Nakodisha shamba kwa wajasiriamali wadogo wanotaka kujaribu Vitunguu

Kipindi cha mavuno gunia ni 70,000 mpaka 120,000.
Na unaweza vuna gunia 60 mpaka 80. Piga hesabu mkuu.

Hiyo bei niya kuuzia shambani ama niyakuuzia sokoni yaani baada ya kusafirisha
 

Good analysis na nimeipenda big up mkuu
 
Mkuu Moudyjr ngoja nianze na wengine wataendeleza. Nianze na mpunga japo sicho ulichouliza, mbona mavuno yako ni madogo kiasi hicho? Hasa kama upatikanaji wa maji si kikwazo hata kama ungepata gunia 20 ingekuwa bado hujafanya kitu! Kama kikwazo ni maji hakuna jinsi. Kwa uzoefu wangu kwa ukanda wa pwani ninawasiwasi kwa tarehe hizi kwa kilimo cha vitunguu tunakwenda kwenye kipindi cha joto kali! Kipindi hicho huwa kuna tatizo la wadudu waitwao THRIPS, itakubidi ujidhatiti sana kwa sumu! Ni kipindi kisichofaa kwa mkulima anaeanza mara ya kwanza kwa sababu kunahatari ukipiga mweleka ukakichukia kilimo hiki jumla. Kama utapenda unaweza kupanda eneo dogo tu la kupima upepo ili kama utaona mambo yanakwenda vema msimu ujao ndiyo upige full throttle! Uzoefu wangu kwa maeneo ya Morogoro kilimo cha vitunguu miezi hii huwa ni cha mbinde sana shauri ya wadudu na ukame! Kama unaweza panga mzunguko wako ili uvune mpunga mapema kuruhusu upande vitunguu mwezi June. Kwa maana hiyo unatakiwa uweke kitalu mwezi mwezi April katikati au May mwanzoni. Kitunguu kinapenda majira ya baridi. Ninakuhakikishia utaweza kupata utaalamu na kufanikisha hili ili mradi tu kama JF itakuwa iko hewani!
 
Kama una maji ya kisima cha kuchimba maeneo ya kimanzichana kuna stawi vi2nguu? Au lazima iwe kando ya mto? Kwa huko Ruaha wanyama wakali vp?
 
Thanks so much mkuu Kubota umenipa mwanga, kwa maelekezo yako basi wacha nitumie mda huu kabla ya msimu wa mpunga kwa ajili ya kulima matikiti maji ingawa nayo bado utaalamu ni hafifu.
Kwa mtazamo wangu nadhani nitahitaji ushauri wa karibu juu ya hilo, nitaku-pm ili tuone namna gani tunaweza fanikisha ndoto yangu ya kilimo chenye manufaa.

Thanks.
 
Kama una maji ya kisima cha kuchimba maeneo ya kimanzichana kuna stawi vi2nguu? Au lazima iwe kando ya mto? Kwa huko Ruaha wanyama wakali vp?
Mkoa wa Tabora kuna eneo maarufu sana kwa kilimo cha vitunguu linaitwa Puge, kule hakuna mto bali ni kwa kutumia maji ya visima. Vitunguu husitawi vizuri sana kwenye umwagiliaji huo. Siyo lazima kulima kando ya mto. Angalia urahisi tu wa kuyapata maji maana huko Puge watu wanapiga mzegamzega wa maji shambani umbali wa kiwanja cha mpira cheza na pesa wewe, sijui kama wazaramo mtaweza. Kwi kwi kwiiii! Kuhusu wanyama pori wa Ruaha Mkuu Nyamgluu atatujuza.
 
Kama una maji ya kisima cha kuchimba maeneo ya kimanzichana kuna stawi vi2nguu? Au lazima iwe kando ya mto? Kwa huko Ruaha wanyama wakali vp?

Habari wakuu, nilikua AWOL kidogo nabishana na maisha. Nimetoka shamba leo kuku zangu 30 zimekufa, kondoo 1 nae kafa wengine 9 wamekimbia. Hehehe ALUTA CONTINUA mpaka kieleweke.
King Kong III sasa wewe tena mazee unaogopa wanyama wakali tena, trust me na sura kama hio watakakimbia wenyewe! Hehehe.
Aisee ruaha mbuyuni hakuna wanyama wakali wakutisha. Kuna mamba kwenye mto lakini ndani ya miaka 15 alibebwa mtoto 1 nae mamba alitaftwa akauliwa. Tembo wapo wanakatiza kwa mbali lakini hawasumbui binadamu. Sema nyani ndugu ndio vita ila hawapendelie sana vitunguu, mimi walinisumbua sana kwenye migomba na mahindi, lakini nilivoleta mbwa ikawa safi.
 

Mkuu kubota mm nakaa sumawanga vijijini je hk kilimo kinafaa kunaa maeneo yenyenye maji msimu wote

Je naweza kupata vijan wa kusaidiana kazi yaani kama wattaaalamu wangu
pia labour sina tatizo
 
Mkuu kubota mm nakaa sumawanga vijijini je hk kilimo kinafaa kunaa maeneo yenyenye maji msimu wote

Je naweza kupata vijan wa kusaidiana kazi yaani kama wattaaalamu wangu
pia labour sina tatizo
Mkuu kitunguu sumbawanga kinastawi bila shaka. Ili mradi maji ya umwagiliaji unayo. Unaweza kupata vijana wa kusaidiana kazi maana wengi wanatafuta ajira. Kuhusu vijana wataalamu kama umepania kulima eneo la kutosha nakushauri uende maeneo yanayolima kilimo hiki ukachukue kijana mzoefu ili akakuhudumie shambani kwako hiyo itatoa fursa kwa vijana wako wa huko wapate utaalamu kwa huyu mzoefu ili akiondoka uendelee kivyako.
 

Mkuu Nyamgluu,

Nikitaka kununua na sio kukodi shamba yanapatikana kwa bei gani?
 
Last edited by a moderator:
Unahitaji roho ya Silver kuwa Mkulima.... unawekeza hizo pesa kisha ukalia hadi machozi yakauke.... na ukabakia kujisemea bora ningenunua Ng'ombe niwe nakunywa maziwa kila siku.....

Kilimo Bongo...!
 
tuko pamoja mkuu

mkuu kubota,inachukua muda gan tangu kuweka mbegu kwenye vitalu kupanda mpaka kuvuna?ma vip vipind vya umwagiliaj vikoje?yaan unamwagilia mara ngapi kwa juma ama mwezi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…