mtanzania in exile
JF-Expert Member
- Feb 17, 2012
- 1,379
- 1,276
Kama ni hivyo basi ni kwa nini bado ameamua kuwa na makamo rais wawili? Kuna haja gani ya kuwa na Rais wa nchi ndogo kama zanzibar kuwa na makamo wawili? na hawa nao wanafanya kazi gani hasa ambazo rais mwenyewe na makamo mmoja hawawezi kuzitekeleza?Kiukweli sehemu moja muhimu ya kupunguza matumizi ya Serikali ni kuwaondoa manaibu waziri kwani zaidi ya kujibu maswali bungeni huwa sioni kazi nyingine ya maana wanayofanya.
Katika hili nakubaliana kabisa na Rais wa Zanzibar Dkt. Mwinyi la kutoteua manaibu Waziri katika baraza lake.
Ni imani yangu utaratibu huu una baraka za chama na hata Rais Magufuli atafanya vivyo hivyo.
Maendeleo hayana vyama!
Swali zuri!Kwani Marekani ina manaibu wa Mawaziri wangapi?
Bora makatibu wakuu wawe wawili kuliko manaibu waziri.Zanzibar ni ndogo sana mkuu hamna haja ya manaibu ila kwa mainland inakuwa ngumu kidgo Tanganyika ina eneo kubwa manaibu muhimu.
Sio kweli...Bwashee umefail sana. Zanzibar na Rwanda inawezekana kuwa na wizara bila manaibu mawaziri kadhalika na makatibu wakuu bila kuwa na manaibu. Ila Tanganyika sio rahisi mkuu. Hili linchi ni likubwa sana bwashee. waziri hawezi hata kidogo kufanya kazi nchi nzima hasa wizara kama ya fedha, Afya, elimu na wizara nyingine nyeti zinazohitaji ukaribu sana kama kilimo. Akifanya hivyo atakuwa amekurupuka na nitampa miezi miwili ataanza upya japo anajiona kichwa ngumu.
Mkuu wizara haimtegemei waziri tu kujiendesha na watendaji wengi Tena walio somea kabisa juu ya mambo ya wizara hiyo na ndo Maana hata kipindi hiki ambapo nchi haina mawaziri bado inaenda na Mambo yanaenda vizuri tu.Bwashee umefail sana. Zanzibar na Rwanda inawezekana kuwa na wizara bila manaibu mawaziri kadhalika na makatibu wakuu bila kuwa na manaibu. Ila Tanganyika sio rahisi mkuu. Hili linchi ni likubwa sana bwashee. waziri hawezi hata kidogo kufanya kazi nchi nzima hasa wizara kama ya fedha, Afya, elimu na wizara nyingine nyeti zinazohitaji ukaribu sana kama kilimo. Akifanya hivyo atakuwa amekurupuka na nitampa miezi miwili ataanza upya japo anajiona kichwa ngumu.
Hakika mkuu!Mkuu wizara haimtegemei waziri tu kujiendesha na watendaji wengi Tena walio somea kabisa juu ya mambo ya wizara hiyo na ndo Maana hata kipindi hiki ambapo nchi haina mawaziri bado inaenda na Mambo yanaenda vizuri tu.
Kazi ya waziri ni kama msimamizi wa wizara tu Ila siyo mtendaji.
Hivyo Basi kila wizara ikiwa na Waziri mmoja, katibu na watendaji Kazi waliobaki hakuna kitakacho haribika. Otherwise Kama wizara ina Mambo mengi Sana ndo unaweza ungeza na naibu Waziri.
Tujifunze kubana matumizi kwa faida ya wote.
Mkuu mambo ya Uturuki utaendeleza mda gani?