Nakubaliana na mchungaji Msigwa kuwa level of thinking Tanzania imeshuka

Nakubaliana na mchungaji Msigwa kuwa level of thinking Tanzania imeshuka

UMEONGEA vyema ndugu...kuna tatizo humu jf kama viongozi wa jf wasipofanya marekebisho mapema kuna hatihati ya hii platform kuja kufa japo siombei iwe hivyo. Kuna wadau wanaoleta mada fikirishi sana kiasi kwamba ukikaa chini ukaichambua ina mantiki ila ndio hivyo wengi wetu humu tunapenda mada za ngono,umbea n.k ndizo zinapewa kipaumbele sana ..kwa mfano leo Kuna member kaleta mada humu ikisema kwamba kwanini mkuu wa nchi(rais) kwenye mitandao ya kijamii hususan Twitter watu wana chuki naye hususan kwenye lile swala la kupigiwa kura mtandaoni la kukuza demokrasia ,watu wanahimizana wasimpigie.lakini ghafla ule uzi ulifutwa haraka sana . nikitafakari nakosa jibu sana. Alichoongea msigwa kina tafakarisha sana kwa kweli.
Na moderator wamekuwa a akili chafu sana za kuwa biased hii miaka ya karibuni.

Kitendo cha kuzuia mijadala fulani isifanyike tayari unaitoa hadhi hii platform ambayo mojawapo ya misingi yake ya asili ni kuzungumza wazi wazi bila kificho ili kutafuta muafaka.

Hapa hatutumii hasira wala nguvu katika kujenga hoja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Angeweza ku-think critically CHADEMA isingeserereka kwa huo mserereko! Kuna tofauti Kati ya muuza maneno ya ujanja ujanja na mtendaji mwenye maono na nia thabiti!
Mfano mwingine wa mamburula, nadhani hii pia inachamgiwa na udumavu wa akili unaosababishwa na lishe duni au utapia mlo...

Sent from my TECNO L9 Plus using JamiiForums mobile app
 
" You are going to come across people in your life who will say the right words at all the right times. But in the ends, it's always their actions you should judge with them by. It's actions not words that matter"
Yesu alitufundisha kuwa tuwasilikilize mafarisayo pamoja na walimu wengine lakini matendo yao tusiyafuate.... kwanini? Walichokuwa wanafundisha sicho walichokuwa wanakifanya. Hivyo basi, ukiona mtu anakushauri jambo zuri, hata kama ni chizi, msikilize na kamwe usitamani kujua yeye anafanya nini... baadhi waliumbwa kwa ajili ya kuwafundisha wengine ili wafike hatua fulani. Ndo mipango ya Mungu hiyo.

KUHUSU MADA HAPO JUU: Awali nikushukuru mwandishi, Mch. Msigwa kasema mambo mengi mazuri, ambayo sisi kama vijana tunapaswa kuyatafakari umakini. Binafsi sijayasikia wala kuangalia hayo mahojiano ila kunaweza kukawa na nadharia mbili katika kuchambua hoja zake kutokana na taarifa aliyoiandika mleta mada hapo juu.

Mosi: Mrengo anauwakilisha Mch. Msigwa binafsi, "critical thinking" katika siasa. Watu wengi tumekuwa na mihemko ya kisiasa hasa sisi vijana kwa kushawishiwa mambo ambayo pengine hatuelewi yana maslahi gani kwa taifa letu. Tunasikiliza maneno ya wanasiasa pasipo kupima nia na madhumuni yaliyo nyuma ya maneno yale kama ni kwa maslahi binafsi au ya taifa letu la Tanzania 🇹🇿.

Pili: Mrengo anauwakilisha Mch. Msigwa binafsi, "critical thinking" katika mambo ya uchumi na kijamii.

A. Licha ya kuwa siasa imekuwa ikiamua mambo mengi katika jamii, matokeo yake hujionesha wazi wazi katika nyanya nyingine ikiwamo uchumi wa nchi. Ni lazima sisi kama vijana, tuweze kuwa na uwezo mkubwa wa ubunifu ndani na nje ya Taifa letu ili kusudi kuchochea maendeleo yetu kiujumla.

B. Kufikiri kuliko sawasawa kunaweza kuleta mageuzi makubwa sana katika kufanya mapindizi ya viwanda kama walivyofanya vijana wa mataifa mengi duniani ambayo kwasasa yanakula matunda ya vijana wao. Hapa lazima tuibue teknolojia hizo hizo ambazo zipo kwa wenzetu lakini kwa kuzioanisha na mazingira yetu ili kutatua changamoto ambazo jamii yetu inakumbana nazo kwa sasa na kizazi kijacho. Na wakati huo huo watu binafsi, mashirika binafsi na ya kiserikali yawe yanatoa mchango wao katika kuwainua wabunifu hawa.

C. Pia, vijana tunapaswa kujua na kukataa kabisa wewe uishi maisha ya kuteseka na kizazi chako kiishi vivyo hivyo. Teseka wewe kwa nguvu zote hata kama ni kwa jasho na damu ili kizazi chako chote kiweze kuishi kwa furaha. Kwa mfano hali ya maisha ya sasa kweli ni ngumu sana, lakini ni lini hali ya maisha iliwahi kuwa rahisi kiasi hicho....??? Kwa mfano mimi kwa zaidi ya miongo miwili sasa nimekuwa nikisikia kila siku maisha ni magumu maisha ni magumu... hata sasa nawaambia wadogo zangu vivyo hivyo... hakuna wakati ambao maisha yaliwahi kuwa rahisi hata enzi za Yesu... tena Yeye alizaliwa kwenye zizi la ng'ome (tujifunze kupitia Yeye). Leo hii watoto wetu wanazaliwa katika zahanati na hospitali zilizo nchi nzima isipokuwa baadhi ya maeneo. "There is no gain without pain".

Ahsante
 
Wapo watu wa aina tofauti katika maisha, wapo waliozaliwa kujisimamia na wale waliozaliwa kusimamiwa. Watu hawa wana utofauti mkubwa sana katika kufikiri kwao na hata mitindo ya maisha yao.


Siyo wote wenye uwezo wa kudadavua hoja ngumu na hata wakati mwingine hoja nyepesi.

Kuna watu wanafikiria kufanya jambo, kuna watu wanafanya, na pia lipo kundi la watu ambao wao kazi yao ni kutazama tu mambo yakiwa yanatendeka.

Niseme tu ukweli humu jf kuna watu wana uelewa MKUBWA sana siyo siri.

Pamoja na yote lazima tufike hatua tukubali utofauti wa uwezo wa kufikiri wa kila mmoja. Mada za ajabu zinapewa kipao mbele kwasababu ni nyepesi na hazihitaji mtu kufikiria sana ndiyo maana wengi wapo huko, ila zile mada ambazo mtu unahitaji kufikiria sana zina wachache kwasababu watu hao pia siyo wengi.


Ni kweli asilimia kubwa ya sisi watanzania suala la kuhoji vitu kwa lengo la kuelewa au kujifunza ni utamaduni ambao wachache ndiyo wanao.

Jf ya sasa ni tofauti na ile iliyonisukuma mpaka kujiunga rasmi.

Kuna watu walikuwa wanatoa elimu kuhusu vitu mbalimbali muhimu sana katika maisha na wachangiaji walikuwa very bright katika kuhoji.
Umenena vyema sana kiongozi.

Naitazamia JF niliyokuwa naisoma sana kipindi cha < 2018 na JF ya 2019> Ni sehemu mbili tofauti sana na hii inaonesha kwamba kipindi cha 2019 > vijana wengi wameegemea sana kwenye siasa za uvyama sana kuliko mambo ya msingi ya kujadili.
Vijana wengi wanakwenda na upepo wa huyu kasema nini mara yule kasema nini mwisho wa siku wanaanza kulalamika kuwa hakuna ajira.
 
Kuna clip iko kwenye mitandao ikionyesha mahojiano aliyofanyiwa mchungu Msigwa na Darmpya tv, ambapo mchungaji Msigwa anasikika akiongelea swala la critical thinking.

Msigwa anasikika akisema, wakati wa Mwalimu, vijana wa chuo kikuu walikuwa na uhuru wa kusema chochote wawapo maeneo ya chuo na walikuwa na kinga ila kinga hiyo ilikuja ondolewa enzi za Mwinyi baada ya wanafunzi wa chuo kikuu wakati huo kumkosoa mzee Mwinyi.

Kwa maelezo yake, Msigwa anasema Mwalimu aliruhusu mijadala vyuo vikuu na kwamba vyuoni ni sehemu ambapo watu wana-think critically tofauti na sasa ambapo wanafunzi wa vyuo vikuu hawawezi hata kuuuliza maswali ya how,why, n.k.

Msigwa amesema wanafunzi hawa sio wa kulaumiwa kwani hata walimu wao nao hawa-think critically huku akitaja kutishwa kuwa ni moja ya sababu ya walimu wao kuwa hivyo.

Msigwa anahoji kama ma-proffesor wetu wanaka chini na kuumiza vichwa kuhusu hatima ya Tanzania yetu kiuchumi, n.k katika miaka 30 ijayo huku akitoltea mfano wa nchi kama Israel ambayo inauza "brain" duniani na wamarekani wanaowaza nishati mbadala ya mafuta kwa miaka 30 ijayo.

Kwa mfano, Msigwa anahoji tumejiandaa vipi kuacha kuitegema bandari kama chanzo cha mapato ikitokea miaka ya mbeleni zinabuniwa ndege kubwa zinazoweza kubeba mizigo mikubwa na kwa gharama nafuu kutokana na kukua kwa teknolojia akitolea mfano wa wamarekani wanaowaza/wanaobuni nishati mbadala ya mafuta ikitokea mafuta yanatoweka duniani.

Msigwa kaongea mengi yanayoeleza ni jinsi gani watanzania wa leo hatuwazi critically.

Binafsi naungana na Msigwa kwasababu moja kubwa: Watanzania wa leo hii sehemu kubwa ya mijadala yetu mitandaoni ni kujadili matukio, maandiko na kauli au matamshi ya watu maarufu (wanasiasa, wasanii, n.k)yanayopatikana mitandaoni na kwenye vyombo vya habari na sio kujadili au kubuni mambo yanaweza kuleta suluhu ya matatizo yetu kama nchi.

Kwa maneno mengine,tunatumua muda mwingi au niseme interest zetu ni kulalamikia matatizo tuliyonayo huku tukitumia muda mchache kuandika, kujadili na kupendekeza solution za matatizo yetu, tunasahau matukio yanakuja na kupita, wakati matatizo yetu yako pale pale huku watawala nao wakiwa hawana solution ya baadhi ya matatizo tuliyonayo.

Kama anavyosema Msigwa, kwa sasa hatuna mijadala sababu mojawapo likiwa ni uoga lakini pia kwa sasa level yetu ya ku-think critically imeshuka.

Kwenye mitandao kwa sasa, mtu aki- post habari kuhusu tukio fulani au kauli ya mwanasiasa fulani, watu wanakuwa interested sana kujadili ila mtu akija na idea kuhusu namna gani tunaweza kutatua tatizo fulani katika jamii na nchi kwa ujumla, mijadala huwa ni ya kiwango cha chini sana(wa kukosoa na kuungana mkono ni wachache mno).

Kwa mfano, hivi sasa watanzania tunatakiwa tuwe na mjadala utakaosaidia kupatikana kwa vyanzo vipya vya mapato, ila hilo alipo, badala yake tunalalamika kukamuliwa kodi huku TRA nao wakiwa wameishiwa ubunifu wa kupata vyanzo vipya vya mapato na matokeo sasa wanatuhumiwa kutoza kodi kubwa inayoua mitaji ya wafanyabiashara(hakuna mwenye solution juu ya vyanzo vipya vya mapato badala yake wote tunalalamika!)

Mimi naamini vyanzo vya mapato nchi bado viko vingi tu, tatizo ni watu kushindwa kukaa chini na kuumiza vichwa ikiwa ni pamoja na kushirikishi wananchi na wataalumu katika mijadala ya pamoja yenye lengo la kubuni vyanzo vipya vya mapato.

Hata mnapoona wasomi na wanaoitwa wataalamu wanakimbilia kwenye siasa, mjue kweli level of thinking imeshuka, hivyo wanashindwa kutumia elimu zao kujiongezea vipato halafu mkabaki mnategemea watu wa aina hiyo ndio wawaletee maendeleo.Kama mnaamini hivyo, mjue tu huko ni kujidanganya mchana kweupe.

Watanzania tubadilike, dunia inatuacha nyuma.
bado mnamwita mchungaji huyo mchumia tumbo???
 
Hakuna nchi isiyo katiba Labda Kama ujui nini maana ya katiba.
Hakuna nchi isiyo katiba Labda Kama ujui nini maana ya katiba.
Wewe ndie hujui uingereza haina katiba inaendeshwa kwa sheria tu waliona katiba ni ujinga mtupu sharia kwao ndio supreme mfano uhuru wa kujieleza kwao hawahitaji kaandika kwenye katiba ni kitu koko obvious jieleze utakavyp ila ukitukana mtu utakumbana na sheria mahakamani ya kutukana mtu
Ukibagia mtu kwa jina is au dini kwenye ajira utakumbana.na sheria ya ajira uliyemwonea atakuburuza mahakamani

Katiba ni useless tool

Utawala wa sheria ndio kila kitu
 
naunga mkono hoja kuhusu watanzania wengi kushughulika na vitu vidogo. mfano wangu upo humuhumu jf kwa 'great thinkers', nilikuja na thread fikirishi kabisa inayohusu haja ya kuajiri walimu wa kike kuanzia miaka 35 badala ya hii 18,19,20....25. mada ilichangiwa na wadau wachache sana huku nikipata kiji'like' kimoja tu. katika hao wachacheee waliochangia, asilimia 98 waliishia kunitukana tu....tena wengine matusi ya nguoni. 😵😵

ajabu ni kuwa threads za kidukulilo za kumiliki visiwa sehemu mbali mbali duniani na magari ya kifahari zaidi ya ronaldo na messi zinapata ma'likes' na 'replies' nyingi ajabu.

kitu kingine nilichogundua humu ambacho kinaendana na ulichoandika mtoa mada ni kuwa hata humu, kwa ma'great thinkers', mada huangaliwa kwanza imetoka kwa nani ili ajibiwe au isomwe......kama hauna jina humu si ajabu mada zako hata kufunguliwa zisifunguliwe. ni dalili tosha ya ulichokisema.....tatizo la kukosa critical thinking limetuvamia hadi humu.
Very true
 
Wewe ndie hujui uingereza haina katiba inaendeshwa kwa sheria tu waliona katiba ni ujinga mtupu sharia kwao ndio supreme mfano uhuru wa kujieleza kwao hawahitaji kaandika kwenye katiba ni kitu koko obvious jieleze utakavyp ila ukitukana mtu utakumbana na sheria mahakamani ya kutukana mtu
Ukibagia mtu kwa jina is au dini kwenye ajira utakumbana.na sheria ya ajira uliyemwonea atakuburuza mahakamani

Katiba ni useless tool

Utawala wa sheria ndio kila kUnaz

Wewe ndie hujui uingereza haina katiba inaendeshwa kwa sheria tu waliona katiba ni ujinga mtupu sharia kwao ndio supreme mfano uhuru wa kujieleza kwao hawahitaji kaandika kwenye katiba ni kitu koko obvious jieleze utakavyp ila ukitukana mtu utakumbana na sheria mahakamani ya kutukana mtu
Ukibagia mtu kwa jina is au dini kwenye ajira utakumbana.na sheria ya ajira uliyemwonea atakuburuza mahakamani

Katiba ni useless tool

Utawala wa sheria ndio kila kitu
Unazungumzia kitu kimoja sheria ndio katiba, sheria ipo ndani ya katiba
 
Lzm ipungue sababu ya ujamaa.
Wafanye wawe masikini ili uwatawale watu wakishauwa masikini thinking yao ni lzm ipungue sababu awatowaza chochote zaidi ya jinsi ya kumudu shibe.
 
Unazungumzia kitu kimoja sheria ndio katiba, sheria ipo ndani ya katiba
Ni repeation kwa nini urudie kuandika kitu kike kile mara mbili uandike katiba halafu uandike sheria?wastage of time and money

Uingereza wako sahihi kukataa kuwa na katiba na kutaka tu utawala wa sheria yaani rule of law kutegemea sheria peke yake sio tabu la kibwege linaloitwa katiba
 
Hakuna serikali iliyifanikiwa kuwafanya wanadamu kuwa marobot kama hii ya bwana Jiwe,hebu fikiria eti wanatoza kodi YouTube channels za Tanzania ila za Kenya,Us nk hawazigusi
 
Hakuna serikali iliyifanikiwa kuwafanya wanadamu kuwa marobot kama hii ya bwana Jiwe,hebu fikiria eti wanatoza kodi YouTube channels za Tanzania ila za Kenya,Us nk hawazigusi
Kenya wanachaji pia zao lazima uwe na leseni
 
Ni repeation kwa nini urudie kuandika kitu kike kile mara mbili uandike katiba halafu uandike sheria?wastage of time and money

Uingereza wako sahihi kukataa kuwa na katiba na kutaka tu utawala wa sheria yaani rule of law kutegemea sheria peke yake sio tabu la kibwege linaloitwa katiba
Sisi tuna vyote na hatuvifuati hapa ttzo Ni nn.Au sababu wao ni civilized
 
Sisi tuna vyote na hatuvifuati hapa ttzo Ni nn.Au sababu wao ni civilized
Tatizo sisi rule of law hatujali wenzetu wanaheshimi sana sheria miliki chochote
Sisi huku katiba haizingatiwi wala sheria

Mfano katiba inasema kila binadamu wanastahili heshima na kuthaminiwa you wake unakuta wanasiasa anaporomoshea matusi mwanasiasa mwenzie walisema ohh katiba ina kipengele cha uhuru wa kujieleza!! Anasahau kuwa koko kipengele kinachokataza kumvunjia mtu heshima na uti wake

Na aliyetukwana haendi mahakamani kushtaki kutumia sheria ya kudhalilishwa kinyume na sheria!!!

Kutojali utawala wa sheria ni kama ndio sababu kubwa ndio maana uingereza ndio nchi inaongoza duniani kwa kujali utawala wa sheria
 
Sasa kwa nini tunachaji za kwetu tu lakini za nchi nyingine au za anonymous hatuzichaji wala hatuna ufumbuzi wa namna gani zichajiwe
YouTube walianzisha YouTube za nchi kujiongezea mapato mfano wewe ukiingia youtube unaingia YouTube ya Tanzania ambayo Tanzania ndie mumililiki na mlipa fees YouTube Tanzania kupeleka YouTube head office ndie owner
Za nje owner ni nchi nyingine e.g. YouTube Kenya huwezi taka TCRA iingilie youtube Kenya au zimbabw nk
 
Kuna clip iko kwenye mitandao ikionyesha mahojiano aliyofanyiwa mchungu Msigwa na Darmpya tv, ambapo mchungaji Msigwa anasikika akiongelea swala la critical thinking.

Msigwa anasikika akisema, wakati wa Mwalimu, vijana wa chuo kikuu walikuwa na uhuru wa kusema chochote wawapo maeneo ya chuo na walikuwa na kinga ila kinga hiyo ilikuja ondolewa enzi za Mwinyi baada ya wanafunzi wa chuo kikuu wakati huo kumkosoa mzee Mwinyi.

Kwa maelezo yake, Msigwa anasema Mwalimu aliruhusu mijadala vyuo vikuu na kwamba vyuoni ni sehemu ambapo watu wana-think critically tofauti na sasa ambapo wanafunzi wa vyuo vikuu hawawezi hata kuuuliza maswali ya how,why, n.k.

Msigwa amesema wanafunzi hawa sio wa kulaumiwa kwani hata walimu wao nao hawa-think critically huku akitaja kutishwa kuwa ni moja ya sababu ya walimu wao kuwa hivyo.

Msigwa anahoji kama ma-proffesor wetu wanaka chini na kuumiza vichwa kuhusu hatima ya Tanzania yetu kiuchumi, n.k katika miaka 30 ijayo huku akitoltea mfano wa nchi kama Israel ambayo inauza "brain" duniani na wamarekani wanaowaza nishati mbadala ya mafuta kwa miaka 30 ijayo.

Kwa mfano, Msigwa anahoji tumejiandaa vipi kuacha kuitegema bandari kama chanzo cha mapato ikitokea miaka ya mbeleni zinabuniwa ndege kubwa zinazoweza kubeba mizigo mikubwa na kwa gharama nafuu kutokana na kukua kwa teknolojia akitolea mfano wa wamarekani wanaowaza/wanaobuni nishati mbadala ya mafuta ikitokea mafuta yanatoweka duniani.

Msigwa kaongea mengi yanayoeleza ni jinsi gani watanzania wa leo hatuwazi critically.

Binafsi naungana na Msigwa kwasababu moja kubwa: Watanzania wa leo hii sehemu kubwa ya mijadala yetu mitandaoni ni kujadili matukio, maandiko na kauli au matamshi ya watu maarufu (wanasiasa, wasanii, n.k)yanayopatikana mitandaoni na kwenye vyombo vya habari na sio kujadili au kubuni mambo yanaweza kuleta suluhu ya matatizo yetu kama nchi.

Kwa maneno mengine,tunatumua muda mwingi au niseme interest zetu ni kulalamikia matatizo tuliyonayo huku tukitumia muda mchache kuandika, kujadili na kupendekeza solution za matatizo yetu, tunasahau matukio yanakuja na kupita, wakati matatizo yetu yako pale pale huku watawala nao wakiwa hawana solution ya baadhi ya matatizo tuliyonayo.

Kama anavyosema Msigwa, kwa sasa hatuna mijadala sababu mojawapo likiwa ni uoga lakini pia kwa sasa level yetu ya ku-think critically imeshuka.

Kwenye mitandao kwa sasa, mtu aki- post habari kuhusu tukio fulani au kauli ya mwanasiasa fulani, watu wanakuwa interested sana kujadili ila mtu akija na idea kuhusu namna gani tunaweza kutatua tatizo fulani katika jamii na nchi kwa ujumla, mijadala huwa ni ya kiwango cha chini sana(wa kukosoa na kuungana mkono ni wachache mno).

Kwa mfano, hivi sasa watanzania tunatakiwa tuwe na mjadala utakaosaidia kupatikana kwa vyanzo vipya vya mapato, ila hilo alipo, badala yake tunalalamika kukamuliwa kodi huku TRA nao wakiwa wameishiwa ubunifu wa kupata vyanzo vipya vya mapato na matokeo sasa wanatuhumiwa kutoza kodi kubwa inayoua mitaji ya wafanyabiashara(hakuna mwenye solution juu ya vyanzo vipya vya mapato badala yake wote tunalalamika!)

Mimi naamini vyanzo vya mapato nchi bado viko vingi tu, tatizo ni watu kushindwa kukaa chini na kuumiza vichwa ikiwa ni pamoja na kushirikishi wananchi na wataalumu katika mijadala ya pamoja yenye lengo la kubuni vyanzo vipya vya mapato.

Hata mnapoona wasomi na wanaoitwa wataalamu wanakimbilia kwenye siasa, mjue kweli level of thinking imeshuka, hivyo wanashindwa kutumia elimu zao kujiongezea vipato halafu mkabaki mnategemea watu wa aina hiyo ndio wawaletee maendeleo.Kama mnaamini hivyo, mjue tu huko ni kujidanganya mchana kweupe.

Watanzania tubadilike, dunia inatuacha nyuma.
Chadema wangekuwa wanathink critically wasingekuwa hivi walivyo kumbukeni maono na mtazamo wa Dr W Slaa. Rest in Peace Chadema
 
Back
Top Bottom