Nyamgluu
JF-Expert Member
- Mar 10, 2006
- 3,160
- 1,726
Habari wakuu, wajenga Taifa na wachukuia mafisadi na ufisadi.
Kutokana na mipangilio yangu ya kikazi nimeamua kutokulima vitunguu kwenye shamba langu la Ruaha Mbuyuni mwaka huu. Nina eka 50 kandokando ya mto ruaha, ila ambazo nilishapanda vitunguu na kuvuna mwaka juzi na jana ni ekari 15 hivi. Kwa maana hio ni kwamba hizo eka 15 zinamiundo mbinu tayari ya upandaji vitunguu na hivyo kumpunguzia yeyote gharama za maandalizi ya shamba kama ambavyo ataamua kuanza shamba jipya kabisa.
Gharama za kukodisha eka 1 ya shamba ni shillingi laki 2 na nusu (Ths 250,000/=) hii gharama ni pamoja na kutumia machine yangu ya kumwagilia ambapo kama watumiaji ni zaidi ya mmoja basi umwagiliaji ni wa zamu.
Kwa wale wageni wa hii kazi mtaji unaohitajika kwa eka moja kuanzia ununuzi wa mbegu,mbolea,palizi,mafuta ya kumwagilia na uvunaji ni 1,700,000/= mpaka 2,000,000/=.
Na kama kila kitu kikifanywa kwa usahihi na mother nature na mwenyezi Mungu asiwe kagadhabika na chochote unao uwezo wa kutoa gunia 60 mpaka 80.
Mimi sitalima kipindi hichi kwasababu nataka nielekeze nguvu zangu kwenye shamba jingine na sababu sina uwezo wa kusimamia sehemu kadhaa effectively nikaona bora nikodishe hili lingine aidha lote au kwa vipande vipande.
Natanguliza shukrani wadau.
ANGALIZO: Ukitaka mafanikio kwenye kilimo, usimamizi wako binafsi wewe mtoa hela ni muhimu sana. LABDA uwe na bahati ndogo kama punje ya mchanga bahari kumpata ndugu au mtu mwaminifu na mwenye usimamizi maridadi wa mali zako. Hivyo zingatia hilo.
Kutokana na mipangilio yangu ya kikazi nimeamua kutokulima vitunguu kwenye shamba langu la Ruaha Mbuyuni mwaka huu. Nina eka 50 kandokando ya mto ruaha, ila ambazo nilishapanda vitunguu na kuvuna mwaka juzi na jana ni ekari 15 hivi. Kwa maana hio ni kwamba hizo eka 15 zinamiundo mbinu tayari ya upandaji vitunguu na hivyo kumpunguzia yeyote gharama za maandalizi ya shamba kama ambavyo ataamua kuanza shamba jipya kabisa.
Gharama za kukodisha eka 1 ya shamba ni shillingi laki 2 na nusu (Ths 250,000/=) hii gharama ni pamoja na kutumia machine yangu ya kumwagilia ambapo kama watumiaji ni zaidi ya mmoja basi umwagiliaji ni wa zamu.
Kwa wale wageni wa hii kazi mtaji unaohitajika kwa eka moja kuanzia ununuzi wa mbegu,mbolea,palizi,mafuta ya kumwagilia na uvunaji ni 1,700,000/= mpaka 2,000,000/=.
Na kama kila kitu kikifanywa kwa usahihi na mother nature na mwenyezi Mungu asiwe kagadhabika na chochote unao uwezo wa kutoa gunia 60 mpaka 80.
Mimi sitalima kipindi hichi kwasababu nataka nielekeze nguvu zangu kwenye shamba jingine na sababu sina uwezo wa kusimamia sehemu kadhaa effectively nikaona bora nikodishe hili lingine aidha lote au kwa vipande vipande.
Natanguliza shukrani wadau.
ANGALIZO: Ukitaka mafanikio kwenye kilimo, usimamizi wako binafsi wewe mtoa hela ni muhimu sana. LABDA uwe na bahati ndogo kama punje ya mchanga bahari kumpata ndugu au mtu mwaminifu na mwenye usimamizi maridadi wa mali zako. Hivyo zingatia hilo.