Nakubaliana na Rais Mwinyi kwamba Manaibu Waziri wanaongeza gharama za Serikali naamini Rais Magufuli atafanya hivyo pia!

Nakubaliana na Rais Mwinyi kwamba Manaibu Waziri wanaongeza gharama za Serikali naamini Rais Magufuli atafanya hivyo pia!

Kiukweli sehemu moja muhimu ya kupunguza matumizi ya Serikali ni kuwaondoa manaibu waziri kwani zaidi ya kujibu maswali bungeni huwa sioni kazi nyingine ya maana wanayofanya.

Katika hili nakubaliana kabisa na Rais wa Zanzibar Dkt. Mwinyi la kutoteua manaibu Waziri katika baraza lake.

Ni imani yangu utaratibu huu una baraka za chama na hata Rais Magufuli atafanya vivyo hivyo.

Maendeleo hayana vyama!
Kama ni hivyo basi ni kwa nini bado ameamua kuwa na makamo rais wawili? Kuna haja gani ya kuwa na Rais wa nchi ndogo kama zanzibar kuwa na makamo wawili? na hawa nao wanafanya kazi gani hasa ambazo rais mwenyewe na makamo mmoja hawawezi kuzitekeleza?
 
Ma Naibu waziri wakitumika vizuri wanakuwa na manufaa,kama tulivyomuona Bashe.
Lakini imezoeleka tabia ya watawala wetu kuwatunukia uwaziri mdogo kama zawadi.
Matokeo yake wanajikuta wanaishia kuwa na ofisi bila majukumu yenye tija.
Nchi tajiri kama Ulaya zina mawaziri kidogo sana ukilinganisha na Afrika. Nguvu nyingi huko Ulaya imewekwa kwenye idara za wizara.
 
Bwashee umefail sana. Zanzibar na Rwanda inawezekana kuwa na wizara bila manaibu mawaziri kadhalika na makatibu wakuu bila kuwa na manaibu. Ila Tanganyika sio rahisi mkuu. Hili linchi ni likubwa sana bwashee. waziri hawezi hata kidogo kufanya kazi nchi nzima hasa wizara kama ya fedha, Afya, elimu na wizara nyingine nyeti zinazohitaji ukaribu sana kama kilimo. Akifanya hivyo atakuwa amekurupuka na nitampa miezi miwili ataanza upya japo anajiona kichwa ngumu.
Sio kweli...

Ni Bora makatibu wakuu wawe wawili na naibu waziri asiwepo.
 
Bwashee umefail sana. Zanzibar na Rwanda inawezekana kuwa na wizara bila manaibu mawaziri kadhalika na makatibu wakuu bila kuwa na manaibu. Ila Tanganyika sio rahisi mkuu. Hili linchi ni likubwa sana bwashee. waziri hawezi hata kidogo kufanya kazi nchi nzima hasa wizara kama ya fedha, Afya, elimu na wizara nyingine nyeti zinazohitaji ukaribu sana kama kilimo. Akifanya hivyo atakuwa amekurupuka na nitampa miezi miwili ataanza upya japo anajiona kichwa ngumu.
Mkuu wizara haimtegemei waziri tu kujiendesha na watendaji wengi Tena walio somea kabisa juu ya mambo ya wizara hiyo na ndo Maana hata kipindi hiki ambapo nchi haina mawaziri bado inaenda na Mambo yanaenda vizuri tu.
Kazi ya waziri ni kama msimamizi wa wizara tu Ila siyo mtendaji.
Hivyo Basi kila wizara ikiwa na Waziri mmoja, katibu na watendaji Kazi waliobaki hakuna kitakacho haribika. Otherwise Kama wizara ina Mambo mengi Sana ndo unaweza ungeza na naibu Waziri.

Tujifunze kubana matumizi kwa faida ya wote.
 
Mkuu wizara haimtegemei waziri tu kujiendesha na watendaji wengi Tena walio somea kabisa juu ya mambo ya wizara hiyo na ndo Maana hata kipindi hiki ambapo nchi haina mawaziri bado inaenda na Mambo yanaenda vizuri tu.
Kazi ya waziri ni kama msimamizi wa wizara tu Ila siyo mtendaji.
Hivyo Basi kila wizara ikiwa na Waziri mmoja, katibu na watendaji Kazi waliobaki hakuna kitakacho haribika. Otherwise Kama wizara ina Mambo mengi Sana ndo unaweza ungeza na naibu Waziri.

Tujifunze kubana matumizi kwa faida ya wote.
Hakika mkuu!
 
Back
Top Bottom