugu au mtu mwaminifu na mwenye usimamizi maridadi wa mali zako. Hivyo zingatia hilo.
Makadirio ya faida.. kwa anaejituma?!
 
Mkuu hivi mwezi wa pili hadi wa sita bei huwa imesimamaje?

Mkuu mwaka jana bei ya ruaha mbuyuni mwezi wa 4 na wa 5 ilifika laki 2 kwa gunia mwaka huu ilikua elfu 90 mpaka laki.
Kilimo tanzania ni kama kamali flani hivi.
 
80*80000= 6400000.
eka moja unayokodi kwa laki mbili unavuna milioni sita na nusu? haya maajabu
 
heka moja uvune gunia 80?? maajabu ya musa
Mkuu unahaki kuona kuwa haya ni maajabu ya Musa na ndivyo wote tunavyostaajabu tunaposikia jambo kubwa kwa mara ya kwanza. Hata mimi niliwahi kukataa niliposoma humu JF kuwa aina mpya ya michungwa umri wa miaka 3 inazaa machungwa 4000. Sijawahi kuona nilibisha sana! Kikubwa kwa hili la vitunguu usiwe mgumu wa moyo kuamini kwa kuwa kitu hicho ni kawaida. Nikupe mahesabu kidogo uweze kupata picha.

Mkuu kwa vitunguu inawezekana hata kuvuka zaidi ya gunia 80 kwa eka! Ujue hawa wanaotoa data hizi huu ni wastani ambao wakulima wengi huwa wanaufikia lakini ukitumia mbegu bora na ufuate utaalamu kikamilifu inavyotakiwa lazima mtu apande juu zaidi ya hapo. Naomba mkuu utofautishe uzaaji wa mazao ya nafaka na mazao ya mizizi! Mavuno ya mazao yenye uzazi wa aridhini kama vitunguu, viazi vitamu, viazi mviringo, mihogo n.k kwa kawaida huwa yako juu sana.

Eka moja ni mita mraba 4000, eka za kienyeji za hatua 70 kwa 70 hazifikii hapo (ekari za kienyeji hizi ni kama theluthi mbili ya eka halisi). Sasa hizi eka za kienyeji ndiyo hizo wanasema zinatoka gunia 80.

Vitunguu vinavyopandwa kwa umbali wa sm 10 kwa sm 10 kama kweli vitazingatiwa vipimo hivyo vitavunwa vitunguu 100 kwenye kila mita mraba moja yaani mita 1 upana kwa 1 moja urefu.

Mita moja ya mraba unatoa vitunguu 100 punguza asilimia 10 vitakufa au kuwa dhaifu tunabakia na vitunguu 90 kwa kila mita mraba moja!

Siyo eneo lote mita mraba 4000 zitapandwa, punguza asilimia 15 kwa ajili ya mifereji ya umwagiliaji na matuta. Eneo halisi litakalopandwa ni mita mraba 3400.

Idadi ya vitunguu shamba zima = mita mraba 3400 x vitunguu 90 kwa kila mita mraba = Idadi ya vitunguu shamba zima 306,000

Je debe moja vinaingia vitunguu vilivyostawishwa vema vingapi?
Je gunia moja hujazwa vitunguu debe ngapi?

Debe moja linaweza kujazwa kwa vitunguu vilivyostawi vizuri 300 au chini ya hapo, lakini kwa mahesabu tuchukulie vitunguu 300!
Ukigawanya idadi ya vitunguu 306.000 kwa ekari moja kwa vitunguu 300 vinavyojaza debe = madebe ya vitunguu kwa eka moja ni 1,020.
Kama gunia moja ni debe 10 kutoka kwenye madebe 1,020 utatoa gunia 102! Haya ni mavuno kwa ekari ya mita mraba 4000.

Kwa makadirio haya utaona ni kweli kabisa kwamba inawezekana eka 1 ya kienyeji ya 70 kwa 70 kutoa gunia 80. Lakini inawezekana kutoa zaidi kwa kuwa nimeweka makadirio ya kujibana sana.


 
80*80000= 6400000.
eka moja unayokodi kwa laki mbili unavuna milioni sita na nusu? haya maajabu
Lakini usisahau kuwa eka moja hiyo unamimina gharama ya Millioni 2! Mkuu kipindi cha kugharimika pesa inatoka mpaka unapata kizunguzungu! Usiangalie upande mmoja tu pamoja na faida kubwa hiyo kunawanaopiga mieleka na kutoka kapa hukumbuka mil 2 walizopotezea kwenye udongo! Milioni 2 kwa eka moja tu si mchezo usitazame hiyo bei ya kukodi shamba ndiyo kiwe kigezo cha kudhania kuwa ni maajabu! Kama umevutiwa tembelea maeneo ya kilimo hiki au kwenye masoko maarufu ya vitunguu utaujua ukweli!! Faida ni kubwa sana kwa wenye uzoefu lakini pia mieleka hupigwa sana na wanaoingia kichwa kichwa bila kujifunza utaalamu wake.
 
Mkuu mwaka jana bei ya ruaha mbuyuni mwezi wa 4 na wa 5 ilifika laki 2 kwa gunia mwaka huu ilikua elfu 90 mpaka laki.
Kilimo tanzania ni kama kamali flani hivi.
Ujanja ni kuwa ndani ya gemu miaka yote mibaya na mizuri, haiwezi kupita miaka 3 mfululizo bila kukutana na bingo. Mwaka wa bei nzuri huvutia watu wengi kuingia kwenye gemu, mwaka unaofuata kunakuwa na mafuriko ya mzigo bei inakata, watu wanakata mitaji wengine wanaaapa na kusema kilimo hiki kinamajini wanajitoa, mwaka unaofuata wakulima wanakuwa wachache sana vitunguu vinakuwa adimu bei inalipuka tena! Mzunguko ni hivyo hivyo miaka nenda rudi kuanzia tanzania, india hadi pakistani! Wavumilivu na wanaokaa sana kwenye gemu ndiyo hutoka, siyo wale wanaosubiri hadi wasikie sauti nzuri ya muziki ndiyo wanaingia!
 
ni biashara nzuri
Haswaa na ndiyo ingeinua walalahoi kwa wingi sana! Haya ndiyo maeneo wanasiasa wangewekeza nguvu kupanua maeneo ya umwagiliaji, kujenga miundombinu mbali mbali, kutoa mikopo kwa wakulima na huduma za utafiti na ushauri n.k. Mkuu Nyamgluu naomba utujuze iwapo mkono wa serikali uko huko kukuza kilimo hiki!? Ningetarajiwa kuwe na kituo cha uhakika kinachotoa ushauri kwa wakulima huko, ninatarajia wakulima wanafuatiliwa kwa ukaribu na wataalamu, ninatarajia kuna shughuri mbali mbali za utafiti zinafanyika huko ili kuja na mbegu bora na teknolojia bora kukuza zao hili huko, ninatarajia kuna maduka ya uhakika yanayouza mbegu bora za vitunguu huko! Hilo eneo ni maarufu kwa kilimo cha vitunguu lakini hali ikoje au ndiyo ile ile ya kuku wa kienyeji kujitafutia chakula mwenyewe mfugaji anamkumbuka siku akija mgeni tu. Au Serikari wao wanawasubiri mkipakia mzigo kwenye Fuso ndiyo wanafunga barabara kudai ushuru tu? Mkuu Nyamgluu na wengine mnaotoka kwenye maeneo maarufu ya kilimo hiki hebu fungukeni hapa!!
 
Nimevutiwa na kilimo cha vitunguu, nina swali direct kwa Mr. Kubota au mtaalamu yeyote.
Nina ekari mbili za shamba maeneo ya Vianzi mpakani mwa Dar na Pwani, kwa kawaida nimekuwa nikilima mpunga na matikiti maji kwa kubadisha nikivuna mpunga na mpunga umekuwa nikivuna mpaka gunia kumi. Ni eneo lenye ukaribu wa maji kwa ajili ya kumwagilia.
Swali- jee naweza kuutumia msimu huu kupanda vitunguu? usimamizi mwenyewe naweza kusimamia lakini jee naweza kupata utaalamu na ushauri ili kufanikisha hili ?
natanguliza shukran
 
Back
Top Bottom